UTAFITI MBALIMBALI KATIKA DINI NA SAYANSI
IMEANDALIWA NA AL-AMIN ALI HAMAD
NAKUKARIBISHENI KATIKA SAFARI MBALIMBALI
MAZUNGUMZO BAINA YANGU NA PROFESA ALIYEKUWA MUHANDISI (ENGINEER) KATIKA MECHANICS HUKO CAIRO (EGYPT)
Al-Hamdililah leo Tarehe 16/09/2022. Namshukuru Mwenyeezi Mungu kwa kutupa uzima kuweza kuendelea kuandika haya machache.
Mwenyeezi Mungu akipenda ningependelea siku ya leo na siku chache zijazo kuwaletea wasomaji wote wa Website hii Mazungumzo baina yangu na Profesa Mbalimbali ambao kwa bahati nilipata kuzungumza nao Asili ya Ma Profesa hawa ni kutoka Misri (Egypt), Syria, Sudan, Algeria, Jordan, Yemen na sehemu Nyinginezo mbalimbali za Dunia.
Umri wa Profesa hawa sio mdogo baadhi yao wana miaka 80 na wengine zaidi ya 80. Na pia kuna Wengine Vijana.
Nilipendelea kukutana na Profesa Wazee kwani nadhani wamekula Chumvi nyingi na Hao wamejaa Elimu mbalimbali za kidunia. Nami nilikuwa na Maswali mengi katika Kuruani Tukufu. Profesa hawa wote wamefanya Utafiti mbalimbali katika Kuruani na Hadithi za Mtume. Kwa hiyo Milango inyokuja itahusu Mazungumzo baina yangu na Wanavyuoni hawa.
Siku ya Leo Mazungumzo yatahusu Profesa ambaye Asili yake Kutoka Egypt-Cairo. Mazungumzo yalifanyika kwa Lugha ya Kiarabu. Na nimefasiri kwa Kiswahili na kama kawaida Kuna Nyongeza na Pungufu katika Maandishi lakini Muhimu ni Madhumuni ya Mazungumzo Haya.
Kabla ya kuleta mazungumzo hayo ningependelea kusema kwamba hapa ninapokaa ninasikia makelele ya watoto ambao nje ya nyumba yangu wanaendesha Baiskeli za Gurudumu moja na kwa kweli inanikera sana kwani makelele hayo yananizuia utulivu wa Fikra zangu katika kuandaa website hii.lakini ni watoto wadogo na kwa hiyo nitawasamehe kwa leo kwani Jua limechomoza na kwa kawaida hupenda kucheza cheza barabarani. Na Pia sisi tulipokuwa Umri wao tulifanya hivyo hivyo.
Mbele yangu kuna Dirisha la kioo na ninaweza kuona Nje ya nyumba Matawi ya Mti mkubwa ambao yanatingishwatingishwa na Upepo mkali. Ni wakati ambao majani yananguka kwa wingi.
Kuanguka kwa majani kunanikumbusha Kauli Ya Mwenyeezi Mungu Sura Namba 6 Aya Namba 59 inayosema:
۞ وَعِندَهُ ۥ مَفَاتِحُ ٱلۡغَيۡبِ لَا يَعۡلَمُهَآ إِلَّا هُوَۚ وَيَعۡلَمُ مَا فِى ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۚ وَمَا تَسۡقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعۡلَمُهَا وَلَا حَبَّةٍ۬ فِى ظُلُمَـٰتِ ٱلۡأَرۡضِ وَلَا رَطۡبٍ۬ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِى كِتَـٰبٍ۬ مُّبِينٍ۬ (٥٩)
TAFSIRI
59. Na ziko kwake (Mwenyczi Mungu tu) funguo za siri; hakuna azijuaye ila Yeye tu. Na anajua yaliyomo barani na baharini. Na halianguki jani ila analijua. Wala (haianguki) punje katika giza la ardhi · (ila anaijua). Wala (hakianguki) kilichorutubika wala kilichoyabisika (ila anakijua). (Hapana cho chote), ila kimo katika Kitabu kidhihirishacho (kila jambo).
Kwa kweli Aya hii inaonyesha uwezo wa Mwenyeezi Mungu. Yaani kila kinachofanyika Ulimwenguni anakijua yaani hakuna asichokijua. Na pia Kila kitu kimo ndani ya Kuruani.
Samahani ndugu msomaji nitasimama hapa kwani lengo la leo ni kuwaletea Mazungumzo baina yangu na Profesa kwa hiyo tuanze.
Kwanza ningependelea kuwajuulisha kwamba Profesa huyu alinikaribisha kwake. Na nilifurahi sana kukaribishwa na kuweza kukutana naye kwa mzungumzo ambayo yalikuwa mazuri sana tena sana.
Tulizungumza mambo mbalimbali ambayo nitachagua baadhi yake ambayo muhimu zaidi na pia kwa ajili ya wakati wenu na pia wangu.
