SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Muujiza Wa Sura-3

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

UPO KATIKA MAANDALIZI  KWA HIYO  USISHANGAE UNPOUONA UNABADILIKABADILIKA KILA WAKATI.

MIONGONI MWA MIUJIZA  MIKUBWA

Tarehe  09/10/2022

SURA FUPI  TATU  ZENYE MAAJABU MAKUBWA

Kwanza ningependelea  kuzinukulu  Sura hizi Tatu na Tafsiri yake na Kisha Nitaelezea Hadithi  Za Mtume ﷺ kuhusu Sura Hizi na Baada Ya Hapo Tutachambua Muujiza Wa  Kiajabu. Allahu Akbar.

SURA NAMBA 1-SURA  YA AL-IKHLAS

سُوۡرَةُ الإخلاص

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ (١) ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ (٢) لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ (٣) وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ (٤)

TAFSIRI

Kwa jina Ia Mwenyezi Mungu, Mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na Mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo.

1 .Sema: Yeye ni Mwenyezi Mungu Mmoja (tu).

2. Mwenyezi Mungu (tu) ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe Vyake vyote kwa kumuabudu na kumuomba na kumtegemea).

3. Hakuzaa wala Hakuzaliwa

4· Wala hana anayefanana Naye hata mmoja.

SURA NAMBA 2-SURA YA AL-FALAQ

سُوۡرَةُ الفَلَق

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ (١) مِن شَرِّ مَا خَلَقَ (٢) وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ (٣) وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَـٰتِ فِى ٱلۡعُقَدِ (٤) وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ (٥)

TAFSIRI

Kwa jina Ia Mwenyezi Mungu, Mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na Mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo.

1. Sema: Ninajikinga kwa Mola wa ulimwengu wote

2. Na shari ya Allvyoviumba

3. Na shari ya giza Ia usiku liingiapo

4· Na shari ya wale wanaopulizia mafundoni,

(wakavunja mashikamano yaliyo baina ya watu)

5· Na shari ya hasidi anapohusudu

SURA NAMBA 3-SURA YA ANNAS

سُوۡرَةُ النَّاس

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ (١) مَلِكِ النَّاسِ (٢) إِلَـٰهِ ٱلنَّاسِ (٣) مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ (٤) ٱلَّذِى يُوَسۡوِسُ فِى صُدُورِ ٱلنَّاسِ (٥) مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ (٦)

TAFSIRI

Kwa jina Ia Mwenyezi Mungu, kuneemesha neema kubwa kubwa na kuneemesha neema ndogo ndogo.

1. Serna: Ninajikinga kwa Bwana mwenye kuwalea

2. Mfalme wa watu

3. Muabudiwa wa watu

4. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma

5. Atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu

6. (Ambaye ni) katika maiini na watu

HADITHI  ZA MTUME ﷺ ZINAZOSHEREHESHA SURA HIZI  TATU

Kwa kweli kuna Sura Nyingi lakini  Nitachagua Chache katika Mlango huu kwani Lengo la Mlango huu ni Muujiza Utakaofuata. Lakini nimeona bora  niongeze  baadhi ya Hadithi  zenye kuonyesha Thamani, Fadhila au Utukufu wa Sura Hizi. 

SURA ZOTE TATU (AL-IKHLAS+ AL-FALAQ +ANNAS)

Hadithi  ambayo  ipo katika kitabi cha Riyadh Aswalihiyn.

وعن عبد الله بن خُبيب -بضم الخاء المعجمة- رضي الله عنه قال‏:‏ قال لي رسول الله صلى الله عليه وسلم‏:‏ ‏ “‏اقرأ‏:‏ قل هو الله أحد، والمعوذتين حين تمسي وحين تصبح، ثلاث مرات، تكفيك من كل شيء‏”‏‏.‏ رواه أبو داود والترمذي وقال حديث حسن صحيح ‏.‏

SHEREHE

Hadithi inayotokana na Abdullahi Ibn Khubayb. (رضي الله عنه).  Alisema kwamba Mtume ﷺ alimwambia  asome Sura ya  Al-Ikhlas, Alfalaq  na  Annas  kila siku  Jioni  na Asubuhi kwani kufanya hivyo Atapata  faida kubwa. Kwanza Mwenyeezi Mungu atamlinda na kila Shari, Atambariki kila atakachikifanya siku hiyo na Atamsaidia na Kila Mahitaji yake.  Kwa kifupi hadithi Hii inatupa faida hii. Tukizisoma KIla siku mara mbili  basi tutapata Faida hizi. Tufanye hivi na hali tuna Imani, Bila kujilazimisha. Tufanye kwa Hamu kubwa yakupata zawadi hizi. Hii ndiyo maana ya Hadithi hii.

TRANSLATION

‘Abdullah bin Khubaib (May Allah be pleased with him) reported: The Messenger of Allah (ﷺ) said to me, “Recite Surat Al-Ikhlas and Al- Mu’awwidhatain (Surat Al-Falaq and Surat An-Nas) three times at dawn and dusk. It will suffice you in all respects.” [Abu Dawud and At-Tirmidhi].

SURA YA AL-IKHLAS

Hadithi ya Kwanza ya Bukhariy-Hadithi  Sahihi Pia ipo katika Kitabu cha Riyadh Aswalihiyn

وعن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال في‏:‏‏{‏ قل هو الله أحد‏}‏‏:‏‏”‏ والذي نفسي بيده، إنها لتعدل ثلث القرآن‏”‏‏.‏ وفي رواية‏:‏ أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال لأصحابه‏:‏‏”‏ أيعجز أحدكم أن يقرأ بثلث القرآن في ليلة‏”‏ فشق ذلك عليهم، وقالوا‏:‏ أينا يطيق ذلك يارسول الله‏:‏ فقال ‏:‏‏”‏ ‏{‏قل هو الله أحد‏}‏ ثلث القرآن‏.‏‏”‏‏.‏ ‏(‏‏(‏ رواه البخاري‏)‏‏)‏‏.‏

SHEREHE

Hadithi  Iliyosimuliwa na Said Al-khudri kwamba Mtume ﷺ alisema “Naapa kwa yule ambaye Roho  yangu ipo mikononi  mwake. (Sura Hii) ni sawa na Theluthi Moja  ya Kuruani na Pia Kuna hadithi  nyingine inayohusu habari hizi inayosema  Mtume ﷺ “Aliwauliza Maswahaba zake “Je miongoni  mwenu  kuna  yeyote  asiyeweza kusoma  kiwango  cha Theluthi  ya Kuruani katika Usiku mmoja? Suala Hili  lilikuwa gumu na kwa hiyo wakajibu “Ewe Mtume wa Mwenyeezi Mungu  “Hakuna kati yetu anayeweza kusoma kiwango hicho kwa muda wa Usiku mmoja”.  Theluthi  Moja  ni Fungu moja  la  Sura za Kuruani ukigawa Kuruani katika Mafungu Matatu. Mtume akawajibu kwa kusema

“Sura  Moja  tu ya Al-Ikhlas ukiisoma itakuwa kama umesoma Theluthi  moja ya Kuruani  yaani Fungu moja  kati ya Mafungu matatu ya Sura  114 ya Msahafu. (ukigawa sura 114 katika  mafungu matatu).  

