UTAFITI MBALIMBALI KATIKA DINI NA SAYANSI
IMEANDALIWA NA AL-AMIN ALI HAMAD
HADITHI ZA MTUME MOHAMAD .ﷺ ZENYE MIUJIZA
Kuna baadhi Hadithi mbalimbali za Mtume Mohamad ﷺ ambazo hapo zamani yaliyoashiriwa hayakuwa na uhusiano na mazingara ya wakati huo.
Hapo zamani katika karne zilizopita yaani kuanzia karne ya 7 na zilizofuatia mpaka Mwanzoni mwa karne ya 20 Elimu za Sayansi zilikuwa bado changa sana na Hadithi kama hizi zilikuwa mbali na fahamu na pia Elimu za watu wakati huo. Wanavyuoni waliziamini na kuziacha hivyo hivyo bila ya kuzipinga.
Leo tunakuta Hadithi hizo zinaleta maana kubwa. Kwani hivi karibuni Utafiti wa kisayansi katika nyanja mbalimbali umegundua mengi ambayo yanathibitisha kwamba aliyoyazungumza Mtume Mohamad ﷺ ni ukweli bila ya shaka yeyote.
Na hadithi hizi zimekuwa Muujiza kwani aliyoyazungumza Mtume ﷺ wakati huo yamegunduliwa hivi karibuni.
Wakati huo kulikuwa hakuna vyombo vya utafiti kama Wakati huu wa kisasa.
Hadithi za Mtume ﷺ ni Wahyi kama inavyosema kuruani Tukufu.
Mfano unaposafiri kutoka mji na kuenda mji mwingine utakuta Barabarani Vibao vya Kutujuuklisha Umbali yaani Maili au Kilomita. Kama ni Maili 100 baada ya kuendelea na Safari utaona 80 kisha 60 kisha 50 kisha 10 na mfano huu huu Mwenyeezi Mungu ameweka Alama za Kukaribia kwa Kiyama.
Hadithi hii ina vipengele Vinne na kama sikosei na vyote vimetokea. na kama Katika Hadithi Nyinginezo za Mtume ﷺ zinazosema kwamba Kiyama Kimekaribia.
Na Kuruani pia inathibitisha kukaribia kwa kiyama. Mwenyeezi Mungu anasema
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ
“IKTARABA|TI ASAAA”
yaani Kiyama Kimekaribia sana tena bila Shaka na ndiyo maana Neno “IKTARABATI” lipo katika “Passive Tense” na Aya Hii pia inathibitisha Kupasuliwa kwa Mwezi. Katika Mojawapo ya Miujiza Ya Mtume Mohamad ﷺ ni Kupasua Mwezi.
Hebu tuchunguze Hadithi mbalimbali za aina hii.
ALAMA AU FITINA KABLA YA KUTOKEA KIYAMA
HADITHI -1 (KITABU CHA FITNA (AL-FITAN)
Jami` at-Tirmidhi Hadithi Namba 2181
حَدَّثَنَا سُفْيَانُ بْنُ وَكِيعٍ، حَدَّثَنَا أَبِي، عَنِ الْقَاسِمِ بْنِ الْفَضْلِ، حَدَّثَنَا أَبُو نَضْرَةَ الْعَبْدِيُّ، عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم “ وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لاَ تَقُومُ السَّاعَةُ حَتَّى تُكَلِّمَ السِّبَاعُ الإِنْسَ وَحَتَّى تُكَلِّمَ الرَّجُلَ عَذَبَةُ سَوْطِهِ وَشِرَاكُ نَعْلِهِ وَتُخْبِرَهُ فَخِذُهُ بِمَا أَحْدَثَ أَهْلُهُ مِنْ بَعْدِهِ ” . قَالَ أَبُو عِيسَى وَفِي الْبَابِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ . وَهَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ غَرِيبٌ لاَ نَعْرِفُهُ إِلاَّ مِنْ حَدِيثِ الْقَاسِمِ بْنِ الْفَضْلِ . وَالْقَاسِمُ بْنُ الْفَضْلِ ثِقَةٌ مَأْمُونٌ عِنْدَ أَهْلِ الْحَدِيثِ وَثَّقَهُ يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ وَعَبْدُ الرَّحْمَنِ بْنُ مَهْدِيٍّ .
TAFSIRI
Abu Saeed Al-Khudri anaelezea kwamba Mtume ﷺ alisema
Swahili Translation
“Naapa kwa yule ambaye Roho yangu ipo mikononi mwake. Kiyama hakitafanyika mpaka Wanyama watakapozungumza na watu, Ncha za fimbo, Kiatu na Paja (lake) litakapomjuulisha habari za familia yake.
English Translation
(Abu Sa’eed Al-Khudri narrated that the Messenger of Allah (s.a.w) said: “By the One in Whose Hand is my soul! The Hour will not be established until predators speak to people and until the tip of a man’s whip and the straps on his sandal speak to him, and his thigh informs him of what occurred with his family after him.”)
SHEREHE
Hadithi hii inashangaza sana. Hebu tujiulize Maswali.