Tulizungumza kuhusu
1/Kukutana na Majini
2/Namba za Ukorofi
Ne Miujiza Mingineyo ikiwezekana.
Ndugu Msomaji fuatilia mazungumzo haya kwa utulivu lakini ingelikuwa bora Utayarishe Chai na Keki kisha usome mazungumzo haya yasiyo na mwisho kwa Raha Yako.
AL-AMIN ALI HAMAD: Hodi , Hodi Hodi. Hodi Profesa. Profesa, Je Upo? Hodi.
(Sauti ya Kufunguliwa kwa Mlango)
PROFESA:Karibu Ndugu Al-Amin
AL-AMIN ALI HAMAD: Salaam Nyingi zikufikie na Baraka zake Mwenyeezi Mungu (Asalaama Alaykum Warahmatullwahi Wabarakatuh).
PROFESA:Na wewe pia Salaam nyingi za Rahema na baraka ziwafikie (Waa’laykum Asaaalaam Warahmatullahi Wabarakatu Ndugu Al-Amin vipi hali? Miaka mingi imepita tangu tukutane. Nimefurahi sana tena sana kukutana tena. Alhamdulilah leo siku kubwa. Nashukuru kwa Mwenyeezi Mungu kutupa Uzima na Afya mpaka Leo
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante sana Profesa kwa kweli nimefurahi kuliko wewe ulivyofurahi. je vipi hali?
PROFESA:Hali mzuri Alhamdulilahi. Nimekualika tupate kuzungumza mambo mbali mbali yanayohusu Kuruani na Dini. lakini kabla ya hapo ningependelea upumzike kidogo. Ndugu Al;-Amin ungependelea kinywaji gani?
AL-AMIN ALI HAMAD:Asante sana kwa kweli usijihangaishe kabisa kwa matayarisho yeyote makubwa. Kahawa ingetosha.
PROFESA: Unaonaje Kahawa na Tende?
AL-AMIN ALI HAMAD:Mwenyeezi Mungu akubariki hiyo inatosha.
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante sana, Tende hizi tamu sana zimetoka wapi?
PROFESA:Hizi ni tende za Madina huko alipozikwa Mtume Mohamad. (Saudi Arabia) Mwenyeezi Mungu Amsalie.
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante sana kwa makaribisho asante sana. mwenyeezi Mungu Akubariki. Kama ulivyonijuulisha kwamba Kuna Masuala Mawili ambayo ungependelea kuzungumza na pia Mengineyo ikiwezekana. Je ni yapi hayo?
PROFESA: Ningependelea tuanze kuzungumzia mambo mawili nayo ni:
1/Kukutana na Majini
2/Namba za Ukorofi
Na Miujhiza Mingineyo Ikiwezekana
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Inatisha sana habari ya majini. Yaani unataka kunikutanisha na Majini? Yaani leo hii?
PROFESA: Naam. Ndiyo hivyo Al_Amin
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Mimi naogopa sana jambo hili. Ningeone bora tuanze na Namba za Ukorofi na Hiyo Ziyara ya Majini tufanye mwisho. kwa kweli inatisha. Nipe Muda.
Eeeeeeeee bwana Wee Majini Yanatisha. Tuifanye iwe Topic (Vipengele)ya Mwisho.
PROFESA: Al-Amin sawa bwana tufanye hivyo. Tuanze na namba za Ukorofi. Je unazijua?
AL-AMIN ALI HAMAD: Namba za Ukorofi sizijui? Tafadhali Nifahamishe.
PROFESA:Namba za Ukorofi ni Odd Numbers na Namba sizizo na Ukorofi ni Even Numbers. Je unakumbuka haya mambo wanafundishwa watoto katika Shule za Msingi.
AL-AMIN ALI HAMAD: Ahhhhh ninafahamu ODD na Even Numbers. Unaziita ODD numbers ni namba za Ukorofi? kwa nini Namba za Ukorofi? na kwa nini Even Numbers Namba zisizo na Ukorofi?
PROFESA: Namba za Odd ni kama vile 1, 3, 5, 7, 9, 11
na kuendelea yaani 13….
na Namba Even ni kama vile 2, 4, 6, 8, 10 Na kuendelea. yaani 12, 14….Na kuendelea kama vile 16, 18…..
