SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Darubini-6/Kuruani

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

01/10/2022

Nashukuru Mwenyeezi Mungu kwa kunipa Uzima na Kuendelea na Miujiza Mipya. Siku  ya leo nimeweka nia kuandika Mlango huu ambao utakusanya Miujiza Mbalimbali. Kwa hiyo  Kwa siku la leo hautaona Miujiza yote lakini Mwenyeezi Mungu akipenda baadhi yake itakamilika Usiku au kesho.  Usishangae unaposoma kwani otaona maudhui na sherehe zinabadilika badilika kwani bado upo katika maandalizi.

Miujiza Hii imenipa faida na nimeona tugawane faida hizi baina yangu na nyinyi wasomaji.

1/MUUJIZA KATIKA SURA YA AL-KAHF

Moja kwa moja Nitaanza na Maajabu Katika Sura Ya Al-Kahf Namba 18.  Nimekwisha Elezea Miujiza Mbalimbali Ya Sura Hii Katika Sehemu mbalimbali za Website hii na Leo kuna Nyongeza.  Kwa kweli Miujiza ya Kuruani haina Mwisho.

Sasa Nitapeleka  Darubini katika  Sura Hii ya Al-Kahf namba 18 Kuanzia  Aya Namba  9  Mpaka 26

Kwanza Nitazinukulu  Aya Hizo  kisha Tupeleke Darubini yetu katika Aya Mbili inayotuhusu. Aya Namba  22  na 25

(Aya hizi Mbili nimebadili Rangi)

سُوۡرَةُ الکهف

أَمۡ حَسِبۡتَ أَنَّ أَصۡحَـٰبَ ٱلۡكَهۡفِ وَٱلرَّقِيمِ كَانُواْ مِنۡ ءَايَـٰتِنَا عَجَبًا (٩)

إِذۡ أَوَى ٱلۡفِتۡيَةُ إِلَى ٱلۡكَهۡفِ فَقَالُواْ رَبَّنَآ ءَاتِنَا مِن لَّدُنكَ رَحۡمَةً۬ وَهَيِّئۡ لَنَا مِنۡ أَمۡرِنَا رَشَدً۬ا (١٠)

فَضَرَبۡنَا عَلَىٰٓ ءَاذَانِهِمۡ فِى ٱلۡكَهۡفِ سِنِينَ عَدَدً۬ا (١١)

ثُمَّ بَعَثۡنَـٰهُمۡ لِنَعۡلَمَ أَىُّ ٱلۡحِزۡبَيۡنِ أَحۡصَىٰ لِمَا لَبِثُوٓاْ أَمَدً۬ا (١٢)

نَّحۡنُ نَقُصُّ عَلَيۡكَ نَبَأَهُم بِٱلۡحَقِّ‌ۚ إِنَّہُمۡ فِتۡيَةٌ ءَامَنُواْ بِرَبِّهِمۡ وَزِدۡنَـٰهُمۡ هُدً۬ى (١٣)

وَرَبَطۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ إِذۡ قَامُواْ فَقَالُواْ رَبُّنَا رَبُّ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ لَن نَّدۡعُوَاْ مِن دُونِهِۦۤ إِلَـٰهً۬ا‌ۖ لَّقَدۡ قُلۡنَآ إِذً۬ا شَطَطًا (١٤)

هَـٰٓؤُلَآءِ قَوۡمُنَا ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦۤ ءَالِهَةً۬‌ۖ لَّوۡلَا يَأۡتُونَ عَلَيۡهِم بِسُلۡطَـٰنِۭ بَيِّنٍ۬‌ۖ فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبً۬ا (١٥)

وَإِذِ ٱعۡتَزَلۡتُمُوهُمۡ وَمَا يَعۡبُدُونَ إِلَّا ٱللَّهَ فَأۡوُ ۥۤاْ إِلَى ٱلۡكَهۡفِ يَنشُرۡ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّن رَّحۡمَتِهِۦ وَيُهَيِّئۡ لَكُم مِّنۡ أَمۡرِكُم مِّرۡفَقً۬ا (١٦)

۞ وَتَرَى ٱلشَّمۡسَ إِذَا طَلَعَت تَّزَٲوَرُ عَن كَهۡفِهِمۡ ذَاتَ ٱلۡيَمِينِ وَإِذَا غَرَبَت تَّقۡرِضُہُمۡ ذَاتَ ٱلشِّمَالِ وَهُمۡ فِى فَجۡوَةٍ۬ مِّنۡهُ‌ۚ ذَٲلِكَ مِنۡ ءَايَـٰتِ ٱللَّهِ‌ۗ مَن يَہۡدِ ٱللَّهُ فَهُوَ ٱلۡمُهۡتَدِ‌ۖ وَمَن يُضۡلِلۡ فَلَن تَجِدَ لَهُ ۥ وَلِيًّ۬ا مُّرۡشِدً۬ا (١٧)

وَتَحۡسَبُہُمۡ أَيۡقَاظً۬ا وَهُمۡ رُقُودٌ۬‌ۚ وَنُقَلِّبُهُمۡ ذَاتَ ٱلۡيَمِينِ وَذَاتَ ٱلشِّمَالِ‌ۖ وَكَلۡبُهُم بَـٰسِطٌ۬ ذِرَاعَيۡهِ بِٱلۡوَصِيدِ‌ۚ لَوِ ٱطَّلَعۡتَ عَلَيۡہِمۡ لَوَلَّيۡتَ مِنۡهُمۡ فِرَارً۬ا وَلَمُلِئۡتَ مِنۡہُمۡ رُعۡبً۬ا (١٨)

وَڪَذَٲلِكَ بَعَثۡنَـٰهُمۡ لِيَتَسَآءَلُواْ بَيۡنَہُمۡ‌ۚ قَالَ قَآٮِٕلٌ۬ مِّنۡہُمۡ ڪَمۡ لَبِثۡتُمۡ‌ۖ قَالُواْ لَبِثۡنَا يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٍ۬‌ۚ قَالُواْ رَبُّكُمۡ أَعۡلَمُ بِمَا لَبِثۡتُمۡ فَٱبۡعَثُوٓاْ أَحَدَڪُم بِوَرِقِكُمۡ هَـٰذِهِۦۤ إِلَى ٱلۡمَدِينَةِ فَلۡيَنظُرۡ أَيُّہَآ أَزۡكَىٰ طَعَامً۬ا فَلۡيَأۡتِڪُم بِرِزۡقٍ۬ مِّنۡهُ وَلۡيَتَلَطَّفۡ وَلَا يُشۡعِرَنَّ بِڪُمۡ أَحَدًا (١٩)