Kwa hiyo Sura Hii  ina Mengi mazuri ambayo  katika Mlango huu Mdogo  Wa Website hii  inatkuwa vigumu kuelezea kila kitu. Nitachagua  Zile hadithi  chache ili  tupate angalau Mwanga  Mdogo.

TRANSLATION

Abu Sa’id Al-Khudri (May Allah be pleased with him) reported about Surat Al-Ikhlas (Chapter 112): The Messenger of Allah (ﷺ) said, “By Him in Whose Hand my soul is, it is equivalent to one-third of the Qur’an.” According to another version, he (ﷺ) said to his Companions, “Is anyone of you incapable of reciting one-third of the Qur’an in one night?” They considered it burdensome and said: “O Messenger of Allah, which of us can afford to do that?” He (ﷺ) said, “Surat Al-Ikhlas [Say: He is Allah (the) One] is equivalent to one-third of the Qur’an.” [Al- Bukhari].

Hadithi Ya Pili Katika Kitabu Cha Sunnan Jamii At-irmidhiy-Hadithi ni Dhaifu lakini Baadhi ya Wanavyuoni  wanathibitisha Kwamba Grade au Kiwango cha Hadithi ni Hasan

حَدَّثَنَا أَحْمَدُ بْنُ مَنِيعٍ، حَدَّثَنَا أَبُو سَعْدٍ، هُوَ الصَّغَانِيُّ عَنْ أَبِي جَعْفَرٍ الرَّازِيِّ، عَنِ الرَّبِيعِ بْنِ أَنَسٍ، عَنْ أَبِي الْعَالِيَةِ، عَنْ أُبَىِّ بْنِ كَعْبٍ، أَنَّ الْمُشْرِكِينَ، قَالُوا لِرَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم انْسُبْ لَنَا رَبَّكَ ‏.‏ فَأَنْزَلَ اللَّهُ ‏:‏ ‏(‏ قلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ * اللَّهُ الصَّمَدُ ‏)‏ فَالصَّمَدُ الَّذِي لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ لأَنَّهُ لَيْسَ شَيْءٌ يُولَدُ إِلاَّ سَيَمُوتُ وَلَيْسَ شَيْءٌ يَمُوتُ إِلاَّ سَيُورَثُ وَإِنَّ اللَّهَ عَزَّ وَجَلَّ لاَ يَمُوتُ وَلاَ يُورَثُ ‏:‏ ‏(‏ لَمْ يَكُنْ لَهُ كُفُوًا أَحَدٌ ‏)‏ قَالَ ‏”‏ لَمْ يَكُنْ لَهُ شَبِيهٌ وَلاَ عِدْلٌ وَلَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ‏”‏ ‏

SHEREHE

Hadithi hii inatokana na Ubayy Ibn Ka’b. Alisema kwamba Makafiri wale ambao waliokuwa wakiabudu Masanamu walikuja kwa Mtume ﷺ na kumpa Mtihani kwa kumwambia yafuatayo:

Ewe Mtume wa mweyeezi Mungu Tutajie Ukoo wa Mwenyeezi Mungu” yenye maana ya “Je Mungu ni nani” “Je ana Familia?” “Je amezaliwa?”

Kwa kweli hivyo ndivyo Makafiri walivyofikiri kwamba Mwenyeezi Mungu  ni sawa na Masanamu yao.

Walitaka kujua Ukoo wa Mwenyeezi Mungu kama vile Baba yake Babu yake Mama yake au Bibi yake.

Kwa kweli ukifikiri utaona Suala silo Rahisi. Jaribu kufikiri Ikiwa mimi au wewe Tunaishi wakati huo wa karne ya Sita na Tumeulizwa Suala kama hili.

Lakini Mwenyeezi Mungu akamsadia Mtume ﷺ na Kumshushia Jibu awajibu Makafiri hawa.

Na ndiyo maana Mwanzoni mwa Sura Hii Mwenyeezi Mungu ametumia neno قُلۡ  “KUL”  lenye maana ya “SEMA” yaani “Wajibu kwa Kusema” na baada ya hapo ikafuatia jawabu katika Sura Hii.

Tafsiri ya Sura Hii Angalia Hapa Juu.

Kwa kifupi Sura Hii inamtakasa Mwenyeezi Mungu kwamba Yeye ni Mmoja tu. Hategemei Viumbe wake bali sisi tunamtegemea. Hakuzaliwa na Hakuzaa na Hakuna Chochote kinachofanana naye katika Viumbe vilivyo hai na Pia viumbe visivyo hai.

TRANSLATION

Abu Al-Aliyah narrated from Ubayy bin Ka’b: “The idolaters were saying to the Messenger of Allah: ‘Name the lineage of your Lord for us.’ So Allah, Most High, revealed: Say: “He is Allah, the One. Allah As-Samad.” So As-Samad is ‘the One Who does not beget, nor is He begotten,’ because there is nothing born except it will die, and there is nothing that dies except that it will be inherited from, and verily. Allah, the Mighty and Sublime, does not die, nor is He inherited from. ‘And there is none comparable to Him.’ He said: ‘There is nothing similar to Him, nor equal to Him, nor is there anything like Him.’”

SURA YA ANNAS  NA  AL-FALAQ

Hadithi  ya Kwanza-Ipo katika Sahih  Muslim na Riyadh Aswalihiyn.

وعن عقبة بن عامر رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال ‏:‏‏ “‏ ألم ترَ آيات أنزلت هذه الليلة لم يرَ مثلهن قط ‏؟‏ قل أعوذ برب الفلق، وقل أعوذ برب الناس ‏”‏‏.‏‏(‏‏(‏رواه مسلم‏)‏‏)‏‏.‏

SHEREHE

Hadithi hii inatokana na ‘Uqbah bin ‘Amir  (رضي الله عنه) Inasema kwamba Mtume ﷺ alisema kwamba Aya za Kuruani  zimeshishwa usiku wa leo ambazo hakuna mfano wake.  Na baada ya hapo akazisoma Aya zifuatazo:

قل أعوذ برب الفلق

وقل أعوذ برب الناس  

TRANSLATION

‘Uqbah bin ‘Amir (May Allah be pleased with him) reported: The Messenger of Allah (ﷺ) said: “Do you not know that last night certain Ayat were revealed the like of which there is no precedence. They are: ‘Say: I seek refuge with (Allah) the Rubb of the daybreak’ (Surah 113), and ‘Say: I seek refuge with (Allah) the Rubb of mankind’ (Surah 114).” [Muslim].

