SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Darubini-7/Kuruani

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MIUJIZA MBALIMBALI

14/10/2022

Alhamdulilah. Leo ni Siku kubwa na pia ni Siku nzuri kuliko Siku zote za Wiki. Ni Siku ya Ijumaa Allahu Akbar. Kuna Hadithi  Mbalimbali za Mtume ﷺ ambazo  zinaelezea utukufu wa Siku ya Ijumaa. Hapa nitataja hadithi Moja tu ambayo  imekusanywa katika Sahih Ya Muslim.

وَحَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ بْنُ سَعِيدٍ، حَدَّثَنَا الْمُغِيرَةُ، – يَعْنِي الْحِزَامِيَّ – عَنْ أَبِي الزِّنَادِ، عَنِ الأَعْرَجِ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ “‏ خَيْرُ يَوْمٍ طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ يَوْمُ الْجُمُعَةِ فِيهِ خُلِقَ آدَمُ وَفِيهِ أُدْخِلَ الْجَنَّةَ وَفِيهِ أُخْرِجَ مِنْهَا وَلاَ تَقُومُ السَّاعَةُ إِلاَّ فِي يَوْمِ الْجُمُعَةِ ‏”‏ ‏.‏

SHEREHE

Abu Huraira anasimulia kwamba Mtume ﷺ alisema “Siku iliyo bora ni Siku ya Ijumaa kwani ni Siku  hiyo ambayo Nabii Adam aliumbwa, Kuingizwa  peponi, Kutolewa Peponi na Hakitakuwa Kiyama isipikuwa ni Siku Ya Ijumaa”

TRANSLATION

Abu Huraira reported the Messenger of Allah (ﷺ) as saying: The best day on which the sun has risen is Friday; on it Adam was created. on it he was made to enter Paradise, on it he was expelled from it. And the last hour will take place on no day other than Friday.

MAAJABU MAKUBWA

AJABU YA KWANZA

Na Katika Siku Kubwa kama hii nimeona bora niwaletee baadhi ya Miujiza niliyosoma kutoka kwa Wanavyuoni mbalimbali. na nitafanya hivyo kwa uwezo wake Mwenyeezi Mungu Mtukufu kwani Sisi Binaadamu ni wapungufu na bila ya Uwezo wa Mwenyeezi Mungu haitawezekana.

Ninaanza na  “BIsmillah Arahmani Arahim”

Kuna siku nilishangaa sana kusoma Utafiti wa Vijana Wachamungu ambao  Unashangaza.

Utafiti wa kwanza  unahusu  Sura Namba 21 Aya Namba 30

سُوۡرَةُ الاٴنبیَاء   Sura Ya Al-Ambiya

أَوَلَمۡ يَرَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضَ ڪَانَتَا رَتۡقً۬ا فَفَتَقۡنَـٰهُمَا‌ۖ وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَىۡءٍ حَىٍّ‌ۖ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ (٣٠)

Nilikwisha zungumzia  Aya Hii katika sehemu nyingine ya Website hii lakini  kipande ڪَانَتَا رَتۡقً۬ا فَفَتَقۡنَـٰهُمَا‌ۖ  hiki  kina Mengineyo makubwa ambayo  sikuyajua hapo mwanzo.  

Aya Hii inasema  kwamba Mbingu na Ardhi zilikuwa Moja au kwa lugha nyingine  zilikuwa kitu kimoja zimeungana na kugandana na kisha Mwenyeezi Mungu anaendelea  kusema kwamba akaleta  Mfunuo au Mpasuo au Mchanuo  kwa kifupi  akasababisha kupasuka, kusambaa na ikafuatia  kuumba kila kitu. Na anatuambia kwamba katika kuumba akajaalia kila kitu kutokana na Maji kuwa Hai na Mwishoni mwa Aya anasema  “Je Hawaamini”  yaani Je sisi Hatuamini baada ya yote haya.

Jambo  jipya ni  kipande hiki  ڪَانَتَا رَتۡقً۬ا فَفَتَقۡنَـٰهُمَا‌ۖ  chenye maana ya Mbingu na Ardhi zilikuwa kitu kimoja na kisha akavitenganisha kwa kupasuka au kusambaa kwa njia na hekima azijuayo yeye mwenyewe. Kipande hiki ukigeuza Herufi  zake katika Namba Zilizotumiwa na Waarabu hapo zamani katika kuwakilisha Herufi na kisha ukazijumlisha kama nilivyofanya hapa chini

ك 20 + ا 1 + ن 50 + ت 400 + ا 1 + ر 200 + ت 400 + ق 100 + ا 1 + ف 80 + ف 80 = ت 400 + ق 100 +ن 50 +ه 5 م 40 ا1

