SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Darubini-5/Kuruani

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

Jumamosi   Tarrehe 27/08/2022

NINAWATUMIA SALAAM  NYINGI  KWA WASOMAJI  WOTE  WA WEBSITE HII. “Assalaam Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh”  Salaam Kwenu, Rahma na Baraka Zake Mwenyeezi Mungu Ziwafikie.

Alhamdulilah.  Leo Jua Zuri limechomoza na Ni Wakati Mzuri  wa kuwaletea Habari Nzuri  kutoka Kwa Mwenyeezi Mungu Mtukufu.  

Ninachukua Kalamu na Kuwaandikia Habari  nzuri Sana ambayo  inatuliza Roho.

Kwanza Ningependelea kuwajuulisha Kuwa Katika Maandishi Yangu huenda utakuta  Makosa Madogo  madogo  ya Herufi  katika Maneno. Makosa haya yanatokana na Uchapishaji  wa haraka  haraka. Nikipata nafasi nitajitahidi kusoma tena makala zangu na kuzisahihisha. Nina hakika kuna makosa makosa ya aina hii lakini ukisoma vizuri  utaelewa maana niliyokusudia na hilo ndilo lengo. 

MUUJIZA WA KWANZA (POLISI  WATATU) 

Sasa  Tuelekeze Darubini Yetu  katika Habari  Nzuri katika Sura Tatu za Kuruani.  Sura Ya  “GHAFIR”, “AL-SWAF”  na  “AL-SHAMS”

Tusiende mbali bali Ninaelekeza Darubini katika Sura Hizi  tatu tu.

Kabla Ya kuchunguza Sura Hizi  ningependelea Kuwajuulisha kwamba Kuruani  Imekusanya Sura  114  na Ina Jumla za Aya 6236  na  Mara ya Kwanza Kutajika  neno  Kuruani Tukufu  kuanzia  Mwanzo  wa Msahafu ni katika  Sura Ya Al-Bakarah  Aya Namba 185.  Yaani  Ukihesabu Kuanzia Mwanzo  wa Msahafu Kuanzia Sura Ya Al-Fatiha ambayo Ina Aya  7 mpaka katika Aya namba 185  utapata Jumla za Aya ni  192.

Aya namba 185  katika Sura ya Al-Bakarah  ni kama ifuatayo

شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْءَانُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَٰتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللَّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَىٰكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ

Kwa hiyo  Aya hii  ni ya  192  kuanzia Mwanzo  wa Msahafu ambayo  inataja neno  “KURUANI”

Kwa Kifupi  

Kuruani Ina Sura   114

Kuruani Ina Aya 6236

Neno  الْقُرْءَانُ    “KURUANI”  ni la  192 kuanzia Sura Ya Al-Fatiha.

Katika Utafiti huu Kumbuka  Namba Hizi  Tatu.

Sasa Tuelekeze Darubini  katika Hizo Sura Tatu  Tulizozitaja Hapa Juu  Uone Muujiza.  Allahu Akbar.  Muujiza sio  Mdogo.  Unathibitisha Kwamba Kuruani  Imepangwa.  Mpangilio wake wa Kimaneno, Kiherufi na Aya zake  zote  ni Muujiza Mtupu.

Sasa  Tuanze Utafiti:

1/SURA  YA  GHAFIR  NAMBA  40   INA JUMLA ZA AYA 85  NA JUMLA  YA HERUFI  5041

2/SURA YA AL-SWAF  NAMBA 61  INA JUMLA ZA AYA 14  NA  JUMLA YA HERUFI  945

3/SURA YA  AL-SHAMS NAMBA 91  INA JUMLA ZA AYA 15  NA JUMLA YA HERUFI  250

Hebu  Tujumlishe namba za Sura, Aya na Maneno.

Jumla Za  Sura=40 + 61 + 91=192

Jumla Za  Aya=85 + 14 + 15=114

Jumla Za Herufi=5041 + 945 + 250=6236

Je Unaona Maajabu.  Hizi Sura Tatu  zimetupa  habari  za kushangaza. Kwanza namba 192  Inashiria Jina la Kuruani ni Aya ya 192 kuanzia mwanzo wa Msahafu.  Kisha Namba 114 inashiria Jumla Ya Sura za Kuruani na Namba 6236  inaashiria Jumla ya Aya za Kuruani yote.

Allahu Akbar.  Kuruani  Imapimwa kila kitu. Yaani  Baadhi ya Sura Zinathibitisha Ukweli wa Kuruani yote. Sura Hizi Tatu ni kama Polisi  wanailinda kuruani  isigeuzwe.    Ni  baadhi ya Mapolisi  Watatu wa kitabu  hiki. 