Hadithi ya Pili-Ipo katika Vitabu Vya  Imamu Al-Bukhariy na Muslim na Pia Riyadh Aswalihiyn

وعن عائشة، رضي الله عنه، أن رسول الله صلى الله عليه وسلم، كان إذا أخذ مضجعه نفث في يديه، وقرأ بالمعوذات ومسح بهما جسده‏.‏ ‏(‏‏(‏متفق عليه‏)‏‏)‏‏.‏ وفي رواية لهما‏:‏ ‏ “‏أن النبي صلى الله عليه وسلم، كان إذا أوى إلى فراشه كل ليلة جمع كفيه، ثم نفث فيهما فقرأ فيهما‏:‏ قل هو الله أحد، وقل أعوذ برب الفلق، وقل أعوذ برب الناس، ثم مسح بهما ما استطاع من جسده، يبدأ بهما على رأسه ووجهه، وما أقبل من جسده، يفعل ذلك ثلاث مرات‏”‏‏.‏ ‏(‏‏(‏متفق عليه‏)‏‏)‏‏. قال أهل اللغة : (( النفث )) نفخ لطيف بلا ريق‏

SHEREHE

Hadithi inayotokana na Aisha (رضي الله عنه) Mke wa Mtume ﷺ anaelezea kuhusu Mtume ﷺ kwamba unapofika wakati  wa kulala na  anapokuwa kitandani basi Hupulizia  Viganja Vya Mikono  yake miwili kwa kupulizia  na kisha Husoma  Sura ya  Al-Falaq na Annas zinazojulikana kama Muawidhatayni. Maana ya Neno hili ni  “Kinga Mbili”. Na baada ya hapo hujipaka Mwili wake wote katika sehemu zote za mwili ambazo huweza kufikia Mikono yake.

Na kuna Riwaya au Version Ya hadithi  nyingine inayosema  Hupulizia Viganja Vya Mikono yake miwili na Kisha Husoma Sura Tatu: Al-Ikhlas, Al-Falaq na Annas  na kisha baada ya hapo hujipaka Mwili wake wote katika sehemu zote za mwili ambazo huweza kufikia Mikono yake. Huanza Kujifuta au kujipaka  kuanzia Uso na kichwa na kisha Mwilini. Alikuwa akifanya hivyo  Mata Tatu. Yaani Alijipaka Mwili wake mara Tatu. Kisomo  cha Sura Tatu ni mara moja lakini Kujipaka mara tatu. Katika  Kupulizia Viganja Vya Mikono upulizie pumzi ya polepole na siyo  kwa nguvu na kujiepusha na  Mate na ndiyo maana ya ibara

  النفث قال أهل اللغة : (( النفث )) نفخ لطيف بلا ريق

Gentle blowing without saliva   

Kufanya Hivi kuna faida nyingi. Kuna faida tunazozijua na zile ambazo hatuzijui. Kwanza Mwenyeezi Mungu anatuepushia na Shari tusizozijua kama vile  Mashetani na Maradhi. Na ikiwa Utafariki dunia usingizini inakuwa bora Iwe baada ya Kisomo  hicho kuliko  Kulala hovyo hovyo kwani Kila Mtu anatamani Mauti yanapofika angalau awe katika Kumtaja Mwenyeezi Mungu na kwa hiyo Unapolala hujui litakalokupata. Na Lazima tukumbuke kwamba Usingizi  Ni Nusu ya Mauti.

TRANSLATION

‘A ishah (May Allah be pleased with her) reported: Whenever the Messenger of Allah (ﷺ) went to bed, he would blow upon his hands recite Al-Mu’awwidhat; and pass his hands over his body. [Al-Bukhari and Muslim].

Katika Sura hizi Tatu. Sura Iliyotangulia kushuka ni Sura Ya Al-Falaq, Ikafuatiwa na Sura Ya Annas  na baada ya hapo ikafuatiwa na Sura ya Al-Ikhlas.

Fadhila ya Sura Hizi Tatu ni Nyingi ambazo Website ndogo kama hii haiwezekani kuzinukulu  hadithi  zote za Mtume zenye  Maelezo  Mbalimbali Kuhusu Sura Hizi Tatu. Pia Kuna Kauli Mbalimblai za Wanavyuoni  kuhusu Sura Hizi Tatu ambazo ningependelea  kuzinukulu lakini haitawezekana kwa ajili ya lengo la mlango huu ni uchambuzi wa Muujiza na kwa hiyo nitaishia  hapa Lengo  la Mlango  huu ni Muujiza Unaofuata. 

Kwa kifupi  Sura Ya Al-Ikhlas inamtakasa Mwenyeezi Mungu  na Tunaambiwa Tumwite Mwenyeezi Mungu kwa Jina Lake  ambalo ni  “Allah”  na pia  tunaweza kumwita kwa zile Sifa Zake. Lakini tusitumie majina mengineyo bila mpango. Hata Binaadamu hawapendi Kugeuzwa Majina Basi Hivyo hivyo Mwenyeezi Mungu inabidi  tuwe macho  sana.

Sura Ya A-Lfalaq  Inatupa Fundisho tumuombe Mwenyeezi Mungu atuepushie na Shari ya Viumbe vyake tunavyovijua na tusivyovijua. Yaani tumuombe Mwenyeezi Mungu atukinge na Shari hizo.

Sura Ya Annas  Inatupa  Fundisho Tumuombe Mwenyeezi Mungu  atuepushie  na Shari ya Mashetani wa Kijini na Kibinaadamu ambao  Hutia Wasiwasi katika  Nyoyo  zetu.

Mashetani  hatuwaoni  lakini wapo. Ukiwa Muislamu  basi lazima Uamini  Kila Kilichotajwa katika Kuruani kama vile Pepo, Moto wa Jahannam, Malaika, Mashetani. Na hii ndiyo imani ya Ghayb. Lazima Uamini ikiwa wewe Muislamu na Kama huamini basi huna Dini. Kufuatana na Miujiza Tuliyoiona katika Website hii kwa kweli lazima Tuamini kwani Miujiza siyo Midogo. Na Miujiza Hii yote imegusia  Mashetani, Malaika, Pepo (Jannah) Na Moto (Jahannam) Tumeona Hesabu zinavyodhirisha  Muujiza, Namba tulizoziona katika Muujiza wa Kihesabu zinatosha tuamini bila tatizo lolote.