Je Kabla ya Kiyama au kiyama kinapokaribia Vifuatavyo vitaweza kuzungumza na Binaadamu?
1/Mnyama Wa Pori au Baharini. Neno السِّبَاعُ ni Predator. Mfano wa Samaki ambao wanakula samaki wengineo. Au Mbwa Mwitu, Au Fisi. Na wengineo.
2/Ncha ya Fimbo
3/Kiatu
4/Simu Juu ya Paja La Mguu
Wanavyuoni wakati huo waliipokea hadithi hii na mfano wa Hadithi za aina hii na kuzihifadhi bila kuzipinga au kuzitilia shaka.
Tupo katika karne ya 21 na Mtume aliishi katika karne ya 7.
Hebu tufikiri karne ngapi zimepita?
Karibu Karne 14 yaani miaka 1400 iliyopita.
Haya yaliyozungumzwa ni karibu miaka 1400 iliyopita.
Sasa leo hii tupo katika Karne ya 21. Ni Karne ya Sayansi za Hali ya Juu.
Uamini au Usiamini. Wataalamu wametengeneza Viatu ambavyo vina Simu.
Pia Wataalamu wametengeneza Fimbo zenye Simu na hizi zina uwezo Mkubwa wa kuwasaidia Vipofu, Vilema, Wazee na Wenye maradhi mbalimbali. Fimbo zenye uwezo wa kupeleka Habari nyumbani ikiwa Mzee anayeumwa kama amepotea njia au kuanguka kwa sababu yeyote ile ya Maradhi.
Kwa kifupi Fimbo hiyo in uwezo wa Kuwasiliana na Watu ili kumsaidi anayeitumia.
Na Simu za mikono ambazo mara nyingi huwekwa mifukoni yaani Karibu na Paja. Simu hizo kwa wale wanotumia Bluetooth huiacha mifukoni. Kwa hiyo Simu yako inakuwa Mifukoni yaani karibu na Paja lako. Na pia kuna Simu ambazo huwekwa Juu ya Paja na Kufungiwa hapo kwa mkanda maaalum ili kuidhibiti vizuri pajani. Inajulikana kama Thiphone. Angalia Video hapa chini.
Hebu tuichambue Hadithi hii tena.
Tunaambiwa kwamba Kiyama Kitakapokaribia basi kutakuwa na Alama Alama Mbalimbali za kutujuulisha ili tujiandae kwa kubadili vitendo vyetu vibaya kabla ya wakati huo.
Baadhi ya Alama Mbalimbali zimekwisha onekana. Kuna Vitabui mbalimbali vimetaja Alama hizo.
Kwa mfano Kitabu cha Ibn Kathir na wanavyuoni wengineo wameandika Habari hizi kwa urefu.
Kwa kifupi Katika Alama Zilizotajwa katika Hadithi hii temeona kwamba Alama za Kiyama tatu za mwisho zimekwisha tokea.
1/Mnyama wa Pori (Bado kuonekana)
2/Fimbo Itakayozungumza (imeshaonekana angalia Video hapa chini)
3/Kiatu kitakachozungumza (Imeshaonekana angalia video hapa chini)
4/Paja La Mguu Litakalozungumza(Imeshaonekana angalia video hapa chini)
Nimeambatanisha Hapa Chini Video za Viatu, Fimbo “SMART CANE” na Simu ya Pajani. “Thipphone” na Alhamdulilahi leo tarehe 26/08/2022 nimeambatanisha Habari ya Samaki kuzungumza. (Sina uhakika wa habari hizi) lakini Gazeti maarufu la huko Marekani ndovyo linavyosema. Na ikiwa ni kweli basi inathibitisha Hadithi tuliyosoma hapa juu kwamba Mnyama ataweza kuzungumza.
VIDEO-1
Viatu Vilivyoshonwa na kutiwa Computer na Uwezo wa Kuzungumza. Je unaona Aliyotabiri Mtume Mohamad katika Karne ya 7 ? Allahu Akbar
Video-2
Fimbo inayozumgumza inajulikana kama “SMART CANE” ni mojawapo ya Maendeleo ya kisasa. Kama alivyotabiri Mtume Mohamad ﷺ hapo zamani. Allahu Akbar.
Video-3
Simu ambayo imefungwa Katika Paja. Simu ni ya kawaida lakini imefungw ana mikanda hapo mguni. Lengo ni kuidhibiti vizuri. Kwa lugha nyingine ni simu ya Pajani au THIPPHONE. Sikiliza Video inayohusu simu hii. La kushangaza ni Hadithi ya Mtume hapa juu.
Hapa chini Gazeti La Marekani BBC NEWS la mwaka 2003 linatuelezea habari ya samaki aliyezungumza kwa lugha ya kiyahudi na kuonya habari za kukaribia kwa kiyama. Kama hizi habari ni za kweli basi inathibitisha hadithi ya Mtume Mohamad ﷺ kuhusu Mnyama au Samaki atakayezungumza na Binaadamu. Allahu Akbar. Unaweza kusoma makala iliyokamili kwa kutumia anuani ya mtandao ufuatao:
http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/americas/2854189.stm
