UTAFITI MBALIMBALI KATIKA DINI NA SAYANSI
IMEANDALIWA NA AL-AMIN ALI HAMAD
Alhamdulilah leo ni Jumamosi Tarehe 03/09/2022. Nashukuru Mwenyeezi Mungu kwa kutupa Uhai na Afya ya kuweza kuandika machache ambayo lengo ni Kumtukuza na Kufuata anayotaka yeye na siyo tunayotaka sisi.
Kwa furaha na hamu kubwa leo hii ninapendelea kutumia kila Dakika na Sekunde katika kuandika Makala hii.
Ninashika Kalamu na kuanza Kuandika Yafuatayo:
Watalamu wa hali ya hewa wanasema kwamba leo kutakuwa na Mvua lakini katika wakati huu wa Saa Tano Asubuhi naona bado Jua Limechomoza na Ni Zuri Mno na kwa hiyo Huenda Wataalamu hao wamepotea na hakutakuwa na mvua. Kwa kweli Wataalamu ni Hodari wa kukisia lakini si hodari wa kusababisha. Mwenyeezi Mungu peke yake ndiye anayejua Kushuka kwa mvua kwani yeye ndiye anayepeleka Mawingu sehemu atakazo mvua ishuke. Na Kuruani Imethibitisha Hayo.
Katika Mlango huu nitagusia Habari ya Fedha na Mabenki ili kukumbushana Maamrisho ya kuruani kuhusiana na Riba.
Jina la Website hii ni UISLAMUNASAYANSI na Kwa hiyo pia Tunaweza kusema kwamba Tutakachozumzia hapa ni Sayansi ya Harakati za Mabenki na Mizunguko ya Fedha.
Katika Kiingereza na Kiarabu tunaweza pia kusema ni
Islamic banking, Islamic finance (Arabic: مصرفية إسلامية), or Sharia-compliant finance.
Uislamu haukubakiza Elimu yeyote inayohusiana na Maisha. Kila Chenye Uhusiano na Maisha kimefundishwa na Kuruani na Pia Kufafanuliwa na Hadithi a Mtume Mohamad.ﷺ
Uislamu unatufundisha uhusiano wa Binaadamu katika mishughuliko ya Biashara, Mizunguko ya Fedha baina ya Binaadamu kwa njia ya Halali.Kuruani na hadithi za Mtume Mohamad zimekuja na Misingi ya Maingiliano ya binaadamu katika Harakati za Maisha ya kila siku.
Uislamu haukuachia watu wauziane vitu bila mpango wowote, au kukopeshana bila ya mpango wowote bali kuna sheria ambazo lazima kuzifuata.
Kwa mfano Ukiuza kitu chochote basi uhakikishe kumfahamisha anayenunua sifa zote za kile unachokiuza. Usiuze kitu kwa kukisifia kwamba kizuri sana lakini umeficha mengineyo. Kwa mfano siuze Gari ukalisifia kwamba ni zuri sana lakini kuna Tatizo lingine ambalo umelificha. Kwa kifupi usidanganye. Mfano mwingine mzuri usiuze Maziwa na huku umechanganya na maji na hali kwamba mnunuzi hajui uliyoficha. Ndugu Waislamu tuwe macho sana jambo hili kwani ni aina Ya Wizi mbaya. Katika Maingiliano ya kibiashara lazima Tuwe wakweli na Riziki itakayopatikana inakuwa na Baraka. Tusile vya haramu kwani Vinaleta Maradhi.
Ndugu Waislamu wamezungumzia Elimu hizi kwa muda mrefu. Majadiliano na Mabishano mengi yamefanyika kuhusu RIBA. Tatizo kubwa ni Tafsiri ya neno RIBA. Waislamu wengi Waliosomea Elimu hizi za Fedha wamekubaliana kwamba neno RIBA ni INTEREST na kwa hiyo yaliyokatazwa katika Kuruani ni INTEREST yaani hii ndiyo RIBA.
Kwa lugha Rahisi imekatazwa na kuharimishwa kukopesha au kukopeshwa Fedha kwa njia ya RIBA. Hebi nitoe mfano hapa Chini ili RIBA ieleweke vizuri.
MFANYA BIASHARA=HABARI BWANA
BENKI=NZURI
MFANYA BIASHARA=NATAKA MKOPO WA FEDHA
BENKI=HAKUNA TATIZO JE KIASI GANI?
MFANYA BIASHARA=LAKI 36
BENKI=HAKUNA TATIZO. WEWE NI MTU MUAMINIFU NA UNAJULIKANA NA KWA HIYO HAKUNA TATIZO TUTAKUPA
MFANYA BIASHARA=ASANTE SANA BWANA
BENKI=UNGEPENDELEA KULIPA DENI HILI KWA MUDA GANI?
