SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Makala Ya Sayansi-3

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MAKALA  IMEKUSANYA MAMBO  MBALIMBALI

Alhamdulilah. Leo ni Jumamosi Tarehe 10 September 2022

Ni wakati wa asubuhi na ni siku mpya ambayo imeanzia na Mvua. Namshukuru Mwenyeezi Mungu kwa kutupa  Uhai na Afya ambayo ukiwa nayo basi unaweza kufanya mambo  mengi duniani. Njia zipo nyingi lakini kuna njia zilizo nzuri na kuna zilizo mbaya.  Katika wakati huu wa mapema ya asubuhi na huku mvua inapiga kwa sauti kubwa  Juu ya bati za nyumba niyayokaa ningependelea kuchukua fursa hii nzuri kuchukua kalamu na kuanza kuandia makala ya Tatu ya Sayansi ambayo namuomba Mwenyeezi Mungu iwe miongoni mwa zile Njia nzuri alizozibariki. Amin.

Makala Hii ningependelea  kuanza na kuzungumzia Hadithi ya Mtume ﷺ Mohamad inayohusiana na Sayansi. 

Hapana Nimesahau samahani Msomaji  kwanza ningependelea kudokeza  Muujiza kutoka katijka Kuruani Tukufu ili iwe kama Kifunguzi  cha Mlango huu wa Sayansi na Baada ya hapo nitaendelea na Hadithi ya Mtume inayohusiana na Sayansi.

Najua wasomaji wengi wanapenda Miujiza ya Kuruani. Na kwa kweli kila Mtu anapenda. Nani anayejua Huenda katika Kuruani kuna Habari ya Machimbo  ya Almasi katika sehemu duniani. Hebu fikiri jambo hili. 

Kama katika Kuruani kuna siri imetaja habari ya Almasi zilizopo katika sehemu mojawapo duniani na unabidi uitafute katika Kuruani?  hebu jiulize Suala hili.

Kwa kweli kama ipo siri  hiyo basi watu dunia njima wangelijitahidi kwa mashindano  kuisoma ili kupata kujua siri hiyo. 

Binaadamu tunapenda  Utajiri. lakini  Ndugu Binaadamu wenzangu yaliyopo katika Kuruani ni zaidi Ya Almasi. Ukisoma kuruani  basi  yote hayo utayapata kama siyo Duniani basi Akhera. Huu ni uhakika  bila ya shaka yeyote.

Sasa  kwanza nikudokeze kidogo mazungumzo baina yangu na Shekhe wangu hivi karibuni  kisha tutaanza Makala  Yetu ya leo ambayo ina maajabu siyo madogo. Nimekuahidini na siwezi kuwadanganya hata kidogo. Je mumekubali?

Sheikh  wangu (Mwenyeezi Mungu Ambariki) akaniambia;

Sheikh:  kuna Muujiza Mpya nitakupa.

Al-Amin Ali  Hamad:  Asante  Sana natamani unijuulishe

Sheikh: Sura Ya Al-Fatiha Imekusanya Maana ya Msahafu wote

Al-Amin Ali Hamad: Naam, Nimesoma  Habari hii kwamba Elimu ya Msahafu yote imekusanywa katika Sura Ya Al-Fatiha na Elimu ya Sura Ya Al-Fatiha Imekusanywa katika Aya  Ya Basmala  yaani  “Bismi llahi Arrahmani Arrahim” Kuna Wanavyuoni wanaosema hivi. Kwa Kweli inashagaza sana.

Sheikh: Ngojea Nikupe Habari itakayokufurahisha  sana kuhusu Elimu  hii

Al-Amin Ali Hamad: Mwenyeezi Mungu akubariki Sheikh nieleze kwani  nina hamu sana nielewe habari. Nijuulishe Haraka kwani Nina wasiwasi sana nataka nijue haraka haraka.

Sheikh: Usiwe na wasiwasi wowote nitakueleza. Tulia roho. wasiwasi unatokana na Mashetani.

Al-Amin Ali Hamad: Ngoja Nitengeneze  Chai kisha tuzungumze

Sheikh: hakuna tatizo  tengeneza Chai na mimi uniletee na kisha ukae na kinisikiliza kwa makini.

Al-Amin Ali Hamad: Asante Sheikh Mwenyeezi Mungu akuzidishie Elimu.