Baada ya Kuzielezea  Sura Hizi  Tatu naona  Wakati  umefika Wa Kuanza Kuchambua  Sura Hizi Tatu ili tuone Maajabu ambayo  siyo madogo. Maajabu Haya Yamepangwa kwa makusudi. Kama Nilivyosema katika Kila Muujiza wa Website hii kwamba Kuruani  ni Muujiza Mkubwa sana. Kuruani  Imekusanya Vitu Viwili. kwanza ni Ujumbe na Pili ni Miujiza. Na huu ndio Ujumbe wa mwisho  ulivyokusudiwa.

Mitume iliyopita walipewa Ujumbe na Miujiza ambayo ilikuwa ni  Kithibitisho  kwamba Ujumbe wao ni wa kweli Lakini Mtume  wa Mwisho Muhamad ﷺ kapewa Miujiza ya kuthibitisha Ujumbe wake na Pia Muujiza wa Kuruani ambayo  Muujiza wake bado unaendelea na itakuwa hivyo mpaka  Mwenyeezi Mungu atakapopenda au Mwisho  wa Ulimwengu  utakapofika.

Sasa  tuanze na uchambuzi wa maajabu katika sura hizi tatu.

DARUBINI KATIKA  SURA HIZI TATU

SURA NAMBA  112

سُوۡرَةُ الإخلاص

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ (١) ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ (٢) لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ (٣) وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ (٤)

——————————

SURA NAMBA 113

سُوۡرَةُ الفَلَق

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ

ٱلرَّحِيمِ قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ (١) مِن شَرِّ مَا خَلَقَ (٢) وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ (٣) وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَـٰتِ فِى ٱلۡعُقَدِ (٤) وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ (٥)

—————————-

SURA NAMBA 114

سُوۡرَةُ النَّاس

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ

ٱلرَّحِيمِ قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ (١) مَلِكِ النَّاسِ (٢) إِلَـٰهِ ٱلنَّاسِ (٣) مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ (٤) ٱلَّذِى يُوَسۡوِسُ فِى صُدُورِ ٱلنَّاسِ (٥) مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ (٦)

Nitapanga miujiza  kutoka katika Sura Hizi Tatu kwa namba kama ifuatavyo:

MUUJIZA WA KWANZA

Namba  za  Sura  zinashangaza sana kwani Ijapokuwa Namba hizi ziliongezwa baadaye kwa ajili ya kuwasaidia  Wasomaji wa Kuruani lakini  Nyongeza  yoyote ilikuwa chini ya Uangalizi  wa Mwenyeezi Mungu Mtukufu na katika Muujiza huu wa kwanza  Utaona Ukweli huu. Mwenyeezi Mungu ameahidi  kuitunza Kuruani hii yeye mwenyewe baada ya Vitabu vya Manabii  waliotangulia kuharibiwa.  Kuruani ipo  chini  ya Uanagalizi  wa mwenyeezi Mungu. 

hebu sasa Tuchunguze Namba za Sura.

Sura Ya Ikhlas  ni Namba   112 Na ina  Aya  4

Sura Ya Al-Falaq Ni Namba  113 Na ina Aya  5

Sura Ya Annas Ni Namba 114  Na ina Aya  6

Muujiza upo  wazi. Hebu tujimlishe  Namba za Sura.

Al-Ikhlas  Sura Namba 112  tukijumlisha Namba 1 + 1 + 2=4  Na Ajabu ni kwamba Jumla  ya Namba hii ni 4  Na Namba 4 ni Jumla ya Aya za Sura Hii

Al-Falaq Sura Namba 113 tukijumlisha  1 + 1 + 3 =5 Na Ajabu ni kwamba Jumla ya Namba hii ni 5 na Namba 5 ni Jumla Ya Aya za Sura Hii

Al-Nas Sura Namba 114 tukijumlisha 1 + 1 + 4 =6 Na Ajabu ni kwamba Jumla ya Namba hii ni 6 na Namba 6 ni Jumla Ya Aya za Sura Hii

Angalia  maajabu. Dalili ya Mvua ni Mawingu. Kabla Ya Uchambuzi Mkubwa tunapata Muujzia wa Kwanza Bado Mapema Ya Asubuhi. Haya siyo  Madogo kwani Kuruani siyo kitabu kama vitabu vinginevyo  hata kidogo. Hebu tuendelee na Muujiza za pili.

MUUJIZA WA PILI

Muujiza wa pili utahusu   Sura Ya  A-Ikhlas.  Mwenyeezi Mungu  anatuamrisha  Tutumie Jina lake la  “Allah” Katika Aya ya Kwanza ya Sura Hii aliposema

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ (١) .

Sema: Yeye ni Mwenyezi Mungu Mmoja (tu).

Kwa hiyo  Kuna Aya Nyingine  katika Sura Ya Al-AaRaf  Namba 7  Aya Namba 18 Inayotupa Ruhusa  kumwita kwa kutumia Majina Yanayojulikana kama  “Asmaa Alhusna”  Aya hiyo  inasema:

و لله الاسما الحسني فادعوه بها و ذروا الذين يلحدون في اسميه سيجزون ما كانوا يعملون

Katika Aya hii Mwenyeezi Mungu anatuambia kwamba majina yake mengineyo  ni Hizo sifa zake zinazojulikana kama Asmaa Alhusna  na Anaahidi Wanaotumia majina ambayo siyo yake au yale ambayo yana Ukafiri basi Watalipwa Kwa ubaya huo.

Sura Ya Al-Hashr  namba 59  Aya Namba 23 na 24 imetaja baadhi ya majina Haya ambayo yanajulikana kama “Asmaa Alhusna”

هو الله الذي لا اله الا هو الملك القدوس السلم المومن المهيمن العزيز الجبار المتكبر سبحن الله عما يشركون

هو الله الخلق الباري المصور له الاسما الحسني يسبح له ما في السموت و الارض و هو العزيز الحكيم

Almaliki/Alqudusi/Asalaam/Almuumin/ Almuhaymin/Alaziz/ Aljabar/Almutakabir/ Alkhaliq/Albaruy/.  

