SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

University/Kuruani-1

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

SAYANSI  ZA DUNIA

SAFARI ISIYO NA MWISHO KATIKA UNIVERSITY YA KURUANI  TUKUFU

Alhamdulilah nashukuru Mwenyeezi Mungu kwa kutupa Uzima na Afya ya kuweza kuandika haya machache. Kwa uwezo wa Mwenyeezi Mungu leo nitaanza Safari ndefu na Ninawakaribisha wote  tusafiri pamoja katika  Safari hii Kubwa ya Kuchambua Elimu za Sayansi za Duniani.

Baada ya Kuandika Suala la Pili  la Tarehe ya leo 25/09/2022 katika Mlango wa “DARASA LA KILA SIKU” Nimehisi kwamba bado nina nguvu za kutosha za kuendelea kuandika mengineyo yaliyo na uhusiano  na Kuruani Tukufu.

Kama ulivyoona kila mlango wa Website Hii haujamalizika. Na hii inatokana na Kwamba Elimu ya Kuruani haina Mwisho.

Nimejiuliza je Niendelee na Milango Miongoni mwa Milango niliyokwishaanza?  au Nifungue Mlango Mpya?

Nikajiambia “Kwa nini Nisifungue Mlango Mpya?”  

Nikaona Bora Nichague  Topic au Kiini  Kikubwa ambacho Kinalingana na Nguvu za leo. Nikasema nitachambua  “Sayansi Za Dunia”

Ni Kiini siyo Kirahisi na ambacho Hakina Mwisho. Je  Itawezekana Hivyo?

Tatizo la Kuelezea Ni La Kwanza na La Pili  Utafiti katika Kuruanilazima Kuwe na Uhakika Kwani Haya ni Maneno ya Mwenyeezi Mungu na lazima iwe Sahihi  kwa Asilimia  100%. Hakuna  Kubuni.

Nimeona Bora Kwanza Nianze moja kwa moja Na Sayansi na kisha Kuhusu  Kuruani ambayo ndilo Lengo la Makala Hii  nitalishughulikia Mara kwa Mara

Sisi wote ni wanafunzi au kwa lugha safi  “Wanavyuoni” na kwa hiyo  Nitafanya Jitihada zangu zote kwani Nimepania.

Kwa leo Nawakaribisha katika  Mlango huu kwa Salaam za mwenyeezi Mungu zinazosema

“Asalaam Alaykum  Watrahmatullahi Wabarakatuh”

Kisha Ninamuomba  Mwenyeezi Mungu ambaye ameumba kila kitu ajaalie kila NInachoandika hapa kiwe kwa ajili yake tu na siyo kingine. Isiwe  Ujira au Cheo bali Akhera. 

Tafadhali Sana Wasomaji ningependelea kuwajuulisha kwamba Mlango huu hautakwisha kwa siku moja na kwa hiyo kutakuwa na nyongeza kila mara na kwa hiyo ukipendelea Utafiti wa malngo huu basi itabidi urudi kila mara unapopata nafasi.

Sasa Nitaanza Kwa Kujiuliza Suali:

Ni Nini Sayansi?

Jawabu:

Sayansi Ni Njia Ya Kuendeleza Elimu zetu na Kufahamu Ulimwengu Baada ya Kukusanya Ushahidi  wa Maono na Baada ya Itafiti  wa Ushahidi Huo.

Kwa hiyo  Siyo  Rahisi  Kuelezea  Neno Sayansi  lakini  Jawabu Hili siyo  Baya na lipo karibu na Sahihi. Ni Definition iliyo Karibu na Ukweli.

‘Science is a means of improving our knowledge and understanding of the universe based on the collection of observation-based evidence.’

Wanasayansi  wanatumia Mbinu  nne katika Utafiti  wa Kisayansi na Mbinu hizo tunaweza kuzipanga kama ifuatavyo:

1/Observation  (Yaani Kuona au Kuhisi)

2/Hypotheses (Kufikiri Sababu Kwa kile ulichoona au kuhisi).

3/Prediction (Kukisia Jawabu la Suala Lako)

4/Experiment  (Jaribio La Suala)

5/Fact (Baada ya Majaribio Mbalimbali-Several Positive Experiments) 

Hizo Ndizo Njia (Method Nne ambazo Wanasayansi  Wanatumia Katika Utafiti)  Na Baada Ya Experiment jawabu litathibitisha Suala La Utafiti. Ikiwa Experiment mbalimbali zinathibitisha Jawabu Hilo basi Jawabu la Utafiti litakuwa ni La Ukweli na Litaitwa  “Scientific Fact”

Ndugu  zanguni Waislamu Sayansi  zilizopo katika Kuruani  Ni   “FACTS”  tupu na hii inathibitisha Kwamba Maneno ya Kuruani siyo ya Binaadamu.  Allahu Akbar.  Na pia Inathibitisha kwamba Mtume Mohamad  ni Mtume wa kweli.