Total 1929

utashangaa kuona kwamba Namba  tutakayoipata ni  1929  na kwa kweli ndiyo  Mwaka ambao Ushahidi  wa Kithibitisho wa Nadharia kwamba Mpasuko wa Mbingu na Ardhi ni wa ukweli ulifanyika. Ni siku ambayo Mwanasayansi Maarufu  kwa kutumia  Darubini kwa jina la Hubble aligundua kwamba  Nyota na Kila kitu angani  zipo katika Kutengana na hii ilithibitisha kwamba Nguvu za Mpasuko wa Mwanzo  bado unaendelea kusambaza Kila kitu angani na hii inathibitisha kwamba Hapo mwanzo  kila kitu kilikuwa Kimoja na kisha kukatokea Mpasuko. Habari hii haikuwa ikiaminika kwani Wataalamu Wakubwa Duniani walikuwa hawaamini Mtanuko wa Mbingu. Waliamini kwamba Kila kitu kipo  STATIC (Kimetulia) na Hawakuamini kwamba kila kitu ni  DYNAMIC (Harakati) na kwa hiyo Mwaka huu wa 1929  ulikuwa mwaka Mkubwa sana. Ni mwaka ambao  Experiment au Tajruba ilifanyika  na kuthibitisha Asili ya Maumbile. Habari hii siyo ndogo  ni Sayansi ambayo bado inawatatanisha Wataalamu Duniani Mpaka leo. Kwa hiyo huu ni Muujiza mkubwa sana katika Kuruani ambayo  inatuelezea Mpasuko huu na pia Mwaka ambao Kithibitisho kitatokea.

Yaani Kuruani Imetabiri mpaka Mwaka. Je huoni Maajabu. Uislamu ulikuja katika karne ya 6  na Ugunduzi Karne ya 20 yaani mwaka 1929.  Kwa kweli Muujiza Siyo mdogo kwa mtu atakayetaka Kufikiri. Yaani Mwenyeezi Mungu anakua yote yaliyopita na yatakayokuja na ameweka habari hizi katika  Kuruani kwa njia ya Namba. Allahu Akbar.

Nadharia ya Mpasuko  wa Mbingu na Ardhi ilianzishwa mwaka 1927  lakini  Kithibitisho  chake kilikuwa Mwaka  1929  na Mtaalamu Anayejulikana kama  Edwin Hubble na baadaye Darubini aliyotumia Mtaalamu huyu ilitiwa Jina Lake na kuitwa  HUBBLE.. 

Hapa chini  ninawaletea habari hizi kwa Lugha ya Kiingereza. Nimebadili rangi katika Ile habari  ya Utafiti wetu wa leo.

Georges LeMaitre (1894-1966) showed that religion and science — or at least physics — did not have to be incompatible. LeMaitre, born in Belgium, was a monsignor in the Catholic church. He was fascinated by physics and studied Einstein’s laws of gravitation, published in 1915. He deduced that if Einstein’s theory were true (and there had been good evidence for it since 1919), it meant the universe must be expanding. In 1927, the year he got his PhD from MIT, LeMaitre proposed this theory, in which he stated that the expanding universe was the same in all directions — the same laws applied, and its composition was the same — but it was not static. He had no data to prove this, so many scientists ignored it. (Another scientist, Soviet Aleksandr Friedmann, had come to the same conclusion independently, a few years earlier.) Even Einstein was reluctant to endorse this extension of his theory of general relativity. In 1929 at the Mt. Wilson Observatory in California, Edwin Hubble discovered that galaxies were moving away at high speeds. He was, like most people, unaware of LeMaitre’s 1927 theory. But LeMaitre used Hubble’s dramatic discovery as evidence for his theory. It was easy. If you imagined the galaxies rushing away from us as a movie, just run the movie backwards. After a certain time, all those galaxies will rush together. LeMaitre put forth the idea that there was once a primordial atom which had contained all the matter in the universe.

AJABU YA PILI

kwa kweli  kila  Muujiza katika Kuruani unashangaza. Kuna Miujiza Mingine inabidi  Utafiti wa hali ya Juu. Inabidi  Kutumia Vifaa Mbalimbali vya utafiti. Na hii inaonyesha Kwamba Haya siyo maneno ya Mtume peke yake bali ni Ya Muumba aliyeumba kila kitu. Allahu Akbar.

Sasa tufanye uchambuzi wa  Aya Ya Kwanza katika Sura Ya  “A-Qalam”   Utafiti huu unaonyesha Maajabu ya Mpangilio wa Herufi za Kuruani. Hebu  fikiri  Muujiza  mpaka katika Herufi. Sasa  tuchunguze  Herufi  Ya   “NUN” katika Sura Hii namba 68  Aya Ya Kwanza.