Jumla Ya Sifa za Mwenyeezi Mungu ni 99. na kila moja ya Sifa hizi zina maana. Na ni Vizuri tuzitaje Sifa hizi  kufuatana na Maombi yetu. Tunapomumba Mwenyeezi Mungu Riziki basi tumwite kwa Kusema “Ewe  Razaq” Yaani Ewe mwenye Kumiliki  Riziki. Na kisha uombe ulitakalo. Na hivyo hivyo  ukidhulumiwa Umwite kwa kusema “Ewe  Hakimu”  Yaani Ewe Jaji au Hakimu Mkubwa. Na Baadaye umuombe ulitakalo. Kila Jina Linaonyesha Ukubwa wake Mwenyeezi Mungu Katika  Dunia na Ulimwenguni kwani yeye ndiye anayemiliki kila kitu.

SIFA  AU MAJINA AMBAYO TUNAWEZA  KUMWITA MWENYEEZI MUNGU YANAYOJULIKANA KAMA “ASMAA ALHUSNA, MATAMSHI NA MAANA YAKE KWA LUGHA YA KIINGEREZA.

The 99 Names of Allah (SWT) with Transliteration and meaning

1 الرَّحْمَنُ AR-RAHMAAN The Beneficent

2 الرَّحِيمُ AR-RAHEEM The Merciful

3 الْمَلِكُ AL-MALIK The King

4 الْقُدُّوسُ AL-QUDDUS The Most Sacred

5 السَّلاَمُ AS-SALAM The Source of Peace, The Flawless

6 الْمُؤْمِنُ AL-MU’MIN The Infuser of Faith

7 الْمُهَيْمِنُ AL-MUHAYMIN The Preserver of Safety

8 الْعَزِيزُ AL-AZIZ All Mighty

9 الْجَبَّارُ AL-JABBAR The Compeller, The Restorer

10 ُالْمُتَكَبِّر AL-MUTAKABBIR The Supreme, The Majestic

11 الْخَالِقُ AL-KHAALIQ The Creator, The Maker

12 الْبَارِئُ AL-BAARI The Evolver

13 الْمُصَوِّرُ AL-MUSAWWIR The Fashioner

14 الْغَفَّارُ AL-GHAFFAR The Great Forgiver

15 الْقَهَّارُ AL-QAHHAR The All-Prevailing One

16 الْوَهَّابُ AL-WAHHAAB The Supreme Bestower

17 الرَّزَّاقُ AR-RAZZAAQ The Provider 1

8 الْفَتَّاحُ AL-FATTAAH The Supreme Solver

19 اَلْعَلِيْمُ AL-‘ALEEM The All-Knowing

20 الْقَابِضُ AL-QAABID The Withholder

21 الْبَاسِطُ AL-BAASIT The Extender

22 الْخَافِضُ AL-KHAAFIDH The Reducer

23 الرَّافِعُ AR-RAAFI’ The Exalter, The Elevator

24 الْمُعِزُّ AL-MU’IZZ The Honourer, The Bestower

25 ٱلْمُذِلُّ AL-MUZIL The Dishonourer, The Humiliator

26 السَّمِيعُ AS-SAMEE’ The All-Hearing

27 الْبَصِيرُ AL-BASEER The All-Seeing

28 الْحَكَمُ AL-HAKAM The Impartial Judge

29 الْعَدْلُ AL-‘ADL The Utterly Just 3

0 اللَّطِيفُ AL-LATEEF The Subtle One, The Most Gentle

31 الْخَبِيرُ AL-KHABEER The All-Aware

32 الْحَلِيمُ AL-HALEEM The Most Forbearing

33 الْعَظِيمُ AL-‘AZEEM The Magnificent, The Supreme

34 الْغَفُور AL-GHAFOOR The Great Forgiver

35 الشَّكُورُ ASH-SHAKOOR The Most Appreciative

36 الْعَلِيُّ AL-‘ALEE The Most High, The Exalted

37 الْكَبِيرُ AL-KABEER The Most Great

38 الْحَفِيظُ AL-HAFEEDH The Preserver

39 المُقيِت AL-MUQEET The Sustainer

40 اﻟْﺣَسِيبُ AL-HASEEB The Reckoner

41 الْجَلِيلُ AL-JALEEL The Majestic

42 الْكَرِيمُ AL-KAREEM The Most Generous, The Most Esteemed

43 الرَّقِيبُ AR-RAQEEB The Watchful

44 ٱلْمُجِيبُ AL-MUJEEB The Responsive One

45 الْوَاسِعُ AL-WAASI’ The All-Encompassing, the Boundless

46 الْحَكِيمُ AL-HAKEEM The All-Wise

47 الْوَدُودُ AL-WADUD The Most Loving

48 الْمَجِيدُ AL-MAJEED The Glorious, The Most Honorable

49 الْبَاعِثُ AL-BA’ITH The Infuser of New Life

50 الشَّهِيدُ ASH-SHAHEED The All Observing Witnessing

51 الْحَقُ AL-HAQQ The Absolute Truth

52 الْوَكِيلُ AL-WAKEEL The Trustee, The Disposer of Affairs

53 الْقَوِيُ AL-QAWIYY The All-Strong

54 الْمَتِينُ AL-MATEEN The Firm, The Steadfast

55 الْوَلِيُّ AL-WALIYY The Protecting Associate

56 الْحَمِيدُ AL-HAMEED The Praiseworthy

57 الْمُحْصِي AL-MUHSEE The All-Enumerating, The Counter

58 الْمُبْدِئُ AL-MUBDI The Originator, The Initiator

59 ٱلْمُعِيدُ AL-MUEED The Restorer, The Reinstater

60 الْمُحْيِي AL-MUHYI The Giver of Life

61 اَلْمُمِيتُ AL-MUMEET The Creator of Death

62 الْحَيُّ AL-HAYY The Ever-Living

63 الْقَيُّومُ AL-QAYYOOM The Sustainer, The Self-Subsisting

64 الْوَاجِدُ AL-WAAJID The Perceiver

65 الْمَاجِدُ AL-MAAJID The Illustrious, the Magnificent

66 الْواحِدُ AL-WAAHID The One

67 اَلاَحَدُ AL-AHAD The Unique, The Only One

68 الصَّمَدُ AS-SAMAD The Eternal, Satisfier of Needs

69 الْقَادِرُ AL-QADEER The Omnipotent One

70 الْمُقْتَدِرُ AL-MUQTADIR The Powerful

71 الْمُقَدِّمُ AL-MUQADDIM The Expediter, The Promoter

72 الْمُؤَخِّرُ AL-MU’AKHKHIR The Delayer

73 الأوَّلُ AL-AWWAL The First

74 الآخِرُ AL-AAKHIR The Last

75 الظَّاهِرُ AZ-ZAAHIR The Manifest

76 الْبَاطِنُ AL-BAATIN The Hidden One, Knower of the Hidden

77 الْوَالِي AL-WAALI The Sole Governor

78 الْمُتَعَالِي AL-MUTA’ALI The Self Exalted

79 الْبَرُّ AL-BARR The Source of All Goodness

80 التَّوَابُ AT-TAWWAB The Ever-Pardoning, The Relenting

81 الْمُنْتَقِمُ AL-MUNTAQIM The Avenger

82 العَفُوُ AL-‘AFUWW The Pardoner

83 الرَّؤُوفُ AR-RA’OOF The Most Kind

84 َمَالِكُ ٱلْمُلْكُ MAALIK-UL-MULK Master of the Kingdom, Owner of the Dominion