Namba Odd ni zile ambazo hazigawanyiki katika mafungu mawili ya sawa kama vile namba 3 huwezi kugawanya na namba 2 na ukifanya hivyo basi utapata mabaki ya namba 1 na hivyo hivyo huwezi kugawa namba 11 na ukifanya hivyo yaani kugawa mafungu mawili basi utapata mafungu mawili ya namba 5 na mabaki yaani masalia ya namba 1
lakini Even Numbers zinagawanyika mafungu mawili na hakuna Masalia au mabaki. Kwa mfano unaweza kugawa namba 4 katika mafungu mawili ya namba 2 na hakuna masalia au mabaki. Na namba 8 pia unaweza kugawa katika mafungu mawili ya namba 4 bila ya Masalia au mabaki. Je umefahamu maana ya Namba za Ukorofi na zisizo na ukorofi? Kwa hiyo namba za Odd ni zile namba zenye Ukorofi yaani zinakataa kugawanywa katika mafungu mawili na namba za Even ni namba sizizo za ukorofi kwani zinakubali kugawanywa katika mafungu mawili bila tatizo
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa leo hii sikutegemea Utanielezea habari za Namba za ukorofi kwani ni masomo ya watoto wadogo yaani shule za Msingi. Nilitegemea kunifundisha mambo ya wakubwa na wewe ni Profesa mkubwa. Yaani sikutegemea…. Mimi nina Diploma za Vyuo vikuu naona Mazungumzo haya ni ya watoto wadogo.
PROFESA: Ndugu Al-Amin usidharau Elimu. Elimu ni Elimu hakuna ya watoto au wakubwa. Haya ninayokuelezea siyo madogo hata kidogo.
AL-AMIN ALI HAMAD: Je kuna Makubwa?
PROFESA:Nisikilize vizuri. Fungua Masikio. Kwanza Je unataka Kahawa kisha tutazungumza?
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Sana kwa kahawa. Kisha Nielezee zaidi Siri ya haya makubwa.
PROFESA: Mimi sizungumzi upuuzi. Nimefanya Utafiti katika Kuruani Miaka 40 na Nimefanya utafiti wa Kuruani na Hadithi za Mtume si chini ya Utafiti Elfu 10. Sikukukaribishi nikupotezee wakati bure bure nisikilize vizuri haya nitakayokuambia leo hii:
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa nina hamu sana ya kuelewa tafadhali niambie. nahamu sana kusikiliza habari za Kuruani.
PROFESA:Hebu Tuichunguze Sura Ya Al-Masad au Abi Lahab katika Kuruani.
Sura Al-Masad, Tafsiri Na Sherehe yake hapa chini:
سُوۡرَةُ لهب / المَسَد
بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
تَبَّتۡ يَدَآ أَبِى لَهَبٍ۬ وَتَبَّ (١) مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُ ۥ وَمَا ڪَسَبَ (٢) سَيَصۡلَىٰ نَارً۬ا ذَاتَ لَهَبٍ۬ (٣) وَٱمۡرَأَتُهُ ۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ (٤) فِى جِيدِهَا حَبۡلٌ۬ مِّن مَّسَدِۭ (٥)
TAFSIRI
I.Pana kuangamia mikono miwili ya Abu Lahab! Naye amekwisha angamia.
2. Hayatamfaa mali fake wala alivyovichuma.
3. (Atakapokufa) atauingia Moto wenye mwako (mkubwa kabisa)
4. Na mkewe, mchukuzi wa kuni (za fitina), (fattani, anayefitinisha watu wasiingie katika dini; atauingia naye Moto huo) ·
5. (Kama kwamba) shingoni mwake iko kamba iliyosokotwa (anayochukulia kuni za fitina hizo).
SHEREHE
Sura Hii ilishushwa kwa ajili ya Ami (Uncle) yake Mtume ambaye alimfanyia UKOROFI mtume. Hapo mwanzo wa kupewa Utume Bwana wetu Muhammad (s.a.w.) aliamrishwa awabashirie jamaa zake walio karibu naye kwa kizazi; akawakusanya akawabashiria na kuwakhofisha na adhabu ya Akhera, Abu Lahab, Ami yake, akakasirika, akamwambia ‘Mwana kuangamia wee! Ndilo ulilotwitia hili?’ Ndipo iliposhuka sura hii kuapizwa Abu-Lahab na mke wake, Ummu-jamil, aliyekuwa akijipinda sana katika kumuudhi Mtume, na kuwashakiza makafiri wamuue na kufanya kila aliwezalo katika kuizuilia dini isifuatwe. “Yana kuangamia mikono miwili ya Abu-Lahab!” ni maapizo ya kuapizwa Abu-lahabi aangamie yeye, badali ya Mtume (s.a.w.). Na alipokuwa Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuapiza, imekuwa hapana shaka maapizo hayo tu yenye kumpata, na kwa hivyo Mwenyezi Mungu anatupa habari kuwa “amekwishaangamia.” Huyu mke wa Abu-Lahab alikuwa Msengenyaji(sakubimbi). Kazi yake kuchukua maneno ya huku akipeleka huku kwa kutia fitina na fisadi. Na mtu namna hii Waarabu humshabihisha na “mchukuzi wa kuni.” Na dasturi, mchukuzi wa kuni huwa na “kamba” katika shingo yake ya kufungia hizo kuni zake, na kuni ndizo zinazowasha moto. Na huyu mwanamke akiwasha moto wa kuwazuilia watu wasisilimu na kuwatoa waliosilimu
PROFESA:Kwa hiyo Bwana Abu Jahl na Mkewe walikuwa Wakorofi.
