SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Changamoto

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

28/08/2022

Jumapili Jioni. Alhamdulilah Ninashukuru Mwenyeezi Mungu kunipa Nafasi hii kuwaletea Muujiza Mzuri  kutoka katika Hotuba Na Mwongozo wa Mwenyeezi Mungu.

Hotuba Hiyo na Mwongozo huu hakuna mwingine isipokuwa Maneno Yake Matukufu yaliyohifadhiwa katika Kitabu Kitukufu cha Msahafu.

Mlango huu nimeuita Changamoto yaani  Challenge

Mwenyeezi Mungu anawapa Viumbe Vyake Mtihani.

Kwa hiyo nitakusanya katika mlango huu  kila Aya zinazohusu  Changamoto

Na kwa kweli Makafiri  Kuanzia Kushushwa kwa Kuruani Wamefeli Mitihani iliyotolewa Na Muumba 

Makaburini kuna Vilio na Siku ya kiyama pia kuna Vilio. (Mwenyeezi Mungu atuepushie na Kutusamehe makosa na madhambi yetu).

Hebu  Tuchunguze na Tuielekeze darubini  yetu katika Aya Ifuatayo:

قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا الْقُرْآنِ لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

TAFSIRI

88. Sema “Hata wakijikusanya watu (wote) na majinni ili kuleta mfano wa hii Qurani basi hawangaliweza kuleta mfano wake; hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao.,

SHEREHE

Aya hii ni mtihani  mkubwa. Mwenyeezi Mungu aliyeumba kila kitu anatuambia kwamba Sisi Binaadamu wote tungekusanyika na  Majini  yote na kisha tukasaidiana kuandika Maandhishi mfano wa Kuruani  basi  tungelifeli.  Hebu fikiri  mtihani huu. Na kweli miaka  zaidi ya Elfu imepita na hakuna aliyeweza kufanya hivyo.

Yaani  Profesa  wa Duniani ambao wana Elimu mbalimbali, Walio na PHD’s  au Diploma nyinginezo mbalimbali wangekusanyika na kisha  Majini yenye Elimu pia na wote wangefanya kazi kwa umoja kujaribu kutunga mfano wa Kuruani basi wasingeliweza kabisa.  Kwa kweli huu sio Mtihani  mdogo. 

Hakuna aliyeweza na atakayeweza hata tufanye juhudi zote. Ujanja wetu na mali zetu zote zingetumika  kwa kazi hii pia Ingelifeli.

MUUJIZA

Hebu Tuichunguze  Mfumo  au  Structure tu ya Aya hii tuone  Mpangilio  wake wa Kiherufi na Kimaneno.

قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا الْقُرْآنِ لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

Kipande Cha Aya  Kabla ya neno الْقُرْآنِ  Kuruani  kina Herufi 38

قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا

——————————–

Na Kipande Cha  Aya Baada ya neno الْقُرْآنِ  kina herufi 32

لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

——————

Sasa  tukigeuza Herufi  hizi katika namba.

(Kama nilivyoelezea katika sehemu nyinginezo za Website hii kwamba Lugha ya Kiarabu inajulikana kama  Alphanumeric  kama lugha nyinginezo (kama vile Hebrew) za sehemu hiyo na wakati huo  wa karne ya 7)

Wakati huo  Kulikuwa hakuna Namba  kama hizi tunazotumia leo na kwa hiyo Herufi zilitumika kama Namba. Kwa mfano

Herufi Alif  Iliwakilisha Namba 1

Herufi Baa Iliwakilisha Namba 2

Herufi Taa iliwakilisha Namba 3

Na hivyo hivyo  herufi zote zilipewa Namba.

Herufi  Sin  iliwakilisha Namba 60

Herufi Ghain iliwalilisha Namba 1000

Nitaishia Hapa kwani  Nilikwisha Elezea Sehemu nyingine ya Website hii. Kitu muhimu  uelewe Madhumuni Ya habari hii).

Nitazinukulu tena Vile Vipande vya Aya kisha tuone Maajabu yanayofuata:

1/قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا

——————————–

Na Kipande Cha Aya Baada ya neno الْقُرْآنِ kina herufi  32

2/ لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

——————

Ukigeuza  Kipande cha kwanza katika Namba za hapo zamani  utapata Jumla ya namba hizo  ni  3214

Na Ukigeuza Kipande cha pili  katika Namba za hapo zamani utapata Jumla ya namba hizo ni 4123

Hebu  Angalia Namba Hizi Mbili  zinavyoshangaza.

