SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Miujiza Ya Kuruani-7

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MIUJIZA MBALIMBALI YA KUSHANGAZA

Kabla ya Kuanza kuandika Mlango huu ninamuomba Mwenyeezi Mungu atakabali kazi hizi zisiwe isipokuwa kwa ajili yake tu pekee na siyo kutaka tamaa nyingine yeyote ya duniani. Na dua nyingine ni kumshukuru kwa kila alichotupa na pia kwa kila asichotupa. Kwani kila Alichotupa kuna hekima ndani yake na pia asichotupa pia kuna hekima ndani yake. Tunasema “Alhamdulilahi” katika kila hali. 

Mlango huu utahusiana na Miujiza Mbalimbali ya Kuruani Tukufu.

Mlango huu na Mingineyo ya Miujiza na Sayansi ni Maoni ambayo huenda tumepata na huenda tumekosa katika Utafiti wetu. Kwa hiyo ipo wazi na kama una maoni yako unaweza kugeuza maana yake kama upendavyo mradi tu uwe katika ukweli.

Nia na Lengo kubwa ya kazi yangu ni kuitakasa kuruani na Kila Uwongo unaosema kwamba kuruani siyo maneno ya Mwenyeezi Mungu au Kuruani imeguswa kwa kubadili, kuzidisha au kuounguza  Herufi, Aya au Sura zake. 

Friday 15 April 2022=14 Ramadan 1443

MUUJIZA WA SHAHADA NA KUKUA KWA MIMEA

1/MUUJIZA WA SHAHADA

Sura Namba 47 Ya Mohamad Aya Number 19

فَٱعۡلَمۡ أَنَّهُ ۥ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ وَٱسۡتَغۡفِرۡ لِذَنۢبِكَ وَلِلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَـٰتِ‌ۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مُتَقَلَّبَكُمۡ وَمَثۡوَٮٰكُمۡ (١٩)

TAFSIRI

29.Jua ya kwamba hakuna aabudiwaye kwahaki ila Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa dhambi zako na (dhambi) za Waislamu wanaume na Waislamu wanawake. Na Mwenyezi Mungu anajua mahali penu pa kwenda na kurudi (Yaani harakati za kila siku) na mahali penu pa kukaa.

Sura Namba 48 Ya Fath Aya Number 29

مُّحَمَّدٌ۬ رَّسُولُ ٱللَّهِ‌ۚ وَٱلَّذِينَ مَعَهُ ۥۤ أَشِدَّآءُ عَلَى ٱلۡكُفَّارِ رُحَمَآءُ بَيۡنَہُمۡ‌ۖ تَرَٮٰهُمۡ رُكَّعً۬ا سُجَّدً۬ا يَبۡتَغُونَ فَضۡلاً۬ مِّنَ ٱللَّهِ وَرِضۡوَٲنً۬ا‌ۖ سِيمَاهُمۡ فِى وُجُوهِهِم مِّنۡ أَثَرِ ٱلسُّجُودِ‌ۚ ذَٲلِكَ مَثَلُهُمۡ فِى ٱلتَّوۡرَٮٰةِ‌ۚ وَمَثَلُهُمۡ فِى ٱلۡإِنجِيلِ كَزَرۡعٍ أَخۡرَجَ شَطۡـَٔهُ ۥ فَـَٔازَرَهُ ۥ فَٱسۡتَغۡلَظَ فَٱسۡتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِۦ يُعۡجِبُ ٱلزُّرَّاعَ لِيَغِيظَ بِہِمُ ٱلۡكُفَّارَ‌ۗ وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ مِنۡہُم مَّغۡفِرَةً۬ وَأَجۡرًا عَظِيمَۢا (٢٩)

TAFSIRI

Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao. Utawaona wakiinama kwa kurukuu na kusujudu (pamoja), wakitafuta fadhila za Mwenyezi Mungu na radhi (yake). Alama zao zi katika nyuso zao, kwa taathira, (athari) ya kusujudu.Huu ndio mfano wao katika Taurati. Na mfano wao katika lnjili (umetajwa hivi): Kuwa (wao) ni kama mmea uliotoa matawi yake; kisha (matawi hayo) yakautia nguvu; ukawa mnene ukasimama sawasawa juu ya kigogo chake, ukawafurahisha walioupanda; ili awakasirishe makafiri kwa ajili yao. Mwenyezi Mungu amewaahidi walioamini na kutenda mema katika wao; msamaha na ujira mkubwa.

