SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Makala Ya Sayansi-1

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

Alhamdulilah  leo ni Ijumaa  tarehe  02  September 2022. Ni siku  kubwa ya Kiislamu na  Kwa munasaba huu ningependelea kuanza Makala Mpya inayohusiana na Sayansi  za Kidunia, Na Katika Sherehe hiyo  Mwenyeezi Mungu akipenda nitakuwa Nikipeleka  Darubini mara kwa mara katika Aya za Kuruani tukufu  ambazo  zina Uhusiano na Maelezo ya Sherehe hii.

MAKALA ZA SAYANSI KATIKA KARNE YA ISHIRINI

Hii ni Makala ya kwanza inayohusu uwanja wa Sayansi  za karne ya 20.

Mwanzoni mwa karne ya 20 wanasayansi walikuwa na tumaini kubwa la maendeleo ya kisayansi katika nyanja za Sayansi Duniani na pia kujihisi na mafanikio makubwa.

Sayansi katika Karne  ya 19 ilikuwa Haina Msimamo  madhubuti bali Nadharia  zilikuwa zikiyumba yumba.

Charles Darwin Na Richard Owen   walikuja na  Nadharia inayojulikana kama “Evolution”  ambayo inaamini kwamba Kila kilichopo ulimwenguni kimezuka bila kuumbwa.

Mpaka leo bado Nadharia hii inafuatwa na baadhi ya watu na pia inafundishwa mashuleni. Kwa kweli Nadharia hii imekufa na imetupwa katika Madebe ya Takataka Ya Kihistoria.

Walioitupa ni Wanasayansi Na Wataalamu wa kileo ambao wamegundua Mengi yaliyo  kweli.

Nadharia ya Evolution haisimami mbele ya Sayansi za kileo na Pia hazikubaliani na Dini ya Kiislamu. Mwenyeezi Mungu amekwisha tuambia katika Kuruani tukufu kwamba Yeye ndiye aliyeumba kila kitu hatua kwa hatua.  Kwa hiyo  Darwin na Timu yake  walikosea sana waliposema kwamba Viumbe vimezuka  hovyo hovyo Hatua Kwa Hatua.

Katika Wakati  huo wa karne ya 19   Mtaalamu  Charles Lyell Alielezea Muhtasari wa Historia ya Jiologia ya Ardhi. (Gelology). 

Na Elimu ya Saikolojia (Psychology”) ilizuka na kuhesabiwa miongoni mwa  Sayansi Mpya.

James Clerk Maxwell aligundua “Spectrum ya SumakuUmeme”  au  Electromagnetic Spectrum. 

Haya ni  Mawimbi (Waves) ya Nishati za Umeme katika Anga.

Vipimo vya urefu wa Mawimbi na Harakati zake ndiyo inayosababisha kuweko kwa aina mbalimbali ya Mwanga Angani  kwa mfano

Kuna Mawimbi  Marefu yenye  Harakati  ndogo  ndogo na Mawimbi haya yanatumika kwa Radio na  Yanajulikana kama Radio Spectrum. 

Kuna Mawimbi Mafupi yenye Harakati kubwa  sana na Haya yanatupa aina ya Mwanga unaojulikana kama Gamma Spectrum.

Baina Ya  Mawimbi marefu na Mafupi kuna Mawimbi ya Urefu (size0mbalimbali na pia kuna aina mbalimbali ya Mianga. 

X-Ray

Ultraviolet

Visible

Infrared

Microwave

Kila Aina ya Mianga au Spectrum  hutumika kwa kazi maalum. 

Kwa mfano Binaadamu  tunatumia Visible  Light  ili kuona. X-Ray ni mwanga ambao unatumiwa Hospitalini.  Microwave ni aina ya mwanga unotumiwa katika Majiko ya Umeme.Kuna wanyama ambao wanatumia mwanga wa Ultraviolet ili kuona.

Ukisoma Ulimwengu utamjua Mwenyeezi Mungu aliyeumba haya. Tunashangaa ya dunia lakini hatushangai Utukufu wa Mola.

Katika  Karne ya 19  Louis Pasteur alituelezea Namna ya Vijidudu (Microbes) wanavyoweza kuleta Maradhi na aliweza kutengeneza  Chanjo ziilizoleta faida kubwa na zikawa msingi wa Dawa za Ganzi (Anaesthetics) na Antiseptics na hizi  ndizo zinazosaidia leo hii katika  Kufanya Operesheni za Miili.

Wakati huo  Mandeleev aliweza kuchapisha Periodic Table ya Elements  au Jaduali ya Elements na kutuelezea Tabia za Chemicals.  

Miaka ya mwisho wa karne ya 18   Kuligunduliwa Electron, Virusi,  Antibodies, na Kuweza kutibu maradhi kama vile  Diphtheria.

Namna ya Kutibu maradhi kama haya kwa kutumia ufundi  wa mwanzo katika wakati huo unaonyesha mwanzo wa Muamko  wa Sayansi  katika karne hiyo. 

Vijana ambao waliingia katika Mkondo  wa Sayansi walikuwa wakijiuliza maswali mbalimbali. Walijiuliza watakachofanya na kipi kilichobaki cha Kugundua?

Binaadamu  tunasahau kwamba Kuna mengi ambayo bado hatujui. Kuna wakayi mwingine tunafikiri kwamba tumekwisha maliza. 