AL-AMIN ALI HAMAD:Ahhha sasa nimeanza kukuelewa kidogo. lakini bado nina swali.Ulinielezea kuhusu Namba za Ukorofi yaani ODD NUMBERS na sasa Sura Ya Al-Masad unasema Bwana Abu Jahl ambaye Sura Hii ilishushwa kawa ajili yake alikuwa pia Mkorofi na Mke wake pia. Lakini kuna uhusiani gani kati ya Namba za Odd na Sura Hii?
PROFESA:Fanya Subira. Kidogo kidogo.,Wazungu wanasema Step by Step Na Waswahili wanasema Haraka Haraka haina Baraka. Kwa hiyo wewe nisikilize tu. Wewe umekuja Kwangu kwa hiyo niache nikueleze mambo usiyoyajua.
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Profesa. Mungu akubariki.
PROFESA:Mwenyeezi Mungu ameshusha Sura Hii kiajabu sana. Ni Sura Ndogo lakini ina miujiza isiyo na Mwisho
AL-AMIN ALI HAMAD: Allahu Akbar. Allahu Akbar.
PROFESA: Hebu Nianze. Sikiliza kwa makini miujiza ifuatayo katika Sura Hii:
Kwanza Sura Hii ni Namba 111 na namba hii ni ODD yaani kama kusema kwamba Namba hii ni namba Ya Ukorofi. Yaani Ukijifanya Mkorofi basi Mwenyeezi Mungu ana Ukorofi zaidi. Ndiyo maana yake. na kwa hiyo ameipanga katika kuruani namba 111
AL-AMIN ALI HAMAD:Hiyo tu. Mimi sioni Muujiza wowote
PROFESA: Nimekuambia Usiharakishe. Subiri huu siyo Muujiza Mdogo
AL-AMIN ALI-HAMAD: Samahani nitasubiri. Profesa endelea.
PROFESA: Sura Hii ina Aya 5 na Hii namba 5 ni Namba ODD yaani Namba ya Ukorofi
Angalia sasa tuchunguze Jumla ya Herufi katika Kila Aya ya Sura Hii.
Aya ya Kwanza ina Herufi 15 ambayo ni Namba ODD
Aya ya Pili ina Herufi 19 na hii ni Namba ODD
Aya ya Tatu ina Herufi 15 na hii ni Namba ODD
Aya ya Nne ina Herufi 17 na hii ni namba ODD
Aya ya Tano na ni ya Mwisho ina Herufi 15 na Hii ni Namba ODD
Yaani Jumla ya Herufi katika Kila Aya Ni ODD yaani Ukorofi kama Ukorofi wa yule aliyeshushiwa hizi Aya yaani Abu Lahab na Mkewe.
AL-AMIN ALI HAMAD:Allahu Akbar. Profesa Umenipa Mambo Mapya. Allahu Akbar. Je ni haya tu?
PROFESA: Tulia. Usiharakishe kwani sijamaliza. Subira yavuta Heri.
AL-AMIN ALI HAMAD: Samahani Profesa siharakishi bali nina hamu ya kuelewa zaidi. Nakusikiliza.
PROFESA: Kwa kweli haina mwisho usifikiri nakudanganya. Nimesema
Aya ya 1 ina Herufi 15
Aya ya 2 ina Herufi 19
Aya ya 3 ina Herufi 15
Aya ya 4 ina Herufi 17
Aya ya 5 ina Herufi 15
Tumeona Odd Numbers za Herufi sasa angalia kwa makini Namba za Aya. Angalia Namba za Aya zenye Herufi 15 utaona Namba 1 ni ODD, Ya 3 ni ODD na Ya mwisho ni ODD pia
Angalia Mpango wa kushangaza. Angalia Maajabu je binaadamu anaweza kupanga mfano huu? Je unaona Mwenyeezi Mungu alivyoshusha. Sikiliza Al-Amin Hatujamaliza niache Niendelee na Safari isiyo na Mwisho. Ebu angalia Namba za Ukorofi zilivyopangwa katika Kuruani. Ikiwa mtu anajifanya Mkorofi basi ujue Mwenyeezi Mungu ni Mwingi wa Ukorofi. Ukijifanya Mjanja basi yeye ndiye mwenyewe aliye Mjanja pia kuliko wewe. Kaishusha Sura Hii na Maajabu. Ukorofi kwa ukorofi. Abu Jahl na Mkewe kashushiwa Aya za kulingana na Ukorofi wake. Hebu tuendelee kama nilivyosema hakuna Mwisho.
AL -AMIN ALI HAMAD: Yaani Hatujamaliza?
