UTAFITI MBALIMBALI KATIKA DINI NA SAYANSI
IMEANDALIWA NA AL-AMIN ALI HAMAD
NAKUKARIBISHENI KATIKA SAFARI MBALIMBALI
MAZUNGUMZO BAINA YANGU NA PROFESA WA PHYSICS KATIKA CHUO KIKUU PARIS (FRANCE)
Alhamdulilah leo Tarehe 17/09/2022 Wakati wa Jioni. Kuna utulivu na ni wakati mzuri sana kuendelea na kuandika Mazungumzo yangu na Professor wa Physics ambaye asili yake ni kutoka Algeria. Kwa sasa Amestahafu na Nilifurahi sana kwamba alikubali makaribisho katika nyumba yangu. Mazungumzo yetu yalikuwa kwa Lugha ya Kifaransa. Kama unavyoelewa Algeria ilitawaliwa na Wafaransa. Asili yake ni Mwarabu kutoka Algeria lakini anazungumza Kiarabu cha Lahaja ya Algeria na Pia Lugha yao Nyingineyo ambayo inaitwa Berber. Pia aliweza Kuzungumza Lugha ya Kiarabu Fasihi. Niliweza kuzungumza naye kwa Kiarabu cha Fasihi lakini amezoea sana Kifaransa na kila ninapoanza kuzungumza Kiarabu basi ananijibu Kifaransa kwani ameishi miaka Mingi huko Ufaransa. Sikupendelea kumpa Taabu na kwa hiyo niliwasiliana naye kwa kifaransa. Namshukuru Mungu ninaizungumza Lugha Ya Kifaransa vizuri bila Tatizo.
Nilisoma mambo mengi yanayohusu Dini ya Kiislamu na Sayansi. Nilifurahi sana kukutana na Mtaalamu kama huyu ambaye alikuwa Mwalimu katika University ya Ufaransa inayojulikana kama Sorbourne mjini Paris kwa muda karibu Miaka zaidi ya 50.
Bwana huyu ana Experience ya Ualimu wa Sayansi kwa muda mrefu na Somo alilokuwa akifundisha ni Physics.
Hapa chini nimefasiri Mazungumzo yangu na Profesa huyu kwa lugha ya Kiswahili. Kuna Ziyada na Pia Upungufu lakini Muhimu ni Madhumuni. Nimenukulu kila kitu ili utamu wa Mazungumzo usipotee.
Ijapokuwa Siku ya Leo kuna Utulivu lakini kuna Watoto wa Majirani ambao wanasukuma vile Vibaskeli vidogo vidogo vya Gurudumu Moja na kwa hiyo kuna Sauti hizo ambazo nimezizoea kwa sasa. Sehemu ambayo Wanacheza ni Mbele ya Nyumba yangu. Sipendelei kuwakemea kwani watoto wote wanafanya haya na mimi pia nilipokuwa mtoto nilikuwa mtundu zaidi yao.
Nilipokuwa umri wao nilikuwa nikisukuma Matairi ya Baskeli ya Chuma Barabarani na Pia Matairi hayo yalikuwa na Ukelele kuliko Matairi ya watoto hawa ambayo ni ya Mpira.
Nilikuwa nikitengeneza Vigari vidogo vidogo vya Miti na kutumia Gundi ya asili kutoka katika Shina la Miti ya Gundi. Magari haya tulikuwa tukiyaburuza Barabarani kwa hatari kubwa kwani Magari pia yalikuwa yakitupitia. Tulifanya Utundu wa kila aina. Nakumbuka Tulipokuwa tukitembelea Mto uliokuwa katika Kijiji changu. Mto huo una mchanga Mweupe kama ule wa Baharini na Hapo tulikuwa tukicheza Mipira. Na wakati mwingine tulikuwa tukicheza katika Mawe makubwa ya asili ambayo yalikuwa katikati ya mto kwa kutereza kuanzia juu mpaka chini. Wazazi na wazee wa Mji walitukataza tusiende katika Mto huo kwani wakati mwingine kuna Maji yanayoweza kuja kwa nguvu na maji haya yana nguvu sana. Yanapokuja huwa yamebeba mapande makubwa ya mawe na hata kuchukua Magari na Matrekta ambayo yalijaribu kupita katika Mto huo.