إِنَّہُمۡ إِن يَظۡهَرُواْ عَلَيۡكُمۡ يَرۡجُمُوكُمۡ أَوۡ يُعِيدُوڪُمۡ فِى مِلَّتِهِمۡ وَلَن تُفۡلِحُوٓاْ إِذًا أَبَدً۬ا (٢٠)

وَڪَذَٲلِكَ أَعۡثَرۡنَا عَلَيۡہِمۡ لِيَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقٌّ۬ وَأَنَّ ٱلسَّاعَةَ لَا رَيۡبَ فِيهَآ إِذۡ يَتَنَـٰزَعُونَ بَيۡنَہُمۡ أَمۡرَهُمۡ‌ۖ فَقَالُواْ ٱبۡنُواْ عَلَيۡہِم بُنۡيَـٰنً۬ا‌ۖ رَّبُّهُمۡ أَعۡلَمُ بِهِمۡ‌ۚ قَالَ ٱلَّذِينَ غَلَبُواْ عَلَىٰٓ أَمۡرِهِمۡ لَنَتَّخِذَنَّ عَلَيۡہِم مَّسۡجِدً۬ا (٢١)

سَيَقُولُونَ ثَلَـٰثَةٌ۬ رَّابِعُهُمۡ كَلۡبُهُمۡ وَيَقُولُونَ خَمۡسَةٌ۬ سَادِسُہُمۡ كَلۡبُہُمۡ رَجۡمَۢا بِٱلۡغَيۡبِ‌ۖ وَيَقُولُونَ سَبۡعَةٌ۬ وَثَامِنُہُمۡ ڪَلۡبُہُمۡ‌ۚ قُل رَّبِّىٓ أَعۡلَمُ بِعِدَّتِہِم مَّا يَعۡلَمُهُمۡ إِلَّا قَلِيلٌ۬‌ۗ فَلَا تُمَارِ فِيہِمۡ إِلَّا مِرَآءً۬ ظَـٰهِرً۬ا وَلَاتَسۡتَفۡتِ فِيهِم مِّنۡهُمۡ أَحَدً۬ا (٢٢)

وَلَا تَقُولَنَّ لِشَاْىۡءٍ إِنِّى فَاعِلٌ۬ ذَٲلِكَ غَدًا (٢٣)

إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ‌ۚ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ إِذَا نَسِيتَ وَقُلۡ عَسَىٰٓ أَن يَهۡدِيَنِ رَبِّى لِأَقۡرَبَ مِنۡ هَـٰذَا رَشَدً۬ا (٢٤)

وَلَبِثُواْ فِى كَهۡفِهِمۡ ثَلَـٰثَ مِاْئَةٍ۬ سِنِينَ وَٱزۡدَادُواْ تِسۡعً۬ا (٢٥)

قُلِ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا لَبِثُواْ‌ۖ لَهُ ۥ غَيۡبُ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ‌ۖ أَبۡصِرۡ بِهِۦ وَأَسۡمِعۡ‌ۚ مَا لَهُم مِّن دُونِهِۦ مِن وَلِىٍّ۬ وَلَا يُشۡرِكُ فِى حُكۡمِهِۦۤ أَحَدً۬ا (٢٦)

TAFSIRI

Aya Namba 22 na 25.

22. (Wengine) wanasema: “Walikuwa watu watatu wa nne wao ni mbwa wao., Na (wengine) wanasema, “Walikuwa watano, wa sita wao ni mbwa wao.” (Wanasema) kwa kuvurumiza (tu) kwa wasioyajuwa. Na (wengine) wanasema, “Walikuwa saba, na wa nane wao ni mbwa wao.” Sema: “Mola wangu ndiye ajuaye sawasawa hisabu yao., Hakuna anayewajua (hakika yao) isipokuwa wachache tu. Basi usibishane (usishindane) juu yao ila kwa mabishano ya juu juu tu hivi (kwani hapana faida juu ya mabishano ya kuwa walikuwa wangapi). Wala usiulize khabari zao kwa yoyote yule. (M wenyezi Mungu ameshakutajia. Basi hivi alivyokutajia ndio ndivyo).

25.Na walikaa katika pango yao myaka mia tatu, na wakazidisha (myaka) tisa. 

SHEREHE

Aya hizi  zinahusu wachamungu  ambao walikuwa wakimbizi wa Siasa ya Ukafiri katika Enzi  Hizo. Kulikuwa na Mfalme Kafiri Katika Mamlaka hiyo na Watu hawa  Wakaondoka mji huo  kwa Siri na kukimbilia katika Pango. Ni Wachamungu walikuwa na Imani Kubwa sana Kama Mwenyeezi Mungu alivyowasifu katika  Aya Hizi. Na Muujiza Mkubwa ukazuka. Mwenyeezi Mungu akawalaza usingizi  mkali  kwa muda wa miaka  309. Angalia Muujizahuu ambao siyo Mdogo. Miujiza mingine katika Sura Hii inathibitisha kwamba Kisa hikini cha ukweli. Kama nilivyoelezea katika Sehemu ntyinginezo za Website hii.

Kwanza Maneno Ya Kisa Hiki ni   309  Pia kama Miaka waliyolazwa.!!!!!

Pili Ukihesabu Kurasa za Msahafu kuanzia Pale palipotajwa miaka  309  mpaka mwisho wa Msahafu utapata Jumla ya Kurasa ni 309  Pia.  Angalia Maajabu!!!!!.

Kisa hiki  kimetajika Kwa Jumla ya  Aya 18  na Sura Hii  ambayo  imetiwa Jina Hili la Al-Kahf ni ya 18  Pia. Je unaona Maajabu?!!!!! 

Alhamdulilah  Leo Nitapeleka Darubini katika Aya Mbili tu  za Aya zilizopo hapa juu ili tuone Muujiza Mwingine wa Kushangaza. Yaani Miujiza ya kuruani Haina Mwisho.  Allahu Akbar.