سُوۡرَةُ القَلَم

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

نٓ‌ۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ (١)

TAFSIRI

(Naapa Kwa Herufi ya )NUN. Na Kalamu yenye Kuandika.

SHEREHE

Mwenyeezi Mungu anaapia Herufi hii na Pia Kalamu ambayo kazi yake ni kuandika. Kwa hiyo  kila kinachotusaidia katika Kuandika asili yake ni Kalamu na hata Computer  pia msingi wake ni Maandishi.

Ukichunguza  Aya zote zilizotumia  Herufi  Hii ya NUN  نٓ‌ۚ  kuanzia  Aya ifuatayo  mpaka  Mwisho  wa Kuruani. Yaani  Kuanzia Aya Namba 2  mpaka mwisho wa Kuruani  utakuta Jumla  Aya ambazo zimetumia Herufi hii ni  681  sasa angalia maajabu. Namba hii siyo  ya kawaida kwani inaashiria  Herufi ya NUN  ambayo ipo katika Aya Namba  Moja ya Sura Ya Al-Qalam. Namba Ya Sura na Aya ni 68 Aya namba 1  au    68:1  hebu angalia maajabu. Tulipofanya utafiti  wa herufi hii tukapata Jumla  za Aya zilizotumia herufi hii ni  681  je huoni  maajabu?  Allahu Akbar. Angalia Muujiza hata katika Herufi. Utafiti Huu huwezi kuufanya kirahisi  bila ya Programs . Na hii inaonyesha kwamba Kuruani siyo maneno ya kibinaadamu kwani katika Enzi za Mtume ﷺ kulikuwa hakuna Ufundi  wa utafiti kama nyakati hizi za kisasa. kwani haiwezekani Mtume ﷺ ajiandikie hii kuruani na kisha apange herufi  mpangilio kama huu ili aonyeshe watu. mwenye Kufikiri hivyo basi ni Mjinga au Mwongo  hakuna lingine.

AJABU YA TATU

Hesabu  zinazungumza. Hebu tufanye hesabu na kisha tujadili maana ya Baadhi ya Aya za Kuruani.

Mwaka wa Ardhi kuzunguka Jua kwa siku 365  unajulikana kama SOLAR  YEAR

Mwaka wa Mwezi Kuzunguka Ardhi  kwa siku  354 unajulikana kama “LUNAR  YEAR”  na huu ndio mwaka wa Kiislamu.

Hebu  tugawe namba hizi Mbili

365/354=1.03

Sasa  tuchunguze  Idadi ya Miaka ya watu waliolazwa katika Pango.  (Ashaab  Alkahf). Sura Ya Al-Kahf.

Mwenyeezi Mungu alisema walilazwa kwa muda wa miaka  300 na wakazidisha miaka  9  yaani Miaka 309 Kauli hii isitubabaishe kwani Miaka waliyolazwa ya Solar Year ni  300 na Miaka hii ni sawa na ya Lunar Year (Miaka ya Kiislamu) ambayo ni 309. Kwa hiyo Sherehe itakuwa 

“Watu hawa walilazwa kwa muda wa miaka  300 lakini  Waislamu katika hesabu zao inabidi  wazidishe Miaka  9  kwani wanatumia Mzunguko wa Mwezi katika Ardhi.. Kwa lugha Rahisi unaweza kusema kwamba Walilazwa kwa Muda wa Ardhi Kuzunguka Jua (Miaka 300)  na miaka hii ni sawa na  Mwezi Kuzunguka Ardhi (Miaka  309)

Na ili kuthibitisha Vizuri kama kauli hii ni sahihi  hebu tugawe Miaka  hii.

309/300=1.03

Je unona  namba Hii ni sawa na Namba tuliyopata hapa juu ya Mgawanyo  wa miaka ya Solar na Lunar

Sasa Tuchunguze Maana na Uhusiano baina ya maneno mawili عام  na سنة   haya maneno mawili yametumika katika Kuruani kwa maana mbili.  عام  ni Miaka ya Neema na سنة  kwa maana ya Miaka ya Shida.(Nimezungumzia Habari Hizi katika Website Hii na Nimechambua Baadhi ya Aya)  Lakini katika Hesabu nitakazofanya hapa chini  inaonyesha pia kwamba neno عام  na سنة  Ukigeuza Herufi  zake katika Namba walizokuwa wakitumia Waarabu hapo zamani utapata Neno عام Jumla ya Herufi  zake ni  111  na neno  سنة Jumla ya Herufi zake ni  115

عام=

ع 70 + ا 1 + م 40= 111

سنة=

س 60 + ن 50 + ة 5=115

Hebu  tuchunguze kihesabu kwa kugawanya kama tulivyofanya hapa juu.

