SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Hesabu/Mshangao-2

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MAAJABU

1/ Herufi  Tatu  za  Mwanzo wa Sura ya ABASA (A’in,  Baa  na Sin)Namba 80. Jumla ya Kutumika kwake katika Sura hii ni  Sawa na namba ya Aya Zake?

Herufi  A’in  Imetumika katika Sura ya Abasa mara 13

Herufi  Baa  Imetumika katika Sura Ya Abasa mara 19

Herufi  Sin Imetumika Katika Sura Ya Abasa mara  10

Jumla ni  13 + 19 + 10=42

Ajabu kubwa ni kwamba Sura hii ya Abasa ina Jumla za Aya 42.  Allahu Akbar. Angalia Mpangilio wa Kiajabu. Hata Super Computer haifikii ufundi wa aina hii.

—————————-

2/Sura Ya Yasin Ni  Namba 36  na Idadi ya Aya zake ni 83.   Ukifanya  hesabu  36 x  83 utapata  namba 2988.  La kushangaza ni kwamba  Idadi ya Herufi za Sura hii ni  2988. Allahu Akbar. 

Unaona Mpangilio wa kiajabu. Leo hii kuna kitabu gani Duniani kinachohesabu Herufi mfano huu.  Hebu Fikiri. Kila  herufi katika Kuruani Imhesabiwa kimuujiza sana tena sana. Allahu Akbar.

—————————————————-

3/Herufi za Mwanzo wa Sura Ya Bakarah ambayo ni namba 2 ni  Alif, Lam na Mim.  Ajabu ni kwamba Herufi ya Kwanza kutajika kwa wingi katika Sura hii ni Alif, na Ya Pili kutajika kwa wingi ni Lam na ya Tatu kutajika kwa wingi ni  Mim.  Hebu angalia Mpangilio huu wa kimuujiza. Sura inanziwa na الم Yaani  Alif, Kisha Lam na kisha  Mim.

ِKatika Sura ya Bakarah  Kuna Herufi Alif 4213

Inayofuatia ni  Herufi  Lam   3198

Na ya mwisho  ni Mim 2192

Unaona Mpangilio wa kiajabu. Siyo bure bure bali kwa Hekima kubwa. Hata Super Computer haiwezi kupanga maneno na habaro zote na hukukuhesabu Herufi kwa mfano huu.  Allahu Akbar.

—————————————-

3/Sura Ya  Ashura  Namba 42  imetanguliwa na Herufi  zifuatazo

حم عسق كذلك يوحي اليك والي الذين من قبلك

Na Sura Ya Qaf namba 50  imetanguliwa na Herufi  َQaf 

ق والقران المجيد

ٍMwanzoni mwa Sura Hizi Mbili zinazungumzia Kuruani Tukufu.  Yaani Wahyi au  Revelation.

Sasa  la kushangaza ni kwamba Katika Sura ya Ashura  Herufi  QAF  imetumika mara  57

Na katika Sura Ya Qaf  Pia Herufi  Qaf  imetumika mara 57

Jumla  la Herufi hizi mbili ni  57  + 57=114

Je unaona Muujiza?  Sura mbili zinazungumzia Kuruani  na Ukijumlisha Herufi  QAF  ambayo pia ni ya kwanza katika Neno  Quran  yaani Kuruani unapata idadi ya Sura za Kuruani tukufu ambazo no 114.  Allahu Akbar.  Unaona Muujiza ambao sio  mdogo. Kwa kweli haya yanatosha kutuzidishia imani. Na pia wasio Waislamu. Muujiza mbele yetu. Allahu Akbar.  Hizi Herufi zimehesabiwa na Mwenyeezi Mungu. Hakuna Binaadamu anayewweza kufanya hivi hata kidogo asikudanganye mtu yeyote.  Tufumbue macho na Tusilale. Allahu Akbar.