MFANYA BIASHARA=IKIWEZEAKANA MIAKA MITATU
BENKI= SAFI. SASA TUFANYE HISABU.
1/KWANZA KUNA INTEREST YA ASILIMIA 2 YA HIZO LAKI 36 KWA HIYO INTEREST ITAKUWA SHILINGI ELFU 72 KILA MWEZI.
2/NA CAPITAL YA PESA UNAZOKOPA NI MALIPO YALAKI MOJA KILA MWEZI
3/KWA HIYO UTALIPA KILA MWEZI NI LAKI MOJA NA ELFU 72
KWA HIYO LAKI MOJA NI DENI NA ELFU 72 NI INTEREST YAANI GHARAMA YA MKOPO WAKO. JE UNAKUBALI?
MFANYA BIASHARA=ASANTE SANA BWANA. KWA KWELI SINA BUDI BALI KUCHUKUA KWANI NINA SHIDA NA NINAHITAJI SANA FEDHA.
BENKI=KWA HIYO NDUGU MWISHO WA MWAKA WA TATU DENI LAKO LITAKUWA LIMEKWISHA NA WEWE UTAKUWA UMELIPA JUMLA YA FEDHA NI LAKI 61 NA ELFU 92 JE MAMBO SAFI
MFANYA BIASHARA=SAFI SANA BWANA.
BENKI=LAKINI KUNA MASHARTI. LAZIMA ULIPE KILA MWEZI KWANI USIPOLIPA BASI UNAWEZA KUNYANGANYWA BIASHARA AU NYUMBA YAKO AU CHOCHOTE KILE KISHA KIUZWE NA ITUMIKA KATIKA KULIPA DENI LETU.
MFANYA BIASHARA=NIMEFAHAMU. ASANTE SANA HAYO YOTE NINAYAELEWA.
——————–
Kama tulivyoona INTEREST hapa juu ilivyokuwa kubwa. Yaani mkopaji anataka laki 36 na baada ya miaka Mitatu atakuwa amelilipia deni hilo Asilimia 2 ya pesa hizo yaani 2% ya Laki 36 na jumla atakuwa amelilipa deni hilo na gharama zake zote ni Laki 61 na Elfu 92
yaani RIBA ambayo inajulikana kama Interest ni karibu nusu ya Deni hili. Mfanya Biashara amekopa Laki 36 na atalilipa deni hili mara mbili yake. Hebu fikiri kidogo.
Mfanyi biashara amekopeshwa pesa na anapofeli kulilipa basi atanyang’anywa alichonacho kama vile biashara yake au nyumba au cochote alichonacho na kisha alipie gharama hizo.kwa kweli hii hatari kubwa. Yaani hakuna ubinaadamu wowote. Benki haiangalii matatizo yako kama umepata faida au hasara katika biashara yako na kwa hiyo kutaweza kulipa deni hilo bali Benki wanataka deni lao na faida tu yaani hakuna ubinaadamu au udugu au huruma yeyote. Yaani Benki haiangalii yaliyokupata katika Biashara yako bali wanaangalia fedha zao tu.
Sasa umeona Hatari za RIBA au Interest na ndiyo maana Mwenyeezi Mungu akakataza RIBA ili kumsaidia Kiumbe chake. Imeharimishwa kabisa hakuna utani na mwenyeezi Mungu amesisitiza kwamba atampiga vita yule atakayechukua RIBA.
Wataalamu wa Kiislamu wamekuja na Mbinu mbalimbali ili kujiepusha na Bidhaa za Mabenki duniani. Wametafuta mbinu ili Mabenki pia washiriki katika Hasara. Yaani Mkopaji na Mkopeshaji washiriki katika Heri na Shari au katika Faida na Hasara. Na hii inajulikana katika Elimu ya Fedha kama “Profit and Loss Sharing”.
Huu Mfano wa Mazungumzo baina ya Mfanya Biashara na Benki pia katika Manunuzi ya Kila kitu. Kwa mfano Ukinunua Gari na Kulipa hapo hapo bila ya Deni inakuwa hakuna Tatizo kwani umenuua kaka kawaida na umelilipia Bila ya Kuongeza Riba yeyote lakini ukilipia kidogo kidogo yaani Installements kila mwenzi kwa muda mtakaowafikiana basi kutakuwa na RIBA kwani Muuzaji anakuwa amekukopesha na Anaongeza gharama za Interest katika Bei ya gari hilo. Ukishindwa kulilipia Gari hilo basi litataifishwa na Muuzaji. Ukinunua Gari kwa mkopo basi utalilipia zaid ya Bei ya gari hilo. Kama ni Milioni 10 basi mwisho wa Installement utakuwa umelilipia Milioni 15. MIlioni 5 hapa ni RIBA. kwa hiyo tuwe macho sana katika Maisha na tusione kwamba mambo haya ni mazuri.