SHEREHE YA MUUJIZA KATIKA NGUZO YA KWANZA KATIKA UISLAMU-SHAHADA 

Aya Ya Kwanza Tunapata Kipande cha Ibara ya Shahada لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ na Aya ya Pili tunapata kipande cha pili cha Ibara ya Shahada مُّحَمَّدٌ۬ رَّسُولُ ٱللَّه

Tafsiri Ya لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّه ni “Hakuna Ilaha (Mungu) isipokuwa Allah (Mwenyeezi Mungu)”

Tafsiri Ya مُّحَمَّدٌ۬ رَّسُولُ ٱللَّه ni “Mohamad Ni Mjumbe wa Allah (Mwenyeezi Mungu)”

Vipande Vya Ibara viwili ndivyo vinavyohitajika katika Kuukubali Uislamu. Unapoingia katika dini ya Kiislamu inabiri Ukiri kwamba Mwenyeezi Mungu ni Mmoja Na Mtume wake ni Mohamad.

Ibara Hii pia ina Miujiza yake.

Muujiza wa leo ambao ningependelea kuuzungumzia ni Jumla ya Herufi ya Ibara hii ya Shahada.

Hebu Tuchunguze zaidi ibara hizi mbili

لَاۤ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ

مُّحَمَّدࣱ رَّسُولُ ٱللَّهِ

Herufi ya Alif ni ya Kwanza (Yaani Namba 1) kwa wingi wa kutumika katika kuruani

Herufi Lamu ni Ya Pili (Yaani namba 2) kwa wingi wa kutumika katika kuruani.

Herufi Ha ni ya Saba (Yaani Namba 7) Kwa wingi wa kutumika katika kuruani

Ukijumlisha Thamani Ya Herufi za Ibara لَاۤ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ utapata Jumla ni 29 Herufi Lam zipo 5 kwa hiyo 5 x 2 (Kukariri kutumika katika kuruani) =10 Herufi Alif zipo 5 kwa hiyo 5 x 1 (Kukariri kutumika katika kuruani) =5 Herufi Ha zipo 2 kwa hiyo 7 x 2 (Kukariri kutumika katika kuruani)=14 Jumla ni 29 (10 + 5 + 14)

Na Ukihesabu Ibara ya Pili katika Shahada: مُّحَمَّدࣱ رَّسُولُ ٱللَّهِ kama tulivyofanya hapa Juu utapata Jumla ya Thamani za herufi ni 85. (Yaani Utafute Thamani ya herufi zote za ibara hii. kama vile Herufi Mim, Haa, Dal, Raa, Sin, Waw, Lam na Alif)

Sasa Tujumlishe Thamani Ya Ibara Hizi Mbili za Shahada. 85 + 29= 114 Unaona Ya kushangaza!!!

Yaani Ibara Ya Shahada ambayo ni nguzo ya kwanza katika Uislamu ikifuatiwa na Sala, Zakati, Saumu na Haji (kwenda Hija)

لَاۤ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ مُّحَمَّدࣱ رَّسُولُ ٱللَّهِ (La ilaha ila llah, Mohamad Rasulullah) = 114

Ibara hii inawakilisha Sura zote za kuruani ambazo ni 114.

Huu siyo Muujiza mdogo. Thamani ya Ibara hii ni sawa na Sura zote za kuruani ambazo idadi yake ni Sura 114. Mpangilio huu wa kiajabu siyo wa kawaida hata kidogo. Imepangwa na Aliyeshusha Kuruani Hii. Ameipanga Kiajabu sana. Huwezi Kugeuza,Kupunguza au kuzidisha Sura, Aya au Herufi za Kuruani kwani ingekuwa hivyo basi Mizani hii isingelikuwako. Kuruani Imepimwa mpimo wa hali ya juu sana. Ni Engineering ya hali ya Juu sana hakuna mfano na hakutakuwa na mfano mpaka Mwenyeezi Mungu apende mwenyewe. Amesema kwamba Ataitunza na hivyo ndivyo ilivyo imetunzwa kuanzia karne ya 7 mpaka leo. Karne 14 (Miaka 1400) imepita na kuruani ipo vile vile kama ilivyopokelewa.