PROFESA: Tupo Mwazoni. Bado sana kama nilivyosema hakuna mwisho.
AL-AMIN ALI HAMAD: Allahu Akbar
PROFESA:Kuhusu ODD numbers au Namba za Ukorofi kuna mengi mengineyo kama ifuatavyo:
SURA HII INA MANENO 23 NA NAMBA HII NI ODD
SURA INA HERUFI 81 NA NAMBA HII NI ODD
JINA LA SURA NI المَسَد (MASAD) LINA HERUFI 5 NA NAMBA HII NI ODD
JINA المَسَد UKILIGEUZA KATIKA NAMBA ZA ABJAD YAANI THAMANI YA HERUFI ZILIZOTUMIKA KATIKA ENZI YA MTUME KWANI WALIZITUMIA KAMA NAMBA BASI UTAPATA JUMLA YA HERUFI NI 135 NA NAMBA HII NI ODD
JUMLA YA HERUFI ZA KIARABU NI 28 NA JUMLA YA HERUFI ZILIZOTUMIKA KATIKA SURA HII NI 21 NA NAMBA HII NI ODD
AYA ZOTE 5 ZA SURA HII UKIZIGEUZA KATIKA THAMANI YA ABJAD YAANI THAMANI YA HERUFI ZILIZOTUMIKA KATIKA ENZI YA MTUME KWANI WALIZITUMIA HERUFI KAMA NAMBA BASI UTAPATA JUMLA YA HERUFI ZA SURA HII NI 5431 NA NAMBA HII NI ODD
AL-AMIN ALI HAMAD: Allahu Akbar. Allahu Akbar. Kwa kweli siyo mambo madogo. Kwa kweli inatisha. Hebu fikiri ukaidi tunaoufanya katika maisha yetu? Ndiyo maana Maisha yamejaa matatizo. kwa ajili ya Ukorofi wetu na Mwenyeezi Mungu Mkorofi zaidi yetu. Hii Sura haikushuka Bure. Allahu Akbar. Kumbe kuna Siri kubwa namna hii. Haya siyo madogo hata kidogo. Profesa Haya mambo kweli makubwa sana.
PROFESA: Haina Mwisho. Kama nilivyosema kwani kuna Ya Ajabu Zaidi wewe nisikilize tu.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa hizi Elimu unazijua vipi? umesoma wapi
PROFESA: Huko kwetu Arabuni kuna wanavyuoni wanaofanya Utafiti Usiku na Mchana kwa juhudi kubwa sana na kisha Wanasahishishana kama kuna Makosa katika Utafiti.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Mwenyeezi Mungu akuzidishie Elimu. Asante Sana kwa Kunikaribisha na kunipa Habari Nzuri Sana
PROFESA: Sijamaliza kwani bado ndiyo mwanzo. Hii Sura ina Mengi. Ukiingia Usiku basi utalala Kwangu usiwe na wasiwasi.
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante sana Profesa. Nitasubiri. Waswahili wanasema “Mtaka cha Uvunguni Sharti Ainame” basi mimi nitafanya Uvumilivu kwani kwa kweli nina hamu sana ya kusoma Elimu hii kubwa. Allahu Akbar.
Lakini Kuna Mtu Mmoja alisema “Mwenye Kutaka Cha Uvunguni basi Inua Tanda” Huyu aligeuza Msemo. Ana maana ya Kusema Mwenye Kutaka Cha Uvunguni basi Ainue Kitanda yaani Asiiname. Ha ha ha ha ha ha ha ha ha. Huu Ni Utani. Yaani Huyu aliyegeuza hivi ni Mvivu yaani alikuwa hataki kuinama. Ha ha Ha Ha Haha (kicheko)
PROFESA: Na sisi Pia kwetu tunapenda kutaniana sana. Watu wanapenda sana Utani baina yao. Kwa mfano wanaposalimiana wanasema
“KAYFA HALUKA WA ZAMMANI SHOROMBOROM”
Je unajua maana yake? Yaani “VIPI HALI KATIKA HAYA MASIKU YA MVURUGO” Yaani masiku ya Taabu Duniani”. Lakini Lugha inachekesha. Neno SHOROMBOROM ni neno la kuchekesha. Sijui Warabu walilipata Neno Hili wapi.
Asante sana. Sasa Tuendelee Muujiza.
Hebu Niilete tena Sura Ya Al-Masad tuichunguze vizuri zaidi.
