SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Darubini-4/Kuruani

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MIUJIZA ISIYO NA MWISHO

Baada ya kufikiri sana Maajabu ya Kuruani nikakumbuka Usemi au Methali  walizoniambia  Rafiki zangu miaka  Mingi  iliyopita  (Zaidi ya miaka Arubaini) tulipokuwa wanafunzi katika Chuo  Kikuu.

Rafiki wa Kwanza ni Sheikh (Ndugu) kutoka Mwanza na wa pili ni Sheikh (Ndugu) kutoka Zanzibar. 

Katika mazungumzo  Rafiki wa Mwanza aliniambia Usemi  Mzuri  sana wa Kiswahili unaosema 

“KULIKOUNGUA SHOKA KUKABAKI MPINI”

Kwa hiyo ningependelea kuutumia usemi huu  katika Mlango huu kwa kusema 

“ELIMU ILIYOPO KATIKA KURUANU TUKUFU NI NYINGI MNO NA KWA KWELI  KATIKA KITABU HIKI NDIPO PALIPOUNGUA SHOKA KUKABAKI MPINI”

Na Rafiki wa pili kutoka Zanzibar  alikuwa akiniambia kila tukikutana.  

SHEIKH  AL-AMIN JE TUTAFIKA HUKO?

Kwa usemi huu alikuwa ana maana kwamba 

KAZI  YA HAPO SHULENI  YAANI MASOMO SIYO RAHISI NA INABIDI JUHUDI KUBWA NA KWA HIYO JE TUTAYAWEZA?

Leo hii Usemi huu ninaukumbuka mpaka leo na kila ninapofikiri Aya za Kuruani. Kwa kweli ninajiuliza Suala hili kwa kusema.

“JE TUTAFIKA HUKO?  JE TUTAFIKIA LINI KUMALIZA KUSOMA MIUJIZA YA KURUANI YOTE? JE INAWEZEKANA?”

Kwa usemi  huu ninaona “HATUTAFIKA KABISA” Kwani hakuna Mwisho. Kuruani imejaa Elimu isiyo na Mwisho. 

Mwenyeezi Mungu amefanya hivyo ili watu wauukubali Uislamu na waingie katika Dini hii ili Mwisho wa Dunia kusiwe na Hoja. Tusije tukabisha na kusema  hatukuletewa Ujumbe wowote.

Katika Mlango huu nitajitahidi kuweka  Miujiza mbali mbali. Kwa kweli Inashangaza sana. Inathibitisha kwamba Kuruani siyo maneno ya Binaadamu hata kidogo.

Allahu Akbar.  Kama huamini basi endelea kufuatilia habari za mlango huu kwani Mwenyeezi Mungu  akipenda kila nitakapo pata nafasi nitakuwa nikiongeza mapya yaani kila mara kama bado nipo hai katika dunia hii. Afya au Uzima ni muhimu sana. Na pia Usinisahau katika Dua zeni kwani ni muhimu sana. Mimi sina uwezo isipokuwa Uwezo  unatoka kwa Mwenyeezi Mungu. 

Pia Nawashukuru wale ambao nasoma kwao. Kila anayenifundisha Mwenyeezi Mungu ampe kila la kheri katika Dunia na Akhera. Mengine ni yangu na Mengine  ni ya Walimu zangu.  Namuomba Meenyeezi Mungu awape kila la kheri kwa Juhudi zao kubwa.

Sasa Tuanze  kazi.

MUUJIZA WA KWANZA

Hebu  Tupeleke Darubini yetu katika   Sura Ya Al-Fatiha ambayo pia ina majina Mbalimbali. Na katika majina hayo mojawapo ni  “UMMU AL_KITAAB”  yaani MAMA WA KITABU. (The Mother of The Book)  au  “ASABAA ALMATHANI”  yaani  AYA SABA ZINAZOKARIRI. (The seven repeatedly recited) yaani Ni Aya Saba ambazo zinatumika katika Kila Sala na kwa hiyo matumizi yake yana kariri  kariri kila wakati. Na Mwenyeezi Mungu anathibitisha Jina hili katika Sura Ya Al-HIjr  namba  15  Aya namba 87

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَـٰكَ سَبۡعً۬ا مِّنَ ٱلۡمَثَانِى وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ (٨٧) 

Mwenyeezi Mungu anamwambia Mtume Mohamad ﷺ

Kwa hakika Tumekupa Aya Saba zenye kukariri na pia Kuruani Tukufu. yaani Sura ya Alfatiha na pia Sura nyinginezo 113 za kuruani Tukufu.

سُوۡرَةُ الفَاتِحَة

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ (١) ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَـٰلَمِينَ (٢) ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ (٣) مَـٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ (٤) إِيَّاكَ نَعۡبُدُ وَإِيَّاكَ نَسۡتَعِينُ (٥) ٱهۡدِنَا ٱلصِّرَٲطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ (٦) صِرَٲطَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِمۡ غَيۡرِ ٱلۡمَغۡضُوبِ عَلَيۡهِمۡ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ (٧)

SHEREHE

Hebu tuchunguze idadi ya Herufi  za Jina lake Mwenyeezi Mungu katika Sura Hii. Yaani Jina lake la

الله   (ALLAH)

ALIF= imetumika mara 22

Alam= imetumika mara 22

Ha= imetumika mara 5

Jumla  ni   22 + 22 + 5=49

Je unaona maajabu.  Namba  49  ni sawa na kusema

7 x7  ambayo  ni   49

Je unaona Namba 7. Yaani  Sura imepewa Jina na Mwenyeezi Mungu  “Aya Saba Zinazokariri” na herufi za Jina lake  Yaani الله (ALLAH)  pia zimakariri mara 49 ambayo ni sawa na 7 x 7.  Hapa  Namba 7 ni Muujiza  na siyo bure bure. Mpangilio wa hekima kubwa.

MUUJIZA WA PILI

Sura ya Mohamad namba  47  Ina Jumla za Aya 38

Hebu Tuelekeze Darubini Katika Sura Ya Mohamad.

Tuchunguze Herufi za Jina Mohamad  katika Sura hii ambayo imepewa Jina lake. 

MIM=Imetumika mara 223

HAA=Imetumika mara 23

MIM=Imetumika mara  223

DAL=Imetumika mara   35

Jumla ya Herufi katika Sura hii ni

223 + 23 + 223 + 35=504

Kwa hiyo  504 kihesabu  ni sawa na kusema  63  X 8   

yaani  63 x 8=504

Unaona Muujiza katika Jina la Mtume?

Aliishi miaka  63 tu.  kwa hiyo Umri wake ulikuwa umefichika katika Idadi ya Herufi ya Jina lake.  Allahu Akbar. Yaani Hata yeye mwenyewe alikua hakujua kwani hakuna anayejua  siku atakayofariki dunia.  Angalia Maajabu haya. Siyo mambo  madogo. 

MIUJIZA INAENDELEA….