Kama tulivyosema kuna mbinu mbalimbali za kutatua tatizo hili. Kuna Benki mbalimbali za Kiislamu na hata ambazo siyo za Kiislamu hivi sasa wameanza kujiepusha na RIBA ili kuwavutia Waislamu na pia wameona Ukweli kwamba RIBA siyo kitu kizuri na hivyo hata wasiokuwa waislamu wanapendelea kujiepusha na RIBA.
Hebu nitoe mfano wa Benki ya Kiislamu na Mnunuzi ili tupate kufahamishana vizuri.
MNUNUZI=Habari Bwana
MUUZAJI AU BENKI YAKIISLAMU=Nzuri. Karibu
MNUNUZI=Ningependelea kununua Gari lakini sina Fedha za kutosha. Nimekuja kuwaomba mnisaidie Mkopo wa milioni 36
MUUZAJI AU BENKI YAKIISLAMU=Hakuna Tatizo. Benki yetu inafuata Sheria Ya Kiislamu na kwa hiyo tunajiepusha na RIBA. Na ili tuweze kukusaidia sisi pia tuna Gharama zetu. kwa hiyo Tutanunua Gari lako na kisha tutakuuzia kwa kukukodishia wewe kwa Milioni 38 yaani Milioni mbili ni faida yetu na ndiyo itatuwezesha kulipa Gharama zetu pia.Tutakukodishia ulipe kidogo kidogo kufuatana na muda ambao tutakubaliana baina yetu. Je unakubali Biashara hii? Yaani Sisi tutanunua Gari hilo kutoka katika Kiwanda na kisha Tutakuuzia kwa Kukukodishia kwa faida. Na kisha Utatulipa Kwa muda tutakaokubaliana baina yetu na wewe. Na siku utakapomaliza Deni basi Gari litakuwa lako. Yaani Wewe utakuwa Mnunuzi na Sisi Wauzaji. Angalia Bwana. Tunafanya hivi ili kujiepusha na RIBA yaani Interest. Kama ukilinganisha na Mabenki yasiyokuwa ya Kiislamu utaona Watakukopesha na kisha Wataongeza Asilimia Ya Pesa katika Mkopo wako.
Sisi tutakuwa Wauzaji na kwa hiyo ukiwa na Tatizo kulipa deni tutatafuta Njia ya Usalama kwani tunajua Maisha yalivyo. Ukitaka kulilipa lote au baadaye au kila mwezi basi tunaweza tukapanga baina yetu, Tupange ili wewe na sisi tusiwe katika tatizo. Ukipata Hasara au Faida basi ni sisi sote na siyo wewe tu au sisi tu pekee. Je umefahamu
MNUNUZI=Ahsante sana. Sasa je Mpangilio huu au System hii inaitwa kwa jina gani?
BENKI YA KIISLAMU=Inaitwa “IJARAH Hii ni mbinu moya ya kujiepusha na RIBA kwani Tumeamrishwa katika Dini ya kiislamu (Kuruani na Hadithi za Mtume) tujiepushe na RIBA lakini Biashara ni Halali na ndiyo maana hatuongezi Gharama zetu kwa njia ya RIBA Yaani Interest bali tunakuuzia kwa Faida ili tupate faida sote wewe upate Gari na sisi tupate hizo Milioni Mbili. Na iwapo Gari lako limeharibika lenyewe bila ya kosa lako basi wakati ule bado lipo katika matengenezo hutatakiwa ulipe malipo yoyote. Na ikiwa una matatizo Mengineyo na huwezi kulipa Deni lako kwa muda maalum kama tulivyoahidiana basi utasamehewa wakati huo mpaka upate fedha na kisha ulipe lakini kuna masharti ambayo tutakufahamisha.
Je umefahamu?
MNUNUZI= Ahasante sana nimefahamu. Kwa kweli kuna Misamiati mingi ambayo inatatanisha. MURABAHA, MUSHARAKAH AU MUDARABAH. NA mingineyo chungu nzima.
BENKI YA KIISLAMU=Ndugu kwa kweli Kuruani imeshusha Aya Chache zenye kutukataza tusichukue au kulipa RIBA na pia kuna Hadithi za Mtume pia Chache lakini karne hii ya leo imekuja na mambo mbalimbali ambayo hayakuweko wakati huo wa Mtume na kwa hiyo Waislamu wamejitahidi kuja na Mbinu mbali mbali za kujiepusha na RIBA na ndiyo maana Misamiati imekuwa mingi. MIsamiati au Mbinu hizi hazikuweko wakati wa Mtume bali imeundwa hivi karibuni.