Sheikh: Nilikuelezea hapo zamani kwamba Hapo zamani Waarabu na Makabika Mengineyo  ya wakati huo kama vile Mayahudi katika Enzi ya Mtume Mohamad ﷺ walikuwa wakitumia herufi kama Namba. Yaani wakati huo kulikuwa hakuna Namba. Kwa Mfano  Alif ilitumika kama Namba  1, Herufi ya Baa ilitumika kama Namba 2 na hivyo hivyo namba zote ziliwakilishwa kwa Herufi. Kwa hiyo  Angalia Namba  zifuatazo zinavyoshangaza:

383 + 525=114 + 794

Al-Amin Ali Hamad: Sheikh  wangu mimi sijaelewa chochote naona Namba tu.

Sheikh: Ngojea nifafanue zaidi.

Namba 383 Ni Jumla Ya Herufi za neno “KURUANI” unapoligeuza katika Namba walizotumia Waarabu wakati huo.

Namba 525 Ni Jumla Ya Herufi za neno “ALFATIHA” unapoligeuza katika Namba walizotumia Waarabu wakati huo. Kwa Mfano  Herufi ا, ل.ف  na nyinginezo  zote.

Namba 114 ni idadi ya Sura za Kuruani.

Na Namba 794 ni Majina Ya neno  ALFATIHA unapoligeuza katika Namba walizotumia Waarabu wakati huo. Yaani  Majina Ya Herufi kama vile أَلِف    ina Herufi  Tatu  na لاَم   ina  herufi  Mbili

Mgozea nipange  vizuri;

383 + 525=114 + 794  ni sawa na kusema

383 + 525=908  na   114 + 794=908

Je unaona Muiwano wa kushagaza.

Yaani  

Kuruani  ambayo  ni  383  +  Alfatiha  ambayo ni 525  ni sawa na Sura za Kuruani  ambazo ni 114 + Majina Ya Herufi za neno  Al-FATIHA

Ngojea nikupangie tena  vizuri  ili ieleweke:

383 + 525=114 + 794 

Neno Kuruani + Neno  Al-Fatiha= Sura za Kuruani + Majina Ya Sura Ya Al-Fatiha

yaani

Kuruani + Al-Fatiha= Sura za Kuruani + Majina Ya Herufi za  neno  Al-Fatiha

Al-Amin Ali Hamad= Naanza Kufahamu kiidogo

Mbona Muiano huu  unashangaza. Ni Kama nilivyosoma katika Chemistry.  Nilisoma kuhusu  Balance Equations.

Ni kama vile kusema Ukichanganya Majani ya miti ya aina hii na  Majani ya Miti ya aina hiyo  unapata  Dawa ya aina fulani. 

Sasa  hapa  Je  ina Maana kwamba  Elimu ya Msahafu wote imekusanyanywa katika Sura ya Al-Fatiha? je ni hivyo?

Sheikh;  Tafadhali  Acha  Kujibabaisha kabisa. Je unaamini Elimu ya  Yaliyo wazi na yaliyo fichika?  yaani Dhwahira Na Batina?  basi soma Hii miujiza ikuzidishie imani lakini usiichambue kwa kuzidisha au kupunguza kwani utapotea. yaani  ni hatari  usichikonoe chokonoe.

Al-Amin Ali Hamad: Unasema kweli kwani  Inashangaza lakini hatuwezi  kujua siri ya Miujiza Mikubwa kama hii lakini huenda watu wa baadaye wakagundua lakini sisi tusijihangaishe. Mwenyeezi Mungu anasema katika  sura Namba 17 Aya namba 46  

َلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِۦ عِلْمٌ ۚ إِنَّ ٱلسَّمْعَ وَٱلْبَصَرَ وَٱلْفُؤَادَ كُلُّ أُو۟لَـٰٓئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْـُٔولًۭ

Aya ina maana kwamba Usifuate yasiyo na Uhakika. Yaani jiepushe na Kubuni. Yaani Guess Work. Usifasiri Aya za Kuruani  kwa kubuni bali kwa uhakika. Hii ndoyo maana ya Aya hii. Huenda kuna siri. Inashangaza sana angalia tena Muiano wa kiajabu

383 + 525=114 + 794

Neno Kuruani + Neno Al-Fatiha= Sura za Kuruani + Majina Ya Sura Ya Al-Fatiha.

Yaani  kila upande tunapata jawabu   908

Allahu Akbar.