Hebu Fikiri mwenyewe uone haya maajabu makubwa. Mapolisi  watatu  wanailinda Kuruani Tukufu. Yaani Kuruani  inajilinda yenyewe. 
Hakuna Upuuzi.  Hakuna Atakayeibadili kwa kuongeza au Kuipunguza. Allahu Akbar.  Ingegeuzwa au kupunguzwa basi Tusingepata Miujiza kama hii.. 

Ufundi huu  tunaweza kuuita kwa ibara inayosema

“Iterlocking Mathematical Values”  (Thamani za Kihesabu zilizofungamana au Makufuli  yaliyofungamana.)

Allahu Akbar.  Allahu Akbar.  Kwa kweli Nimeivulia Kofia Kuruani.  Ukubwa wa Kuruani  unathibitisha ukubwa wa Mwenyeezi Mungu. Ni Hotuba Yake. Na Ikiwa ni  Hotuba yake basi je Aliyeiandaa  atakuwa vipi?

MUUJIZA WA PILI (NAMBA ZA AYA NA IDADI ZA AYA)

Sasa nitawaletea Muujiza wa pili.  Kwa kweli inafurahisha Nafsi.  

Nilipokuwa bado kijana wa umri mdogo   Rafiki yangu alikuwa akiniambia kwama  Pesa ndiyo  “SABUNI YA ROHO”  kila akiniona ninashika Pesa  mkononi basi ananiambia  hiyo  Bwana ndiyo Sabuni ya Roho.  Rafiki huyu alikuwa hakukosea. Kwa kweli  Pesa ni Sabuni  ya Roho kweli sio  kosa hata kidogo. 

Usemi huu ningependelea kuutumia leo pia  na kusema 

“KURUANI  NDIYO SABUNI YA ROHO  KUBWA KULIKO PESA AU

CHOCHOTE KILE TUNACHOKIJUA NA TUSICHOKIJUA”

Hebu  tujifurahishe kwa Muujiza Mtamu  wa Kuruani. Sasa tuelekeze Darubini katika Aya Hizi Nne tuone Ya Kushangaza. Allahu Akbar.

Jina La Mtume  ﷺ Yaani   Mohamad ﷺ Limetajika katika Kuruani Mara 4  tu katika Aya Zifuatazo Nne.

Kabla Ya kuendelea na Muujiza huu ningekushauri  Utengeneze Chai iwe karibu yako na ikiwezekana Mandazi au Vitumbua Pia.

Huku unakunywa na kula kwa Raha yako bila  wasiwasi soma  Muujiza unaofuata Wenye Utamu zaidi Ya Asali 

Umetengenezwa na Muumbaji wa kila kitu. Ni zawadi aliyotengeneza kwa ajili ya Viumbe vyake.

1/SURA  YA AL_IMRAN  NAMBA 3  AYA NAMBA 144

وَمَا مُحَمَّدٌ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ أَفَإِين مَّاتَ أَوْ قُتِلَ انقَلَبْتُمْ عَلَىٰ أَعْقَٰبِكُمْ وَمَن يَنقَلِبْ عَلَىٰ عَقِبَيْهِ فَلَن يَضُرَّ اللَّهَ شَيْءًا وَسَيَجْزِي اللَّهُ الشَّٰكِرِينَ

2/SURA YA AL-AHZAB  NAMBA 33  AYA NAMBA 40

مَّا كَانَ مُحَمَّدٌ أَبَا أَحَدٍ مِّن رِّجَالِكُمْ وَلَٰكِن رَّسُولَ اللَّهِ وَخَاتَمَ النَّبِيِّنَ وَكَانَ اللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا

3/SURA YA SURA YA MOHAMAD NAMBA 47  AYA NAMBA 2

وَالَّذِينَ ءَامَنُوا وَعَمِلُوا الصَّٰلِحَٰتِ وَءَامَنُوا بِمَا نُزِّلَ عَلَىٰ مُحَمَّدٍ وَهُوَ الْحَقُّ مِن رَّبِّهِمْ كَفَّرَ عَنْهُمْ سَيِّءَاتِهِمْ وَأَصْلَحَ بَالَهُمْ