115/111=1.03

Lakini Huu ni utafiti wa Kihesabu wakati mwingine unababaisha. Namba zinafanana  lakini tumeona katika Kuruani Maana ya Maneno mawili. Yaani neno  “AAM”  maana ya Miaka ya Neema na Neno  “SANA” Lina maana Ya Miaka Ya Shida. 

Katika Utafiti Huu wa leo Tunapata Pia kwamba neno  “AAM”  linaleta  maana ya Miaka ya Lunar na Neno  “SANA”  Lina maana Ya Miaka Ya  Solar kwani  Ratio ni sawa na Mgawanyo  tuliofanya hapa juu yaani 1.03

Kwa hiyo  Maneno haya mawili  huenda yanabadilika maana ya matumizi yake kufuatana na Matumizi  yake. Yaani kuna wakati huweza kutumika kwa maana ya Neema na Shida na wakati mwingine  Solar au Lunar  Year. Na Mwenyeezi Mungu anajua zaidi iwapo tumepata au tumekosea. Allahu Akbar.

AJABU YA NNE

Kwa kweli Kuruani  ni Muujiza Usio na Mwisho. Na Mtume Mohamad ﷺ ametimiza amri ya Mwenyeezi mungu kama ipasavyo. Ujumbe aliouleta haukubadilishwa hata kidogo. Huu sio muujiza mdogo.  Herufi, Maneno, Aya, Sura, Majina Ya Sura  Na Mpangilio wake Yote Ni Muujiza Mkubwa ambao  bado mengi hatuyajui. Allahu Akbar.  Allahu Akbar. Allahu Akbar. Kwa kweli wakati  umefika tuamke na tusilale usingizi kwani inatisha na ni hatari sana kwani ulimwengu siyo  wetu. Miaka inapita haraka, Nyumba zetu ni Makaburi na yanatusubiri na wadudu humo Makaburini  wana Njaa na wanatusubiri kwa hamu sana watutafune. Kwa kweli haya ninayosema kwanza najiambia mwenewe na kisha kila atakayepata bahati kusoma nasiha hizi. Allahu Akbar.

Sasa tusome Katika Muujiza Huu wa nne  maneno mawili tu na tuone maajabu mengine.  

Neno  الإيمان  “IMANI”   na  neno  الكفر “KUFURU”

Haya Maneno  mawili yametumika  katika Kuruani Katika Aya na Mifumo mbalimbali lakini maana yake ni ile ile. 

Imani kinyume chake ni  Kutokuwa na imani  na Ndiyo  Kufuru. Na Kufuru kinyume chake ni Imani na Imani maana yake Kuwa na Imani.  Haya maneno mawili yanapingana.  Neno na Kinyume chake. Kufuru Kinyume chake ni  Imani na Imani kinyume chake ni Kufuru.

Hebu  tugeuze maneno  haya mawili katika Namba  kwa kutumia namba za hapo zamani kama nilivyofanya katika Miujiza mingineyo hapa juu.

Ukigeuza Herufi hizi  katika Namba Utapata Namba na Kinyume chake kiajabu sana hebu tuone hapa chini:

الإيمان=133

الكفر=331

الإيمان=  

ا 1 + ل 30 + إ 1 + ي 10 + م 40 +  ا 1 + ن 50  = 133

الكفر=

ا 1 + ل 30 + ك 20 + ف 80 + ر 200=331

Je unaona namba na Kinyume chake?  Unaona ya kushangaza?  Namba 133  kinyume chake ni  namba 331

Yaani  Imani  na kinyume chake  ni Kufuru. Hebu  ziangalie namba hizi mbili kisha uzilinganishe:

133

331

Namba na Kinyume chake. Angalia maajabu. Imani ni namba 133 na kafiri  331.  Allahu Akbar. Allahu Akbar.

Hebu tujumlishe Namba Hizi Mbili:

133 + 331=464

sasa tuchunguze katika Kuruani Aya  Ya 464  kuanzia mwanzo  wa Msahafu tuone Aya gani  tutakayoipata.

يَسْتَبْشِرُونَ بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّهِ وَ فَضْلٍ وَ أَنَّ اللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجْرَ الْمُؤْمِنِينَ

Hii ni aya ya 464  kuanzia Mwanzo  wa Msahafu  nayo inasema  

Katika Aya Hii Mwenyeezi Mungu anaelezea Neema watakazopata waliofariki kwa ajili yake yaani Mashuadaa wake.  Katika Aya Hii Mwenyeei Mungu anasema kwamba Hao Mashahidi  wanabashiri  habari nzuri za Neema kutoka kwa Allah na Fadhila Na  Mwenyeezi Mungu hatampotezea  Ujira Muumini  yeyote.

Angalia neno  MUUMINI  yaani mwenye Imani.

Hebu  tufikiri. Tulipojumlisha Namba 133 na 331  tukapata  464  na namba hii  imetupeleka katika Aya yenye neno MUUMINI  yaani mwenye Imani na pia habari  nzuri ya zawadi watakazopewa na Mwenyeezi Mungu.