Ngojea nizinukulu  zile Aya Mbili Nilizobadili rangi hapa Juu ili tuone  Vizuri:

سَيَقُولُونَ ثَلَـٰثَةٌ۬ رَّابِعُهُمۡ كَلۡبُهُمۡ وَيَقُولُونَ خَمۡسَةٌ۬ سَادِسُہُمۡ كَلۡبُہُمۡ رَجۡمَۢا بِٱلۡغَيۡبِ‌ۖ وَيَقُولُونَ سَبۡعَةٌ۬ وَثَامِنُہُمۡ ڪَلۡبُہُمۡ‌ۚ قُل رَّبِّىٓ أَعۡلَمُ بِعِدَّتِہِم مَّا يَعۡلَمُهُمۡ إِلَّا قَلِيلٌ۬‌ۗ فَلَا تُمَارِ فِيہِمۡ إِلَّا مِرَآءً۬ ظَـٰهِرً۬ا وَلَاتَسۡتَفۡتِ فِيهِم مِّنۡهُمۡ أَحَدً۬ا (٢٢)

 وَلَبِثُواْ فِى كَهۡفِهِمۡ ثَلَـٰثَ مِاْئَةٍ۬ سِنِينَ وَٱزۡدَادُواْ تِسۡعً۬ا (٢٥)

TAFSIRI

22. (Wengine) wanasema: “Walikuwa watu watatu wa nne wao ni mbwa wao., Na (wengine) wanasema, “Walikuwa watano, wa sita wao ni mbwa wao.” (Wanasema) kwa kuvurumiza (tu) kwa wasioyajuwa. Na (wengine) wanasema, “Walikuwa saba, na wa nane wao ni mbwa wao.” Sema: “Mola wangu ndiye ajuaye sawasawa hisabu yao., Hakuna anayewajua (hakika yao) isipokuwa wachache tu. Basi usibishane (usishindane) juu yao ila kwa mabishano ya juu juu tu hivi (kwani hapana faida juu ya mabishano ya kuwa walikuwa wangapi). Wala usiulize khabari zao kwa yoyote yule. (M wenyezi Mungu ameshakutajia. Basi hivi alivyokutajia ndio ndivyo).

25. Na walikaa katika pango yao miaka mia tatu, na wakazidisha (myaka) tisa.

NAMBA ZA KUSHANGAZA

Muujiza ni kwamba  Namba  zilizotajika katika Aya hizi  ukizipanga  vizuri unapata Jina la Mwenyeezi Mungu  Allah Akbar. 

Usibabiske kwani Nitaambatanisha Video hapa Chini ieleweke na uone ya Maajabu.

Namba hizi ni Idadi ya Hao  wachamungu na Mbwa wao. KIsa kiantuelezea kwamba Watu wanabuni buni  idadi yao  Na Mwenyeezi Mungu anatusimulia  habari za mazungumzo  hayo.

Namba  Hizi kama nilizozitia Rangi katika Aya hizi  ni

3, 4, 5, 6,7.8,3, na 9

Sasa  Nitaambatanisha Video Namba 1 hapa chini uzione kwa macho yako kwa vizuri. Tafadhali Angalia Namba Hizi  unapozipanga  na Kuziunga  unapata Jina La Mola. Kwa kweli Inashangaza. Ukiangalia VIzuri Utafahamu.  KIla Namba Nimetia DOA  Kwa mfano  Namba 3  Nimetia Doa

. . .

Namba  4

. . . .

Namba  5 

. . . . .

Kwa kiarabu Maandishi yanakuwa kuanzia   Kulia na kwenda kushoto. Kwa  kiingereza  ni Kinyume Maandishi yanakuwa  Kushoto  kwenda Kulia  na hivyo hivyo Lugha ya Kiswahili. Kwa hiyo Namba pia za Kiarabu Pia zitakuwa Kuanzia Kulia na Kwenda Kushoto.

Kwa Mfano  Namba  15  Kwa kiarabu  Namba  1  itakuwa Kulia na Namba 5 itakuwa kushoto yaani kinyume na Kiswahili. Kwa hiyo  Madoa Haya Yatakuwa kwa Kufuata nidhamu  ya lugha ya Kiarabu Kama ilivyo Kuruani ilivyo yaani Siyo Tafsiri ya Lugha Nyingine bali  Kwa Kiarabu. 
Sasa Naishia Hapa. Angalia Video  Hapa Chini.  Ni Fupi sana karibu  Dakika 5.  

Ukiangalia  Utafahamu Vizuri  habari hii.  Kwa Kweli Kuruani  ina maajabu yasiyo na mwisho. Allahu Akbar.

Video-1

MAAJABU YA KURUANI HAYANA MWISHO. NAMBA TULIZOZIONA KATIKA AYA MBILI YA 22 NA 25 KATIKA SURA YA AL-KAHF ZINASHANGAZA SANA. TUKIZIGEUZA KATIKA MADOA NA KISHA KUZIPANGA NA KUZIUNGA PAMOJA TUNAPATA JINA LA MWENYEEZI MUNGU “ALLAH” KWA KWELI MUUJIZA SOYO MDOGO HATA KIDOGO.

2/MUUJIZA WA MZUNGUKO  WA MWEZI NA JUA  (LUNAR MOON CYCLE) NA AYA ZA KURUANI  TUKUFU

Alhamdulilah  Nilizungumzia Kuhusu  Metonic  Cycle katika  Mlango  wa  “BLOGS ZA KURUANI”  wa  website hii nikaelezea  kwa picha  kwamba Metonic Cycle ni Uhusiano unaosababishwa na Mwezi Na Jua. Harakati za Mwezi katika kuizunguka Ardhi na wakati huo huo Mwezi na Ardhi kuzunguka Jua. Kila baada ya Miaka 19 Mwezi Na Jua zinakutana na kukaribiana tena katika Positions au sehemu zake za asili.

Kuruani imetaja majina mawili katika Aya 19 na Kila Aya inaambatanisha Jua na Mwezi.

الشَّمْسَ وَ الْقَمَرَ

“Jua na Mwezi”

Nimeorodhesha katika Mlango  huo Aya zote 19 ambazo kila Aya inatumia ibara hii.

الشَّمْسَ وَ الْقَمَرَ

yaani “Jua na Mwezi”.