MNUNUZI=Kwa nini Waislamu wameunda na kuja na mambo mapya ambayo hayakuwako wakati huo. kwa kweli Tunababaika
BENKI YA KIISLAMU-=Usibabaike Ndugu. Maendeleo ya kileo yamesababisha Wanavyuoni wa Kiislamu kuja na Mbinu mbalimbali ili Sheria za Kuruani zifuatwe. Usibabaike na Misamiati. Sheria Ni Moja nayo ni kujiepusha na RIBA na Pia kuna aina za RIBA mbalimbali. Hadithi za Mtume zimeelezea vizuri sana Tofauti zote hizi. na pia Biashara na Maingiliano ya Binaadamu na Fedha zimesababisha Kuweko kwa MISAMIATI mbalimbali ili tupate kuelewa tofauti ya Vipengele vya Elimu hii. kwa hiyo usibabaike. Mabenki yamekuja na bidhaa au Mikopo pia ya aina mbalimbali na kwa hiyo Wataalamu wa Kiislamu wamekuja na Elimu mbalimbali zenye MISAMIATI mbalimbali ili kuwianisha na Bidhaa au Mikopo ya aina hizo. Kwa hiyo ukitaka kununua Bidhaa yeyote ambayo ipo katika Njia ya RIBA basi ujue kwamba Wanavyuoni Waislamu wameshatafuta Alternative au Bidhaa Ya kiislamu isiyo na RIBA na ambayo ingependelea ununue Bidhaa hiyo kwa njia ya Kiislamu yaani ujiepushe na ile ya RIBA na usije ukasema nimenunua bidhaa hii yenye RIBA kwa sababu Waislamu hawana au bado hawana.
MNUNUZI=Ahsane sana bwana kwa maelezo na msaada wako mzuri. Mwenyeezi Mungu akubariki.
BENKI YA KIISLAMU=Amin
Katika Mfano nilioutoa hapa juu ni Mkopo wa Kununua Kitu unachohitaji kama vile Gari. Kuna Mikopo ya aina Nyingi. Kwa mfano Ukitaka Pesa kwa mahitaji ya haraka kama vile unaumwa na unataka pesa ili umlipe dakitari au chochote kile basi Benki ya kiislamu pia wanafuata Sheria ya kiislamu katika kukukopesha. Utakopeshwa lakini hutatakiwa kulipa RIBA yoyote.
Katika Benki isiyokuwa ya Kiislamu pia wanakopesha lakini wanahitaji ulipe RIBA yaani Interest. kwa mfano ukihitaji Laki 5 basi kwa muda mtakaowafikiana kulipa itabidi uongeze pesa za Interest juu ya hizo laki 5 yaani mwishowe utakapomaliza deni utakuwa umelipa zaidi ya laki 5.
Benki ya kiislamu hawataki ulipe ziyada yeyote lakini lazima uweke Rehani ambayo utakaposhindwa kulipa deni lako na baada ya kupewa muda wa kuhurumiwa kwisha basi watakujuulisha kwamba hakuna budi isipokuwa watauza Rehani uliyoweka na kisha watachukukua deni la Benki na wewe utapewa masalia yaani kitakachobaki. Kwa hiyo kuna Utu katika maingiliano baina ya mkopaji na Benki ya kiislamu. Kuna Huruma na kukusaidia bila ya malipo yeyote. Lakini uwe macho kwani ukishindwa kulipa deni lako basi unaweza kupoteza Rehani yako pia.
Mikopo ipo mbalimbali. Ukitaka mkopo wa kununua nyumba pia Benki ya kiislamu inaweza kukupa mkopo unaojulikana kama Musharaka Al-Mutanaqisa au kwa kiingereza inajulikana kama DIMINISHING MUSHARAKA na aina hii pia ina maelewano baina ya mkopa na mkopwa. Watashirikiana kununua nyumba. Kwa mfano Mnunuzi atatoa aslimia 30 na Benki ya kiislamu itatoa asilimia zilizobakia yaani 70 na kisha baada ya hapo mnunuzi ataendelea kuilipa Benki Installements (Gharama za Kodi + Gharama za Kununua hiyo Asilimia 70) kwa muda watakayowafikiana bila ya Benki kuongeza RIBA na baada ya muda kwisha Nyumba itakuwa ya mnunuzi.
Wataalamu wa kiislamu wametafuta mbinu mbalimbali katika kutatua Tatizo la RIBA katika Mataifa ya kileo na Uchumi wa kisasa. Yaani Uislamu unakwenda na wakati. Hakuna Tatizo. Uislamu ni dini Dynamic yaani yenye Uhai. Dini hii Inakubaliana na Mazingara na Wakati wowote Tangu karne ya 7, Kuja kwa Uislamu mpaka Mwisho wa Dunia.