Mwenyeezi Mungu akubariki Sheikh. Siku ya leo  umenipa habari ya majabu makubwa. Neno Kuruani kujumlisha neno  Al-fatiha  jawabu ni 908  na Jumla ya Sura za kuruani  114 kujumlisha Majina Ya hefufi ya Neno  Al-Fatiha unapata jawabu ni 908  pia.  Allahu Akbar.  Sheikh haya kweli  ni maajabu. Nadhani siwezi kulala leo hii. Nitakuwa nikifikiri hizi namba tu usiku wote.  Nitakuwa nikifikiri  siri gani imefichwa  katika  Muiano  huu. 

Sheikh namuomba Mwenyeezi Mungu anionyeshe  siri ya Muiano huu wa kiajabu. Allahu Akbar

Najua kwamba wasomaji wa Website hii bado wana hamu sana ya kusoma ahadi niliyotoa hapo juu ya kwamba Nitazungumzia katika Mlango huu habari za Sayansi. Naona Sasa wakati umefika na Nitaanza. Nitaacha Yasiyohusu Website hii na kwa haraka Nitaanza na mapya. Haya  Tuanze:

KUZIMA MOTO

Miaka mingi  wanasayansi wametafuta njia mbalimbali za ufundi wa kuzima moto kwa njia safi kwani Kutumia Vyombo vya  kisasa yenye kutumia madawa pia yana hatari  nyinginezo kwa mimea na kuharibu hali ya hewa.  madawa haya yana “Toxic Chemicals” 

Hivi karibuni Wataalamu  wamegundua Ufundi mpya ambao huenda ukawa Mfundi wa hali ya juu na wa siku za mbeleni. 

Wataalamu Huko Marekani  kutoka George Mason University wamegundua njia mpya kuzima moto kwa kutumia Sauti. Habari  zinasema:

(Two former U.S. electrical engineering students have discovered a cutting-edge and unconventional way to fight fires: with sound. Specifically, bass frequencies between 30 and 60 Hz)

KIla siku Wataalamu wanatafuta Njia mbalimbali za kuleta Maendeleo katika Uzimaji a Moto na hasa wakati huu ambao Mashamba Makubwa makubwa yanaungua kama tunavyoona katika News au Habari za Dunia.

Je uamini au usiamini  Mtume  Mohamad alidokeza habari  hizi  katika Hadithi  yake hapa chini:

س/ صحة حديث اذا رأيتم الحريق فكبروا ؟

ج/ يُروَى حديث في ذلك عن عبد الله بن عمرو بن العاص أن النبي صلى الله عليه وسلم قال : ( إِذَا رأيْتُمُ الحَرِيقَ فَكَبِّرُوا فَإِنَّ التَّكْبِيرَ يُطْفئُهُ ) أخرجه ابن السني في “عمل اليوم والليلة” (295) ، والطبراني في “الدعاء” (1/307) ، ولكنه حديث ضعيف لا يصح, لكن استحب بعض العلماء التكبير عند الحريق. يقول ابن القيم رحمه الله في “زاد المعاد” (4/194) : ” لما كان الحريق سببه النار ، وهي مادة الشيطان التي خلق منها ، وكان فيه من الفساد العام ما يناسب الشيطان بمادته وفعله ، كان للشيطان إعانة عليه وتنفيذ له ، وكانت النار تطلب بطبعها العلو والفساد ، وهذان الأمران – وهما العلو في الأرض والفساد – هما هدي الشيطان ، وإليهما يدعو ، وبهما يُهلِك بني آدم ، فالنار والشيطان كل منهما يريد العلو في الأرض والفساد ، وكبرياء الرب عز وجل تقمع الشيطان وفعله ، ولهذا كان تكبير الله عز وجل له أثر في إطفاء الحريق ؛ فإن كبرياء الله عز وجل لا يقوم لها شئ ، فإذا كبر المسلم ربه أثَّر تكبيره في خمود النار وخمود الشيطان التي هي مادته ، فيطفئ الحريق ، وقد جربنا نحن وغيرنا هذا فوجدناه كذلك ، والله أعلم #الكلام_دا_صح؟

Katika Mazungumzo  yaliyopo katika Habari nilizonukulu hapa. Yaani Suali na Jibu kuhusu Hadithi Ya Mtume  ambayo insemekana kwamba ni Hadithi Dhaifu. Kwa kweli kuna Hadithi  ambazo zilikusanywa na  Kupewa sifa za Udhaifu lakini  huenda zikawa Hadithi sahihi kwani baadhi yake zinakubaliana  na Mambo  mengi  katika maisha yetu.