Nimefikiri sana Muujiza Wa  Maneno haya mawili na nikajiuliza Kwa nini  tukijumlisha namba hizi mbili  tunapata namba ambayo inahusu  IMANI.

Ninasema  Huenda Kwani Mwenyeezi  Mungu anajua zaidi. Huenda  Maana  tunayopata ni kama ifuatavyo:

Batili  na Imani  inaposhindana basi Imani itashinda  bika shaka yeyote na ndiyo maana  namba 133 tukijumlisha na namba 331 tunapata aya inayohusu  Imani.

133 + 331= 463  ni sawa na kusema 

Imani  + Kufuru=Imani

Je unaona maajabu?  Na fikira hii inatibitishwa na Aya ya kuruani  inayosema

وَقُلْ جَآءَ ٱلْحَقُّ وَزَهَقَ ٱلْبَـٰطِلُ ۚ إِنَّ ٱلْبَـٰطِلَ كَانَ زَهُوقًۭا

“Sema Haki Imekuja Na Ubatili Umeondoka Kwa Hakika Ubatili ni wa kuondoka”

(The truth has come and falsehood has vanished. Indeed, falsehood is bound to vanish)

Kwa hiyo  huu ni Utafiti lakini mwenyeezi mungu anajua zaidi. Ni Juhudi  ndogo za Mja lakini huenda tunakosea. Tunamuomba Mwenyeezi Mungu atakabalie kazi hizi ndogo ndogo. Allahu Akbar.

MUUJIZA WA TANO

Muujiza Huu ni wa Kisayansi. Kwa kweli unashangaza na Inaonyesha Kuwa kuruani siyo maneno  ya Kibinaadamu hata kidogo., Haiwezekani hata chembe.  Ni wachache  wajinga wasiolewa ndiyo wanaota ndoto  na kufikiri  kuruani iliandikwa na Mtume. Kwa kweli Haiwezekani kabisa. Hebu  tupeleke Darubini katika Aya Ifuatayo kutoka Katika Sura Ya Al-Anaam Namba 6  Aya Namba 35 kisha tuone Maajabu mengine katika maajabu yasiyo na Mwisho. Allahu Akbar.

سُوۡرَةُ الاٴنعَام

وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيۡكَ إِعۡرَاضُہُمۡ فَإِنِ ٱسۡتَطَعۡتَ أَن تَبۡتَغِىَ نَفَقً۬ا فِى ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ سُلَّمً۬ا فِى ٱلسَّمَآءِ فَتَأۡتِيَہُم بِـَٔايَةٍ۬‌ۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَمَعَهُمۡ عَلَى ٱلۡهُدَىٰ‌ۚ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡجَـٰهِلِينَ (٣٥)

TAFSIRI

35. Na ikiwa ni makubwa Kwako huku kujitenga kwao (na haya unayowaambia kwa kuwa wanataka waonyeshwe hiyo miujiza wanayoitaka; ukawa unataka sharti waonyeshwe miujiza hiyo, na Mimi sitaki), basi kama unaweza kutafuta njia ya chini kwa chini. katika ardhi (kwenda kutafuta miujiza hiyo) au :(unaweza kupata) ngazi ukapanda mbinguni na kuwaletea miujiza (wanayoitaka, fanya). Na kama Mwenyezi Mungu angependa bila shaka angewakusanya katika uwongozi (huu kwa miujiza hiyo; lakini hataki). Basi usiwe miongoni mwa wasiojua.

ENGLISH TRANSLATION

And if their turning away is hard on you, then if you can seek an opening (to go down) into the earth or a ladder (to ascend up) to heaven so that you should bring them a sign and if Allah had pleased He would certainly have gathered them all on guidance, therefore be not of the ignorant.

SHEREHE

Nabii Muhammad ﷺ alikuwa na hamu kubwa kabisa ya kutaka watu wote wasilimu upesi upesi. Wapewe hiyo miujiza wanayoitaka udhia uishe Lakini Mwenyezi Mungu alikuwa hapendi Uislamu huo. Anapenda wasilimu baada ya kuyafahamu vyema hayo wanayoambiwa. Siyo wanasilimu kwa nguvu za miujiza. Kwa hiyo Mwenyeezi Mungu anamwambia Mtume ﷺ kwamba ikiwa anaona kwamba Miujiza ni muhimu sana basi atafute Mwenyewe ndani ya ardhi yaani atafute njia aende akatafute Miujiza hiyo ardhini au Atafute Ngazi  na aitumie  kwenda Mbinguni  ili kutafuta Miujiza Hiyo.

Jambo  la kushangaza ni   kioande cha Aya  ambacho nimekitia Rangi katika Aya hii.