4/SURA YA AL-FATH   NAMBA 48  AYA NAMBA 29

مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّهِ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ تَرَىٰهُمْ رُكَّعًا سُجَّدًا يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّنَ اللَّهِ وَرِضْوَٰنًا سِيمَاهُمْ فِي وُجُوهِهِم مِّنْ أَثَرِ السُّجُودِ ذَٰلِكَ مَثَلُهُمْ فِي التَّوْرَىٰةِ وَمَثَلُهُمْ فِي الْإِنجِيلِ كَزَرْعٍ أَخْرَجَ شَطْءَهُ فَءَازَرَهُ فَاسْتَغْلَظَ فَاسْتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِ يُعْجِبُ الزُّرَّاعَ لِيَغِيظَ بِهِمُ الْكُفَّارَ وَعَدَ اللَّهُ الَّذِينَ ءَامَنُوا وَعَمِلُوا الصَّٰلِحَٰتِ مِنْهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا

Hizi  ndizo Aya nne  ambazo  zimetaja Jila  Mohamad ﷺ katika Kuruani  yote.

Sasa  Tuelekeze Darubini  Yetu  katika Namba Za  Aya na Sura tuone Muujiza wa Kiajabu  usio na Mwisho. Allahu Akbar.

Kufuatana na Mpangilio wa Sura Za  Msahafu (Yaani Mpangilio  wa Sura za Msahafu ni  tofauti na Mpangilio wa Kushushwa kwa Kuruani) Kama Misahafu tuliyonayo leo hii. Haikupangwa bure bure bali Muujiza.

Kufuatana na Mpangilo wa Sura katika Msahafu Mara ya Kwanza Kutajwa kwa Jina La  Mtume ﷺ ni Katika, 

SURA YA AL_IMRAN NAMBA 3 AYA NAMBA 144 

na mara ya Mwisho  kutajwa Jina La Mtume Mohamad ﷺ ni  katika,

SURA YA AL-FATH NAMBA 48 AYA NAMBA 29

Angalia Vizuri  Namba  za Aya.

Aya namba 144  na Aya namba  29

Kumbuka vizuri namba hizi mbili.

Sasa ukihesabu Aya zote  kuanzia Aya namba 144 mpaka Aya Namba  29  utapata Jumla ya Aya ni  4176

yaani  Elfu Nne Mia Moja na Sabini  na Sita.

Je unajua Kwamba Namba hii kihesabu ni sawa na 

144  mara  29

yaani  144 X 29=4176

Ebwe,  Hebu angalia  Maajabu haya.

Namba 4176  ni sawa na 144 x 29  sasa mbona tunapata Namba ya  Aya  ya kwanza kutajwa kwa Mtume ni  144? 

na Aya Namba 29 ni  mara ya mwisho kutajwa kwa Mtume?

Unaona Maajabu.

Unaona Muujiza.

Mjomba Usibabaike. Fumbua Macho. Hii ndiyo Kuruani Tukufu. 

Muujiza unaopita miujiza yote.

Tumehesabu  Idadi ya Aya kisha tumepata namba 144 na 29  ambazo ni namba ya Aya ya kwanza kutajika kwa mtume na pia Aya ya Mwisho.

Je onaona Ukubwa wa Mwenyeezi Mungu Alivyo?

Nani anayeweza kuandika Kitabu na kafanya hivi?

Ndugu zanguni ni nani Mfalme?

Ni Nani Mfalme?

Jawabu ni moja tu.  Ni Muumba

“Lilahi  Alwahid AlQahar”

Ni Yule Yule Mkubwa Mwenye Nguvu aliyeumba kila kitu.

Allahu Akbar. Allahu Akbar.

Kabla Ya kuendelea na Miujiza   ningependelea  Kukuletea Msemo wa Mshairi wa Kifarsi  (Persian) Maarufu Jalal ad-Din Muhammad Rumi Alizaliwa Mwaka 1207   (CE) yaani miaka ya kikristo.

Mshairi  Huyu  alisema  kwamba

“Lazima Uendelee  Kuuvunja Moyo wako mpaka  Ufunguke”

Katika Usemi huu ana maana kwamba Moyo huwa imefungika na kwa hiyo ufanye juhudi kuufungua kwa juhudi zako zote. Yaani Uufungue kwa kusoma kila cha faida katika maisha yako. Usijifungie na fikra zako mbaya bali uufungue moyo wako katika kila la kheri na faida.

Aliulizwa pia Suala lifuatalo

“Je Unapata Faida Gani katika  Sala?”

Akajibu “Sipati Faida Yeyote bali Nimepoteza”.