2/MUUJIZA WA KUKUA KWA MIMEA-PHOTOSYNTHESIS

كَزَرۡعٍ أَخۡرَجَ شَطۡـَٔهُ ۥ فَـَٔازَرَهُ ۥ فَٱسۡتَغۡلَظَ فَٱسۡتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِۦ

Kipande cha Aya hii kutoka katika Sura Namba 48 Ya Fath Aya Number 29 hapa Juu pia inatufundisha Sayansi ya Kukua kwa Miti. Aya Inasema kwamba Mimea Inazalisha Matawi, Kisha Matawi hayo yanautia Mti nguvu. Aya hii Inatufunulia Sayansi Ya Kukua kwa Mimea. Mashina Ya Mimea inakuwa minene na yenye nguvu kutokana na Matawi Yake. Sayansi inathibitisha Elimu hii kwamba Sababu ya kutia Mashina ya Mimea Nguvu na Kukua Kwake inatokana na chakula chake cha Hewa ya Carbondioxide, Maji na Mwanga wa Jua kutokana na Matawi (pamoja na majani yake) ya Mimea ambayo inachangia katika kubadili vifaa hivi katika Carbonhydrates na Kusababisha Kukua kwa mashina ya mimea. Kuruani Imetupa zawadi ya Kutufahamisha Sayansi hii kwa ufupisho wa Maneno yafuatayo Sita tu Wakati ambao Sayansi za kileo zimendika Vitabu na Vitabu kuhusu Jambo hili.

كَزَرۡعٍ Mimea

شَطۡـَٔهُ Matawi

فَـَٔازَرَهُ Kutia Nguvu

فَٱسۡتَغۡلَظَ Mimea Kuwa Minene (Mukubwa)

فَٱسۡتَوَىٰ Kusimama

سُوقِهِۦ Shina la Mmea

Nyongeza kutoka katika Elimu Ya Sayansi.

(Plants take in carbon dioxide and convert it to energy for growth. When the plant dies, carbon dioxide is given off from the decomposition of the plant. The role of carbon in plants is to foster healthier and more productive growth of the plants Plants absorb carbon dioxide from the air, combine it with water and light, and make carbohydrates — the process known as photosynthesis)

 14/05/2022

MUUJIZA WA AYA INAYOZUNGUMZIA “MAONO MAKALI”

Alhamdulilah Leo Mwenyeezi Mungu akipenda Nitazungumzia  Aya Namba  22 Kutoka katika Sura Ya Qaf. 

لَّقَدۡ كُنتَ فِى غَفۡلَةٍ۬ مِّنۡ هَـٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٌ۬ (٢٢)

Nitaanza na Tafsiri Ya Aya hii na Kisha nitasherehesha Na kudokeza Muujiza Wa Kisayansi. Ningependelea kusema kwamba Nitaunganisha  Sherehe za Wanavyuoni na Maoni Kisayansi. Siwezi kusema kwamba Kuna Maoni bora kuliko Nyingine. Ni jitihada za kibinaadamu na kama ilivyo Binaadamu anaweza kukosea. Nitajitahidi kuweka Rai mbalimbali na wewe msomaji uchague katika Rai hizi ile Rai unayohisi ni nzuri. Kuruani ni Muujiza Mkubwa. Miujiza yake haina mwisho. Allahu Akbar.

Wanavyuoni wamejitahidi sana katika kuelezea Aya Hii. Na utakuta Maoni mbalimbali kuhusu  Ibara فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٌ۬  ya Aya Hii.

TAFSIRI 

22. (Aambiwe): “Kwa hakika ulikuwa umo katika ghafla na jambo hili. Basi tumekuondolea (leo) pazia yako; kuona kwako leo kumekuwa kukali.”

SHEREHE

1.Aya hii inahusu mauti yanapomfika Binaadamu. Yaani Siku ya Kufariki Mwenyeezi Mungu atamjaalia mtu yule kuona  ukweli wa maisha yake. Ataona Mabaya na Mazuri.

2.Huenda Aya Hii Ina Husiana na Kuruani Tukufu. Hapo    mwanzo Mtume Mohamad ﷺ hakujua kitu chochote Yaani Kiliwa na Pazia lakini Mwenyeezi Mungu akamteremshia Kuruani yenye Mwanga na kuona Mazuri ya kutenda na Mabaya ya Kujiepusha.

