SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Kuruani Kwa Ufupisho

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

HISTORIA FUPI YA KURUANI TUKUFU

Salaam Nyingi kwa Wasomaji wa Website hii.

Alhamdulilah  Nashukuru Mwenyeezi Mungu kwa kunipa  uwezo siku ya leo Tarehe  11 September 2022  Jumapili Jioni kuweza kuandika machache kuhusu  Historia Fupi Ya Kuruani.  Kuna Habari nyingi na Mbalimbali za Kuzungumza lakini nimeona bora Nigusie machache kuhusu Historia Fupi ya Kuruani Tukufu. Lengo langu siyo kuelezea Tarehe kwa Tarehe kuanzia Kushuka kwa Aya za Kuruani mpaka mwisho kwani hiyo Mwenyeezi Mungu akinipa uzima ningependelea kuandika katika Mlango  wa “HISTORIA YA UISLAMU” ambao bado sijaumaliza na hapo ndipo ningependelea kuandika Historia Ya Kuruani kwa njia hii lakini siku ya leo ningependelea kuelezea tu tofauti ya Maneno kama vile   “Versions”, “ManualScript” ,”Quran Recitations” na  “Quran Huruf”  kwani nimeona tofauti ya Maneno haya yatasadia kutupa mwanga zaidi katika  kuelewa Historia ya Kuruani Tukufu. Maneno  haya siyo madogo bali yameleta  Utatanishi  Mkubwa katika Uislamu na Pia kuwapa  wale wasiojua  Uislamu  njia ya Kupitisha Uongo na hila katika kuuvuruga Uisamu. Kwani  Ukweli ni Ukweli na Huwezi Kudanganya watu kwa Uongo. 

Versions au Toleo kwa Kiswahili katika Maandishi lina maana yake ni  Kitabu kilichoandikwa na Mwandishi na kisha akakiandika Tena baada ya  Masahihisho  kwa kuzidisha au kupunguza na kwa hiyo Versions hazifanani. Na iwapo mwandishi  huyo ataandika kitabu chake hicho  mara kumi  basi  Versions zake zote zitakuwa tofauti kwani kila version au Toleo litakuwa limekuja na ziyada au upungufu  wa alichoandika.

Manuscript  maana yake ni Maandishi ya Mkono. Kwa hiyo unaweza kukuta Manuscript mbalimbali za  Toleo au Version Moja. Neno  Manu ni kifupi cha neno Manual  na maana yake ni  Kwa mkono  na Neno Script ni Herufi zilizotumika katika Kuandika na kwa hiyo  ManuScript maana yake  Maandishi Ya Mkono  au Mashine ya kuandikia kwa kutumia Herufi. ManuScript inaweza kuwa kwa lugha yeyote. Kwa mfano Manuscript ya Kiswahili au Kiarabu au Kiingereza au Kifaransa au Kijerumani au Kihindi au Kiyahudi au Lugha yeyote Duniani.

Biblia za zamani  sana zipo  Versions Mbalimbali na ningependelea kuzipanga kufuatana na Miaka. Biblia hizi siyo  zote ambazo zimekamilika bali nyinginezo ni badhi tu ya Vitabu au Kurasa na Kwa hiyo zote zimetofautiana na hivi ndivyo Wakristo  wanavyotufundisha na siyo Waislamu. Siwezi kuzitaja Versions zote bali chache tu. kwa mfano:

Wanatufundisha kwamba Hivi karibuni walivumbua  SCROLLS  kama vile 

1/VERSION YA KETEF HINNOM SCROLLS. Wanadai kwamba haya ndiyo maandishi ya BIBLIA  ya zamani sana yaani katika karne ya 600  kabla ya Ukristo na kwa hiyo ni maandishi ya Nabii  Musa au  Agano la Kale.

2/VERSION YA DEAD SEA SCROLLS  ambayo  inadaiwa kwamba iliandikwa mwaka c. 150 BCE – 70 CE

Herufi  C  yaani Century “Karne” na BCE  yaani Kabla Ya Ukristo  na CE  yaani Kipindi cha Ukristo.  Sasa ngojea nikupangie Versions  zilizofuata  yaani Baada Ya SCROLLS  hizi  mbili.

3/Version ya Septuagint  Nitazitaja mbili  hapa chini

1/Codex Vaticanus 2nd century BCE (Vipande Vya Makaratasi)

na  2/ Version ya Codex Sinaiticus 4th century CE (Iliyokamilika)

Huu ni mfano  tu wa Baadhi ya Vitabu  Vya Toleo Mbalimbali za Biblia za Zamani kwani kuna zaidi ya hizi nilizozitaja.

Tusichanganye na Kuruani kwani  Kuruani ni Version au Toleo Moja tu. Hakuna Versions katika  Kuruani. Huu ndio ukweli.  Kuruani ya Leo ni ile ile ya Karne ya 7 hakuna Tofauti.

Lakini kuna Maandishi ya mkono mbalimbali yaani Manual Script na Haya maandishi ukichunguza utakuta hakuna tofauti  na Kuruani ya Mwanzo. 

Wasiojua wanachanganya na kudhani  Script mbalimbali zilizopo ni Versions na kwa hiyo  Kuruani zinatofautiana ukisema hivyo basi unapotosha. 