85 ذُوالْجَلاَلِ وَالإكْرَامِ DHUL-JALAALI WAL-IKRAAM Lord of Glory and Honour, Lord of Majesty and Generosity

86 الْمُقْسِطُ AL-MUQSIT The Just One

87 الْجَامِعُ AL-JAAMI’ The Gatherer, the Uniter

88 ٱلْغَنيُّ AL-GHANIYY The Self-Sufficient, The Wealthy

89 ٱلْمُغْنِيُّ AL-MUGHNI The Enricher

90 اَلْمَانِعُ AL-MANI’ The Withholder

91 الضَّارَ AD-DHARR The Distresser

92 النَّافِعُ AN-NAFI’ The Propitious, the Benefactor

93 النُّورُ AN-NUR The Light, The Illuminator

94 الْهَادِي AL-HAADI The Guide

95 الْبَدِيعُ AL-BADEE’ The Incomparable Originator

96 اَلْبَاقِي AL-BAAQI The Everlasting

97 الْوَارِثُ AL-WAARITH The Inheritor, The Heir

98 الرَّشِيدُ AR-RASHEED The Guide, Infallible Teacher

99 الصَّبُورُ AS-SABOOR The Forbearing, The Patient

HADITHI  YA MTUME ﷺ KUHUSU MAJINA  YA HUSNA

حَدَّثَنَا أَبُو الْيَمَانِ، أَخْبَرَنَا شُعَيْبٌ، حَدَّثَنَا أَبُو الزِّنَادِ، عَنِ الأَعْرَجِ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ “‏ إِنَّ لِلَّهِ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ اسْمَا مِائَةً إِلاَّ وَاحِدًا مَنْ أَحْصَاهَا دَخَلَ الْجَنَّةَ ‏”‏‏.‏

SHEREHE

Hadithi  hii imekusanywa na Bukhariy katika Vitabu vyake vya hadithi.

Hadithi  inatokana na Swahaba wa Mtume ﷺ

Abiy  Hurayra. Anasema kwamba Mtume ﷺ alisema kwamba “Mwenyeezi Mungu ana Majina 99 atakeyeyajua (Kuyataja, kuyafahamu  na  Kuyazingatia) majina haya ataingia Peponi”

TRANSLATION

Narrated Abu Huraira:

Allah’s Messenger (ﷺ) said, “Allah has ninety-nine names, i.e. one-hundred minus one, and whoever knows them will go to Paradise.” (Please see Hadith No. 419 Vol. 8)

Baada ya Sherehe hii kuhusu Sura Ya  Al-Ikhlas ninaona umefika wakati wa Kuelezea Muujiza Wa Sura Hii Ya Al-

Ikhlas: Tutachunguza  Vokali  au Voyel  inayojulikana kama   “KASRAH”.    Katika Lugha ya Kiarabu kuna Vokali (Voyels)  Sita. zinajulikana kama FATHA (Fupi na Ndefu), KASRA (Fupi na Ndefu) NA DHUMMA (Fupi na Ndefu). Yaani Vokali  Tatu Fupi zinajulikana kama    a,  i  na u

Na Vokali  Tatu  Ndefu Zinajulikana kama  aa, ii, uu

Kabla ya Kuendelea ningependelea kutaja kwamba Hizi Vokali (Voyel) ziliongezwa baada ya Wahyi wa Kuruani Tukufu  ili kurahishisha Usomaji wa Kuruani. ili kuwasaidia  Wasomaji  wasifanye Makosa katika Matamshi Kwa mfano Herufi  QAF  katika Neno 

قلب Likitiwa  KASRA  chini yake قِ matamshi yatakuwa  “Qi” na Ikitiwa  FATHA  Juu yake قَ matamshi yatakuwa  “Qa”  na Ikitiwa DHUMMA  Juu yake قُ

Matamshi yatakuwa  “Qu”  na hii inasaidia sana kwa wageni wa Lugha ya  Kiarabu kwani   Waarabu wa hapo zamani  katika Enzi ya Mtume ﷺ  alipokuwa hai walikuwa hawahitaji Alama hizi kwani walijua Lugha yao Vizuri,  lakini  kwa Wageni au wasomi wa Lugha hii  wanahitaji Alama hizi kwani zinasaidia Kutamka Maneno kama  Inavyotakikana. Kwani Kama hakuna Alama Hizi basi Matamshi huenda yakabadilika na ikiwa hivyo basi maana pia itabadilika. 

Yaani maana ya neno  litabadilika kwa Kugeuza Matamshi ya Herufi.Kwa  Hiyo  Utafiti  wetu  Utakuwa katika Vokali  au Voyel Moja tu nayo  ni    KASRA  fupi.

Hii Kasrah  Fupi ndiyo tutakayoifanyia  Utafiti katika Mlango  huu.Kwa Kweli Ni Muujiza siyo  Mdogo  kwani  Aya Ya Kwanza Kushushwa Herufi Ya Kwanza katika  Aya hiyo ilitiwa KASRAH.  Angalia Aya Ya Kwanza Kushushwa na Herufi ya Kwanza ambayo  ina KASRAH chini  yake na Inatamkwa   “i”  katika Neno   iKRAA

اِقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ

Matamshi  Yanakuwa   IQRAA  yenye maana ya  “SOMA”

Kwa hiyo Alama Ya KASRA  imetumika Katika Aya ya

kwanza Kushushiwa Mtume. ﷺ Hebu tuchunguze Sura Ya Kwanza Aya ya Kwanza na Pia Sura Ya mwisho Aya ya Mwisho katika Mpangilio wa Msahafu kwani Mpangilio  ni tofauti na Kushushwa kwa Kuruani. Kwa  Hiyo Mpangilio unatokana na Malaika Jibril siyo bure bure tu na ndiyo maana Kuna Miujiza mingineyo ambayo inatokana na Mpangilio wa Sura za Kuruani Tukufu.