3. Maoni ya Tatu na ambayo yana ushahidi zaidi ya maoni Mawili niliyotaja hapa juu ni kwamba Aya Hii inahusu Siku ya Kiama. Kwa sababu Aya zilizotangulia Aya Hii na zile zinazofuata zinazungumzia Siku ya Kiama. Kwa hiyo Aya hii inasema kwamba Siku ya Kiama Ndiyo Ukweli utakapodhihirika.  Tutaona kila kitu. Mazuri na Mabaya Yote yatakuwa wazi. Macho yatapewa uwezo wa kuona Haki na Batili. Tutaona Tuliyoyafanya yote. Yaani Kila kitendo kizuri na kibaya kitadhihirika. Na siku hiyo tutaona Moto wa Jahannam, Pepo na Mengineyo ambayo tuliyotajiwa katika Kuruani.

SAYANSI KATIKA AYA HII

Na Maoni ya Mwisho Ni Sayansi katika Aya Hii. Kwanza tuizungumzie na kisha Tutaunganisha na Kilinganisha na Maoni niliyotaja hapa Juu.

فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٌ   Katika Kipande hiki Neno  حَدِيدٌ   limefasiriwa kwa maana ya  “Kali” 

Na kwa hiyo Tafsiri inakuwa  “Maono  yako yanakuwa Makali sana” 

Yaani kuona Vizuri sana” Na  hii ndiyo Tafsiri  inayotupa maana ya kwamba siku ambayo Binaadamu atapewa nguvu ya kuona vizuri sana. 

Na neno  حَدِيدٌ   pia lina maana ya “CHUMA”  na ikiwa neno hili lina maana hiyo  basi Tafsiri inakuwa  “Macho au Maono yako yatakuwa na  CHUMA”   

Ukifikiri Kisayansi utakuta hakuna kosa kwani  Damu inayojulikana kama RED CELLS  inabeba Hameoglobin ambayo kazi yake ni Kubeba hewa ya Oxygen na ambayo ndiyo inayozipa Nguvu  Vyungo vya Mwili  Chuma (Iron) Katika Mwili wa Binaadamu ni Muhimu sana Katika Afya zetu. Sayansi inasema kwamba Maradhi mbali mbali kama vile Anaemia yanasababishwa na Upungufu wa hemoglobin ambayo kazi yake ni kubeba  Iron (Chuma).

Mwili wa binaadamu unahitaji Chuma. Kuna faida nyingi za chuma katika mwili wa Binaadamu. Kwa mfano  Afya ya Macho na kuona vizuri kunahitaji Chuma (Iron). Kwa hiyo Tafsiri ya Aya  inaonyesha kwamba Binaadamu anapofariki basi  Mwenyeezi Mungu anajaalia  Kuwepo kwa Chuma kwa wingi katika Macho na kusababisha Kuona Vizuri zaidi kuliko siku za kawaida. Na hiyo pia inawezekana kwani  hakuna Kisichowezekana Mbele ya Mwenyeezi Mungu. Angalia Hapa Chini Kauli ya Wanasayansi Kuhusu  “Chuma”  (Iron).

Red blood cells contain a substance called haemoglobin, which transports oxygen around the body.Iron is needed to form hemoglobin, part of red blood cells that carry oxygen and remove carbon dioxide (a waste product) from the body. Iron is mostly stored in the body in the hemoglobin. About one-third of iron is also stored as ferritin and hemosiderin in the bone marrow, spleen, and liver.Anemias occur when the level of healthy red blood cells (RBCs) or hemoglobin (an iron-binding, oxygen-carrying protein within RBCs) is too low. 

Iron is a necessary mineral for many of the body’s functions, including vision. But too much iron – or problems with utilizing, storing, or transporting iron properly – can lead to vision loss in the form of conditions such as age-related macular degeneration and hyperferritinemia syndrome, according to recent research findings.

.

21/05/2022

MUUJIZA WA CHROMOSOMES ZA BINAADAMU

Nimeshazungumzia Katika sehemu nyinginezo za Website hii kuhusu Chromosomes  za Binaadamu na Pia za baadhi ya Viumbe vinginevyo. Tuelewe kwamba Chromosomes ziligunduliwa mwaka 1888 (karne ya 19) Kutajika katika kuruani Elimu hii ni Muujiza mkubwa sana. Sayansi imefanya kazi kubwa kugundua Elimu hii lakini Kuruani ipo juu ya kila Sayansi za kidunia. Allahu Akbar.

Katika Mlango huu nitafanya uchunguzi katika Aya  namba 28  Sura Ya Al-Nisaa Namba 4. 