Ukifikiri utaona Maneno  Haya Hayakupangika bure bure bali kimiujiza. Hizi ni Aya Pekee katika Kuruani yote. Huu Sio Muujiza Mdogo. 

Alhamdulilah  Leo  Mwenyeezi Mungu akipenda Nitaelezea  Muujiza Mwingine  wa Kila Miaka   33 na pia Kila Miaka 11.

Kuhusu  Miaka Tunasoma katika Elimu ya Astronomy kwamba Mwezi Unazunguka Ardhi kwa siku 354  na  Ardhi linazunguka Jua kwa siku  365  kwa hiyo tofauti ni siku  11. Calendar ya Mwezi Kuzunguka Jua  inajulikana kama Lunar Calendar  na Calendar ya Ardhi Kuzunguka Jua inajulikana kama Solar Calendar.

Calendar  zote mbili ni zake  Mwenyeezi Mungu Mtukufu. Kwa hiyo  Baina Ya Calendar hizi Mbili kuna Tofauti ya Siku 11. 

Ukijumlisha Tofauti  hii ya siku 11. Katika Kila Miaka  33 inatimia Siku  363 (11 x 33=363) Na siku hizi  363 ni karibu  Mwaka. Yaani  Baada ya Miaka  33  Jua, Mwezi na Kila kitu kitarudi katika Sehemu (Position)  zake ya Asili.

Na Tarehe  zitajirakibisha na Kuanza tena. Yaani  Tuaanza kuhesabu  tofauti ya siku 11 na baada ya Mwaka ufuatao itakuwa 22 na baada ya Mwaka Ufuatao itakuwa 33  na hivyo hivyo mpaka  Utakuwa mwaka tena na baada ya hapo kila kitu kitakuwa  mahala pake pa  asili na Hesabu Itaanza upya.

Ni sawa na Saa ya Mkono. Inaanza na 1  mpaka  12 na baada ya hapo inaanza 1 tena. Inazunguka hivyo  1  mpaka  12  na tena 1 mpaka 12.  Nadhani imeeleweka. Na kwa hivyo  Jua na Mwezi na kila kitu  baada ya Muda huo wa miaka 33 kila  Tofauti  ya Masiku hujirekibisha na Kuanza tena Upya.  Na Mwenyeezi Mungu anaelewa vizuri zaidi ikiwa sivyo.  Allahu  Aliym.

Na Kuhusu  Smaku (Magnetic) ya Jua Pia inalizunguka Jua na hii Inajulikana kama “Solar Cycle”  Yaani kila baada ya Miaka  11   Kunakuwa na mzunguko wa Smaku na Mzunguko huo unasababisha  North Pole na South Pole ya Jua  Kubadilika.  North inakuwa South na South inakuwa Pole.  

(The Sun’s magnetic field goes through a cycle, called the solar cycle. Every 11 years or so, the Sun’s magnetic field completely flips. This means that the Sun’s north and south poles switch places. Then it takes about another 11 years for the Sun’s north and south poles to flip back again).

Kwa kifupi:

1/Miaka  33  Ni Miaka ya Jua Na Ardhi Kujirekibisha Tofauti zake za Masiku

2/Masiku 11  ni Tofauti Ya Calendar ya Lunar (Calendar Ya Kiislamu)  Na Solar (Calendar za Gregorian au za Kisasa)

3/Miaka  11  ni Mzunguko  wa Smaku  juu ya Jua na Kubadilika Kwa South na North Pole.  au  Kwa kiingereza. “Flip”

Sasa  umefika wakati wa Kupeleka Darubini  yetu katika Kuruani  Tukufu Tuone Maajabu Yasiyo  Na Mwisho na Pia Maajabu Makubwa.  Allahu Akbar.

Sasa  Umefika wakati wa Kupeleka Darubini  yetu katika Aya  Ya Kuruani tuone  hizi namba tulizotaja hapa juu.  Yaani namba  33, na 11

Aya  Ifuatayo  Moja tu Itatupa namba hizi mbili. Sasa  tujiulize Swali Kwa vipi?  

Jawabu  linafuata hebu tufanye  Utafiti.  Tizama vizuri linalofuata.  Alhamdulilah. Allahu Akbar.  Fumbua macho katika Aya ifuatayo  Sura Ya Al-Ambiyaa  Namba 21 Aya namba 33

وَهُوَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّہَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ‌ۖ كُلٌّ۬ فِى فَلَكٍ۬ يَسۡبَحُونَ (٣٣)

TAFSIRI

33.Na yeye ndiye aliyeumba usiku na mchana . na jua na mwezi; vyote vinaogelea katika duara (zao).

SHEREHE  YA MAAJABU  YA KURUANI

Kila Mtu  ataona namba  33  ni namba ya Aya  kwa hiyo  mtasema naam  ni Namba ya Aya.  Kwa kweli mmepata.  Ni Namba Ya Aya na Jawabu ni sahihi lakini kuna Namba 33  iliyofichika  Hebu  tuitafute.

Ukiangalia vizuri utaiona na pia Namba  11 imefichika.

Tuichunguze Aya tena kwa pamoja:

وَهُوَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّہَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ‌ۖ كُلٌّ۬ فِى فَلَكٍ۬ يَسۡبَحُونَ (٣٣)

Angalia  Vipande Nilivyotia Rangi

Kipande Chekundu cha Aya kinasema:

“Yeye Ndiye aliyeumba Mchana na Usiku na Jua Na Mwezi”

Ndugu  Msomaji Jumla ya  Herufi  za Kipande hiki  ni 33  pia!!!!!!   na ndicho  kinachotuhusu kwani Kinazungumzia  Jua na Mwezi Na kama tulivyoona Kwamba Jua na Mwezi zinazunguka  kwa muda wa miaka  33  na baada ya hapo  Tarehe inajisawazisha.  Allahu Akbar.  Allahu Akbar.  Angalia Maajabu.  Mara ya kwanza tumepata  Namba Ya Aya na Sasa Tumepata Jumla ya Herufi  ni 33.  Je huoni Maajabu?  Huoni  Kukariri  kariri  huku siyo  Bure bure tu.

Sasa  Tuchunguze namba 11  Katika Aya Hii. Ngojea Niinukulu tena hapa chini.

وَهُوَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّہَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ‌ۖ كُلٌّ۬ فِى فَلَكٍ۬ يَسۡبَحُونَ (٣٣)

Hebu tusogeze darubini  tena  katika Aya hii.

Je unaione namba 11?

Ngojea  Niinukulu  tena Aya Hii:

وَهُوَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَ ٱلنَّہَارَ وَ ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ‌ۖ كُلٌّ۬ فِى فَلَكٍ۬ يَسۡبَحُونَ (٣٣)

Tumesema  Kuzunguka kwa Smaku ya Jua katika Jua  Inachukua Miaka  11  na Pia  Tofauti ya  Siku 11  ni  Mzunguko  wa  Mwezi katika Ardhi  na  Ardhi  katika Jua.

Kwa hiyo  Angalia  kipande  cha aya  katika  Aya Hii 

ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ‌ۖ

Maneno  Haya Mawili  yana maana ya  Jua Na Mwezi. Na Jumla Ya  herufi zake ni  11  pia!!!!!

Kwa kweli Inashangaza sana.  Allahu Akbar.  Angalia  Ukubwa wa Kuruani  Ulivyo. Kwa kweli Inatisha  na siyo Uwongo. Kuruani  imejaa Ulimwengu au Malimwengu  wote. Unajionea  kwa Macho yako Mwenyewe Maajabu Yasiyo na Mwisho. Allahu Akbar. 

Na Mwenyeezi Mungu anajua zaidi ikiwa siyo hivyo. Lakini sisi  binadamu tunashangaa sana na Maajabu Haya. Je unaonaje?  Namuomba Mola  Anisamehe iwapo sivyo. Kitu muhimu  Tumefanya Jitihada kuinua Jina lake.  Allahu Akbar.

Inaendelea  kwani kuna Miujiza Mingine  katika Mlango huu. Ukirudi  tena utaikuta Mwenyeezi Mungu akipenda.

02/10/2022

Alhamdulilah Mwenyeezi Mungu Akipenda Siku ya Leo Nitaanza na Kuendelea Kuelezea Miujiza Mingineyo katika  Mlango huu.

3/MUUJIZA WA HERUFI  ZA MAAJABU KATIKA KURUANI (Muqaṭṭaʿāt, Arabic: حُرُوف مُقَطَّعَات ḥurūf muqaṭṭaʿāt, “disjoined letters” or “disconnected letters)

Herufi Tutakazozichunguza ni Tatu.  Nun, Qaf na Swad. Na Tutakapoziunga Pamoja Tutapata Neno  نَقُصُّ  “NAQUSU”  lenye maana ya “Tunakuhadithia” au “Tunakusimulia”  Tuanze Utafiti katika Kuruani wa neno  Hili نَقُصُّ  “NAQUSU”  na kisha Tuangalie Sura Ambazo zimetumia Mwanzoni mwake Herufi hizi Tatu. Kwanza Ningependelea kuelezea Herufi hizi  kwamba  Herufi  za Muqataa  zimetumika mwanzoni mwa Sura 29 kati ya Sura 114 za Kuruani  Tukufu. Jumla ya Herufi ni  79  lakini tukiondoa zilizokariri zinabaki  14  tu. Ni Herufi ambazo ni Muujiza Mkubwa Hakuna ajuaye isipokuwa Mwenyeezi Mungu Tu peke yake. Lakini  kuna Miujiza ambayo imepatika hivi karibuni kutokana na matumizi ya Herufi hizi.  Katika Sehemu Hii tutachunguza Herufi  Tatu  ambazo zimetumika Mwanzoni mwa Sura Tatu kati ya hizo Sura 29.  

Sasa  Tuzitaje zile Sura Zilizotumia neno  نَقُصُّ au “NAQUSU”

Sura Namba 7 Al-Arraf Aya Namba 101

تِلْكَ الْقُرَى نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنْبَائِهَا وَ لَقَدْ جَاءَتْهُمْ رُسُلُهُمْ بِالْبَيِّنَاتِ فَمَا كَانُوا لِيُؤْمِنُوا بِمَا كَذَّبُوا مِنْ قَبْلُ كَذَلِكَ يَطْبَعُ اللَّهُ عَلَى قُلُوبِ الْكَافِرِينَ

Sura Namba 11 Hud Aya Namba 120

وَ كُلًّا نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنْبَاءِ الرُّسُلِ مَا نُثَبِّتُ بِهِ فُؤَادَكَ وَ جَاءَكَ فِي هَذِهِ الْحَقُّ وَ مَوْعِظَةٌ وَ ذِكْرَى لِلْمُؤْمِنِينَ

Sura Namba 12 Yusuf Aya Namba 12

نَحْنُ نَقُصُّ عَلَيْكَ أَحْسَنَ الْقَصَصِ بِمَا أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ هَذَا الْقُرْآنَ وَ إِنْ كُنْتَ مِنْ قَبْلِهِ لَمِنَ الْغَافِلِينَ

Sura Namba 18 Al-Kahf Aya Namba 13

نَحْنُ نَقُصُّ عَلَيْكَ نَبَأَهُمْ بِالْحَقِّ إِنَّهُمْ فِتْيَةٌ آمَنُوا بِرَبِّهِمْ وَ زِدْنَاهُمْ هُدًى

Sura Namba 20 Twaha Aya Namba 99

كَذَلِكَ نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنْبَاءِ مَا قَدْ سَبَقَ وَ قَدْ آتَيْنَاكَ مِنْ لَدُنَّا ذِكْرًا

Neno نَقُصُّ Lina maana ya “Kuhadithia” au “Kukuelezea Kisa” Neno hili نَقُصُّ kwa matamshi ni “NAQUSU” Katika Kuruani Neno Hili limetumika katika Aya Nilizonukulu hapa juu yaani Hizi tu na hakuna Nyingineo. Yaani neno hili limetumika mara 5 Tu katika Kuruani Tukufu.

Mara Ya Kwanza Kutumika ni katika Sura Namba 7 Al-Arraf Aya Namba 101 katika Msahafu ni Kurasa namba 163  

Na Mara Ya Mwisho Kutajika ni katika Sura Namba 20 Twaha Aya Namba 99 katika Msahafu ni Kurasa namba 319

Neno Hili نَقُصُّ limetumia herufi Tatu NUN, QAF na SWAD na ambazo   ni katika Herufi za Maajabu.