Sayansi Imegawanywa na Wanasayansi katika Mafungu au Matawi Matatu:

A/Natural Sciences

B/Social Sciences

C/Formal Sciences

Sasa Tuchambue  Matawi Haya Matatu:

A/Natural Sciences

Mlango  wa Sayansi  Hii Pia Umegawanywa katika Mafungu  Matatu Yafuatayo:

1/Physical Sciences

2/Life Sciences

3/Earth Sciences

Kila Fungu katika Mafungu Haya Matatu Yamekusanya Matawi MbaliMbali:

1/Physical Sciences

Physics

Mechanics

Electromagnetics

Thermodynamics

Kinetics

Chemistry

Inorganic Chemistry

Electrochemistry

Analytical Chemistry

Earth Sciences

Planetary  Science

Oceanography

Geology

Astrophysics

Polymer Science

Meteorology

etc.

2/Life Sciences

Anatomy

Botany

Biology

Zoology

Neurobiology

Marine Biology

Embryology

Ecology

Palaeontology

Genetics

Cell Biology

Ethology

NeuroScience

BioChemistry

Taxonomy

Morphology

Microbiology

Marine Biology

Biotechnology

Entomology

etc.

3/Earth Sciences

Astronomy

Meteorology

Atmospheric Sciences

Glaciology

Climatology

Structural Geology

etc.

Tuanze Kuchambua Kipengele cha pili cha Sayansi. Nacho ni  Social  Sciences

B/SOCIAL  SCIENCES

Social  Sciences pia zimegawanyika katika Mafungu mbalimbali yafuatayo:

Anthropology

History

Archaeology

Human Geography

Economics

Law

Development Studies

Education

Criminology

Political Science

Translation Studies

Media Studies

Business and Management

Philosophy

Health

International Relations

Linguistics

Custural Studies

Sociology

Physiology

etc.

C/FORMAL SCIENCES

Tuanze Kuchambue Kipengele cha Tatu cha Sayansi. Nacho ni Formal Sciences

Mathematics

Logic

Computer Science

Data Science

Statistics

Systems Science

Artificial Intelligence

Information Technology

etc.

Tuendelee na Safari Yetu isiyo na Mwisho.

Kuna Matawi Mengine  Yameungana na Kuzalisha Tawi za Elimu Mpya.

Physics + Chemistry=Physical  Chemistry

Astronomy + Physics=Astrophysics

Biology + Chemistry=BioChemisty/Organic Chemistry

Biology + Physics=BioPhysics

Biology +Geology=Palentology

Geology + Chemistry=GeoChemistry

Geology + Physics=Geophysics

Astonomy + Geology=AstroGeology

Sherehe Za kazi za baadhi ya Matawi Ya Elimu Mbalimbali  yaliyozozuka  hivi karibuni nazo ni kama zifuatazo:

Agronomy: Crop plants

Anthropology: Human past, behaviours, and cultures

Aeronautics: Airplanes and flights

Astronomy: Celestial Objects

Astrophysics: Understanding the working of the universe

Biotechnology: Creating/developing products using microorganisms

Cytology: Cell study

Engineering: Scientific principles and their applications

Exobiology: Extraterrestrial life

Forensic Science: Application of Science in legal process/criminal investigations

Materials Science: Study of properties of solid materials

Mycology: Study on Fungi

Ornithology: Study of birds

Psychology: Understanding the human mind and behaviour

Petrology: Rocks, origin, and characteristics

Radiology: Diagnosing and treating various diseases

Toxicology: Chemical components and their effects on living organisms

Virology: Study of Virus

Hapa Juu nimeelezea  Orodha kubwa ya Elimu Mbalimbali za Kisasa ambazo hazikuwapo  katika karne za Nyuma.  Hizi ni Elimu za Kisasa ambazo zimezuka Kwa ajili ya Kuusoma Ulimwengu. Binaadamu tangu zamani anajitahidi kuusoma Ulimwengu na Dunia ili apate Kuishi Vizuri. 