Kwanza Nitainukulu  Aya, Nitafuatia na Tafsiri na Kisha Sherehe Ya Aya Kisayansi.

Na pia Mwenyeezi Mungu akipenda nitaelezea  Ujumbe wa Aya hii.  

يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡ‌ۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا (٢٨)

TAFSIRI

28. Mwenyezi Mungu anataka kukukhafifishieni maana mwanaadamu ameumbwa dhaifu (Hana nguvu kubwa kabisa za kiwiliwill wala nguvu kubwa za kupigana na moyo na shetani).

SHEREHE

Mwenyeezi Mungu anatuhakikishia katika Aya hii kwamba Tumeumbwa Dhaifu  kiwiliwili na pia Kinafsi. Miili yetu ni Dhaifu na Pia  Nafsi zetu pia ni Dhaifu. Na kwa hekima yake kubwa anatunasihi tushikane na Anayotufundisha katika Kuruani na Hadithi za Mtume Mohamad. ﷺ.  Shetani wanataka kumharibu binaadamu aharibikiwe na maisha yake na tumeumbwa Dhaifu. Mwenyeezi Mungu anatunasihi na kutujuulisha kwamba Tumeumbwa Dhaifu na anatupa  Silaha ya Kujikinga na Hatari za Sheitan. Ili tuwe Salama na hatari hizo inabidi tufuate njia anayotaka yeye na siyo njia tunazotaka sisi. Tumuombe Mwenyeezi Mungu atulinde na Maradhi mbalimbali. Atulinde na Shari zinazotokana na Viumbe vingine kama vile Corrona na Mengine yaliyo hatari zaidi ya Corrona. 

MUUJIZA WA KISAYANSI

Aya hii pia inashangaza sana. Tukichambua Herufi, Maneno Yake na Mpangilio wake katika Kuruani tunapata Miujiza Mingine ya Kiajabu.

Hebu  Tufanye kazi pamoja ya kuichambua Aya hii. Na kisha Tufikiri na Tuone yenye kushangaza. Nitainukulu tena Aya hii ili tuichambue pamoja na tuone Maajabu.

يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡ‌ۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا (٢٨)

Namba Ya Aya Hii ni  28  na Ukihesabu Herufi za Aya Hii kuanzia Mwanzo wa Aya Mpaka Neno  ٱلۡإِنسَـٰنُ  “Insan”  utapata Jumla ya herufi ni  28.   Suala la Kujiuliza ni Kwamba Aya hii inazungumzia  Habari za Binaadamu yaani “INSAN” na kuanzia mwanzo wa Aya  hii mpaka mwisho wa Neno “INSAN” wa Aya hii  unapata jumla ya Herufi  ni 28.

Je unaona ya Maajabu kwamba Namba Ya Aya pia ni  28.  Hebu sasa tuchunguze  Hii Namba 28  je inaashiria kitu gani?  Sasa angalia Yanayofuata.

Katika Elimu Ya Hesabu tunafundishwa kwamba  Kuna Number System Mbali Mbali. 

Kuhusu Kuruani  tumeelezea Miujiza inayoambatana na Namba 19   kwamba Namba hii ni Muujiza mkubwa Katika baadhi ya Milango ya website hii nimedokeza habari za Namba 19.

Kuna Utafiti mbalimbali kuhusu namba hii inayoshangaza katika Kuruani lakini uwe macho kwani Namba hii inaambatana na yule aliyeigundua Aliyejulikana kwa jina kama  Rashadi Mtu huyu asili yake ni kutoka  Misri, lakini alifanya makosa makubwa kwani  baada tu ya kugundua Muujiza wa namba hii katika kuruani akaendelea kufanya makosa kwani aliichukulia  kama kipimo cha kupimia Aya za kuruani na kisha kuanza kukosoa Kuruani. Hayo ni makosa ya bwana huyu. Na isitoshe akadai  Utume Yaani Unabii.

Mwenyeezi  Mung atuipushie Uchafu kama huu. Na mwishowe mtu huyu aliyekuwa akiiishi huko America aliuawa katika Msikiti.

Haya ni makosa siyo  madogo kwani  Tusichukuwe Kipimo chochote na kisha kuanza Kukosoa Kuruani. Usisahau kwamba Kuruani ni  kama Rula ya maisha yetu.

Tumia kuruani kukosoa Kila kitu lakini usitumie vipimo vingine kuikosoa Kuruani.