Kuna Sura Tatu Katika Kuruani Ambazo zimenziwa na Herufi hizi Tatu nazo ni Sura ZIfuatazo:

Sura Ya Qalam Namba 68 Imeanziwa na Herufi ya Nun Sura Ya QAF Namba 50 Imenziwa na Herufi QAF        Sura Ya Swad Namba 38 Imeanziwa na Herufi SWAD

Sasa Ttuendelee na  Utafiti. Hebu tupeleke Darubini katika Kuruani.

Tuhesabu Namba za Sura Hizi Tatu 68 + 50 + 38=156

Tumepata 156 Hebu Tuchunguze Zile Kurasa Tulizozipata hapo juu 319 na 163

Hebu tutoe namba 163  (Namba Ya Ukurasa wa mara ya Mwanzo kutumika neno نَقُصُّ) kutoka katika Namba 319 (Mara ya Mwisho kutumika neno نَقُصُّ) 

(319-163=156)

Kwa kweli inashangaza hebu angalia Maajabu yasiyo na Mwisho.

ukijumlisha Namba za Sura Tatu (Qalam Iliyoanziwa na herufi NUN + Qaf + Swad) tumepata namba 156 Tulipotoa Aya Ya Mwisho kutoka katika Aya Ya Kwanza ambazo zimetumia neno نَقُصُّ NAQUSU tumepata namba 156 Mbona Namba hizi zinalingana.

Huu ndiyo Muujiza. Maajabu Makubwa. Huu siyo Uchawi bali Muujiza. hii ni Lugha Ya Muumbaji. Ni Lugha ya Mwenyeezi Mungu aliyetukuka sana tena sana. Lugha ya Kiajabu Tupu. Allahu Akbar.

Kwa kweli tumeshindwa. Hatuwezi chochote mbele ya Maandishi yaliyopangika Kiajabu. Kuna siri Kubwa ambazo hatuzijui. Labda inawahusu Majini au Viumbe vya Baadaye au Sisi. Ukifanya hiki unapata hiki, Ukifanya hiki unapata hiki. Ajabu Kubwa. Hebu fikiri. Tumeangalia Herufi na kisha herufi katika Neno na mara Jawabu Limefanana. Allahu Akbar.

MUUJIZA WA KIPANDE CHA AYA ان الدين عند الله الاسلم KATIKA KURUANI RUKUFU

Tutafanya Utafiti wa Kipande cha Aya ان الدين عند الله الاسلم katika Sura Zifuatazo:

Sura Ya Al-Imran Namba 3 Aya Namba 19

ان الدين عند الله الاسلم و ما اختلف الذين اوتوا الكتب الا من بعد ما جاهم العلم بغيا بينهم و من يكفر بايت الله فان الله سريع الحساب

TAFSIRI

19.Bila shaka dini (ya haki) mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na waliopewa Kitabu (Mayahudi na Manasara) hawakukhitalitiana ila baada ya kuwajia ilimu. (Walikhitalifiana) kwa sababu ya uhasidi uliokuwa baina yao. Na anayezikataa Aya za Mwenyezi Mung’u (mara moja Mwenyezi Mungu atamuadhibu huko Akhera), na Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.

Sura Namba 3 Al-Imran Aya Namba 85

وَمَن يَبۡتَغِ غَيۡرَ ٱلۡإِسۡلَـٰمِ دِينً۬ا فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡهُ وَهُوَ فِى ٱلۡأَخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَـٰسِرِينَ (٨٥)

TAFSIRI

85.Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa).

Sura Namba 5 Al-Maidah Aya Namba 3

حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةُ وَٱلدَّمُ وَلَحۡمُ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦ وَٱلۡمُنۡخَنِقَةُ وَٱلۡمَوۡقُوذَةُ وَٱلۡمُتَرَدِّيَةُ وَٱلنَّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلسَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيۡتُمۡ وَمَا ذُبِحَ عَلَى ٱلنُّصُبِ وَأَن تَسۡتَقۡسِمُواْ بِٱلۡأَزۡلَـٰمِ‌ۚ ذَٲلِكُمۡ فِسۡقٌ‌ۗ ٱلۡيَوۡمَ يَٮِٕسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِ‌ۚ ٱلۡيَوۡمَ أَكۡمَلۡتُ لَكُمۡ دِينَكُمۡ وَأَتۡمَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ نِعۡمَتِى وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلۡإِسۡلَـٰمَ دِينً۬ا‌ۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ فِى مَخۡمَصَةٍ غَيۡرَ مُتَجَانِفٍ۬ لِّإِثۡمٍ۬‌ۙ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ۬ رَّحِيمٌ۬ (٣)

TAFSIRI

3. Mmeharimishiwa nyamafu na damu na nyama ya nguruwe, na kinyama kilichochinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kilichokufa kwa kusongeka koo, na kilichokufa kwa kupigwa, na kilichokufa kwa kuanguka, na kilichokufa kwa kupigwa pembe (na mwengine), na alichokila mnyama (kikafa), ila mkiwahi kukichinja (kabla hakijafa). Na (pia mmeharimishiwa) kilichochinjwa panapofanyiwa ibada isiyokuwa ya Mungu (kama mizimuni). Na ni (haramu kwenu) kutaka kujua siri kwa kuagua kwa mabao (na yaliyo kama hayo). Hayo yote ni maasiya. Leo waliokufuru wamekata tamaa katika dini yenu, basi msiwaogope, bali niogopeni Mimi. Leo nimekukamilishieni dini yenu, na kukutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni Uislamu uwe dini yenu. Na mwenye kushurutishwa na njaa, pasipo kuelekea kwenye dbambi, (akala hivi vilivyoharimishwa, basi hapana kitu); hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha (na) Mwingi wa rehema.

Sura Namba 61 As-Saf Aya Namba 7

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُوَ يُدۡعَىٰٓ إِلَى ٱلۡإِسۡلَـٰمِ‌ۚ وَٱللَّهُ لَا يَہۡدِى ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ (٧)

TAFSIRI

7. Na ni nani dhalimu mkubwa wa nafsi yake kuliko yule anayemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, na hali anaitwa katika Uislamu? Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhalimu (wa nafsi zao).