AYA ZA KURUANI NA HADITHI ZA MTUME MOHAMAD ZINAZOHUSU RIBA
Jumapili Tarehe 04/09/2022. Alhamdulilah leo nitaendelea na kazi niliyoianza jana. Je tutafika huko? Sijui kwani kuna mengi na siyo rahisi. Hebu nijaribu…..
Sasa Nitakusanya hapa chini Aya za Kuruani na hadithi za Mtume na Tafsiri zake na Kisha tutaekdelea na Sherehe kuhusiana na Elimu hii ambayo ni Kubwa.
Mwenyeezi Mungu anaelewa kwamba binaadamu anapenda Mali na kwa hiyo Aya zilizoshuka kukataza RIBA zilishushwa kwa hekima kubwa yaani kukatazwa kidogo kidogo. Hatua kwa hatua. Hazikushushwa Mara Moja bali Step By Step. Kwani watu wakati huo walizama katika biashara hii na walijitajirisha kwa njia hii. Siyo Rahisi kumuamrisha mtu aache kitu haraka haraka na ndiyo maana Ilikuwa Step By Step. Aya za mwanzo hazikuwa na Maamrisho makali ya kukataza RIBA baadaye Kila Aya ifuatayo ilikuwa ikihimiza kwa nguvu zaid Kujiepusha na RIBA na ukiangalia Aya ya mwisho utaona Amrisho ni Kali zaidi. Katika Aya ya mwisho Mwenyeezi Mungu anasema kwamba Yeye mwenyewe atampiga Vita mwenye kujishirikisha na RIBA.
1/Sura Namba 30 Aya Namba 39
وَمَآ ءَاتَيۡتُم مِّن رِّبً۬ا لِّيَرۡبُوَاْ فِىٓ أَمۡوَٲلِ ٱلنَّاسِ فَلَا يَرۡبُواْ عِندَ ٱللَّهِۖ وَمَآ ءَاتَيۡتُم مِّن زَكَوٰةٍ۬ تُرِيدُونَ وَجۡهَ ٱللَّهِ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ هُمُ ٱلۡمُضۡعِفُونَ (٣٩)
TAFSIRI
39.Na zile (pesa za kukopeshea) riba mtoazo (katika kuwakopesha watu) ili zizidi katika mali ya watu, mbele ya Mwenyezi Mungu hazizidi (pesa hizo; bali zinaingia nuhusi na shakawa); lakini (mali). mnayoyatoa kwa ajili ya Zaka kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi hao (wenye kufanya haya) ndio wazidishao (mali zao).
2/Sura Namba 4 Aya Namba 161
وَأَخۡذِهِمُ ٱلرِّبَوٰاْ وَقَدۡ نُہُواْ عَنۡهُ وَأَكۡلِهِمۡ أَمۡوَٲلَ ٱلنَّاسِ بِٱلۡبَـٰطِلِۚ وَأَعۡتَدۡنَا لِلۡكَـٰفِرِينَ مِنۡہُمۡ عَذَابًا أَلِيمً۬ا (١٦١)
TAFSIRI
16 Na kwa (sababu ya) kula kwao riba, na hali wamekatazwa wasile, na (kadhalika) kwa kula kwao mali za watu kwa batili. Basi tumewaandalia makafiri-nao ndio wao–adhabu iumizayo.
3/Sura Namba 3 Aya Namba 130-132
3/يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَأۡڪُلُواْ ٱلرِّبَوٰٓاْ أَضۡعَـٰفً۬ا مُّضَـٰعَفَةً۬ۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ (١٣٠) وَٱتَّقُواْ ٱلنَّارَ ٱلَّتِىٓ أُعِدَّتۡ لِلۡكَـٰفِرِينَ (١٣١) وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ لَعَلَّڪُمۡ تُرۡحَمُونَ (١٣٢)
TAFSIRI
130. Enyi mlioamini! Msile riba, mkizidishazidisha; na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kutengenekewa.