Nakumbuka niliona kwa macho yangu BASI lilokwama wakati maji yamejaa na watu wanatoka madirishani kwa njia ya kamba. Nakumbuka pia kwamba Basi hilo lilizikwa na Maji chini ya Sakafu ya mto mpaka likapotea kabisa lakini watu wote waliokolewa kabla ya Basi hilo kupotea.. Siku moja niliona hapo karibu na mto Chui aliyekufa lakini Ngozi imeshachunwa na huyu aliuawa na watu kwa ajili ya ngozi.
Nakumbuka Sauti za Fisi Usiku. Na pia Sauti ya Mto unapojaa na kunguruma. Kwa kweli inatisha. Katika Kiji hicho kuna Mlima ambao Wataalamu wanasema kuna Volcano na kwa hiyo huenda siku moja utapasuka na kwa hiyo watu wengi wanapotaka kujenga nyumba wanakwenda upande wa pili wa Kijiji kwani waliogopea ule Mlima utakapopasuka basi huenda ukamiminisha Lava ya moto katika Nyumba zao.
Kijiji Kidogo lakini Mengi ya Kuzumgumza. Nakumbuka kuna Daraja lililojengwa na Mjerumani alipokuwa Akitawala. Daraja hili halitumiki tena kwani Limeharibika lakini limebaki hapo hapo na hakuna anayelitumia kwani ni hatari sana.
Kuna Kisima kinachobubujika Maji. Hapo zamani kisima hicho kilikuwa kidogo sana lakini miaka mingi imepita na sasa kimepanuka. Inasemekana kwamba tembo au ngombe aliwahi kuzama katika kisima hicho sijui kama habari hizi ni za kweli.
Tulikuwa tukipita karibu na kisima hicho wakati wa kwenda shule ya msingi kila siku Asubuhi na Pia Tunaporudi Shule. Nakumbuka siku moja tuliona Nyoka Mkubwa Juu ya Mti karibu na Njia ya Kwenda Shule na Tukakimbia na kumjuulisha Mjomba wangu ambaye alikuwa na Bunduki zaidi ya moja Nyumbani kwake. Mjoma alikuwa anapenda kukusanya Bunduki na Kuzitundika Ukutani. Na siku hiyo alichukua Bunduki ya Bomba Mbili na kuja Kumuua Nyoka Yule. Alipiga Risasi Mbili na Mara Lile Joka likaanza Kujiachia Juu ya Mti na Mara Likaanguka Chini. Hakuna Aliyekwenda kuchunguza alipoangukia lakini nina hakika Risasi mbili zilimmaliza.
Kwa kweli Maisha Ya utoto yana Raha zake. Tulikuwa tukicheza Kujificha na Kutafutana na katika Mchezo huo kuna wakati tulijificha Juu ya Miti. Tulikuwa Tukiitana. “NJOO” “NJOO” atakayekumata naye ndiye atakayejificha na wengine watamtafuta na hivyo hivyo. Hatuwasikilizi wazee wetu kwani tulikuwa tukienda miguu mitupu katika pori ambalo lina Miba.
Msomaji Samahani Fikra zangu zimekwenda mbali Katika Utoto na nimesahau kuzungumza ile ziyara ya Profesa. Kwa kweli kuna mengi ya kuelezea ya utoto.
Sasa Wakati umefika wa Kuwaletea yale Mazungumzo.
Ilikuwa Asubuhi saa Tano wakati nilisikia Mlango unagongwa na nilipofungua mara nikamuona Mzee aliyekuwa na Upara uliong’aa sana kama kwamba ametia Mafuta. Mzee huyu alivaa mewani za Duara kama vile Mewani Za Ghandi. Alikuwa na Tabasamu la Kuonyesha Furaha. Kwa kukisia Nilimpa Umri wa Miaka 75 au 80. Huyu ndiye Profesa Mahmood ambaye nilijuana naye katika Chuo Kikuu. Profesa wangu Bwana Phillipson alikuwa Rafiki Yake na Hivi ndivyo nilivyomjua Bwana Huyu.
PROFESA: Asalaam Alaykum Kijana Wangu Al-Amin
AL-AMIN ALI HAMAD: Alaykum Salaam Profesa
PROFESA:Nilifuata ulivyonielekeza na Alhamdulilah sikupata taabu kuja kwako
AL-AMIN ALI HAMAD:Alhamdulilah Nashukuru Mungu umefika Salama bila Tatizo. Na nimefurahi sana kwa kuitikia Makaribisho na kuweza kuja kwangu.
PROFESA:Al-Hamdulilah Namshukuru Mungu
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa kabla ya chochote ningependelea kukukaribisha kinywaji na chakula.