Kuna Tafsiri  au Translations za kuruani mbalimbali. Zile za Kiarabu kwa kiarabu ni Tafsiri ya Kufafanua Aya za kuruani na Zile za Kugha Nyinginezo  kama vile  Tafsiri ya Kuruani iliyoandikwa na Yusuf Ali kwa kiingereza ni  Kuwasaidia wasiojua Kiarabu waielewe Kuruani na hivyo hivyo lugha nyinginezo. Kwa hiyo Tafsiri  siyo Version hata kidogo bali ni  Tafsiri ya Kutoka Lugha moja na kwenda lugha nyingine.

Kuna Visomo  vya kuruani mbalimbali. Kuna Visomo  Saba na kuna  Wanavyuoni wanaosema kwamba Kuna  Visomo ni Kumi. Na kila kisomo  kinatofautiana na Kingine katika Matamshi ya maneno.  Katika Upande wa linguistic, lexical, phonetic, morphological and syntactical forms. Tofauti ya visomo hivi kumi ni ndogo na inakusanya  tofauti ya sheria zinazohusiana na prolongation, intonation, and matamshi ya maneno lakini tofauti katika vituo “stops”, vowels, na consonants (Na kusababisha tofauti ya pronouns na verb forms), na siyo  kubadili Maana ya Maneno au Aya. Yaani tofauti ya Visomo hivi ni Matamshi tu na haibadili maana ya Maneno, Aya au Sura. Na hili ni jambo  zuri kwani Tofauti hii inatusaidia sisi wageni katika Matamshi ya Lugha hii  kwani siyo wote tunaozungumza Lugha Kiarabu.

Kuruani  hakuna Versions au toleo mbalimbali. na hakuna kilichofichwa. Kwa vile Kuruani ilishushwa katika mifumo Saba za makabila ya Kiarabu (saba) katika Enzi ya Mtume Mohamad hapo baadaye  ilibidi uchaguliwe mfumo mmoja tu yaani Standard  Language ili iwe inawakilisha Kuruani iliyokuja kwa lugha saba. Lugha ilityochaguliwa ni ile ya Kabila la Mtume  yaani  Kikureish.  Na ilimbidi  Amiri au Khalifa  Othmani Ibn Affan afanye hivyo kwani  Kuwepo kwa Kuruani katika lugha saba ingeleta matatizo na hivi ndivyo ilivyoanza kwani kila kabila lingesema Kuruani ya kabila langu ni bora kuliko Kuruani ya kabila nyingineyo. 

Kuruani  ni  Version Moja tu lakini  visomo  vipo  mbalimbali vilivyozaliwa kutokana na Mifumo (Ahruf) ile saba na Kuwepo kwa visomo mbalimbali  inasaidia watu duniani kwani lugha za dunia zipo mbalimbali pia  na matamshi ya lugha za dunia yanatofautiana na kwa hiyo inakuwa rahisi  kwa wageni  kuchagua Kisomo  kilicho Rahisi  kufuatana na Matamshi aliyozoea katika Lugha yake ya Asili lakini visomo au mifumo hiyo lazima zisipingane na Kuruani ya Standard iliyopitishwa na Kiongozi Othman Ibn Afan ambaye alifanya juhudi kubwa ya kuandaa Kurfuani moja na kuziodoa nyinginezo ambazo ijapokuwa zilikuwa sahihi na zilipokelewa na Mtume lakini ilikuwa bora wachague Kuruani moja tu ambayo itawakilisha nyinginezo. Lakini hapo baadaye miaka ikiyofuata kulizuka Visomo (Qiraat) nyinginezo 10 ambazo baadhi yake zinatumika mpaka leo katika baadhi ya mataifa ya kiislamu duniani.

Katika  Mlango  Huu ningependelea  kutaja Vile Visomo  Kumi  Vya Kuruani, Walimu wake na Waliotangaza Visomo Hivi.Yaani  QARI au Reader na  RAWI au Tramsmitter. Na  Kisha  Pia kuzitaja  Zile Manuscript za Kuruani ambazo Zilivumbuliwa na Kwa hivi sasa zimehifadhiwa katika  Sehemu Mbalimbali za Dunia. Ningependelea pia Kuwaletea  Picha za Manuscript Hizi.  

Jambo  muhimu la kuelewa ni kwamba  Kuruani ni  Ujumbe aliopewa Mtume Mohamad  kama vile Taurati aliyopewa Nabii Musa. 

Mafundishi ya Nabii  Isa yaliandikwa na Wengine na Siyo Revelation au Wahyi kama vile Kuruani au Tourati  na Pia hakuandika  Nabii Isa Mwenyewe. Yaani Nabii Isa Hakuwa Messenger bali alikuwa Mtume. 

Musa na Mohamad  walikuwa Messengers na Watume pia.

Maandishi kuhusu Nabii Isa Yamepewa Jina katika kuruani  “Injili”  na Kitabu cha Asili cha Injili  tunakiamini hakuna Tatizo kwani Hata  Kuruani imekitaja.

Tatizo  ni kwamba  Baada ya Kupita Muda Maandishi haya Yaliharibiwa kwa kubadilishwa, Kuongeza na Kupunguza na ndiyo maana Mwenyeezi Mungu akashusha Kuruani ili kuwarudisha  watu katika ukweli na wasipotee. kwa hiyo tuwe macho. Na huu ndiyo ukweli 

INAENDELEA HIVI KARIBUNI…………………………..