Kwa kweli tunajidanganya kwani Bado tupo mwanzo Ulimwengu bado hatuujui kabisa. Uvumbuzi bado haujaisha kwani kuna mengi bado hatuyajui.

Kuruani  imekusanya ulimwengu wote bali malimwengu yote pia hivyo hivyo. Tunadhani Tumekwishamaliza Kuruani na kwa hiyo hakuna mengine mapya kwa kweli tunajidanganya.

Ndugu  zangu Kuruani haina mwisho. Elimu yake haina mwisho. Kuna Miujiza isiyo na Mwisho.

Ikiwa Ulimwengu ni Kuruani Tunayoiona na Kuruani ni Ulimwengu tunaousoma Basi itakuaje Temekwisha maliza kuisoma kuruani?

Haiwezekani kabisa. Tunajidanganya. Miujiza katika kuruani haina mwisho kwani Elimu ya Mwenyeezi Mungu haina mwisho kama alivyosema katika Kuruani Tukufu kwamba angejaalia Mabahari yote kuwa Wino na kujaalia Miti yote kuwa kalamu basi Wino huo ungekwisha kabla ya maneno yake kwisha.

Nakumbuka Kuna siku  Nilimpa Rafiki yangu asiyekuwa Muislamu Kuruani Tukufu  iliyoandikwa kwa Tafsiri ya Kiingereza. Nilipokutana naye siku ya pili nilimwuliza je umenza kusoma Kuruni? Akanijibu kwamba ameishamaliza kusoma. Nilishangaa sana. Nikamwambia Umesoma Juu Juu kama Unavyosoma Gazeti. Na hivi  ni kosa. Tusisome Kuruani kama Gazeti kwani Mwenyeezi Mungu amatuambia katika Kuruani  Tunapoisoma lazima tuisome kwa utulivu na tufikiri. Usisome kama vile unasoma vitabu  vya Hadithi za Porojo  au  Michezo za Kuigiza.

Usifanye hivyo kwani Unapoteza Faida kubwa. Unaposoma ingependelea Usome na Tafsiri kama vile  Ya Sheikh  Abdallah Farisi au ya kiingereza kama vile Yusuf Ali.  Usome kisha ufikiri. Usiharakishe bali kidogo kidogo. Kuruani siyo Nyimbo. Usione utamu  wa sauti tu bali Jitahidi ueleqwe maana yake na ikiwezekana Tuifuate.

katika Mwanzoni mwa karne ya 20 kulianza kuonekana juhudi  kubwa za Wanasayansi  wakubwa duniani na hasa katika  Uwanja wa Physics. Mwana Sayansi  Maarufu  Einstein alikuja na Mapinduzi  makubwa ya Kisayansi ambayo yaliwashagaza weataalamu  Dunia nzima. Alikuja na Nadharia ambazo ziliwatingisha WanaSayansi wengineo kama vile Newton. Kwa mfano Einstein alisema kwamba Ulimwengu Ni Dynamic na siyo Static.  Kwa hiyo Ukweli huo  ulipingwa na Wasasaynasi wa wakati huo lakini hesabu za  Einsein zilionyesha kwamba Ulimwengu hauna utulivu bali Dynamic na Upo katika Kutanuka.  “Expansion of The Universe”.  Wakati huo  Wanasayansi  kama vile Newton walikataa  Ukweli huu kwani waliamini Ulimwengu umetulia “Static”  na Kwa hiyo  hakuna  Expansion yeyote. Ajabu ni kwamba baada ya miaka michache iligundulikana kwamba Einstein alisema kweli na hakukosea. Bwana huyu alisikitika sana kwani aligeuza Hesabu zake ili kuwiana na Fikra hizo za makoza za kina Newton za wakati  huo na akasema  usemi maarufu  uliorikodiwa  “This is a blunder of my life”

Baada ya Juhudi zote hizo na baada ya miaka kupita tunakuta Ukweli huu katika kuruani Tukufu. Je uamini au usiamini Mwenyeezi Mungu anasema katika Kuruani kwamba  “Tunatanua  Mbingu”  Allahu Akbar. Je unaona Maajabu? Mtume Mohamad alisoma wapi Elimu hii ambayo imechukua juhudi  kubwa na wakati mrefu.

Ugunduzi huu mkubwa unatuthibitishia kwamba Kuruani ni maneno ya Ukweli. Kuruani inatoka Kwa Mwenyeezi Mungu bila ya shaka yeyote. Kuna wachache  wasiojua chochote na ndiyo wenye kupinga. Na pia kuna wanafiki na waongo ambao watapinga tu na hata kama huu ndiyo ukweli. Huu ni uamuzi wao ambao unatokana na ujinga wao.

Wanasayansi pia walijitahidi katika mwanzo wa karne hii kusoma Ulimwengu wa Atom na kuja kwa Nadharia inayojulikana kama Quantum Theory nayo pia ilifanyiwa utafili. 

Vita vya kwanza Duniani 1918   na Maradhi ya homa ya FLU  duniani  (Pandemic Flu) yalikuja na  Kusababisha Maharibiko ya Juhudi za Kisayansi. 

Lakini ukweli ni kwamba Miaka  ya mwanzo  ya Karne  ya 20 yaani kabla ya Vita vya Dunia ilikuwa ni miaka ya Uvumbuzi Mzuri ambao ni mwanzo wa Maendeleo makubwa yaliofuata miaka ya baadaye.