SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Structure/Kuruani

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

MFUMO/STRUCTURE YA KURUANI

Kwa kadiri  tunavyosoisoma kuruani ndiyo kadiri  tunavyojikuta kwamba Elimu tuzijuazo hapa Duniani ni tonye tu katika mengi ambayo hatujui. Kuruani inathibitisha kwamba Maneno yake siyo ya Kibinaadamu hata kidogo.  Haya ni maneno yake Mwenyeezi Mungu mtukufu. Mwenyeezi Mungu akipenda katika Mlango huu nitagusia tonye tu katika bahari ya Elimu iliyokusanywa katika Kuruani.  

Ni yale nitakayogusia unaweza pia kuhakikisha mwenyewe. kwani Hakuna kilichofichika. Allahu Akbar.

Hapa chini nitaelezea Mishangao mblai mbali:

MSHANGAO WA KWANZA

Sura ya Yasin ina herufi  2988

La kushangaza ni kwamba Sura hiyo ni ya  36  na Aya zake ni 83   na ukifanya hesabu ya Multiplication namba hizi mbili  yaani  83  mara  36  basi utapata kama ifuatavyo:

83 X 36  yaani  Namba ya Sura na Aya zake utapata 

2988   ambazo ni idadi ya herufi ya Sura hii.  Angalia Mpnagilio wa Kiajabu. Angalia Mfumo au Structure na Kuruani. Je Mtume ﷺ alikuwa akihesabu na kupanga yote haya?  huoni kwamba huu ni Kamuujiza miongoni mwa Miujiza mikubwa mingineyo katika Kuruani. Hizi Hesabu zinatisha. Aliyepanga hivi ndiyo aliyeumba ulimwengu huu na Kuruani ni Hotuba yake. Haya siyo manenp  ya Kibinaadamu hata kidogo. 

MSHANGAO WA PILI

Huu mshangao wa pili unahusu  Mwaka Ambao Mtume  ﷺ na Majeshi ya Maswahaba walipoiteka Mji wa Mecca kutoka kwa Makafiri. Ilikuwa mwaka  630 Katika Miaka ya Calendar Ya Kiislamu. Yaani Mwaka 630 wa Hijria ambao ni sawa na Mwaka wa 1233 katika Calendar zetu za Ensi ya Kikristo au Gregorian Calendar.

Kwa hiyo  Mwaka wa Kiislamu ni  630  H  amabo sawa na Mwaka wa Kikristo wa 1233  C.E.  (Christian Era). 

Sasa  hebu tuchunguze na tuendelee na Miujiza ya kiajabu. 

Kwanza Ningependelea kuwajuulisha kwamba Waarabu na Mataifa Mengineyo ya wakati huo wa karne ya 7 yaani katika Enzi ya Mtume ﷺ walikuwa wakitumia Herufi kama Namba. Kwa Mfano

Herufi  Alif iliwakilisha namba 1

Herufi  Baa ilwakilisha  namba 3

Herufi  Jim  iliwakilisha  namba 3

Na hivyo hivyo Herufi Zote zilizobaki ziliwakilisha Namba kwani Wakati huo kulikuwa hakuna Namba .

Katika Enzi ya Mtume ﷺ kulikuwa hakuna hizi namba tunazotumia leo hii bali walitumia Herufi katika maisha ya kila siku. 

Sasa tuchunguze  Maneno Mawili yafuatayo

عام الفتح    (AAM  ALFATH)  yaani “The Year of the Conquest”  Kwa lugha  za kileo ni  “Siku ya Uhuru”  Tukibadili maneno  haya mawili katika Namba zinazowakilishwa na Herufu hapa juu utashagaa kuona kwamba unapata namba 630 na kama tilivyoona hapa kuu kwamba Namba hii 630 ndiyo siku ambayo Waislamu waliiteka Makca. Hebu  tujumlishe Herufi hizi ili tuone Ushahidi:

Herufi Ya Ain inawakilishwa na namba =70

Herufi  Alif inawakilishwa na namba= 1

Herufi  Mim inawakilishwa na namba=40

Herufi  Alif inawakilishwa na namba=1

Herufi  Lam inawakilishwa na namba=30

Herufi  Faa inawakilishwa na namba=80

Herufi  Taa inawakilishwa na namba=400

Herufi  Haa inawakilishwa na namba=8

Jumla ya Namba hizi ni  =

70 +1 + 40 +1 + 30 + 80 + 400 + 8=630

Kwa hiyo  inashangaza kuona Maneno Haya mawili yanatupati namba 630 ambao ni mwaka wa Kuiteka Makca.  

