SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Makala Ya Sayansi-2

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

Alhamdulilah Namshukuru Mwenyeezi Mungu kuweza kuandika Makala/Fedha na Benki kama  nilivyopanga. Kwa kweli sijaimaliza na itachukua muda lakini niliyoandika yanatosha kumpa msingi mtu yeyote.

Leo Ni  Jumapili Jioni  ya Tarehe  04/09/2022. Baada ya Kumaliza Kuandika  Makala ya RIBA  katika Mlango  wa Fedha na Benki nimeona nisimame  hapo kwani nilichoka kuendelea na Habari za Noti na Benki. Nimeona bora siku ya leo nigeuze Juhudi zilizobaki ziende katika Sayansi. 

Ni Wakati wa Jioni  ambao mzuri sana kwa kazi hii na hasa kazi ya Mwenyeezi Mungu. hakuna Lililo zuri kama Kuzungumza habari ya Kuruani ambayo ni Hotuba ya Muumba. Kwani mazungumzo ya kidunia yana Porojo  nyingi  na kwa hiyo nimekimbilia katika Kuruani ili kujiepusha na Porojo. 

Makala hii itahusu  mchanganyiko wa Elimu mbalimbali na kwa hiyo  usibabaike kwani nitakuwa nikirekibisha Darubini Yangu katika kila  kona, au kila Angle ya Kuruani na Viumbe vyake Mwenyeezi Mungu. 

Katika Makala hii tutaanza kwa kuelekeza Darubini yetu katika Sura namba 75  Aya ya  26  mpaka 30

سُوۡرَةُ القِیَامَة كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ (٢٦) وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٍ۬ (٢٧) وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ (٢٨) وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ (٢٩) إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَٮِٕذٍ ٱلۡمَسَاقُ (٣٠)

Hebu kwanza Tufasiri  Aya hizi kisha tushereheshe.

TAFSIRI

26.Sivyo (hivi mnavyofanya)!· (Roho) itakapoflkia katika mitulinga (mifupa ya mabega)

27. Na kukasemwa: “Ni nani wa kumzingua (na kumpoza mgonjwa huyu)?”

28. Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa hiyo ni (saa ya) kufariki (dunia)

29. Na utakapoambatanishwa muundi kwa muundi

30. Siku hiyo ni kucbungwa (tu). kupelekwa kwa Mola wako.

SHEREHE

Aya hizi zinatupa picha ya mtu anapofariki dunia. Kwa kweli  inatisha. Yaani  sisi wote tutayapata haya na siyo uwongo na hata Mitume pia walikutwa na Kifo na huu ndiyo mwisho wa kila kiumbe.  Lengo la Kupeleka Darubini yangu katika Aya hizi ni  neno  ٱلتَّرَاقِىَ  “ATARAQIY”  lenye  maana ya Mfupa wa Mabega. na kabla ya kilielezea neno hili kwanza ningependelea kuelezea Aya za mwisho wa Sura hii.

Inaishia na Aya  zinazozungumzia asili ya Binaadamu  kwanza alikuwa Tonye la Manii yaliyotoka kwa Nguvu, Kisha Kipande cha Nyama kinachonin’ginia katika Tumbo la uzazi  la mama na baadaye akazaliwa na kuwa Kiumbe cha kike au kiume na Mwenyeezi  Mungu anamalizia kusema kwamba Je anayefanya haya bila shaka yeyote ana uwezo wa kumpa kiumbe uhai tena baada ya kufariki dunia. Yaani ikiwa amekuumba kisha akakufisha basi pia atakufufua. Hebu tuone Tafsiri inavyosema hapa chini:

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةً۬ مِّن مَّنِىٍّ۬ يُمۡنَىٰ (٣٧) ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً۬ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ (٣٨) فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ (٣٩) أَلَيۡسَ ذَٲلِكَ بِقَـٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧىَ ٱلۡمَوۡتَىٰ (٤٠)

TAFSIRI

37.Je! Hakuwa tone Ia manii lilotonwa?

38. Kisha akawa kidonge cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha (mwanaadamu kamili)?

39· Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

40. Je! Hakuwa Huyo ni Muweza wa kuhuisha wafu?

SHEREHE

Hebu tufikiri. Aya hizi za mwishowa Sura hii zinazungumzia  asili ya Binaadamu na kuzaliwa kwake.

Kwa kifupi hapo mwanzo wa Sura Hii Aya zimetaja Kifo na Mwisho wa Sura  kuzaliwa.

Baada ya Kuzielezea  Aya za Mwisho wa Sura hii Ningepnedelea kurudi Mwanzo wa Sura Hii.