131. Na ogopeni moto ambao umewekewa wenye kukanusha amri za Mwenyezi Mungu. (Na katika hizo ni huku kutokula riba).
132.Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemewa
4/Sura Namba 2 Aya Namba 275-281
ٱلَّذِينَ يَأۡڪُلُونَ ٱلرِّبَوٰاْ لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ ٱلَّذِى يَتَخَبَّطُهُ ٱلشَّيۡطَـٰنُ مِنَ ٱلۡمَسِّۚ ذَٲلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡبَيۡعُ مِثۡلُ ٱلرِّبَوٰاْۗ وَأَحَلَّ ٱللَّهُ ٱلۡبَيۡعَ وَحَرَّمَ ٱلرِّبَوٰاْۚ فَمَن جَآءَهُ ۥ مَوۡعِظَةٌ۬ مِّن رَّبِّهِۦ فَٱنتَهَىٰ فَلَهُ ۥ مَا سَلَفَ وَأَمۡرُهُ ۥۤ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَنۡ عَادَ فَأُوْلَـٰٓٮِٕكَ أَصۡحَـٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيہَا خَـٰلِدُونَ (٢٧٥) يَمۡحَقُ ٱللَّهُ ٱلرِّبَوٰاْ وَيُرۡبِى ٱلصَّدَقَـٰتِۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ (٢٧٦) إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَوُاْ ٱلزَّڪَوٰةَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ (٢٧٧) يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَذَرُواْ مَا بَقِىَ مِنَ ٱلرِّبَوٰٓاْ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ (٢٧٨) فَإِن لَّمۡ تَفۡعَلُواْ فَأۡذَنُواْ بِحَرۡبٍ۬ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦۖ وَإِن تُبۡتُمۡ فَلَڪُمۡ رُءُوسُ أَمۡوَٲلِڪُمۡ لَا تَظۡلِمُونَ وَلَا تُظۡلَمُونَ (٢٧٩) وَإِن كَانَ ذُو عُسۡرَةٍ۬ فَنَظِرَةٌ إِلَىٰ مَيۡسَرَةٍ۬ۚ وَأَن تَصَدَّقُواْ خَيۡرٌ۬ لَّڪُمۡۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ (٢٨٠) وَٱتَّقُواْ يَوۡمً۬ا تُرۡجَعُونَ فِيهِ إِلَى ٱللَّهِۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٍ۬ مَّا ڪَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ (٢٨١)
TAFSIRI
275.Wale wanaokula riba, hawasimami (kuendesha yao) ila kama anavyosimama yule ambaye Shetani kamzuga kwa kumsawaa; (wako mbioni tu, hawana kituo). (Na) haya ni kwa sababu wamesema, “Biashara ni kama Riba”, bali Mwenyezi Mungu · ameihalalisha biashara na kaiharimisha riba. Na aliyefikiwa na mauidha kutoka kwa Mola wake (ya huku kukatazwa riba), kisha akajizuia, basi yamekwisha mthibitikia yale (mali) yaliyopita (aliyokwisha yapata); na hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Lakini wanaorejea (kula riba) basi hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele.
276. Mwenyezi Mungu huyafutia (baraka mali ya) Riba: na huyatia baraka (mali yanayotolewa) sadaka. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila kafiri (na) afanyae dhambi.
277. Hakika wale walioamini na kufanya vitendo vizuri na kusimamisha Sala na kutoa Zaka, wao watapata ujira wao kwa Mola wao, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
278. Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na acheni yaliyobakia katika riba, ikiwa mmeamini.
279. Na kama hamtafanya (hivyo), basi fahamuni mtakuwa na vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkiwa mmetubu, basi mtapata rasilimali zenu; msidhulumu wala msidhulumiwe.
280. Na kama (mkopi) ana dhiki, basi (mdai) angoje mpaka afarijike. Na kama nyinyi (mnaodai mkizisamehe deni zenu) mkazifanya sadaka, basi ni bora kwenu. Ikiwa mnajua haya (basi fanyeni).
181. Na iogopeni Siku ambayo mtarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha viumbe wote watalipwa kwa ukamilifu yote waliyoyachuma; nao hawatadhulumiwa
SHEREHE
Kufuatana na Aya tulizozinukulu hapa juu utaona kwamba Riba imeharimishwa na Mwenyeezi Mungu ameahidi kumpiga vita mwenye kuchukua au kutoa Riba. Riba maana yake Ziyada au Kukua. Ni tamaa ya Kujitajirisha kwa njia hii ya Kutaka ziyada kutoka kwa Mhitaji. Ni Kinyume na Sadaka. Sadaka ni kusaidia na huku unatarajia ujira kutoka kwa Mwenyeezi Mungu lakini Riba ni kutarajia Malipo ya Mali peke yake. Mwenyeezi Mungu amepiga vita RIBA lakini amehimiza Biashara. Amemlaani Anayejishirikisha na Biashara kama hii. Kwa hiyo tuwe macho sana kwani kama Tulivyosoma Aya hapa juu Mwenyeezi Mungu ameamua Kumpiga Vita Mwenye Kujishirikisha na Riba. Je nani anaweza kupigana vita Na Muumba?