PROFESA:Maji ya kunywa yanatosha Asante sana.
AL-AMIN ALI HAMAD:Profesa leo ni mara ya kwanza kunizuru haiwezekani uondoke bila ya kula chochote. Katika Nchi yangu unapozuru nyumba ya mtu basi huwezi kuondoka bila ya kula chochote kwani utapewa chochote angalau Kahawa.
PROFESA: Asante sana sina budi kwa hiyo nitakula chochote ulichonacho.
AL-AMIN ALI HAMAD: Nitakutengenezea Chakula Cha Kitamaduni. Yaani Chakula Kinachoitwa Ugali na Mchuzi wa Samaki wa Nazi.
PROFESA: Asante sana. Kwa kweli sijawahi kula chakula chenye jina hilo. Je Ugali ni kitu gani?
AL-AMIN ALI HAMAD: Ugali ni Unga ambao unachamganywa na Maji na kisha Unasongwa. Ni Chakula kizuri sana kwa Afya. Ni cha Asili. Ni Chakula Safi. Wenye kukila wanakuwa na nguvu. lakini uwe macho kwani utakapokuja katika Nchi Yangu na Kula Ugali basi utasahau huko Arabuni na Pia unaweza kumsahau Mkewe na kujikuta unaoa Kwetu. Yaani kama umeoa basi usije kwetu.
PROFESA: hahahahaha Al-Amin wewe Matata Sana.
AL-AMIN ALI HAMAD: karibu Profesa Chakula Tayari.
PROFESA: Alhamdulilah Ugali na Samaki Tamu sana. Usipojiangalia unaweza kujiuma Vidole.
AL-AMIN ALI HAMAD: Ungepata Mboga Ya Mchicha na Kirumbu ungeimba Nyimbo za Kiarabu zote.
PROFESA: HAHAHAHAHAHAHAHAHA (Profesa Anacheka)
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa sasa tunywe kahawa na Tende.
PROFESA: Asante sana Mwenyeezi Mungu akupe kila la kheri kwa kunikaribisha.
AL-AMIN ALI HAMAD: Mwenyeezi Mungu Akubariki kwa Kuja Nyumbani kwangu.
PROFESA:Nia Yangu leo tuzungumze mambo mbalimbali.
AL-AMIN ALI HAMAD: Amin
PROFESA: Nitakuelezea Jambo la kushangaza katika Kuruani Tukufu ambalo bado ninalifanyia utafiti.
AL-AMIN ALI HAMAD:Ningependelea kukusikiliza na nina hamu sana ya kusoma mapya.
PROFESA:Hapo zamani Waarabu na Mataifa Mengineyo ya wakati huo yalikuwa yakitumia Herufi kuwakilisha Namba kwa mfano Herufi Alif Iliwakilisha Namba 1, Herufi Baa Iliwakilisha Namba 2 na hivyo hivyo namba zote tunazozijua leo ziliwakilishwa na Herufi. Hizi zilijulikana kama Thamni Za Herufi za Abjad
AL-AMIN ALIHAMAD: Naam Profesa
PROFESA: Sasa tuone Maajabu yafuatayo:
Abjad Ya Neno SURA + 21=Abjad Ya Neno AMBIYAA + 10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 +71
AL-AMIN ALI HAMAD:Bado Sijaelewa. kwa kweli utafikiri kichina kwani inababaisha sana.hebu fafanua Profesa.
PROFESA:Pole Pole nitakufahamisha.