أَوۡ سُلَّمً۬ا فِى ٱلسَّمَآءِ

Kipande hiki  kinasema  au atafute ngazi  na kwenda Mbinguni. Hebu tupeleke Darubini  yetu katika Kipande hiki. Inayozungumzia  Ngazi  ya Kwenda Angani. 

Je unajua hivi sasa Wanasayansi  wapo mwanzoni katika Utafiti Mpya ambao mchanga sana wa kutengeneza Ngazi au  Elevator  ambayo  kazi yake ni  kwenda Katika  Mwezi  au  katika Satelites  huko Angani. Fikira Hii ilizaliwa hapo zamani mwishoni mwa karne ya  19 (Mwaka 1895)  lakini mpaka leo bado  inafanyiwa utafiti. Angalia Hapa Chini Video na Picha Kuhusu Habari hizi za Kushangaza. Kwa kweli unaweza kufikiria Upuzi lakini la kushangaza zaidi ni Aya Ya Kuruani ambayo  imetaja  Fikra hizi kuanzia Karne ya 6 sasa Mtume Mohamad ﷺ alijua vipi Habari  hizi? kwa vipi Kuruani imeweza kuja na fikra na kutaja Ngazi? katika wakati  huo wa zamani wakati kulikuwa hakuna Sayansi kama leo.

Hii  inaonyesha Kwamba maneno ya Kuruani ni Yake Mwenyeezi Mungu Mtukufu. Ni yule yule aliyeumba ulimwengu na ni yule yule  ndiye aliyeshusha kuruani hii. Allahu Akbar. Alijua ya Baadaye na Tutakayoyafanya yote.

Hapa Chini Habari  Nimenukulu  kutoka katika  Utafiti  wa Wataalamu Duniani:

The Penn State University researchers had a hunch that these diamond nanothreads, which are remarkably light and strong at the same time — could prove to be an ideal material for a space elevator, a long cable anchored on Earth and reaching into space to attach to a satellite in orbit.

Just recently, a team from the Queensland University of Technology in Australia modeled the diamond nanothreads using large-scale molecular dynamics simulations and concluded that the material is far more versatile than previously thought and has great promise for aerospace properties. The simulation was published in early November.

LIft au Elevator ya Anga Inathibitisha Maajabu Ya Meneno ya Kuruanu Tukufu. Allahu Akbar

VIdeo-1

Video-2

Ngazi za Anga. Kuruani Imataja Habari ya Ngazi za Angani. Maajabu siyo Madogo. Kuruani imetaja haya Tangu karne ya 6 na Sayansi imekuja na fikra hizi hivi karibuni katika Karne ya 19 je unaona Maajabu?

MUUJIZA WA MIAKA  23 YA KUSHUKA KWA KURUANI-(MIAKA  23 YA UJUMBE WA MTUME MOHAMAD ﷺ)

Hebu tuchunguze Herufi  za Sura Ya Kwanza na Kisha Sura Ya Mwisho  katika Msahafu.  Yaani Sura Namba 1  na Namba 114.

SURA YA ALFATIHA-SURA NAMBA 1

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ (١) ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَـٰلَمِينَ (٢) ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ (٣) مَـٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ (٤) إِيَّاكَ نَعۡبُدُ وَإِيَّاكَ نَسۡتَعِينُ (٥) ٱهۡدِنَا ٱلصِّرَٲطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ (٦) صِرَٲطَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِمۡ غَيۡرِ ٱلۡمَغۡضُوبِ عَلَيۡهِمۡ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ (٧)

SURA YA  AL-NAS -SURA NAMBA  114

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ (١) مَلِكِ النَّاسِ (٢) إِلَـٰهِ ٱلنَّاسِ (٣) مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ (٤) ٱلَّذِى يُوَسۡوِسُ فِى صُدُورِ ٱلنَّاسِ (٥) مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ (٦) 

Maajabu ni kwamba  Katika Herufi  28  za Lugha ya Kiarabu  tunakuta  Herufi    23  tu ambazo  zimetumika katika Sura Ya Kwanza (Al-Fatiha)  na 23 Katika Sura Ya Mwisho  (Al-Nas). 