تَبَّتۡ يَدَآ أَبِى لَهَبٍ۬ وَتَبَّ (١) مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُ ۥ وَمَا ڪَسَبَ (٢) سَيَصۡلَىٰ نَارً۬ا ذَاتَ لَهَبٍ۬ (٣) وَٱمۡرَأَتُهُ ۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ (٤) فِى جِيدِهَا حَبۡلٌ۬ مِّن مَّسَدِۭ (٥)
Hebu Tuchague maneno ya ODD na EVEN Katika Sura Hii na Kisha Tuone Maajabu Yasiyo na Mwisho:
Angalia Maneno niliyoyatia Rangi Nyekundu ni Maneno ya ODD kwani neno تَبَّتۡ ni la Kwanza yaani Namba 1, Neno أَبِى ni la tatu yaani namba 3 yaani ODD na hivyo hivyo mpaka Mwisho kwa hiyo Jumla ya maneno ODD katika Sura Hii ni maneno 12 na Jumla ya Maneno yaliyobaki ni EVEN nayo ni 11
Sasa angalia Muujiza ufuatao:
Ukigeuza maneno ya ODD katika Namba za Kiarabu za ABJAD hapo zamani (kwani walitumia Herufi kama namba) na kisha ukajumlisha utapata Jumla ni 3049 na Ukigeuza Maneno 11 ambayo yapo katika sehemu (Position) ya EVEN Numbers katika Namba za ABJAD utapata Jumla ni 2382
Yaani ODD=3049 na EVEN =2382
Angalia Maajabu Jumla ya Maneno ODD namba tuliyopata ni ODD pia nayo ni 3049
Na Jumla ya Maneno ya EVEN Numbers tuliyoyapata ni EVEN pia nayo ni 2382
Angalia Maajabu. Katika Kuruani Kila Kitu Kimehesabiwa.
Tumehesabu na Kujumlisha Thamani ya Maneno yaliyokuwa ODD tumepata namba ODD na Tumehesabu na kujumlisha Thamani ya Maneno yaliyokuwa EVEN na tumepata Namba ya EVEN.
AL-AMIN ALI HAMAD: Allahu Akbar. Haya Maajabu hayana mwisho. Hakuna Mwisho. Allahu Akbar. Hivi Tutamaliza Sura Hii Leo?
PROFESA: Haiwezekani kabisa. Hakuna Mwisho. Mwenyeezi Mungu Mkubwa.Hii ni Lugha Yake. Inashangaza sana. Allahu Akbar.
Tumeona maneno ya ODD na EVEN hapo juu yanavyoshangaza. Sasa Tufanye hivyo hivyo na Herufi. Ngoja Nilete zile Aya za Sura Hii ya Al-Masad kisha Tugawe herufi za ODD na EVEN tuone Maajabu yasiyo na Mwisho:
تَبَّتۡ يَدَآ أَبِى لَهَبٍ۬ وَتَبَّ (١) مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُ ۥ وَمَا ڪَسَبَ (٢) سَيَصۡلَىٰ نَارً۬ا ذَاتَ لَهَبٍ۬ (٣) وَٱمۡرَأَتُهُ ۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ (٤) فِى جِيدِهَا حَبۡلٌ۬ مِّن مَّسَدِۭ (٥)
Herufi ODD ni TAA ya kwanza, Kisha TAA inayofuata yaani ya Tatu, kisha DAL yaani herufi ya 5 na ukigechagua Herufi zote hivi mpaka mwisho na Kisha Uzigeuze katika Thamani Ya Herufi zilizotumika Hapo Zamani. (Waarabu na Mataifa mengineyo hapo zamani walitumia Herufi kuwakilisha Namba kwa mfano Alif ilikuwa ikiwakilisha Namba 1, Baa ilikuwa ikiwakilisha namba 2 na hivyo hivyo namba zote ziliwakilishwa na Herufi). Ukifanya Hivyo kisha ujumlishe Thamani ya Herufi Hizi utapata Jumla yake ni 3049. Na ukifanya hivyo na Herufi za ODD kwa mfano Herufi EVEN ya kwanza katika Sura Hii ni BAA kwani ni ya pili na YAA kwani ni ya Nne. Hivyo hivyo ukikusanya Herufi zote za EVEN katika Sura Hii kisha uzigeuze hatika Thamani ya Namba za hapo zamani na kisha ujumlishe basi utapata Jumla ni 2382.
Angalia Maajabu Ya Namba hizi.
Herufi ODD tumepata namba ODD pia yaani 3049
Herufi EVEN tumepata namba EVEN pia yaani 2382
Yaani Mpangilio wa Herufi za ODD na Jumla ya Thamani yake ni ODD na Pia Mpangilio wa EVEN tumepata Jumla ya Thamani yajke EVEN
Hebu sasa Tulinganishe na Utafiti wa maneno Tuliyofanya hapa Juu.
Tumesema
Maneno ODD ya Sura Hii Thamani Yake ni 3049
Maneno EVEN ya Sura Hii Thamani Yake ni 2382
Na sasa Herufi pia inalingana
Herufi ODD ya Sura Hii Thamani Yake ni 3049
Herufi EVEN ya Sura Hii Thamani Yake ni 2382
Hebu Tushangae. Allahu Akbar. Mbona Namba za Maneno na Herufi Zinalingana? Angalia Muujiza?