Aya Ya Kwanza Kushushwa ni

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

Angalia Alama ya Kasra katika Herufi ya Kwanza “BAA” Ya neno la Kwanza “BISMI” ya Aya Ya Kwanza katika Sura Ya Kwanza Kufuatana na Mpangilio wa Msahafu. Utaona Herufi Baa Imetiwa Kasrah na Inatamkwa BISMI

Na Aya Ya Mwisho  Kushushwa ni 

مِنَ الْجِنَّةِ وَ النَّاسِ

Angalia Alama ya Kasra katika Herufi ya Kwanza “MIM” Ya neno la Kwanza “MINA ya Aya Ya Mwisho ya Sura Ya Mwisho  Kufuatana na Mpangilio wa Msahafu. Utaona Herufi Baa Imetiwa Kasrah na Inatamkwa “MINA”Kwa hiyo kuna maajabu ya kushangaza.  Herufi  KASRA  ina Maajabu. Imechaguliwa Iwe ya Kwanza  Kutumika katika Neno la Kwanza ya Aya Ya Kwanza Kushuka. Na Pia ya Kwanza Katika Neno la kwanza ya Sura Ya Kwanza Katika Mpangilio wa Msahafu na Pia katika neno la Kwanza ya Aya ya Mwisho katika Sura Ya Mwisho katika Mpangilio wa Msahafu.Kwa hiyo Utafiti wetu wa leo tutachunguza  Alama Hii ya KASRA ambayo  ni Vokali  au Voyel  Fupi katika  Sura Ya  Al-Ikhlas. Kama tulivyoona kwamba  Alama Hii  au Harakati hii ya KASRA  ina maajabu maajabu. Tumeiona Ni Ya kwanza  katika Aya tilizozitaja hapa Juu na Sasa tuichunguze katika Sura Ya Al-Ikhlas.

MAAJABU YA ALAMA YA VOKALI AU VOYELI AU HARAKA INAYOJULIKANA KAMA KASRA KATIKA SURA YA AL-IKHLAS

سُوۡرَةُ الإخلاص

بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ (١) ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ (٢) لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ (٣) وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ (٤)

Sura Hii imeshushwa ili kuwajibu makafiri walipomuuliza mtume ﷺ kuhusu Mwenyeezi Mungu ni nani? Sura ikashushwa kuwajibu suala hilo. Sura inahusu kumpwekesha Mwenyeezi Mungu. Angalia Maajabu Kuna Alama ya KASRA moja tu katikati ka SURA hii je unaiona? ipo chini ya Herufi LAM ya neno يَلِدۡ  herufi hii inatamkwa “LI” kwa ajili ya hiyo KASRA. KASRA ipo katikati chini ya Herufi Lam na matamshi ni “LI” Hebu tuchunguze zaidi. Alama hii ni kama inazungumza Kwani Sura Hii inampwekesha Mwenyeezi Mungu na Alama Hii ni Moja tu. inathibitisha kwamba Mwenyeezi mungu ni Mmoja tu peke yake. Sasa tuiangalie vizuri. Ngoja Nisogeze Darubini tuone Vizuri. Katika Sura Hii Jumla ya Herufi za Upande wa Kushoto wa Herufi hii ya LAM ambayo imetiwa KASRA ni 23 na Herufi za Upande wa kushoto wa Herufi Hii ya LAM ambayo imetiwa KASRA ni 23 pia. Angalia Maajabu. Yaani Alama ya KASRA chini ya herufi Lamu inatupa Maajabu Mengineyo. Imegawa Aya za Sura Hii kiherufi. Yaani herufi 23 kushoto na herufi 23 kulia. Haya kweli siyo madogo. Huenda kuna Siri ngoja tuendelee na Safari hii huenda Mwenyeezi Mungu atatufunulia mengineyo. Hebu tuchunguze zaidi. Maneno pia Yamegawanywa. Kushoto kuna maneno Saba na Kulia Kuna maneno Saba pia!!!!! Angalia Maajabu. Herufi Lamu imefanya Kazi ya Kugawa Herufi Na maneno sawasawa. Yaani Herufi na maneno upande wa kushoto na kulia wa Herufi Lam ambayo imetiwa Alama ya Kasra ni sawa sawa utafikiri Computer imefanya hivyo. Haya siyo madogo. hebu tuendelee kwani kuna Mengi ya Ajabu yanakuja mbele.

Ajabu ni kwamba Binaadamu ameumbwa na Chromosomes  46. Mbegu za Mama ni  23 na Baba  23. Kila kiumbe kina Mbegu zake tofauti na Kiumbe kingine. Nimegusia katika Milango ya Webiste hii kuhusu  Mbegu hizi za Binaadamu na baadhi ya viumbe vinginevyo. Kwa hiyo  ukichunguza  Namba  23  za upande wa Kushoto  wa Herufi  LAM  iliyotiwa KASRA  katika Sura hii ya Al-Ikhlas utaona Maajabu mengine  yanayojitokeza. Mtume ﷺ  alipoulizwa Suali na Makafiri  Kuhusu Dhati ya Mwenyeezi Mungu au asili yake ni nini au ukoo wake ni upi  kwani hao  Makafiri hao walikuwa wakifikiri Mwenyeezi Mungu ni sawa na Binaadamu basi Mwenyeezi Mungu akashusha Jibu kwa Njia ya Sura Hii.  Kwani  alipojibu  Suala lao  kwa kusema kwamba “Mwenyeezi Mungu ni mmoja, Hategemei na Amejitosheleza, Hakuzaa na Hakuzaliwa na Hakuna Mfano wake na chochote”  Jawabu hili linatosha Kujibu Suali la makafiri lakini Aya hizi zimebeba Siri nyinginezo ambazo tunazigundua siku za leo kama kwamba Mwenyeezi Mungu alikuwa akisema kwamba 

“Yeye hana Mfano  na siyo kama Binaadamu ambaye nimemuumba kwa njia ya Manii ambayo asili yake ni Chromosomes  23 za baba na 23 za Mama”. Aya hizi hazikusema habari hizi za  Chembe cha uzazi kiwaziwazi  (Chromosomes) lakini zimebeba  habari hizi  kiajabu sana kwa njia ya Hesabu. Na hii imekuwa Muujiza mkubwa katika Karne yetu hii ya leo ambayo  imajaa elimu za Sayansi.  Kwa hiyo  ukifikiri utaona Kama kwamba Mwenyeezi Mungu alikuwa an maana hiyo  kutufahamisha kwamba  Yeye  hana mfano  wa chochote lakini  nyinyi  nimewaumba kwa chembe za uzazi 23 za Baba na 23 za Mama. 