Ukihesabu Herufi  Zote utakuta Herufi za Sura Ya Al-Fatiha ni   139 Na herufi za Sura Ya Al-Nas ni  80  lakini hapa ninazungumzia  ni Herufi zisizokariri. Katika  Herufi  za Sura Ya Al-Fatiha  ambazo  ni 139  kuna  23 tu peke ambazo zimejenga  Sura hii lakini kuna zaidi ya moja Kwa mfano Herufi  ya LAM  zipo  22, Herufi  ya Alif zipo 19  Na hivyo hivyo nyinginezo. Kwa hiyo  ukichukua Herufi  Moja ya LAM na Herufi Moja ya Alif na Ukifanya hivi katika  Sura Hii ya Al-Fatiha na Pia Sura Ya Al-Nas utapata kila Sura katika hizi mbili  zimetumia  Herufi  23 tu katika Herufi  28 za Lugha ya Kiarabu. Lwa kweli inashangaza. Kwa nini  Namba 23.  Namba hii siyo  Bure Bure. Namba  23 inaashiria Muda wa Ujumbe wa Mtume Mohamad ﷺ  Ujumbe au  Wahyi (Revelation) ilichukua muda wa Maiaka 23 tu. Ujumbe ulianza Mtume ﷺ alipokuwa na miaka  40 na kwa muda wa miaka  23  ujumbe alikuwa akiletewa Aya za Kuruani  mpaka alipofikia Miaka  63  akafariki dunia. Je unaona Maajabu. Yaani Kuruani aliyepewa Ujumbe alikuwa yeye mwenyewe hajui  Ghaib. Yaani hakujua kwamba Muda wa Wahyi  utakuwa miaka  23. Kuruani  ilificha habari hizi mpaka hivi  leo  mimi na wewe tunagundua haya maajabu. Je huoni  Muujiza wa kushagaza. Allahu Akbar.

Katika Maandishi ya Hapo Mwanzoni  ukihesabu Herufi  utapata  20  lakini  ukihesabu Herufi  Maandishi Ya Herufi za Othman  au Rasm  Othman  Utapata Herufi  23 kwa sababu Kuliongezwa  Herufi ya  Hamza mojawapo ni Ya Hamza yenye  Fatha na  ya pili yenye Kasra na Imetumika juu na chini ya Alif.  Iliyopo juu ya Alif

inatamkwa   “a”  kama katika neno  أَعُوذُ na Iliyopo  chini ya Alif inatamkwa  “i”  kama katika Jina  إِلَٰهِ

Na Pia Kulionegezwa  Taa Marbouta  kama vile katika neno الْجِنَّةِ   inatamkwa   “ti”

Hizi ziada  ziliongezwa kuwasaidia watu   watamke maneno haya bila makosa.

Jambo  la kushangaza ni kwamba Namba  23  ambayo  inaashiria miaka ya WAHYI  tunaipata  tena katika Aya Ifuatayo ambayo ni Aya inayowajibu Makafiri  hapo zamani walipomuuliza Mtume ﷺ  kwa nini  Kuruani  isishushwe mara moja yaani Kwa kiswahili kizuri  Kwa Mpigo mmoja.  Yaani Kwa nini ilichukua Muda wa Miaka  23?  Hebu  tuichunguza Aya Hiyo  iliyoshuka Kuwajibu Makafiri Na Muujiza Mungine wa Kushangaza.

Sura Ya Al-Furqan Namba 25  Aya Namba 32

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلۡقُرۡءَانُ جُمۡلَةً۬ وَٲحِدَةً۬‌ۚ ڪَذَٲلِكَ لِنُثَبِّتَ بِهِۦ فُؤَادَكَ‌ۖ وَرَتَّلۡنَـٰهُ تَرۡتِيلاً۬ (٣٢)

TAFSIRI

32.Na wakasema wale waliokufuru: “Mbona hakuteremshiwa Qurani yote mara moja?” Kama hivi (unavyoona tumeiteremsha kidogo kidogo kwa mpango mzuri ) ill tuuthubutishe, (tuutilie nguvu) moyo wako (kwa hizo Aya mpya mpya zinazoteremka wakati baada . ya wakati), na tumeipanga kwa uzuri.

SHEREHE 

Kuruani  ina miujiza isiyo na Mwisho  Allahu Akbar. Hebu angalia Aya Hii. Kwa kweli  utashangaa sana nikikuambia  kwamba  Aya hii pia ina Herufi  23!!!!

Yaani Mwenyeezi Mungu  aliwajibu makafiri  lakini  hata Namba zinathibitisha kwamba Wahyi (Revelation) ni Miaka 23.

Makafiri Walikuwa wanamuuliza Mtume ﷺ kwa nini  WAHYI Unashuka Kidogo kidogo Na jibu likatolewa kwa kushuka Aya hii lakini Mtume ﷺ  pia Hakujua Habari za Miaka  23  kwani ni Ghayb. Hizi tumegundua  leo hii yaani Mimi na wewe ili iwe Muujiza.  Mwenyeezi Mungu hakutaka Kumfunulia Mtume ﷺ Muda wa WAHYI  au Revelation. na  Yeye  Mtume ﷺ wakati huo  hakujua Muda utakaochukua  wa Ujumbe huo kwani ni Siri yake Mwenyeezi  Mungu. Mwenyeezi  Mungu  hawezi kutuambia Siku ya Kufariki Dunia  na hivyo hivyo  hakumwambia Mtume Mwisho wa WAHYI  na Baadaye atafariki  haiwezekani kuwa hivyo lakini Katika Aya Hii imebeba Muujiza ambao Ulifichwa kwa hekima kubwa. Leo  ndiyo tunagundua iwe Muujiza Kwetu . Allahu Akbar. Allahu Akbar. Angalia Muujiza ambao Unatupita Kipimo. Allahu Akbar.