SHEREHE

Maana Ya Kipande cha Aya Katika Aya Ya Kwanza Hapa Juu ان الدين عند الله الاسلم Imekariri katika Aya Tatu nyinginezo hapa Juu. Yaani Ukichunguza Utaona Maana Iliyokariri ni “Uislamu Ndiyo Dini Inayokubalika Mbele ya Mwenyeezi Mungu.

Nimetia Rangi Nyingine  Hapa Juu Vile vipande vyenye Kuleta maana hii katika Aya zote Nne ili ieleweke vizuri. Ijapokuwa Maana za Aya ni Tofauti lakini kila Aya Imeelezea Umuhimu wa Dini ya Kiislamu.

Sasa Tufanye Utafiti WA Aya Ya Kwanza Hapa Juu ambayo maana yake ipo katika Aya Nyinginezo Tatu. Ukikigeuza Kipande hiki ان الدين عند الله الاسلم katika Hesabu au Thamani ya Namba.

(Warabu na mataifa mengineyo hapo zamani walikuwa wakitumia Herufi kuwakilisha Namba. Kwa hiyo walitumia Alif Kuwakilisha Namba 1 na Baa kuwakilisha Namba 2 na hivyo hivyo namba zote. Nimekwisha zungumzia habari hii kwa urefu katika milango ya Website hii)

tutapata namba 498 Hebu Tupange namba za Sura,

Aya Na Herufi za Aya Hizi Nne:

Sura Namba 3 Aya Namba 19 Jumla ya Herufi Za Aya Hii ni 105

Sura Namba 3 Aya Namba 51 Jumla Ya Herufi Za Aya Hii ni 51

Sura Namba 5 Aya Namba 3 Jumla Ya Herufi Za Aya Hii ni 276

Sura Namba 61 Aya Namba 66 Jumla Ya Herufi Za Aya Hii ni 66

Tumesema kwamba maana ya kipande ان الدين عند الله الاسلم katika Sura Namba 3 Aya Namba 19 imakariri katika Aya Tatu nyinginezo hapa Juu.

Na Tumesema kwamba Thamani ya Herufi ya kipande hiki ni 498

Sasa hebu tujumlishe Herufi za Aya hizi Nne tuone Jawabu. 105 + 51 + 276 + 66=498

Haya kweli ni maajabu. Thamani Ya Kipande ان الدين عند الله الاسلم na ambacho kina maana katika Aya zilizotajwa hapa juu yaani namba 498 ambayo ni  sawa na Jumla ya herufi ya Aya Hizi Nne.

Hebu Nipange tena vizuri ili tuone:

Thamani Ya Kipande ان الدين عند الله الاسلم hiki ni 498

Na Jumla Ya Herufi za Aya Hii pia Ni 498

Haya Kweli Maajabu. je ni Uashirio kwamba Maana Ya Kipande Cha Aya Ya Kwanza ni sawa na Maana Iliyopo katika Aya Nyinginezo?

Labada Hivyo kwani Hesabu Ndizo zinavyotuambia.

Kwa kweli Muujiza Wa Kuruani Hauna Mwisho. Allahu Akbar.

Na Ajabu Nyingine ni kwamba Ukihesabu Namba za Aya zake Tunapata Idadi nyingine ya kushangaza: Hebu Tuone: 19 + 85 + 3 + 7=114

Angalia Maajabu Tukijumlisha Namba za Aya tunapata Idadi ya Sura za Kuruani ambazo ni 114!!!!

Yaani Kipande hiki cha Aya ان الدين عند الله الاسلم ambacho kinasema kwamba “Dini Inayokubaliwa Mbele ya Mwenyeezi Mungu” Kina Miujiza Isiyo na Mwisho. Tumepata hapa Maajabu mawili. Kwanza Kukariri kwa Namba 489 na Pili Idadi ya Sura za Kuruani 114. Kwa kweli Kuruani imekusanya Ulimwengu. Haya siyo Madogo. Allahu Akbar.

UMRI WA MTUME  MOHAMAD, MUDA WA UJUMBE WA MWENYEEZI MUNGU (UISLAMU) NA KANDA ZA KIZAZI (CHROMOSOMES) NI BAADHI YA MIUJIZA MIKUBWA KATIKA KURUANI TUKUFU

Jambo  la kushangaza ni kwamba  Umri  wa Mtume Mohamad ﷺ ambao ni miaka  63, Na Muda wa Ujumbe wake ambao ni  Miaka  23 na Chromosomes 23 ambazo ni kanda za Uzazi  wa Binaadamu zote zimeashiriwa katika Kuruani  tukufu kiajabu sana. Na Mwenyeezi Mungu anajua zaidi iwapo tunakosea.

Ajabu ya Kwanza ni Jumla ya Kanda hizi za Uzazi ni 23 na Namba  hii inalingana na Muda wa Ujumbe wa Mtume Mohamad ﷺ katika Dunia. Kanda za Uzazi  wa Binaadamu 23 kutoka kwa Baba na 23 Kutoka Kwa mama  jumla ni 46 

Kila Mwaka Mtume Mohamad ﷺ alifundishwa Kuruani Na Jibril mara Moja (Mwezi wa Ramadhan) na Katika Mwaka wa Mwisho wa Maisha Yake Yaani Mwaka wa Mwisho wa Ujumbe wake yaani ule mwaka wa 23  alisomeshwa Kuruani Mara Mbili Katika Mwezi wa Ramadhan (Revision of Quran  was  2 Times)

Na katika Elimu ya Kizazi  (Embryology) Mbegu ya Baba na mama ni sawa na   23 X 2  pia!!!!

Angalia Maajabu. Je Huu siyo mpangilio wa kiajabu? Je huoni  Namba zinavyozungumza?  Allahu Akbar.

Miaka  23 ni Miaka Ya Ujumbe aliolingania Dini Mtume Mohamad. ﷺ

Sasa tuendelee na Utafiti  huu katika Kuruani Tukufu tuone Maajabu  Mengineyo.

Tuchukuwe  Majina Ya Sura Zote Za kuruani  yaani Majina 114. Kwa mfano  Jina La Kwanza  ni  “Al-Fatiha”  La pili ni  Al-Bakarah  na hivyo hivyo mpaka majina yote  ya Sura 114 ya Msahafu. 