Matawi mbalimbali ya Elimu yamezuka  Baada ya maendeleo ya Kisayansi. Elimu hizi  zimekuja ili kutatua Matatizo ya Binaadamu na Kumsaidia aishi kwa salama na amani na pia katika kutafuta maisha yaliyo bora zaidi ya haya tunayoishi. Nadhani Katika Mlango huu sikutaja Matawi yote yaliyozuka kwa hiyo huenda kuna mengineyo zaidi ya haya lakini nina uhakika yaliyobaki  siyo Mengi na kwa hakika yanatosha kwa kuendelea na utafiti wetu wa Kuruani na hadithi  za Mtume.

Hebu Tuangalie Ufupisho  wa Uhusiano baina ya Matawi  tuliyokusanya hapa juu:

SCIENCE

Tunaweza Kugawa Sayansi Katika Mafungu Makubwa Matatu Makubwa.

A/Formal  Science

Empirical Sciences

B/Natural Science

C/Formal Science

Kila  Moja Ya haya matawi matatu tunaweza  kuyagawa katika Foundation na Application. Yaani Msingi na Matumizi ya Elimu Hizi.

A/FORMAL  SCIENCE

1/FOUNDATION YA FORMAL SCIENCE

Logic, Mathematics, Statistics 

2/APPLICATION YA FORMAL SCIENCE

Matumizi ya Elimu  hizi zimeweza Kutumika katika  Computer Science etc.

Empirical Sciences

Empirical Sciences zimegawanyika katika Mafungu Mawili.

1/Natural Sciences

2/Social Sciences

Sasa Tuangalie Foundation na Application ya Matawi haya Mawili.

B/NATURAL SCIENCE

1/FOUNDATION YA NATURAL SCIENCE

Physics; Chemistry; Biology; Earth science; Astronomy

2/APPLICATION YA NATURAL SCIENCE

Engineering; Agricultural science; Medicine; Dentistry; Pharmacy

C/SOCIAL SCIENCE

1/FOUNDATION YA SOCIAL SCIENCES

Economics; Political science; Sociology; Psychology; Cultural anthropology

2/APPLICATION YA SOCIAL  SCIENCES

Business administration; Jurisprudence; Pedagogy

KURUANI TUKUFU NA  ULIMWENGU/MALIMWENGU

Elimu zote tulizozitaja hapa juu na nyinginezo ambazo hatukuzitaja na zile ambazo bado  kuzuka yaani za siku za mbele zinashuhudia kwamba Mwenyeezi Mungu  ni mkubwa sana tena sana. Kwa kweli Binaadamu bado  wanahangaika Kuusoma Ulimwengu na kwa kweli tupo mwanzoni. Mpaka Leo kuna Mengi ambayo hatujui juu ya ujanja wetu wote tulionao.

Elimu za Mwenyeezi Mungu hazina Mwisho kama alivyosema katika kuruani tukufu  kwamba Bahari  zingelikuwa Wino na miti kalamu basi  Wino ungelikwisha lakini Elimu zake hazina Mwisho. Tunaambiwa na Wataalamu kwamba Kuna  Zillions  na Zillions ya Galaxies. Huko hakuna ajuaye isipokuwa Mwenyeezi Mung tu peke yake. Ikiwa Hatujaisoma Galaxy  yetu (inajuklikana kama Milky Way) je  zinginezo?  Kwa kweli  hizo itabaki ndoto tu yaani haiwezekani hata kufikiria kwani zipo mbali sana. Leo hii wacha Galaxy bali Ardhi tu bado Hatujaimaliza. Hakuna Nchi iliyoweza Kufikia Planets zilizo mbali na sisi. Wanasayansi wameweza kufika katika Mwezi lakini hata huo Mwezi Bado  hakuna aliyeweza kuisoma kila kitu. Kwa kweli Binaadamu bado tupo nyuma sana na hakuna Anayeweza  Kujigamba. Allahu Akbar.

AYA ZA KURUANI  ZINASHUHIDIA UKUBWA WA MWENYEEZI MUNGU MTUKUFU

Tumechambua hapa juu Elimu za Kisayansi na Mwono wa Wanasayansi  Duniani  kuhusu Matawi  Mbalimbali. Sasa imefika wakati tufanye Utafiti  katika Kuruani Tukufu kwa kupima Matawi tuliyoorodhesha  hapa Juu na Maneno ya Kuruani ili tuone Picha Kamili. Nina imani kwamba Safari hii itatupa faida kubwa sana kwani  Elimu hizi  zote ni zake Mwenyeezi Mungu na Kuruani ni maneno  yake.