Hebu tulichunguzae Neno ٱلتَّرَاقِىَ “ATARAQIY” lenye maana ya Mfupa wa Mabega.

Sayansi ya leo inatuthibitishia kwamba Mtoto anapokuwa katika Tumbo la mama  mfupa wa kwanza kukua au kutokea ni huu  wa mabega yaani ٱلتَّرَاقِىَ “ATARAQIY”  na Mfupa wa mwisho  kukua kwa binaadamu anapokamilika yaani  Ujanani ni huu huu  ٱلتَّرَاقِىَ “ATARAQIY” 

hebu tujiulize swali.  Je huu siyo  Muujiza?  hebu fikiri. Binaadamu ana mifupa 206  mwilini lakini  huu ndiyo alioutaja katika Sura hii na ndiyo wa kwanza kukua katika tumbo la mama Na  ndiyo  huu huu alioutaja wakati Roho ya Binaadamu inapotoka na huu mfupa ndiyo wa mwisho kukua katika mwili wa binaadamu. Je unaona Ya kushangaza. Kuna maajabu makubwa katika Sura hii na nyinginezo pia.

katika National Library of Medicine (National centre of Biotechnical Information) tunasoma  habari hizi kama ifuatavyo yaani baada ya utafiti wa Wataalamu.

The clavicle has the honor of being the first bone to start the ossification process and the last to finish it. It has also been described as the most frequently injured bone in children less than 10 years of age

Na hii clavicle  ndiyo  ٱلتَّرَاقِىَ “ATARAQIY”  Kwa hiyo utafiti mbalimbali umefanywa na kutupa habari kama hizi kwamba huu ndiyo mfupa wa kwanza kukua katika Tumbo la uzazi wa mama na ndiyo mfupa wa mwisho kukua katika ujanani. 

Wataalamu wanaendelea kutufahamisha zaidi kwamba Mifupa ya kitoto katika tumbo la mama ndiyo ya kwanza kuonekana au kukua kabla ya Misuli. Na Kuruani  haikukosea   kabisa. Utafiti wa Wataalamu mbalimbali wanatuthibitishia Mpangilio huu ambao ni wa kisasa baada ya Uchunguzi kwa machine za kisasa. Hakuna aliyejua hapo zamani. Kauli zao ni kama zifuatazo:

(The Signaling For Bone Formation is Present Earlier Than The Signaling For Muscle Formation. Cartilage is Present Before Muscle Formation)

Nishati  ya Alama za Kukua kwa mifupa huonekana kabla ya Nishati ya Alama za kukua kwa Misuli. Cartilage au Kwa Kiswahili   Gegedu  inakuwapo kabla ya Misuli. Na hii  Gegedu ndiyo inayogeuka na kuwa Mifupa. Sasa hebu  tuzilete zile Aya zinazoelezea  mpangilio huu wa Kiajabu ili tuzione.  Allahu Akbar.

Sura Namba 23 Aya namba 12  mpaka 14

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَـٰنَ مِن سُلَـٰلَةٍ۬ مِّن طِينٍ۬ (١٢)

ثُمَّ جَعَلۡنَـٰهُ نُطۡفَةً۬ فِى قَرَارٍ۬ مَّكِينٍ۬ (١٣)

ثُمَّ خَلَقۡنَا ٱلنُّطۡفَةَ عَلَقَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡعَلَقَةَ مُضۡغَةً۬ فَخَلَقۡنَا ٱلۡمُضۡغَةَ عِظَـٰمً۬ا فَكَسَوۡنَا ٱلۡعِظَـٰمَ لَحۡمً۬ا ثُمَّ أَنشَأۡنَـٰهُ خَلۡقًا ءَاخَرَ‌ۚ فَتَبَارَكَ ٱللَّهُ أَحۡسَنُ ٱلۡخَـٰلِقِينَ (١٤)

TAFSIRI

12. Na kwa yakini tulimuumba mwanadamu kwa udongo ulio safi.

13. Kisha tukamuumba kwa tone Ia manii, (mbegu ya uzazi) lililowekwa katika makao yaliyohifadhika.

14·Kisha tukalifanya tone hilo kuwa pande Ia damu, na tukalifanya pande Ia damu hilo kuwa pande Ia nyama, kisha tukalifanya pande Ia nyama hilo kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama, kisha tukamfanya kiumbe kingine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.