KIsha  Tutafute  Thamani au Namba  za Herufi Hizi kufuatana na  Mpangilio wa Alphabet za Lugha Ya Kiarabu. (Tafadhali usichukue zile Namba walizotumia Waarabu na Mataifa mengineyo hapo zamani yaani kama  nilivyosema katika sehemu nyinginezo kwamba Hapo zamani Waarabu na Mataifa mengineyo walitumia Herufi kuwakilisha Namba.  Utafiti huu hutachukua Namba hizo bali namba  za Mpangilio wa Herufi za Lugha ya Kiarabu. Kwa mfano  katika Herufi zote 28   Alif itakuwa namba   1  na  Baa 2   hivyo hivyo  mpaka herufi zote 28  na kwa hiyo  Herufi ya Mwisho itakuwa  ya 28).

Tukifanya hivyo  na kisha Tuzichunguze namba  zote na kujaalia au kuzipanga   Namba Kubwa iwe ya Kwanza na Hivyo hivyo itakayofuatia  ndogo  yake na ufanye hivyo mpaka  namba ya mwisho ambayo itakuwa ndogo  kabisa.  Ukifanya Hivyo  utapata Maajabu mengineyo ya Kushangaza.  Yaani Ukiangalia Namba Ya Majina Ya Sura zote  114  utaona zile Namba 3 kubwa za kwanza zinashangaza sana. 

Namba Ya Kwanza Itakuwa    176

Namba Ya Pili itakuwa   167

Na Namba ya Tatu  Itakuwa 157

Sasa Tuchunguze Majina Ya Sura Ya Namba Hizi:

Namba 176  Inawakilisha  Sura Namba 23

Namba 167  Inawakislisha Sura Namba 63

Namba 157 Inawakilisha Sura namba 83

Angalia Maajabu Tuliyoyapata katika Majina Ya Sura

Yaani  Hizi Ndizo  Sura Tatu katika Sura ambazo Thamani Ya Herufi za Majina Yake  ni za Juu kuliko Zote  nyinginezo.

Namba 23 hapa Ni  Muda wa Ujumbe wa  Mtume Mohamad.ﷺ

Namba 63  Ni Umri alioishi Mtume Mohamad

Na Namba  83  Ni Namba ya 23 katika  Namba  zinazojulikana kama Prime Numbers.

Na Namba hii  23 ya Tatu inaashiria  Kama tulivyosema hapa Juu.  Muda wa Ujumbe wake Mtume Mohamad.ﷺ

Na Kwa vile kuna namba 23 mara 2  basi  huenda ni ile miaka ya Kisomo cha Kuruani  alichofundishwa na Malaika Jibril  katika Mwaka wa Mwisho  wa  Ujumbe wake yaani mwaka wa 23 alijiwa na JIbril mara Mbili.

Katika Bukhari kuna Hadithi  Ya Mtume inayotokana na Fatima  Inasema:

عَنْ فاطمة عَنْ النَّبِيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ أَسَرَّ إِلَيَّ إِنَّ جِبْرِيلَ كَانَ يُعَارِضُنِي الْقُرْآنَ كُلَّ سَنَةٍ مَرَّةً وَإِنَّهُ عَارَضَنِي الْعَامَ مَرَّتَيْنِ وَلَا أُرَاهُ إِلَّا حَضَرَ أَجَلِي وَإِنَّكِ أَوَّلُ أَهْلِ بَيْتِي لَحَاقًا بِي فَبَكَيْتُ فَقَالَ أَمَا تَرْضَيْنَ أَنْ تَكُونِي سَيِّدَةَ نِسَاءِ أَهْلِ الْجَنَّةِ أَوْ نِسَاءِ الْمُؤْمِنِينَ فَضَحِكْتُ لِذَلِكَ 3376 صحيح البخاري كتاب المناقب باب علامات النبوة في الإسلام

TAFSIRI

Imepokewa kutoka kwa Fatimah: Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: “Jibril alikuwa akinijia ili Kunifundisha (Revision au Marejeo ya Kisomo) Quran mara moja kila mwaka na Mwaka huu alinifundisha (Revision au Marejeo ya Kisomo)Mara Mbili . Sidhani kama ina maana yoyote (Sielewi  Undani wake) bali huenda muda wangu (Wa Maisha na Ujumbe) utafikia mwisho. Hakika wewe utakuwa wa kwanza kukutana nami katika watu wa nyumba yangu. Kwa hiyo nililia na Mtume akasema: “Je, hufurahii kuwa kiongozi wa wanawake wa Peponi au Waumini wanawake? Kwa hiyo nilicheka kwa hilo.

English Translation

Fatimah reported: The Prophet, peace and blessings be upon him, said, “Gabriel would come to me to revise the Quran once every year. This year he revised with me twice. I do not think it means anything but that my term will come to an end. Verily, you will be the first of the people of my house to meet me.” So I wept and the Prophet said, “Are you not pleased with be the master of the women of Paradise or the believing women?” So I laughed at that.

Source: Ṣaḥīḥ al-Bukhārī 3376 Grade: Sahih (authentic) according to Al-Bukhari

Na Huenda Pia ni  Kanda za Uzazi wa Binaadamu (Chromosoms)  23 za baba na 23 za mama  na Jumla ni  46.

Au  23 ya mwanzo  ni Muda wa Ujumbe na  23 ya pili ni Chromosomes za Binaadamu.

Kwa kweli Huu siyo Muujza mdogo. Hakuna Dogo hapa kwani miashirio Mingi kama hii siyo bure bure. Kuruani haina Mchezo au Upuuzi.  Hizi ni Alama za kuthibitisha Ujumbe aliokuja nao Mtume Mohamad.ﷺ Hata siyo mambo ya Utani.  Ni Mambo ya Kutisha  sana. Allahu Akbar. Allahu Akbar.  Uhusiano  Baina Ya Ujumbe Huu na

Chromosomes za Binaadamu  yaani Kanda za Uzazi unaonyesha Ujumbe huu ni wa Binaadamu wote Duniani kwani KIla Binaadamu ana Chromosomes  hizi  23. Je unaona Namba zinavyozungumza?  Na pia Namba tulizopata katika  Majina Ya Sura Za Kuruani pia Inaonyesha uhusiano wake na Kanda za Uzazi (Chromosomes) pia. Kwa hiyo  Ujumbe Huu ni Dunia Nzima. Kuruani ni  Mafundisho kwa kila Mtu Duniani.  Allahu Akbar.