Biashara ni kununua na kuuza na kwa hiyo hii haina tatizo bali imehimizwa. Lakini RIBA haiwi hivyo bali unakopesha Pesa na kisha unasubiri ulipwe ziyada. Pia Kuna aina za RIBA ambazo nitazungumzia hapa chini kwa Msaada wa Hadithi za Mtume Mohamad. ﷺ
Hadithi Ifuatayo kutoka katika Sahih Al-Bukhari Hadithi namba 2312 inazungumzia aina nyingine ya RIBA
حَدَّثَنَا إِسْحَاقُ، حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ صَالِحٍ، حَدَّثَنَا مُعَاوِيَةُ ـ هُوَ ابْنُ سَلاَّمٍ ـ عَنْ يَحْيَى، قَالَ سَمِعْتُ عُقْبَةَ بْنَ عَبْدِ الْغَافِرِ، أَنَّهُ سَمِعَ أَبَا سَعِيدٍ الْخُدْرِيَّ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ جَاءَ بِلاَلٌ إِلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم بِتَمْرٍ بَرْنِيٍّ فَقَالَ لَهُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ” مِنْ أَيْنَ هَذَا ”. قَالَ بِلاَلٌ كَانَ عِنْدَنَا تَمْرٌ رَدِيٌّ، فَبِعْتُ مِنْهُ صَاعَيْنِ بِصَاعٍ، لِنُطْعِمَ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عِنْدَ ذَلِكَ ” أَوَّهْ أَوَّهْ عَيْنُ الرِّبَا عَيْنُ الرِّبَا، لاَ تَفْعَلْ، وَلَكِنْ إِذَا أَرَدْتَ أَنْ تَشْتَرِيَ فَبِعِ التَّمْرَ بِبَيْعٍ آخَرَ ثُمَّ اشْتَرِهِ ”.
TAFSIRI/TRANSLATION
Abu Sa`id al-Khudri alisema kwamba:
Once Bilal brought Barni (i.e. a kind of dates) to the Prophet (ﷺ) and the Prophet (ﷺ) asked him, “From where have you brought these?” Bilal replied, “I had some inferior type of dates and exchanged two Sas of it for one Sa of Barni dates in order to give it to the Prophet; to eat.” Thereupon the Prophet (ﷺ) said, “Beware! Beware! This is definitely Riba (usury)! This is definitely Riba (Usury)! Don’t do so, but if you want to buy (a superior kind of dates) sell the inferior dates for money and then buy the superior kind of dates with that money.”
SHEREHE
kwa hiyo hii ni aina nyingine ya Riba. hadithi inasema kwamba Kubadili Tende (Kwa Wingi) za Hali ya Chini kwa tende (Kwa Uchache) za Thamani za hali ya Juu haifai na ni aina ya RIBA na kwa hiyo kwa njia iliyo sahihi kwanza ni Kuuza tende iliyo na thamani ndogo na kisha ununue kwa pesa ile iliyo na thamani kubwa.
Hadithi kutoka katika Sahih Al-Bukhariy Hadithi Namba 2174
حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنِ ابْنِ شِهَابٍ، عَنْ مَالِكِ بْنِ أَوْسٍ، أَخْبَرَهُ أَنَّهُ الْتَمَسَ، صَرْفًا بِمِائَةِ دِينَارٍ، فَدَعَانِي طَلْحَةُ بْنُ عُبَيْدِ اللَّهِ فَتَرَاوَضْنَا، حَتَّى اصْطَرَفَ مِنِّي، فَأَخَذَ الذَّهَبَ يُقَلِّبُهَا فِي يَدِهِ، ثُمَّ قَالَ حَتَّى يَأْتِيَ خَازِنِي مِنَ الْغَابَةِ، وَعُمَرُ يَسْمَعُ ذَلِكَ، فَقَالَ وَاللَّهِ لاَ تُفَارِقُهُ حَتَّى تَأْخُذَ مِنْهُ، قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم “ الذَّهَبُ بِالذَّهَبِ رِبًا إِلاَّ هَاءَ وَهَاءَ، وَالْبُرُّ بِالْبُرِّ رِبًا إِلاَّ هَاءَ وَهَاءَ، وَالشَّعِيرُ بِالشَّعِيرِ رِبًا إِلاَّ هَاءَ وَهَاءَ، وَالتَّمْرُ بِالتَّمْرِ رِبًا إِلاَّ هَاءَ وَهَاءَ ”.