SHEREHE

Aya hizi  zipo wazi wazi. Aya namba 14 inasema Kwanza  ilikuwa mifupa na kisha nyama.  Yaani  kitoto katika tumbo la mama kwanza alianza kuwa na mifupa  na baadaye nyama.  Na hii ndiyo Sayansi ya leo inavyotuhakikishia. Utafiti mbalimbali umefanywa na Jawabu linawafikiana na Kuruani kama vile Soksi unavyoivalisha Miguuni. Je  Mtume Alisoma wapi wakati huo ambao hakukuwako na vyombo vya hali ya juu vya kuchunguza mambo yanayopita Matumboni. Hebu fikiri. Huoni Maajabu. Allahu Akbar.  Hii inathibitisha kwamba Kuruani ni Muujiza mkubwa sana. Allahu Akbar. 

Kwa Kweli hakuna mwisho. Hebu tuendelee na Uchunguzi wa kushangaza. Tupeleke  Darubini katika Sura Ya Zumar na hapo Kuna Aya inayohusiana na Elimu ya Kizazi. Tuchunguze zaidi Maajabu na Mishangao.

Sura Namba 39  Aya Namba 6

خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٍ۬ وَٲحِدَةٍ۬ ثُمَّ جَعَلَ مِنۡہَا زَوۡجَهَا وَأَنزَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡأَنۡعَـٰمِ ثَمَـٰنِيَةَ أَزۡوَٲجٍ۬‌ۚ يَخۡلُقُكُمۡ فِى بُطُونِ أُمَّهَـٰتِڪُمۡ خَلۡقً۬ا مِّنۢ بَعۡدِ خَلۡقٍ۬ فِى ظُلُمَـٰتٍ۬ ثَلَـٰثٍ۬‌ۚ ذَٲلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡ لَهُ ٱلۡمُلۡكُ‌ۖ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ‌ۖ فَأَنَّىٰ تُصۡرَفُونَ (٦)

TAFSIRI

6.Amekuumbeni katika nafsi moja, kisha kamfanya mwenziwe (mkewe) katika jinsi ile ile, na akakuteremshieni (akakuumbieni) wanyama wanane (hawa wenye nafuu kubwa kwenu) madume na majike. (Ngamia, Ng’ombe, Kondoo na Mbuzi).Hukuumbeni matumboni mwa mama zenu- umbo baada ya umbo – katika viza vitatu. Huyu ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu: Ufalme ni wake; hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye. Basi nyinyi mnageuzwa wapi?

SHEREHE

Tutaielekeza darubini katika kipande cha Aya  hapa juu

فِى ظُلُمَـٰتٍ۬ ثَلَـٰثٍ۬‌ۚ  Yaani  Viza au Kiza Tatu.  Hebu tufikiri  Ajabu ya maneno haya. Je Mtume ﷺ amepata wapi habari kama hizi. haiwezekani mtu ajisemee hovyo hovyo kisha baada ya miaka iwe sio kweli. Kutoa kauli kama  hii inathibitisha haya siyo maneno yake  Mtume ﷺ peke yake hata kidogo. Heiwezekani. Haya  ni maneno makubwa kutoka kwa Mwenyeezi Mungu. Hebu tufikiri. Wataalamu wa siku hizi  za Teknologia na Sayansi  wamefanya uchunguzi yanayopita katika tumbo la uzazi kwa kutumia  Mashine za hali ya juu na kutueleza habari hizi  za kushangaza. Allahu Akbar.

Sayansi inasema kwamba  Giza Tatu ni:

1- The darkness of the anterior abdominal wall (Abdomen)

Giza la Ndani ya ngozi ya  Tumbo

2- The darkness of the uterine wall

Giza la ndani ya Tumbo la Kizazi  (Uterus)

3- The darkness of amniochorionic membrane

Giza la Mfuko unaomfunika Kijitoto

Wanatuambia tena kwamba maisha katika  Tumbo la uzazi  unapitia  Hatua Tatu kama zifuatazo:

1- Pre-embryonic stage; (first two and a half weeks).

2- Embryonic stage; (up to the end of the eighth week).

3- And the Fetal stage; (from the eighth week to the birth).

Na Hata Ngozi ya Embryo  yaani Inayomfunika katoto pia imegawanyika katika  Matabaka matatu  yaani Ngozi moja lakini ina Matandiko au Matabaka (layers) ya Ngozi nyembamba tatu kufanya ngozi moja Wanasema kwamba 

The layers of Embryo are also  Three as follows:

1/Ectoderm will give rise to the skin and nervous system

2/Mesoderm Specifies the development of bones, muscles and connective tissues and

3/Endoderm becomes the lining of respiratory and digestive system as well as other organs

Je unaona Kuruani  inavyotufundisha?  Allahu Akbar.