Kwa hiyo lengo ni kusoma Elimu hizi kwa Msaada wa Kuruani Tukufu. Nadhani Umenifahamu. Nina imani kubwa kwamba Kuruani itatupa Msaada Kusoma Ulimwengu  vizuri zaidi kuliko juhudi zetu. Tutafanya Utafiti kwa mifano. Na Pia Elimu hizi zitatufafanulia zaidi Ufahamu wa Aya za Kuruani. Nina imani kubwa kwamba Kuruani ni Ulimwengu tunaousoma na Ulimwengu ni Kuruani tunayoiona. Kwa hiyo twende mbele na tuanze kazi ambayo siyo ndogo lakini nzuri sana.

Katika Kuruani Sura Ya Al-Bayyina Namba 98 Aya Namba  2 na 3  Insema 

رَسُولٌ۬ مِّنَ ٱللَّهِ يَتۡلُواْ صُحُفً۬ا مُّطَهَّرَةً۬ (٢) فِيہَا كُتُبٌ۬ قَيِّمَةٌ۬ (٣)

2. Mtume kutoka kwa Mwenyeezi Mungu anayewasomea kurasa zilizotakwaswa.

3. Ndani yake humo kuna Vitabu  Madhubuti (Vya Hali Ya Juu)

SHEREHE

Mwenyeezi Mungu anasema kwamba kuruani imekusanya Kurasa zilizotakaswa yaani zimetoharishwa. Hakuna Upuuzi ndani yake. Na kisha anaendelea kutuambia kwamba Katika Kuruani utakuta Vitabu Madhubuti au Vitabu Vya Hali ya Juu, Au Sheria Madhubuti yaani Za Hali ya Juu. Neno linalokaribia zaidi ni Vitabu  kutokana na neno  Kutubun na siyo Sheria peke yake kama wanavyosema baadhi ya Wafasiri wa Kuruani Tukufu.

Suali ni   “Vitabu Gani ambavyo vimekusanywa katika  Kurasa za Kuruani Tukufu?”

Ukifanya Uchunguzi utaona ni  kila Mafundisho  waliyokuja nayo Manabii na Mitume wote waliopita.  Mafundisho hayo au Ujumbe huo umekusanywa kwa njia ya Ufupisho na kwa  hali ya Kimuujiza kwani imekusanya ujumbe wa Mitume wote tuliyoambiwa katika Hadithi za Mtume Jumla yao ni 124000  Ujumbe huo umekusanywa katika Kitabu  hiki cha kuruani. Ukichunguza zaidi utakuta Kuna mafundisho au Vitabu mbalimbali vya nyanja mbalimbali za Elimu  kama vile  Kitabu cha FIqh, Kitabu cha Ndoa au Mafundisho ya Ndoa, Kuna kitabu Cha Hija, Kuna Kitabu Cha Tohara, Kuna kitabu cha Namna Ya Kufanya Biashara, Kuna kitabu cha Sala, Kuna Kitabu cha Zaka, Kuna kitabu cha  Imani, Kuna kitabu cha Zakati, Kuna kitabu cha Elimu za Dunia yaani Kumetajwa kimuujiza Aya  zinazozungumzia Elimu mbalimbali  za Dunia na Vitabu Vinginevyo ambavyo  tunavovijua na vile ambavyo hatuvijui na ambavyo  vitahusu mambo ya baadaye.

KURUANI IMEKUSANYA ELIMU TUKUFU NA ZA HALI YA JUU

Kuruani  Siyo kitabu cha Sayansi lakini  ni Maneno ya Mwenyezi Mungu na maneno  haya ni Tohara yaani Safi. Maneno haya ni mkusanyiko wa Vitabu vyenye Elimu za hali ya Juu sana.

Ukifanya utafiti  utakuta Kuruani imekusanya Aya ambazo zinaashiria  MIlango  yote Mitatu Ya Sayansi za hali ya Juu. kuna Natural Sciences, Social Sciences  na Formal Sciences. Kuruani Imekusanya Elimu za Sayansi za hali ya Juu. Ukisoma Kuruani kwa fahamu nzuri utaona ikekusanya Elimu za Ulimwengu wote na hakuna kilichobakia lakini kwa njia ya ufupisho na hekima ya hali ya juu. Hakuna Binaadamu anayeweza kufanya hivi. Kitabu cha Kuruani ni Muujiza mkubwa sana.

Inaendelea katika Mpango  wa pili   

UNIVERSITY/KURUANI-2