SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Darasa Za Ijumaa-1

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

DARASA KILA IJUMAA

MLANGO HUU UTAKUSANYA AYA ZA KURUANI, HADITHI ZA MTUME MOHAMAD ﷺ NA HADITHI ZA QUDSIY AMBAZO NI KAULI YA MWENYEEZI MUNGU KUTAKUWA NA TAFSIRI NA SHEREHE ZAKE

23/09/2022

SUALA LA KWANZA

Alhamdulilah  leo ni siku  tukufu. ni ijumaa. Mwenyeezi Mungu akipenda katika Mlango huu nitakuwa nikiwaletea vipande vidogo vidogo vya kila zuri. kwanza Vipande hivi vitaninasihi mimi mwenyewe na pia wewe msomaji wa Website hii. Kwa hiyo nakukaribisha kwa Salaam Tukufu inayosema. 

“Salaam Nyingi kwenu, Rehema na Baraka Za Mwenyeeezi Mungu Ziwafikieni popote mlipo”

Mwenyeezi Mungu akipenda Siku za  Ijumaa Nitaweka Kipande kimoja na Nitakitia Namba na kwa hiyo leo  nitaanza na Namba Moja.

1/Kipande cha leo ni Hadithi Ya Qudsiy ambayo Ina nasiha Nzuri sana.

Kuna Tofauti  baina ya Sunnah Za Mtume ﷺ na Hadithi  za Qudsiy ambayo nilizungumzia katika Mlango  wa “Elimu Za Kiislamu”.  Kwa Kifupi  Hadithi  Qudsiy  ni Ujumbe Kutoka Kwa Mwenyeezi Mungu lakini Imefikishwa kwetu  kwa Lugha ya Mtume Mohamad ﷺ Yaani  Maneno  ni ya Mtume ﷺ lakini  Ujumbe ni kutoka Kwa Mwenyeezi Mungu.  Na Kuruani  ni Ujumbe kutoka Kwa Mwenyeezi Mungu na Pia Lugha. Yaani Maneno ni Ya Mwenyeezi Mungu na Siyo yake Mtume.ﷺ Na Hadithi  Za  Mtume  au  Sunnah  za Mtume ﷺ ni  Mazungumzo na Vitendo vya Mtume ﷺ na  Vile alivyokiri au alivyowakubalia Maswahaba  zake.

Ngoja nifupishe hapa chini ili  ieleweke vizuri:

1/Kuruani ni Ujumbe kutoka kwa  Mwenyeezi Mungu Mtukufu na Maneno  ni Yake.

2/Hadithi  za Qudsiy pia ni  Ujumbe Kutoka Kwa Mwenyeezi Mungu lakini kwa Maneno ya Mtume Mohamad ﷺ

2/Hadithi  za Mtume ﷺ ni Kila alichosema, kutenda na vile vitendo alivyowakubalia Maswahaba zake. ukichunguza utaona Hadithi  za Qudsiy zinaishia Na  “Alisema Mwenyeezi Mungu” na Hadithi  za Sunnah au za Mtume Mohamad ﷺ zinaishia na “Alisema Mtume”.

Je imeeleweka? Inshaallah Itaeleweka.

Katika Siku ya leo nitawaletea Hadithi Qudsiy.

Hadithi Hii ipo katika Volume au Kitabu cha  Sunan  Ya Tirmidhiy

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ إِنَّ اللَّهَ تَعَالَى يَقُولُ يَا ابْنَ آدَمَ تَفَرَّغْ لِعِبَادَتِي أَمْلَأْ صَدْرَكَ غِنًى وَأَسُدَّ فَقْرَكَ وَإِلَّا تَفْعَلْ مَلَأْتُ يَدَيْكَ شُغْلًا وَلَمْ أَسُدَّ فَقْرَكَ

2466 سنن الترمذي كتاب صفة القيامة والرقائق والورع باب منه

Hadithi  Hii iliyotajwa na Abu Hurayra na ambayo inatokana na Mtume Mohamad ﷺ inasema kwamba

“Mwenyeezi Mungu anasema Ewe  Binaadamu Fanya  Ibada kwangu na mimi  nitajaza Moyo wako na Utajiri na pia  nitakuondolea  Ufakiri na kama  hutafanya haya  basi nitajaza Mikono yako  na Shughuli zisizo na mwisho na sitakuondolea Ufakiri.

ENGLISH

Abu Huraira reported: The Prophet, peace and blessings be upon him, said, “Allah Almighty said: O son of Adam, be free for My worship and I will fill your heart with riches and alleviate your poverty. If you do not do so, I will fill your hands with problems and never alleviate your poverty.”

SHEREHE

Ukifikiri  Hadithi  hii utaona  mifano hii kila mara katika maisha. Wakati  Binaadamu anashughulika na kazi sana usiku na mchana  lakini mapato  hayatoshi kujilipia  Gharama za maisha. Kazi  mchana na usiku lakini mapato hayana Baraka, na shida zipo pale pale haziishi.  kazi zinafanyika kwa juhudi zote lakini bado ufakiri hauondoki. Na Mtu anajikuta anazunguka kama Pia, Na  mahangaiko yasiyo na mwisho. Haya Mambo yapo kila siku katika maisha yetu na siyo geni. Na Iwapo mtu akafanya Ibada iliyo ya kweli na kujishughulisha na Yale yanayomridhisha Mwenyeezi Mungu basi kazi hazimchokeshi  mtu na Mapato yatakuwa na Baraka. Yaani Mapato yatazidi na Kwa kweli huu ni ukweli ambao  tunauona kila siku katika Maisha. 

Mwenyeezi  Mungu tutakutana tena siku ya  Ijumaa na Mapya………….