“Nimepoteza Majivuno”

“Nimpoteza  Hasira”

“Nimepoteza Maradji ya nafsi”

“Nimepoteza Ulafi”

“Nimepoteza  Hamu ya Udanganyifu”

“Nimepoteza Hamu ya Kufanya Maasi”

“Nimepoteza Kukata Tamaa”

Haya ndiyo majibu ya Bwana Rumi.  Alikuwa Philosopher na Mshairi mkubwa katika wakati wake na alikuwa mashuhuri sana. Mwenyeezi Mungu ambariki.

Baada ya Kujiburudisha na Mashairi  ya Bwana Rumi Sasa  tuendelee na Miujiza Yetu.

MUUJIZA WA TATU (SURA YA  AL-IKHLAS)

Nimekwisha Kuzungumzia Miujiza mbalimbali ya Sura Hii katika Milango  mingineyo ya Website hii. 

Kama nilivyosema  Kuruani ina miujiza isiyo na mwisho. Kwa hiyo leo nitaelezea Nyongeza  ya Muujiza kutoka katika Sura Ya A-lIkhlas.

Sasa  Tuelekeze Darubini yetu katika Sura Hii  tuone Maajabu yasiyo  na Mwisho.

Sura Ya Al-Ikhlas Namba 112  Aya  4

قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ/ اللَّهُ الصَّمَدُ/ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ/ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ

Kwanza Tuelewe kwamba Katika Lugha ya Kiarabu Hapo zamani kulikuwa na Herufi ambazo zilijulikana kama ABJAD na baadaye Herufi  zikageuzwa na kuitwa HIJAI

herufi za  ABJAD  zimepangika kama ifuatavyo

Alif

Ba

Jim

Daj

….  Na zote Nyinginezo Mpaka mwisho yaani Hamzah

Na Herufi Za Hijai za kisasa ni kama ifuatavyo:

Alif

Baa

Taa

Thaa

………Na zote Nyinginezo Mpaka mwisho yaani Hamzah.

kwa hiyo mipangilio ya  aina ya herufi hizi mbili inatofautiana.

Muujiza wa leo tutafanya  utafiti kwa kutumia Herufi za hapo zamani yaani Herufi za ABJAD

Ukizipanga herufi hizi kwa kutumia Namba kama ifuatavyo

Alif  Ni Namba 1

Ba  Ni Namba 2

Jim ni Namba 3

Dal ni Namba 4

Ufanye hivyo mpaka mwisho wa herufi zote.

Sasa  tuanze Utafiti wetu. Tuje na Darubini na tuanze uchunguzi katika Aya hizi 4 za Sura hii ya Al-Ikhlas.

قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ/ اللَّهُ الصَّمَدُ/ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ/ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ

Ukichunguza Aya hizi nne utaona Kuna Alama Ya Haraka moja tu ya Kisrah nayo ipo  chini ya Herufi Ya LAMU nayo imegawanya Aya hii katika Herufi  23 kwa upande wa kushoto na  23 kwa upande wa Kulia.

Ngoja nigawe Upate kuona kwa macho:

قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ/ اللَّهُ الصَّمَدُ/ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ/ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ

Herufi ya Lamu yenye Kasrah chijni yake ipo katika Neno يَلِدْ  “YALID”

Sasa  tukigeuza Herufi  23 za upande wa kushoto katika Namba kwa kufuata sehemu (Positions)  za Herufi   za ABJAD  tulizozitaja hapa juu na kuzijumlisha utapata Jumla ya  herufi  hizi 23 ni =  198

Ajabu Ni Kwamba Ukifanya hivyo hivyo na Herufi 23 za Upande wa Kushoto utapata Jumla ya Herufi hizo  23 ni   198 Pia

Sasa  tuelekeze Darubini kuanzia Sura Hii namba 112 mpaka mwisho yaani katika Sura Ya Al-Nas.

Angalia Muujiza. Ukihesabu Aya zote kuanzia Mwanzo wa Sura Ya Al-Ikhlas mpaka Mwisho wa Msahafu yaani katika Sura ya Al-Nas basi Jumla Ya Aya zote ni 198  Pia!!!!!

Angalia  Mpangilio  wa Kushangaza. Je unaona Maajabu yasiyo na Mwisho.

Namba 198 Ilivyokariri  mara 3  mfululizo. Ndugu Yangu, Mjomba wangu huoni Muujiza  huu?   Kwa nini imepangika hivi?

Jawabu  ni  “HII NDIYO KURUANI TUKUFU ILIVYO”

Hakuna Mfano wowote wa kitabu chochote ulimwenguni kama hiki. Je unaona?

Allahu Akbar.  Allahu Akbar.  Kwa kweli Nimeivulia Kofia. Hata  Super Computer  haiwezi kufua Dafu.