Neno سورة lina herufi 4
ukiligeuza katika Values au Thamani ya Namba za hapo zamani utapata kama ifuatavyo:
Herufi SIN=60 Herufi Waw= 6 Herufi Ra=200 Herufi Taa Marboutta = 5
Tukijumlisha tutapata= 60 + 6 + 200 + 5=271
Kwa hiyo Neno سورة Thamani yake ni 271
Na tukifanya hivyo Hivyo neno الانبياء tutapata Jumla ya Herufi zake ni 96
sasa tuzijumlishe ili tuone ya kushangaza
Abjad Ya Neno SURA=271 + 21=Abjad Ya Neno AMBIYAA=96 + 10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 +71
yaani
271 + 21 (Hii 21 Ni Namba ya Sura Ya Manabii katika Kuruani yaani AL_AMBIYAA au الانبياء
Ngojea Nirahisishe Zaidi Tumesema
271 + 21= 96 +10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 + 71
271 ni Thamani ya neno SURA سورة
21 ni Namba ya Sura Ya Al-Ambiya الانبياء
96 ni Thamani Ya Neno Al-Ambiya الانبياء
10 Ni Sura Ya Nabii Yunus
11 Ni Sura Ya Nabii Hud
12 Ni Sura Ya Nabii Yusuf
14 Ni Sura Ya Nabii Ibrahim
Sura Namba 31 Ni Sura Ya Luqman au Nabii Luqman (Wanavyuoni wamegawanyika. Wengi wanasema alikuwa siyo Nabii lakini Mtu wa Busara)
47 Ni Sura Ya Nabii na Mtume Mohamad
71 Ni Sura Ya Ni Sura Ya Nabii Nuhu
Hizi Ni Jumla Ya Sura 7 ambazo zimeitwa majina ya Manabii. Kuhusu Luqman kuna Mgawanyiko. Waliosema kwamba ni Nabii wanahesabu Sura 7 na wanaosema kwamba alikuwa Mtu mwenye Busara basi wanahesabu Sura kuwa 6
Hebu tuzilete tena zile Namba na kisha tuzijumlishe:
271 + 21= 96 +10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 + 71
271 + 21=292 na 96 +10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 + 71=292
Unaona ya Kushangaza.
Tunapata Namba zinazowiana. au Balanced Equations
Kila Upande una 292.
Je unaona ya Kushangaza.
Ngojea nifafanue zaidi:
Abjad Ya Neno SURA + 21=Abjad Ya Neno AMBIYAA + 10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 +71
Mstari huu hapa Juu ni sawa na Mstari hapa chini
271 + 21= 96 +10 + 11 + 12 + 14 + 31 + 47 + 71
Ni kama kusema:
Thamani ya Neno SURA Kujumlisha Namba Ya Sura Ya AL_AMBIYAA ni sawa na Thamani ya Neno Al-Ambiyaa Kujumlisha Sura Zote ambazo zimetiwa majina Ya Mabii katika Kuruani Tukufu.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Kwa kweli inashangaza lakini inababaisha. Kwa nini jawabu ni 192? kwa nini Jawabu kila upande linalingana? kuna siri gani hapa?
Kinachotatanisha zaidi ni Kuihesabu Sura Ya Luqman katika Sura Ya Manabii. Kwani Wengi wanasema kwamba Luqman alikuwa siyo Nabii lakini ni Mtu wa Busara. Tumesoma kwamba Kuruani imetaja Manabii 25 tu sasa tukimhesabu Luqman kuwa Nabii basi inakuwa Jumla ya Manabii kutajika katika Kuruani ni 26. Angalia Mtatanisho. Lakini Ushahidi wa Kihesabu tuliouona hapa Juu wa Namba kulingana unaonyesha kwamba Luqman alikuwa Nabii. Mbona Hesabu Zinababaisha.
PROFESA: Elimu zetu bado changa na Kwa uwezo wake Mwenyeezi Mungu huenda kuna siku tutajua zaidi na ikiwa sisi hatutajua basi vizazi vya baadaye vitagundua mapya. Kwa sasa tuendelee kufanya utafiti. Kwa Kweli hapa ndiyo mwisho wa Elimu yangu. Sijui zaidi, Kwa kweli namba zinashangaza sana. Na kwa upande mwingine Namba hizi zinathibitisha kwamba Luqman alikuwa Nabii lakini sina Uhakika. Mwenyeezi Mungu anajua zaidi. Allahu Akbar.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Mwenyeezi Mungu akubariki kwa Utafiti huu wa kiajabu. Ni Utafiti mzuri sana na huenda tukagundua mengi hapo baadaye. Utafiti wako umeweka msingi wa ugunduzi wa baadaye. Allahu Akbar. Profesa Je ungependa Kahawa Nyingine na Tende?
PROFESA: Asante sana. Niletee na Tafadhali punguza kahawa isiwe kali kwani itanizuia nisilale vizuri kwani sasa jioni imeingia. Kuna Mengi tutazungumza ikiwezekana.
AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Tafadhali ikiwezekana Ulale kwangu leo hii tupate Kuzungumza zaidi na Ukipenda Kesho Pia je unaonaje?
PROFESA:Asante sana. Naona ni fikira nzuri sana. Leo Nitalala kwako na Ikiwezekana Tutazungumza Mengi Kwa uwezo wake Mwenyeezi Mungu
AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Sana. Mwenyeezi Mungu akubariki.
PROFESA: Amin.
MAZUNGUMZO YANAENDELEA…………………….