Tukizidi  utafiti utaona maajabu Mengineyo ya kushangaza. Tukigeuza Namba 630  kutoka katika Mwaka huu wa Kiislamu  wa Hijriya  kwenza katika Mwaka wa Kikristo utakuta Ilikuwa mwaka 1233

kwa hiyo  mwaka wa kiislamu wa 630  ni sawa na mwaka wa kikristo wa Hijriya wa 1233

Mshangao mwingine ni kwamba Aya inayozungumzia Kutekwa kwa Mecca au Conguest of Mecca au Uhuru wa Mecca Ukigeuza Herufi zake basi utashagaa unapozijumlisha kwani namba utakatopata ni 1233 tulioisoma hapa juu. 

Aya hiyo ni  katika Sura ya Al-Fath Namba 48  Aya Ya Kwanza.

إِنَّا فَتَحۡنَا لَكَ فَتۡحً۬ا مُّبِينً۬ا

Tafsiri ya Aya ni  “Tumekufunulia Mfunuo Ulio wazi”  yaani Tumekupa Mfunuo  wa Uhuru wa Mji wa Mecca. 

Aya hii Inazungumzia  Uhuru au Conquest ya Mecca. upapogeuza herufi zake katika namba na kuzijumlisha namba hizo utapata Jumla namba 1233.

Na kama tulivyyona namba hii ni mwaka wa Kikristo (Calendar ya Ardhi kuizunguka Jua)  ambao unalingana na mwaka wa Kiislamu  wa 630 (Calendar ya Mwezi Kuizunguka Ardhi)  wa Uhuru au Kutekwa kwa Mecca. Unaona Maajabu wa Namba zinavyozungumza? Je unaonaje haya Maneno ya Kuruani? Ninavyoona haya siyo maneno ya kawaida. Ikiwa mfumo wa Maandishi tu unatushangaza sasa je Maana ya Aya hizi?  Kila kitu kinatushangaza, Mpangilio wake, Herufi zake, Maneno yake, Maana Yake na mengineyo tunayoyajua na tusiyoyajua. Allahu Akbar.  Allahu Akbar.,

MSHANGAO WA TATU

Tuendelee na safari yetu ya Mshangao wa Tatu.

Kuruani haina mwisho. Itakuwaje na mwisho na Haya ni maneno ya Mwenyeezi Mungu aliyeumba kula kitu. Amesema mwenyewe katika kuruani kwamba Bahari zinegkuwa Wino na Miti kalamu basi Wino ungekisha lakini maneno yake hayataisha. Je huoni Maajabu.

Hebu tuchunguze Sura Ya Al-Naml  namba 27.  Tuchunguze  Neno   “KURUANI” ambalo ni la pekee katika Ukurasa huo namba 383  na lipo katika Aya namba 76.

Jambo  linalonishangaza sana ni kwamba Neno  “KURUANI”  yaani الْقُرْءَانَ   ukiligeuza Herufi za neno hili katika namba za Hesabu  kama tulivyofanya katika Mshangao Namba 2 hapa juu basi utachagaa kuona Kwamba Jumla ya Herufi ni  namba 383  na namba hii ndiyo namba ya Ukurasa huo. 

Alif=1

Lam=30

Qaf=100

Raa=200

Hamzah=1

Alif=1

Nun=50

1 + 30 + 100 +200 + 1 + 1 + 50=383

Je unaona Maajabu. Baada ya Kujumlisha Namba zilizotumika hapo zamani ambazo zilikuwa zikiwakilishwa na Herufi tunapata  Namba 383 ambayo ni Jumla ya Herufi za neno  الْقُرْءَانَ   Yaani  “KURUANI”.

na namba hii ni  Namba ya Kurasa ambayo Lipo neno hilo KURUANI katika Aya Namba 76.

Sasa linalojitokeza na kutushangaza zaidi ni kwamba namba  383 ni Prime Number namba 76, Je unaona Maajabu.  Katika Elimu ya Hesabu  Kuna Prime na Common Numbers. Na Namba 383 ni Prime Number ya 76 yaani ukihesabu Prime Numbers zote kuanzia ya kwanza mpaka ya 76  utapata namba 383. Je onaona ya maajabu. Na 76 ni Aya ambayo ina neno  الْقُرْءَانَ   “KURUANI”.  

Hebu tuchunguze zaidi. Hebu tuhesabu Herufi kuanzia mwanzo wa Ukurasa huu mpaka mwisho wa neno  KURUANI na kisha Tuhesabu MANENO kuanzia mwanzo wa Ukurasa huu mpaka Mwisho wa neno  “KURUAN” katika Aya Namba 76.