Hayo na Makosa makubwa. Kuruani ni maneno ya Mwenyeezi Mungu na siyo upuuzi  wa Kukosolewa. Allahu Akbar.

Sasa tuendelee na Utafiti  wa leo.

NUMBER SYSTEMS  (MFUMO WA NAMBA)

Namba  zimegawanyika katika Syatems mbalimbali  kama ifuatavyo:  Kwa mfano

Base-2 (Binary Number System)

3. Base-8 (Octal Number System)

4. Base-10 (Decimal Number System)

5. Base-16 (Hexadecimal Number System)

6  Base-19  (Enneadecimal  Number System)

Utashangaa unapogeuza Namba  28 kutoka katika     

10 Base System kwenda katika  19 Base System . Ukifanya hivyo kwa kutumia  Calculator ya Mtandao utapata  Jawabu ni namba 19 ambayo ni namba ya Muujiza. (Nimezungumzia namba 19 kwingineko katika website hii).   

Sasa Angalia yanayofuata ambayo yanashangaza zaidi. Utashangaa unapogeuza Namba 28 kutoka katika 19 Base System kwenda katika 10 Base System Utapata Namba 46.  Na Namba 46  ni  Chromosomes za Binaadamu. 

Je unaona ya kushangaza.  Chromosomes ni Kanda 46 ambazo asili yake  ni 23  za Mbegu ya Mume na 23 za Mbegu ya Mke.  Na Katika kanda hizo Kuna GENES ambazo  zina habari ya umbile la kiumbe.  Kwa mfano Aya tuliyoisoma hapa Juu inazungumzia UDHAHIFU WA BINAADAMU   Udhaifu huu upo katika  GENES  za kanda hizo.  Kwa hiyo Aya hii ina mengineyo ya kushangaza ambayo kama tunavyoona hapa ni  Udhaifu wa binaadamu ambao upo katika  Damu yetu. Kila mtu amezaliwa nao. Yaani sisi wote tuna sifa hiyo. Tuasomeshwa katika Elimu ya Genetics kuhusu  Sifa za Urithi wa Maumbile. Lakini Sayansi bado ipo nyuma. Kuruani Inatupa mambo ambayo hata Sayansi bado haijajua. Elimu ya Genetics Haijasema kwamba  binaadamu wote ni Dhaifu. Na haijatufundisha kwamba Udhaifu huu unatokana Na GENES lakini Baada ya Utafiti Huu Maoni yangu ni Kwamba Hivyo ndivyo ilivyo. Naam.

Kuruani inatuma mapya na ninaamini hivyo 100% kwamba binaadami wote ni dhaifu na sifa hii ipo katika kila GENES za binaadamu. Ninaamini hivyo kwa sababu kuruani ni maneno ya aliyetuumba. Wataalamu wakisema vinginevyo mimi siamini hata kidogo. Ninaamini Kuruani na Ninajua kwamba Ipo juu ya kila Elimu. Kuruani  haina kosa hata moja. Allahu Akbar.

Usifikiri  Nimemaliza kuichambua Aya hii. Ndugu wasomaji bado nipo mwanzoni.

Kuna Uthibitisho unaofuata ambao  utakutoa Povu mdomoni. 

Sasa tuendelee na Utafiti Huu hapa chini wa Aya  tuliyoitaja hapa juu. Angalia Maajabu yanayofuata:

tuichambue Aya hii kipande kipande kwa kuhesabu herufi zake.

يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡ‌ۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا (٢٨)

kutumika na kukariri kwa herufi za kipande hiki  وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا   peke yake chenye maana ya “Binadamu ameumbwa Dhaifu”  katika aya hii yote ni kama ifuatavyo: 

Waw imetumika Mara 1

Kha imetumika Mara 2

Lam imetumika mara 4

Qaf imetumika mara 1

Alif imetumika mara 5

Lam imetumika mara 4

Alif imetumika mara 5

Nun imetumika mara 4

Sin imetumika mara 1

Nun imetumika mara 4

Dwad imetumika mara 1

Ain imetumika mara 2

Ya imetumika mara 4

Fa imetumika mara 3

Alif imetumika mara 5

sasa tujumlishe namba hizi

1 + 2 + 4 + 1 + 5 + 4 + 5 + 4 + 1 + 4 + 1 +2 + 4 + 3 + 5=46

je unaona ya kushangaza. Tunapata tena idadi za Chromosomes za binaadamu ambazo ni  46. huu  ni ushahidi kwamba hesabu tulizofanya hapa juu ni sahihi. je unaona ya maajabu hebu sasa tuendelee.