Wanasema mashekhe katika Suali na  Jibu hapa kwamba Hadihi inayosema kwamba 

إذا رأيتم الحريق فكبروا؛ فإن التكبير يطفئه

Mtume ﷺ anasema kwamba Ukiona moto  basi  Useme

“Allahu  Akbar” kwani kwa kusema hivyo unauzimisha moto.

Mashekhe wanasema kwamba ukisema Allahu Akbar  unaondoa Shari ya Mashetani kwani hao ndiyo sababu ya Moto huo.  Mashetani  wanapenda kuleta Uharibifu na ndiyo kazi yao.  Kwa  hiyo ukisema  “Allahu Akbar” basi  hao  Mashetani unawashinda na Shari inaondoka na kwa kusema hivyo itasadia kuuzimisha  Moto huo.

SHEREHE YA KISANYANSI

Hebu  tuifasiri Hadithi hii Kisayansi. Je huoni  kwamba Kwa kusema  “Allahu Akbar” Ni Kutumia Sauti  katika Kuuzima Moto na hasa hizo  herufi za “Allahu Akbar”  . Kwa mfano Herufi  HAA  katika HU  ya Allahu  ni herufi  inafuatiliwa na  Upepo. Hizi ni  Herufi zinazojulikana kama “bass frequencies”  Yaani ni herufi za frequencies ya chini. Kwa mfano Herufi ya SIN ni  herufi yenye  frequencies za Juu na hakuna Herufi  za aina hii katika  ” “Allahu Akbar” Je huoni Muujiza wa Kisayansi  uliotolewa na Mtume hapa?  kwa kusema  Allahu Akbar  unakuwa umemtukuza Mwenyeezi Mungu na Unaondoa Shari ya Sheitani na hapo hapo  unaondoa Moto Kisayansi.  Kwa Kweli Sayansi ni Yake Mwenyeezi Mungu. Tunafundishwa Sayansi  ya Hali ya Juu. Sisi tunadharau na tunafikiri kwamba mambo haya ya kidini yana uhusiano na Mashetani ambao hatuwajui na hatuamini lakini ukweli ni kwamba  Kuna Siri nyinginezo za Kisayansi  zimefichika. Tungeliamini hadithi hii na kuisoma basi  tusingelingojea Mpaka Wataalamu kutoka  Marekani waje  kutufundisha.  Na ndiyo maana Tukawa Nyuma kwani  tumeipuuza Dini  kwa  ujinga wetu.  Kuruani na Uislamu  una kila kitu lakini tupo nyuma ya binaadamu wenzetu kwani tumeiacha kuruani.  Wanakuja wengine kugundia mambo kisha tunasema ilikuwapo katika Kuruani  au katika Hadithi za Mtume. Huu ndiyo ujinga wetu na ndiyo maana tupo nyuma. Allahu Akbar.

INAENDELEA………

NGUVU YA SAUTI NA MATUMIZI YAKE

Wengi hawajui kwamba Kuruani Imekusanya tunayoyajua na tusiyoyajua. Ulimwengu bali Malimwengu yote yapo katika Kuruani. 

Hebu tusome Aya zifuatazo kutoka katika Kuruani Tukufu kisha Tuone Faida kutoka Katika Aya hizi.

لَوْ أَنْزَلْنَا هَذَا الْقُرْآنَ عَلَى جَبَلٍ لَرَأَيْتَهُ خَاشِعًا مُتَصَدِّعًا مِنْ خَشْيَةِ اللَّهِ وَتِلْكَ الْأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ) [الحشر: 21]

وَلَوْ أَنَّ قُرْآنًا سُيِّرَتْ بِهِ الْجِبَالُ أَوْ قُطِّعَتْ بِهِ الْأَرْضُ أَوْ كُلِّمَ بِهِ الْمَوْتَى بَلْ لِلَّهِ الْأَمْرُ جَمِيعًا) [الرعد: 31]

Aya ya kwanza kutoka katika Sura ya Al-Hashr Aya namba 21 inasema kwamba

21.Lau kama tungaliteremsha hii Qurani juu ya mlima, ungaliuona ukinyenyekea (na) kupasuka kwa sababu ya hofu ya Mwenyezi Mungu. Na hii ni mifano tunawapigia (tunawaeleza) watu ili wafikiri.