AL-AMIN ALI HAMAD: Ma Profesa wa Vyuo Vikuu Ukiwaonyesha Haya watabaki watashangaa sana. Hebu angalia Maajabu. Huu Muujiza Mkubwa sana. ODD number ya Maneno na Herufi tu inatutoa Povu Mdomoni. Profesa Ninakuomba Tunywe Kahawa na Ikiwezekana Uniletee zile Tende Za Madina kwani Mambo haya Yahitaji Nguvu Mpya . Profesa Umetoa Kubwa Na Ninahitaji Nguvu Mpya.. Unajua Haya Mambo makubwa sana tena sana.
PROFESA:Ndugu Al-Amin Haya ni Tonye la Bahari, Kuna mengi yanakuja. Ngojea nilete Kahawa na tende. Nisubiri.
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Sana Profesa Tende hizi tamu sana. Leo siwezi kulala kwani Nikinywa kahawa huwi silali. Lakini Nitakuwa nikifikiri haya uliyonifundisha.
Kwa vipi? Jumla Maneno Ya ODD tumepata namba ODD na Jumla ya maneno ya EVEN tumepata Namba Even. Na hivyo hivyo Jumla ya Herufi pia. Yaani Jumla ya Herufi ODD tumepata Namba ODD na Jumla Ya Herufi EVEN tumepata namba EVEN. Na Ajabu Ni kwamba Jumla ya Herufi na Maneno ODD ni ile ile 3049 na Jumla ya Herufi na Maneno EVEN ni ile ile 2382. Angalia Ilivyopangwa. Heiwezekani Binaadamu kuhesabu na kupanga hivi.
Ngoja Nifupishe na Nipange ili nione vizuri:
MANENO ODD=3049
MANENO EVEN-=2382
HERUFI ODD=3049
HERUFI EVEN=2382
Allahu Akbar. Angalia Muujiza. Allahu Akbar Allahu Akbar.
Hivi Binaadamu anaweza kupanga hivi? Nani duniani anaweza kuandika na kuhesabu mfano huu? Haiwezekani Hata Kidogo. Kuruani siyo Mchezo.
Profesa Mbona Hakuna Mwisho. Muujiza baada ya Muujiza katika Sura hii Moja tu. Sasa Je Msahafu?
Tutafika Huko?
PROFESA: Rafiki yangu hatufiki kabisa. Huko Tunapokwenda kunatisha. Kila kitu kinatisha. Mauti, Makaburini. Yote yanatisha. Kweli siyo uongo, Hatujui lini tutaondoka Dunia, Wapi na Kwa njia gani. Mwenyeezi Mungu ameficha.
AL-AMIN ALI HAMAD: Allahu Akbar. Kwa kweli Inatisha sana tena sana.
PROFESA: Sasa tuendelee na Miujiza kwani bado mengi ya kuzungumza kuhusu Sura hii Ya Al-Masad.
Ngojea tuilete ile Sura Tena Ili tuichunguze vizuri zaidi:
تَبَّتۡ يَدَآ أَبِى لَهَبٍ۬ وَتَبَّ (١) مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُ ۥ وَمَا ڪَسَبَ (٢) سَيَصۡلَىٰ نَارً۬ا ذَاتَ لَهَبٍ۬ (٣) وَٱمۡرَأَتُهُ ۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ (٤) فِى جِيدِهَا حَبۡلٌ۬ مِّن مَّسَدِۭ (٥)
Tumeona kwamba Jumla ya Thamani Ya Maneno Yote Yaliyo katika Sehemu (Position) Ya ODD tumepata Jumla Ya Thamani yake ni 3049 ambayo namba hii pia ni ODD na hivyo hivyo Jumla ya Thamani Ya Maneno Yaliyo katika Sehemu (Position) Ya EVEN tumepata Jumla ya Thamani yake ni 2382 na namba hii ni EVEN
Kwa kifupi
POSITION AU SEHEMU YA ODD NUMBER=3049
POSITION AU SEHEMU YA EVEN NUMBER=2382
Sasa Tupange Namba Zote Tulizopata katika Sura Hii na kisha Tuchukue Namba ODD na EVEN kisha Tujumlishe. Hapo Mwanzo tulichukua zile Namba za Positions za Maneno ya ODD na EVEN na hivi sasa tusiangalie Positons au Sehemu ya Maneno bali Namba Peke yake za maneno yote na kisha Tuchunguze namba za Kila Neno na Tuchague EVEN na ODD.
Ukifanya Hivyo na kizijumlisha zile Namba ODD utapata Jumla yake ni 3153 na Ukifanya Hivyo hivyo na Even Numbers utapata Namba 2278
Ngojea nipange vizuri kwa mfano namba zote tulizosoma hapa juu ili tupate kuelewa vizuri zaidi Jumla ya Namba Tulizosoma katika Aya za Sura Ya Al-Masad.