Tufanye utafiti wa kipande kinachofuata kama tulivyofanya hapa juu. tuchinguze idadi ya kukariri kwa herufi ya kipande hiki katika aya namba 28 ya sura ya  Al-Nisaa.

يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡ‌ۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا (٢٨)

وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ

kama tulivyofanya hapa juu tuhesabu kukariri ka herufi za kioande hiki katika aya hii. kipande hiki kina maana ya “Binaadamu Ameumbwa” hebu tuone ya kushangaza hapa chini:

Waw Imekariri mara 1

Kha Imekariri mara 2

Lam imekariri mara 4

Qaf imekariri mara 1

Alif imekariri mara 5

Lam imekariri mara 4

Alif imekariri mara 5

Nun imekariri mara 4

Sin imekariri mara 1

Nun imekariri mara 4

Sasa tujumlishe 

1 + 2 + 4 + 1 + 5 + 4 + 5 + 4 + 1 + 4=31 Jawabu ni namba 31.

Tusibabaike kwani utajiuliza kwa nini siyo  46. Wewe tulia acha wasiwasi. Kuruani inataka Elimu mbalimbali kwa hiyo usifikiri kuna kosa. 

Ukienda katika  Composite Numbers. (usisahau nimeelezea  prime na composite numbers katika milango mingine ya website hii)  utashangaa unapohesabu kuanzia Composite Number ya 1  mpaka ya  31 kwamba ni 46.  Yaani Composite Number  46  ni ya 31. Angalia maajabu. Tunapata Chromosomes  46 tena mara nyingine kwa nija ya kiajabu. Je unaona tena na tena inathibitisha kauli tuliyosema hapo juu. Allahu Akbar.

Sasa tuchambue  herufi za Neno  la ٱلۡإِنسَـٰنُ katika Aya ifuatayo. Tufanye kama tulivyofanya hapo juu. Tuone ya kushangaza tena na tena:

يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُخَفِّفَ عَنكُمۡ‌ۚ وَخُلِقَ ٱلۡإِنسَـٰنُ ضَعِيفً۬ا (٢٨)

ٱلۡإِنسَـٰنُ

Neno Hili  la “Alinsan” lina maana ya “Binaadamu”  Ukihesabu herufi zake zilivyotumika na kukariri katika aya hii utashangaa kuona kama ifuatavyo: 

Alif imekariri mara 5

Lam imekariri mara 4

Alif imekariri mara 5

Nun imekariri mara 4

Sin imekariri mara 1

Nun imekariri mara 4

5 + 4 + 5 + 4 + 1 + 4=23

Je  unaona ya kushangaza. Tunapata namba 23. Namba hii ni Mbegu za baba au mama. Kwani 23 za baba unapochanganya na 23 za mama zinakuwa jumla ni 46.  Tena na Tena tunaonyeshwa Muujiza wa kanda  46 za Chromosomes. Angalia  ya Kututoa Mapovu midomoni. Hatuna Ujanja. Ukifikiri unaona ukweli kwamba aliyetuumba ndiye yule yule aliyeshusha kuruani. Na Hii ni hotuba yake. Allahu Akbar.

KUKARIRI KWA NENO  ٱلۡإِنسَـٰنُ “Insan” 

Tunaendelea Kuichambua Aya tuliyoitaja hapa juu katika Muujiza wa Chromosomes za Binaadamu ambazo ni 46.

Katika  Kuruani yote  Neno ٱلۡإِنسَـٰنُ    “Insan” Limetumika na kukariri mara 65 katika Aya 63 ambazo  zipo katika Idadi ya Sura  43. 

Muujiza Mwingine wa Kushangaza ni Namba  65 ya Idadi ya Neno   “INSAN”  lilivyotumika katika Kuruani yote. 

Ukichunguza Namba hii 65 utaikuta ni  Compound Number ya 46. 

Yaani ukihesabu Compund Number kuanzia namba 4, 6, 8, 9, 10  mpaka  65  utakuta namba 65 ni ya 46 katika mpangilio wa hesabu za Compound Numbers.

Allahu Akbar Angalia Muujiza tena na tena tunapata Namba  46 ambayo inaashiria Chromosomes tulizozitaja hapa Juu.