Na Aya Ya Pili kutoka katika Sura Ya  Al-Raad Aya Namba 31  inasema kwamba:

31.Na kama ingalikuwako Qurani ambayo kwa Qurani hiyo milima ingaliondoshwa (inaposomwa). au kwa hiyo ardhi ingalipasuliwa, au wafu wangalisemeshwa kwa hiyo (basi ingekuwa Qurani hii ndiyo ya kufanya kazi hiyo, lakini hiyo siyo kazi ya Qurani). Siyo! ·Mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Je! Hawajajua walioamini ya kwamba Mwenyezi Mungu angalipenda bila shaka angaliwaongoza (Uislamuni) watu wote? (Akawaumba kama Malaika, hawana matamanio. Lakini amewapa akili na matamanio wapigane baina ya viwili hivi, washinde waingie Peponi). Wala msiba hautaacha kuwapata wale waliokufuru kwa sababu ya yale waliyoyafanya, au utashuka karibu na nchi zao, mpaka ifike ahadi ya Mwenyezi Mungu (ya kuwatoa roho). Hakika Mwenyezi Mungu havunji miadi (yake). 

SHEREHE

Hizi  Aya Mbili  zinaelezea  Utukufu na ukubwa wa maneno ya Mwenyeezi Mungu. Maneno  yake yana  utukufu na ukubwa wa hali  ya juu sana. Watu wengi hawajui na wanafikiri  maneno ya utani kwa kucheka kwamba Je Kuruani inaweza kutingisha na kuondoa Milima?  Je Kuruani Inaweza Kupasua Ardhi? Je Kuruani inaweza Kumzungumza Maiti aliyefariki Dunia? Wengi  wanadharau na kuona upuzi na uongo. 

Ndugu zanguni  wajinga ni sisi  wenyewe.  Kuruani tumeiacha na ndiyo maana tumekuwa nyuma na wajinga. laiti  tungeifuata na kuisoma Kuruani basi tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana katika maisha yetu yote.  

Hizi Aya zimeficha mengineyo  tusiyoyajua na katika yale machache tunayoyajua ni Sauti. Kwa mfano  Neno  “KURUANI” maana yake Kisomo yaani kwa kutumia Sauti.  Aya hapa zinasema  kwamba Maneno ya Mwenyeezi Mungu na siyo MSAHAFU yaani Kitabu cha Kuruani  bali Yale maneno ya Kuruani  yaani Kisomo cha Sauti. Lazima tuelewe hivyo. Maana ya neno  Kuruani ni  KISOMO na siyo makaratasi ya MSAHAFU.

Na kisomo chochote  kinataka Sauti. Kwa hiyo katika Aya hizi tunapewa faida nyinginezo  za ishara ya Faida ya Sauti tulizopewa na Mweenyeezi Mungu.

Jambo  la kwanza Aya Zinatuelezea  Muujiza na Ukubwa wa Kuruani Tukufu na Pia hapo hapo kuna Siri nyinginezo zimefichika.  Na Mwenyeezi Mungu anajua Zaidi.

Hivi karibuni  Wataalamu wamefanya Utafiti namna ya Kutumia SAUTI  katika  Kusukuma na Kuinua vitu.  Habari zinasema kwamba Timu ya Watafiti wa Vyuo vikuu vya Sao  Paulo huko Brazil na Huko  Edinburgh  Scotland (UK) wameweza Kuinua kampira kadogo cha Polysterine kwa kutumia sauti.

(Research team at University of São Paulo in Brazil and Heriot-Watt University in Edinburgh has now successfully levitated a polystyrene ball 3.6 times bigger than the wavelength lifting it)

Hapa chini nitaweka Picha ya Kapira na Pia Video yenye kuzungumzia mambo haya ya Kushangaza.

Kuruani  siyo mchezo. Imekusanya Faida kubwa ambazo unaweza kugundua Mambo  makubwa yenye kuleta faida duniani kwa hiyo tuwe macho tusilale.  Angalia picha na Video hapa chini iliujionee mwenyewe. Allahu Akbar.

Kapira Kadogo Chekundu kinainuliwa na Sauti. Hii ni Experiment angalia Video hapa

Video-1

Video ya Utafiti. Nguvu Ya Sauti inavyoweza kuathiri Vitu. Allah Akbar

Video-2

Sauti – Experiment