SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Siasa/Dunia/Sayansi

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

SIASA ZA DUNIA NA SAYANSI

Alhamdulilah. Leo  Tarehe 10  September  2022. Baada ya Kuandika machache katika Mlango  wa “Makala ya Sayansi-3” nimeona bora  nijipumzishe na kuanza kuandika Mlango huu mpya ambao  kulikuwa na Habari  zilizokuwa katika Fikra zangu tangu  Jana na kwa kuchelea kuzisahau nimeona bora niharakishe katika Mlango huu mpya. Kuna methali  inayosema  “Kipya kinyemi ingawa Kidonda”  kwa hiyo  hebu tuanze na Mlango  Mpya.

Tulisomeshwa Mashuleni kuhusu  Historia ya Ukoloni.,Kwamba baada tu ya Vita kuu ya pili  Duniani  Mataifa Makubwa wakaa  Kitako kupanga  mipango ya kugawana Nchi za Dunia.  Dunia nzima  ikagawanywa  vipande vipande, Vinyang’anyiro  vikaanza, Mipaka ya Nchi za Dunia  Ikachorwa. Mtawala na Mtawaliwa, Vita vya Mapaka na Mapanya. au Papa na Dagaa. Katika Utawala Utamaduni Mpya ukaja na kuenezwa na Huu ndiyo Ukoloni kwa Ufupi.  Na ilikuwa Dunia Nzima. Sizungumzii hapa nchi moja bali Dunia Nzima.

Sasa Tuache  Vita Vya Dunia  hebu turudi Nyuma Hapo zamani sana yaani katika Karne  za Nyuma  kuanzia Mwaka 711  (8th  Century) Uislamu ulienea huko  Ulaya. Na baada ya Miaka Mingi waislamu waliishi huko Ulaya. Baadaye  Ulaya  walipata bahati ya Kusoma Elimu walizokuja nazo Waislamu.  Pia Jambo  lingine ambalo ningependelea  kulitaja ni kwamba  Elimu za Waislamu ziliibiwa pia na Majina yao kufutwa katika vitabu vya Historia. Huu ni ukweli. Hapa chini  kuna Video ya Historia hiyo ambayo inashangaza sana. Imetengenezwa na Wajerumani. Isikilize Vizuri. Inazungumza kwa lugha ya Kijerumani lakini imefasiriwa kwa Kiingereza na Kiarabu. Wajerumani wenyewe wanasema ukweli kwamba waliiba Uvumbuzi mbali mbali za Waislamu katika  Nyanja Mbalimbali. Waislamu  walikuwa wamezama  katika Uvumbuzi mbalimbali  na walikuwa mwenge duniani. Elimu hizo chanzo au msingi ni KURUANI Tukufu. Ndugu zanguni angalia Mambo haya ya kushangaza. KURUANI  ndiyo ilikuwa chanzo cha Elimu za  Waislamu hawa wa Mwanzo ambao kama siyo wao basi Kusingekuwako na maendeleo tunayoyaona leo hii. Kuruani ndiyo iliyohimiza kufanya juhudi ya Utafiti  wa kisayansi Duniani.

Sikiliza Video kwa Maelezo zaidi.

Hii  Video imefanywa na Wajerumani wenyewe. Yaani sisi  yetu masikio na macho tu. Tuangalie ili tusome Historia za Dunia. 

Video-1

Video za Elimu za Waislamu na Wizi uliofanyika kuibiwa Elimu hizo. Video imefanywa na Wajerumani. Kwa lugha ya Kijerumani lakini Maandishi ya Tafsiri kwa Kiingereza na Kiarabu

Video-2

Hii Video ni Namba 1 inahusu Elimu zilizoibiwa. Waislamu waliibiwa Elimu zao. Lugha hapa ni Kijerumani na Kiarabu tu peke yake.

Video-3

Video namba 2 Ineendelea habari ya Elimu za Kiislamu zilizoibiwa. Video kwa lugha kijerumani na Kiarabu tu.