Kama tulivyosema kwamba  Neno  “INSAN” limetajika katika Kuruani Mara 65 katika Jumla za Aya 63 Na zote zipo katika Jumla ya Sura  43.

Lingine la kushangaza ni  Namba 63  ambayo ni Compund Number ya 44 katika Mpangilio wa Compound Numebers. Sasa la kushangaza ni Hii Namba 44 

ambayo inaashiria Jumla ya  Autosomes za Binaadamu.  Kama tulivyosema kwamba Binaadamu ana Chromosomes  46 basi pia na Autosomes zipo  44.  Ni Nini Autosomes?  

Autosomes ni Kanda (Chromosomes) Zinazobeba  Genes za sifa za Binaadamu isipokuwa zile Genes za Uzazi (Sex Chromosomes) na ambazo  jumla yake ni mbili. (Moja ya Kiume (XX) na Ya Pili ya Kike (XY) )

Kwa kifupi Chromosomes ni kanda  46 na Autosomes kanda 44.  

kwa hiyo Namba 65  ni Compound Number 46 na 63 Ni Compund Number 44.  (46 ni Chromosomes na  44 ni Autosomes)  Jer unaona Muashirio wa kushangaza?

Allahu Akbar. Je unaona Umbile la binaadamu linavyoashiriwa katika Kuruani Tukufu?  

Kuna Aya Mbili katika Kuruani ambazo zimetaja neno “INSAN mara mbili na hizo ni kama zifuatazo

Sura Namba 17 Aya Namba 11

ويدع الانسن بالشر دعاه بالخير وكان الانسن عجولا

na 

Sura Namba 42 Aya Namba 48

فان اعرضوا فما ارسلنك عليهم حفيظا ان عليك الا البلغ وانا اذا اذقنا الانسن منا رحمه فرح بها وان تصبهم سييه بما قدمت ايديهم فان الانسن كفور

Ukijumlisha  Aya  hizi  mbili zinazotaja Neno “INSAN” na Aya Nyinginezo baina ya Aya hizi mbili ambazo pia zimetumia na Kutaja neno  “INSAN” utapata Jumla ni Aya 23. 

Yaani  kuanzia Sura Namba 17 Aya Namba 11 ambayo imetaja Neno “INSAN” mara mbili  na baada ya hapo Aya zote zinazotaja Neno  “INSAN” mpaka Sura Namba 42 Aya Namba 48 ambayo pia imetaja Neno “INSAN” mara mbili utapata Jumla Ya Aya  ni 23.

Angalia Ya Kushangaza. Tunapata tena Chromosomes 23 ambazo  ni za Kiume au Kike. Kwani  Baba ana Chromosomes 23 na Mama ana Chromosomes 23.  Je unaona Mushirio wa kushagaza? Allahu Akbar.

Ukihesabu  Herufi za Lugha Ya  Arabic  na  kuzipa Herufi hizo Namba. Kwa mfano.

Alif=1

Bas=2

Taa=3

Jim=4

Ukiendelea hivyo  kisha  tugeuze  Neno انسٰن   “INSAN” katika namba utaona maajabu mengineyo.  Hebu tufanye hivyo.  

Alif=1

Nun=25

Sin=12

Nun=25

Tukijumlisha tunapata     1 + 25 + 12 + 25=63

Na kama tulivyosema hapo awali kwamba Namba 63  Ni Compound Number ya 44 katika mpangilio wa Kihesabu wa Orodha ya Compound Numbers.  Je unakumbuka namba 44?  Tulisema ni Autosomes.  Nimekwisha Kuzungumzia hapo Juu maana ya Autosomes.  Hizi ni kanda 44 za Maumbile zisizokuwa na Sex Chromsomes. Na huenda Muashirio  wa namba hii ni Hizi Autosomes ambazo zina sifa za maumbile ya binaadamu.

Pia nakumbuka katika website hii nilikwisha kuzungumzia Kwamba kutumika kwa Herufi za neno  “INSAN” katika Sura Ya Al-Fatiha  ni mara  46. Na namba hii ni jumla ya Chromosomes za Binaadamu.

Mwenyeezi Mungu anajua zaidi haya tunayozungumzia. Ikiwa muradi ni huo. Sisi hatuna zidi isipokua kushangaa Muujiza wa Kuruani ambao hauna mwisho.  Allahu Akbar