4123                     3214

Ngoja nizipange  Chini ya Aya  tuone Maajabu

قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا/ الْقُرْآنِ / لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ

   4123                                                            3214

كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

Angalia Namba Hizi Mbili.

Namba ya Pili ni kinyume  ya Namba ya Kwanza.  4213 na kisha  3124  yaani Kinyume chake.

Hebu fikiri  maajabu ya mpangilio huu.  Hebu waza. Kuna siri  gani imefichika hapa.  Allahu Akbar.

Yaani  Vipande vya Aya hivi ni kama

MABAWA YA KIPEPEO.

Mabawa Mawili ya Kipepeo yanafanana  kila kitu. na pia Mfano mwingine  ni Viungo  vyako  ninavyofanana. Mkono wa Kulia  na Mkono wa Kushoto.  Jicho la kulia na Jicho la Kushoto.  Mguu wa kulia na Mguu wa Kushoto. Sikio la kulia Na Sikio la Kushoto ni sawa na Mfano  huu wa mabawa ya Kipepeo.

Ukiwa Mchoraji  utaelewa habari hii  vizuri zaidi. Wasanii wanajua  ufundi huu vizuri  wanapochora. 

Aya hii ina Neno  KURUANI Katikati  na Kila Upande wa neno KURUANI kuna  Vipande vya Aya vinavyofanana  kinamba.  haya Maajabu ya kweli.

Je binaadamu anaweza kutunga Mfano huu. Huu ni mfano mmoja tu lakini kuruani ambayo haina mwisho wa maajabu. Kuna Mifano  isiyo na mwisho.

Hii ndiyo  Changamoto. Ni Jamba Jamba  kama wanavyosema katika Kiswahili. 

Hebu  tuchunguze idadi ya Maneno na Herufi  katika Aya Hii

قُلْ لَئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنْسُ وَالْجِنُّ عَلَى أَنْ يَأْتُوا بِمِثْلِ هَذَا الْقُرْآنِ لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا

Jumla Ya Maneno  ni 19 na Herufi ni  76

Angalia Maajabu. 

Herufi  76  ni sawa na  19 + 19 + 19 + 19 yaani  19 mara 4

Hebu fikiri mbona namba 19  imekariri  hapa.

Allahu Akbar.

Je  Namba 19  ni sawa na   1 + 9=10 

na 10  ni sawa na  1 +0=1

Namba 1  Inamwakilisha Mwenyeezi Mungu peke yake?  Mimi Najiuliza Suali?

Hebu  Kumbuka Katika  Sura Ya Al-MUdathir Mwenyeezi Mungu ameitaja Namba hii  19.

Mwenyeezi Mungu  amesema katika Sura Ya Al-Mudathir Kwamba Amejaalia Waangalizi  (Malaika) katika  Moto wa Jahannam kuwa 19  na akaendelea kuuliza Kwa nini amejaalia  hao Malaika kuwa 19?

Akajibu kwamba Namba hii ni kuwazidishia Imani  Waumini.  Na Akasema pia Kwamba Namba Hii itawavutia Watu wa Vitabu (Wakristo  na Mayahudi)  waukubali Uislamu na Pia Namba hii  itawafanya Makafiri wababaike na  kujiuliza

“Kwa nini Mwenyeezi Mungu amejaalia Malaika Hao kuwa 19?”

Ukifikiri sana utaona Maajabu sana Tena sana.

Aya ya Basmala  pia inaherufi  19

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

Sura Ya Kwanza Kushuka  ni  AL-Alaq  nayo ni Ya 19

Aya zake  ni 19

Aya za Mwanzo  kushuka za Sura Hii ya Al-Alaq ni

اقرا باسم ربك الذي خلق خلق الانسن من علق اقرا وربك الاكرم الذي علم بالقلم علم الانسن ما لم يعلم

Na  Herufi zake ni  76

Na  namba 76  ni sawa na 19  x 4

yaani  19 + 19 + 19 +19

Hebu fikiri  maajabu haya  yasiyo na mwisho.

Sasa  nakuachia mwenyewe ufikiri.

Chukua Keki na Chai  kunywa kwa Raha yako kisha Rudi  usome haya kwa Raha Yako na ufikiri.  Hakuna Haraka. Pole Pole.

Kwa leo naishia Hapa. 

Miujiza Inaendelea kilicho  muhimu ni Uzima.