15/10/2022

Alhamdulilah leo siku ya Jumamosi Tarehe 15/10/2022 Nia yangu ni kuendelea na Muujiza wa Sura Ya Al-Ikhlas niliyoanza kuelezea hapa Juu. Na Pia Sura za Al-Falaq na Al-Nas.

Kama tulivyoona hapa Juu kwamba Sura Hii imegawanyika katika Mafungu mawili kwa Herufi ya Al-am ambayo imetiwa KASRA.

Tumeona kwamba Jumla Herufi ambazo zipo upande wa kushoto wa Herufi Ya Al-Lam ambayo imetiwa Kasra chini yake ni 23 na zile Herufi ambazo zipo Upande wa Kulia wa herufi ya Al-Lam pia 23

Hii namba 23 pia tunaikuta tena imetajika kiajabu sana.  Hebu tuchunguze zaidi.

Ukihesabu Herufi za kiarabu za Kisasa kuanzia Mwanzo mpaka Herufi ya Al-Lam utaikuta Herufi hii ni ya 23 pia. 

Kwa hiyo Herufi Ya LAM Katika Mpangilio wa Herufi za Kiarabu za Kisasa  (HIJAI  SYSTEM) yaani kuanzia A mpaka Z yaani Kiarabu Alif mpaka Herufi ya “Yaa” utaikuta Lam ni ya 23 pia!!!!!

Je unaona Muashirio wa Kiajabu yaani Inaashiria Chromosomes za Binaadamu. Hebu tuendelee na Safari ya Uchunguzi. Sasa Tuchunguze Uhusiano baina ya Lam hii ya katikati na Lamu za nyuma na mbele yake.

INAENDELEA HAPA CHINI

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ (١) ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ (٢) لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ (٣) وَلَمۡ يَكُن لَّهُ ۥ ڪُفُوًا أَحَدٌ (٤)

Tukichukulia kipimo cha idadi ya herufi za Jina la mwenyeezi Mungu  اللّٰه‎  ambalo lina Herufi  NNE  na kwa hiyo hebu tuhesabu herufi  za LAM  nyuma na Mbele  ya LAM ilityotiwa KASRA katika Sura ya Al-Ikhlas mara  4

Upande wa kushoto  kuna Lam  ya 4 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Upande wa kushoto kuna Lam ya 8 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Upande wa kushoto kuna Lam ya 11 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Yaani uhesabu kuanzia LAM  iliyotiwa KASRA  jumla ni LAM  4

Sasa tujumlishe LAM hizi  Nne 

4  + LAM  8 + LAM  11=23 

Je unaona Tunapata LAM  23!!!  Tunapata tena namba 23  

Sasa  tufanye hivyo  hivyo upande wa Kulia.

Upande wa kulia kuna Lam ya 4 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Upande wa kulia kuna Lam ya 8 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Upande wa kuliakuna Lam ya 11 Kuanzia LAM iliyotiwa KASRA

Sasa tujumlishe LAM hizi Nne

LAM 4 + LAM 8 + LAM 11=23

Je unaona Tunapata LAM 23!!! Tunapata tena namba 23!!!! 

Je unaona Maajabu. 

Kila Upande tumehesabu herufi  za LAM. Katika  upande wa kushoto kuanzia LAM iliyotiwa KASRA  na Upande  wa Kulia hivyo hivyo na baada ya kuzijumlisha tumepata  Namba  23!!! 

Katika Sura Hii  ya Ikhlas Herufi Ya Kwanza ni  QAF  na Ya  Mwisho ni   DAL, Katika Mpangilio wa Herufi za ABJAD  (ABJAD  System) Herufi Ya QAF  ni ya 19  na Herufi  Ya DAL  ni ya 4   tukijumlisha 19 + 4 tunapata Jawabu  23 !!!!!

Allahu Akbar  Angalia Maajabu   Namba 23 ilivyokariri.

haya siyo madogo hata kidogo.  Namba za Kiajabu sana tena sana. Inaashiria Chromosomes tena zaidi ya Mara moja Allahu Akbar.

Katika  Lugha ya Kiarabu  Mpangilio wa Herufi  zake wa kisasa ni tofauti na hapo zamani. Na Tukichunguza Sehemu au Positions za Herufi hizo za zamani zinazojulikana kama ABJAD Syatem  kisha tukipachika katika  Sura hii tutapata maajabu mengine makubwa ya kushangaza. 

Ukipachika  Namba  hizi katika Sura Hii utashangaa kupata maajabu mengine. Kwa mfano  Neno  قُلۡ litakuwa 19 + 12  na hivyo hivyo ukigeuza Herufi zote katika namba utapata Jumla ya Namba  katika Upande wa Kushoto wa Herufi  Ya LAM  iliyotiwa KASRA ni  198  na katika Upande wa Kulia  wa Herufi ya LAM iliyotiwa Kasra ni  198 pia!!! sasa mbona namba hizi zinafanana kiajabu  sana utafikiri zilipimwa na Computer. Kila Mfano  unashagaza. Mbona Namba hizi  zinalingana sana kiajabu sana tena sana.

Lenye kushangaza zaidi ni kwamba  Namba  tuliyopata ya 198 kila upande inaashiria  Jumla ya Herufi za Sura Tatu  yaani 

Sura Ya ALIKHLAS  ina Herufi   47

Sura Ya Al-Falaq ina Herufi  71

Na Sura ya Al-Nasi ina Herufi  80

Tukijumlisha tunapata  maajabu.  (47 + 71 + 80=198!!!)

Allahu Akbar. Allahu Akbar. Angalia Maajabu. Tumepata namba  198 na Namba hii ni Jumla ya Sehemu au Positions za Herufi za Sura Ya Al-Ikhlas. ambayo  tumeona Hapa juu ni 198

Je kuna Siri  gani katika Namba 198?  Inaashiria Jumla ya herufi za Sura Zote Tatu. Labda Linaashiria   Uhusiano wa Sura Hizi tatu. Na ikiwa ni hivyo basi inakubaliana na Hadithi tulizosoma hapa juu kuhusu  Sura Hizi  tatu na umuhimu wake. Hizi Sura Zimeficha Makubwa. Udugu  wa Sura Hizi tatu  unathibitika na hadithi tuliyoisoma haa juu kuhusu Mtume alikuwa akizisoma Sura Hizi tatu kabla ya Kulala na kisha kujipaka Mwilini. Allahu Akbar. Kwa kweli kuna Mengi bado hatujui. Na Mwenyeezi Mungu ni Mkubwa Sana. Kuruani imeficha Makubwa yasiyo na Mfano.