ِAya Hii Ina Jumla ya Herufi  68 lakini  zisizokariri  ni 23 tu peke yake katika  Herufi  28 za Lugh aya Kiarabu. Kukariri  Kariri kwa baadhi ya herufi  ndiyo  inaongeza  Idadi  ya Herufi na Kuwa 68. Kwa Hiyo  Huu  ni Muujiza siyo Mdogo.  Angalia Maajabu. Suala la Makafiri lilijibiwa lakini Muda wa Miaka  23 ulikuwa Umewekwa kwa njia za Namba. Hakuna aliyejua Mpaka Leo. Sisi tunagundua  iwe Muujiza na Ituzidishie Imani na Kutuongoza. Hii ndiyo inaonyesha kwamba Muujiza wa kuruani hautakwisha Mpaka Mwisho wa Dunia na Ulimwengu. Mwenyeezi Mungu amefanya hivyo ili kuwapa imani  watu katika siku hizi za leo na baadaye. Mitume wote wamekwisha  Fariki Dunia na hakuna Miujiza  ya Kuona Kwa Macho  lakini  Kuna Kuruani Tukufu ambayo  inatupa Imani na Inashuhudia Kwamba Mwenyeezi Mungu Yupo. Allahu Akbar.

Aya Mbili zifuatazo ambazo zimeanziwa na Ibara inayosema  “Bila shaka Qurani”  

Aya hizi za mfano huu  ni Mbili tu katika Msahafu  wote. Ajabu Ni Kwamba pia zimeundwa na Herufi  23 katika Herufi  28 za Lugha ya Kiarabu.

Hii inaashiria na kuthibitisha Muda wa WAHYI wa miaka 23 kwa kweli haya siyo madogo. Kuruani Ni Muujiza Siyo Mdogo. Allahu Akbar.

Sura Ya Israa Namba 17  Aya Namba  9

إِنَّ هَـٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ يَہۡدِى لِلَّتِى هِىَ أَقۡوَمُ وَيُبَشِّرُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ ٱلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ أَنَّ لَهُمۡ أَجۡرً۬ا كَبِيرً۬ا (٩)

TAFSIRI

9. Hakika hii Qurani inaongoza katika njia iliyonyoka kabisa; na inawapa habari njema Waislamu wafanyao vitendo vizuri, ya kwamba watapata malipo makubwa (kabisa).

Sura Ya Al_Naml Namba  27  Aya Namba 76

إِنَّ هَـٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ يَقُصُّ عَلَىٰ بَنِىٓ إِسۡرَٲٓءِيلَ أَڪۡثَرَ ٱلَّذِى هُمۡ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ (٧٦)

TAFSIRI

76. Bila shaka Qurani hii inawaeleza wana wa lsraili mengi ambayo kwayo wanahitilafiana.

SHEREHE

Aya Hizi Mbili ni pekee katika Kuruani yote yaani ni Aya Mbili tu ambazo zimeanziwa na Ibara inayosema “Bila shaka Qurani”   na Ajabu Ni kwamba Pia Kila Moja ya Hizi Aya zimetumia Herufi  zisizokariri  23 tu. Huu kweli siyo  Muujiza Mdogo hata kidogo.

Aya Hizi Mbili zimeanziwa na Ibara inyosema  “Bila shaka Qurani”  yaani Kila Aya Katika Aya Hizi Mbili zimetumia Herufi  23 tu katika  Maandishi  yake.

Lakini  ukihesabu  utapata zaidi  ya herufi  23  kwani  kuna badhi ya Herufi  ambazo zimekariri.

Unapohesabu uzihesabu tu zile  zilizotumika mara moja na ukifanya hivi utapata  kila Aya imetumia  Herufi  23  tu. 

Allahu Akbar. Ni Muashirio  wa Miaka Ya Wahyi  (Revelation) Tuliyozungumza Hapa Juu.  Allahu Akbar.

Kwa hiyo  Sura Ya Israa Namba 17 Aya Namba 9 Ina jumla ya Herufi 70  lakini zisizikariri  ni 23 tu  na

Sura Ya Al_Naml Namba 27 Aya Namba 76

Ina Jumla Ya Herufi   47  lakini zisizokariri  ni  23 tu. Je unaona Maajabu?  Allahu Akbar.