TAFSIRI/TRANSLATION
Narrated Ibn Shihab: that Malik bin Aus said, “I was in need of change for one-hundred Dinars. Talha bin ‘Ubaidullah called me and we discussed the matter, and he agreed to change (my Dinars). He took the gold pieces in his hands and fidgeted with them, and then said, “Wait till my storekeeper comes from the forest.” `Umar was listening to that and said, “By Allah! You should not separate from Talha till you get the money from him, for Allah’s Messenger (ﷺ) said, ‘The selling of gold for gold is Riba (usury) except if the exchange is from hand to hand and equal in amount, and similarly, the selling of wheat for wheat is Riba (usury) unless it is from hand to hand and equal in amount, and the selling of barley for barley is usury unless it is from hand to hand and equal in amount, and dates for dates, is usury unless it is from hand to hand and equal in amount”
SHEREHE
Tunasoma na kufahamu katika hadithi hii kwamba RIBA siyo pesa tu peke yake bali hata Mazao pia. Yaani mtu anapokuja na Unga wa ngano wa aina mojawapo na kutaka kubadilishana na Unga wa ngano wa aina nyingine basi Uislamu umeweka Sheria kwamba unaweza kufanya hivyo lakini iwe mkono kwa mkono yaani Biashara ya hapo kwa hapo na pia Uzito wa Unga wa ngano uwe sawa sawa. Usije ukafikiri kwamba Thamani ya Unga wa ngano wa aina moja ni kubwa kuliko nyingine na kwa hiyo mkibadilishana basi yenye Thamani kubwa Itskuwa na Uzito zaidi ya nyingine. Kwa mfano Kilo Moja kwa Kilo Mbili. Yaani Kilo Moja ya Umga wa ngano wa thamani ya chini kwa kilo Moja ya Unga wa ngano wa Thamani ya juu. Hadithi zimekataza haya ili kuepusha RIBA tuliyozungumza hapo juu. Kwa hiyo RIBA siyo katika Mikopo tu peke yake bali katika Biashara pia.
Ili kuepusha Dhuluma na kudanganyana katika Mabadilishano (Barter) ya Mazao au chochote kile basi Tufate Tunayofundishwa katika Dini ya Kiislamu kama ilivyoamrishwa katika Kuruani na Hadithi za Mtume Mohamad.ﷺ
Kuna Hadithi za Mtume ﷺ mbalimbali zenye kufafanua aina za RIBA.
AINA ZA RIBA
Kuna aina mbili za Riba
1. Ya kwanza Inaitwa Riba An Nasiyah, Riba Al Jahiliya au Riba al Quran
Na hii ndiyo tuliyozungumzia katika Mifano ya mazungumzo baina ya Mnunuzi na Bani hapa juu, Ni Ziyada au Interest zinazoongezwa katika Mikopo. na hii ndiyo RIBA iliyotajwa katika Kuruani Tukufu.
2. Ya Pili inaitwa Riba al Fadl, Riba an Naqd, Riba Al Bai.
au Riba al Hadeeth.
Riba Hii imeelezewa na Hadithi za Mtume na ndiyo maana imeitwa pia RIBA ya Hadeeth. na kama tulivyosoma hadithi hapa juu ni aina ya RIBA inayohusiana na Mazao na vinginevyo kama vile Dhahabu, Fedha au Chumvi
Mazao yaliyotajwa katika Hadithi ni kama vile Ngano, Tende au Barley.
Wanavyuoni wamehitilafiana Kuhusu aina Nyinginezo za Mazao na Pia katika Tafsiri ya Aina za RIBA na pia RIBA yenyewe. Na kwa hiyo siyo rahisi kufahamu kwa vizuri kwani kuna Hadithi mbalimbali za Mtume ﷺ ambazo zimeelezea kwa urefu. na Pia kuna kauli mbali mbali za wanavyuoni. Katika Mlango huu nitajitahidi kuelezea hadithi hizo lakini itachukua muda. Inahitaji utafiti wa hali ya juu. Njia nitakayofuata ni ya katikati na kudakua dakua fikra za wanavyuoni huku na huko mpaka tupate picha iliyo safi na kamili. Sijigambi kwamba mimi ni Profesa wa mambo ya Benki na Fedha lakini ni Mtafiti kama watafiti wengineo. Inshaallah Mwenyeezi Mungu akipenda nitafasiri kila Hadithi katika Hadithi za Mtume zinazohusu RIBA.
Uislamu haukubakiza kitu. Kila Uwanja katika Nyanja za Kidunia umeshaelezea kwa urefu. Alhamdulilahi Neema kubwa hii. Tuna kila Kitu kilichobaki ni Kusoma na Kufuata.
Elimu ya Biashara Ni Mlango mkubwa wa FIQH “Jurispridence” ya Kiislamu na katika Mlango huu tumegusia Kipengele kimoja tu cha Mlango huu wa Business. Yaani RIBA peke yake.
Kwa hiyo Mwenyeezi Mungu akipenda na kupata nafasi nitaendelea na Hadithi za Mtume hapa chini na pia Kuzifasiri. Kisha Nitaelezea Faida gani tunapata kwa Kujiepusha na Aina za RIBA tulizozitaja hapa juu.
Hebu tuendelee na Hadthi za Mtume. ﷺ
inaendelea……………………