Tukifanya hivyo tutapata mengine ya kushangaza.

Jumla ya Maneno kuanzia mwanzo wa ukurasa huu maka neno KURUANI  ni  133

Na Jumla ya  herufi  kuanzia mwanzo wa Ukurasa huu mpaka mwisho wa Neno  KURUANI ni   516

Hebu  tutoe  Maneno katika Herufi  yaani  tutoe namba 133 kutoka katika namba 133

516-133= 383   Angalia Mshangao wa kiajabu. tukifanya hivyo tunapata Thamani ya Neno  “KURUANI”  tuliyoizungumzia hapa juu na Pia  Namba ya Ukurasa ambao ni  383. Angalia Maajabu. Ndugu Zanguni Waislamu. Mnaona Maajabu. Haya siyo maneno ya Kibinaadamu hata kidogo. Nakuhakikishia  kwa Asilikia 100  yaani    100%  kwamba Haya ni maneno ya MUUMBA. Allahu Akbar.  Angalia Mpangilio wa Kimuujiza usio na Mwisho. Na bado tupo Mwanzoni. Kuruani imejaa tusiyoyajua. Kuna SIri kubwa kubwa za Maajabu Makubwa. Kuruani ni Ya Binaadamu na Majini pia. Allahu Akbar. Tumche Mungu. Je huoni haya tunayozungumza. Je huogopi?

MSHANGAO WA NNE

Tuendelee na Mshangao wa Nne. Kwa kweli inashangaza sana. 

Sura Ya Al-Naml Namba 27  Aya namba 6

وانك لتلقي القران من لدن حكيم عليم

Mwenyeezi Mungu anamwambia Mtume  ﷺ  kwamba 

“Kwa hakika  umepewa au umefundishwa kuruani kutoka kwa mwenye Hekima na Elimu”

Sherehe ya Aya hii ni kwamba Mtume ﷺ ameipokea kuruani kutoka kwa Mola mwenye Hekima na Elimu Kubwa.

Hebu  Tuifanyie Utafiti Aya hii.

Neno لتلقي   yaani  Umepokea au Kufundishwa.  Neno hili ni la pekee  katika Kuruani Yote. Limetumika mara moja tu katika Aya hii.  

Neno hili ni la  40  ukihesabu maneno kuanzia mwanzo wa Sura hii mpaka mwisho wa nenp hili.  Je unaona ya maajabu. Mtume ﷺ  alipewa  WAHYI  au Revalation  au Ufunuo  wa kwanza  alipokuwa na umri wa miaka  40.

Je unaona ya kushagaza. Hebu tuendelee kuchambua ndugu waislamu  hatujamaliza na hatutamaliza kwamwe. Miujiza isiyo na mwisho. Hebu tusonge mbele.

Hebu tujumlishe  Namba Ya Sura  na Namba ya Aya na Idadi ya Maneno ya Aya hii namba 6

Yaani  Namba ya Sura ni   27

Aya namba 6

Jumla ya Idadi ya Maneno ya Aya hii ni  7

27 + 6 + 7=40

Unaona Maajabu. Tunapata tena Umri aliokuwa nao Mtume ﷺ alipopokea Wahyi kwa mara ya Kwanza yaani alipokluwa katika Pango la HIRA na mara ya kwanza alipokutana na Malaika JIBRIL. Je unaona  Mara ya pili tunapata Unri wa Mtume ﷺ  Allahu Akbar. 

Bado hatujamaliza Hebu tuchunguze zaidi ili tuone ya kushangaza.  

Neno  لتلقي   ambalo tumeshalielezea hapa juu tukiligeuza katika namba. yaani kutumia namba za herufi kama tulivyoelezea katika maelezo ya mishangao mingine  hapa juu utapata namba ya kushangaza zaidi.

hebu tufanye hivyo.

Herufi  Lam=30

Herufi Taa=400

Herufi Lam-30

Herufi Qaf=100

Herufi Yaa=10

Tujumlishe Namba za herufi hizi

30 + 400 + 30 + 100 + 10=570

Ajabu Kubwa. Namba 570 ni Mwaka aliozaliwa Mtume Mohamad. ﷺ  Je  unaona maajabu. Yaani Mwaka aliozaliwa Mtume ni sawa na thamani ya Herufi za neno hili  la  LATULAQAA  yaani Kupokea au Kufundishwa.  Haya siyo mambo madogo. Ni Miashirio ya kiajabu kiajabu. Ni  miashirio ya kushangaza. Hebu fikiri. Allahu  Akbar.