MPANGILIO KUFUATANA NA THAMANI AU NAMBA YA MANENO ODD=3153
MPANGILIO KUFUATANA NA THAMANI AU NAMBA YA MANENO EVEN=2278
MPANGILIO KUFUATANA NA SEHEMU AU POSITION YA MANENO ODD=3049
MPANGILIO KUFUATANA NA SEHEMU AU POSITION YA MANENO EVEN=2382
Hebu tutoe Namba za Hapo Juu. Yaani
3153-3049=104
2382-2278=104
Tumetoa Namba hizi mbili na tunaona Muiano wa Kiajabu.
Majawabu Yanafanana.
Yaani tunapata namba 104
Ajabu Ni kwamba Jina La Sura Ni Al-MSAD
Neno Masad Lina Herufi Tatu yaani
MIM + SIN + DAL
Tukiligeuza Neno Hili katika zile Namba za ABJAD utapata namba 104
40 + 6-0 + 4=104
Angalia Muashirio wa Kiajabu na Namba 104
AL-AMIN: Profesa Hii Kweli Inashangaza. Yaani Namba 104 Tuliyopata Hapa Juu inaashiria Jina La Sura Yaani MASAD.
Kwa kweli Inashangaza.
Kwa nini Muiano Huu Profesa?
PROFESA: Kwa kweli sijui. Huu ndiyo mwisho wa Elimu yangu. Mwenyeezi Mungu anajua zaidi. Labda Kuna Siri Nyinginezo kwa watu wa Baadaye au labda zina maana Kwa Majini. Je unajua Kwamba Kuruani wameshushiwa Majini Pia? Siyo binaadamu Tu peke yao. Mwenyeezi Mungu amesema katika Sura namba 5 Aya 101
يَـٰٓأَيُّہَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَسۡـَٔلُواْ عَنۡ أَشۡيَآءَ إِن تُبۡدَ لَكُمۡ تَسُؤۡكُمۡ وَإِن تَسۡـَٔلُواْ عَنۡہَا حِينَ يُنَزَّلُ ٱلۡقُرۡءَانُ تُبۡدَ لَكُمۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡہَاۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ۬ (١٠١)
Katika Aya Hii Mwenyeezi Mungu anasema kwamba Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatakuchukizeni. Na kama mtayauliza, maadamu inateremshwa Qurani mtabainishiwa. Mwenyezi Mungu amesamehe hayo. Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mpole sana.
Huenda Mwenyeezi Mungu ametufichia Siri nyinginezo ambazo laiti tuzingezilijua huenda ingekuwa Habari mbaya na ingekuwa mbaya kuzijua. Kuna Mengine mengi siyo mazuri kuyajua kwani ni kheri kwetu.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa mwenyeezi Mungu akubariki. Unasema Kweli. Lakini tubaki tukifikiri kwani Huu siyo muujiza Mdogo. Allahu Akbar.
PROFESA:Tumezungumzia Namba za Ukorofi. Na kuna Maudhui (Topic)Nyinginezo bado Kuzianza kama Tulivyopanga. Je unajua Sura Ya Masad Hatujaimaliza Kwani ina mengi. Kwa leo nitaishia Hapa. Mwenyeezi Mungu Akipenda Kesho Asubuhi tutazungumza Safari Yetu kwa Majini
AL-AMIN AKLI HAMAD: Hii Inanitisha. Sijui kama Nitaweza kulala usiku wa leo. Profesa Una Majini Nyumbani kwako.
PROFESA: Nimekuambia Usiwe na Wasiwasi. Utaona Kesho Maajabu Makubwa. Leo Sahau Na Usiogope. Mimi Sina Majini Nyumbani Kwangu kwani hiyo siyo kazi yangu. Nimesema Safari kwa Majini yaani Safari kwenda katika Sura Ya Kuruani Inayoitwa Al-Jinn ili tuweze Kusoma Kisa Kizuri Sana Cha Majini kwa hiyo unielewe vizuri kwani sina maana kwamba tutakutana na majini. Tafadhali Nielewe. Yaani Twende Tukaisome kwa pamoja yaani Tusafiri katrika Sura Hiyo. Nadhani Umenifahamu. Sasa Ngojea Tule Chakula Cha JionI, Tuswali sala Ya Ishaa. Na kisha Tulale. Inshaallah Kesho siku mpya na tutaona mapya. Mola akipenda.
AL-AMIN ALI HAMAD: Alahamdulilah Nakushukuru Profesa kwa wema wako Mkubwa Sana. Mwenyeezi Mungu Akubariki akupe Afya, Elimu Kubwa na Umri Mrefu.
PROFESA:Amin
Mazungumzo (Safari Katika Sura Ya Al-Jinn) yataanza karibuni inshaallah katika Mlango Huu Huu …………………………..