SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

University/Kuruani-2

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

PHILOSOPHY AU FALSAFA فلسفة

Alhamdulilah  leo Tarehe  27/09/2022 na  Mwenyeezi Mungu akipenda nitaendelea  na safari ndefu ya kuelezea Baadhi ya Masomo  tuliyoyataja katika Mlango  ulipita  University/Kuruani-1. Tutaanza na Somo la Msingi wa Elimu za Sayansi Duniani.  Somo hili  ni Philosophy. Lengo ni kuielezea Elimu hii kwa kifupi na Kisha Tuangalie Uhusiano  wake na Kuruani  Tukufu.

Kwanza kabisa ningependelea kusema kwamba Jina Philosophy lisikutishe. Kwa kweli Misamiati  hutisha na utafikiri ni Elimu kubwa sana na ambayo  inawahusu watu wa Vyuo vikuu tu peke yao. Hata Kidogo. Tusibabaike. Ni Elimu  kama Elimu nyinginezo na kila mtu anahaki ya kusoma. Elimu sizizoeleweka siyo Elimu nzuri. Elimu nzuri ni ile yenye kueleweka na yenye faida katika Maisha. Huu ni mwono  wangu.

Katika Mlango huu mdogo  nitajitahidi kufupisha Na kwa njia ya Kueleweka ili tunayosoma yatufaidikie.

Ukisoma Historia ya Elimu hii utakuta  ilianzia Miaka Mingi iliyopita katika Nchi mbalimbali za Dunia kama vile Egypt karibu miaka 4000 kabla ya Enzi za Ukristo (BCE au Before Christian Era).Na katika Enzi  hiyo hiyo kuna Nchi nyinginezo kama vile  Mesopotamia (Iraq) Mwaka 2150 B.C.E.  India  1500-500 B.C.E. Persia  1500 B.C.E. China c. 1046-256 B.C.E. Greece c. 585-322 B.C.E. Rome c. 155 BCE.

Kihistoria Sayansi na Jina pia Limebadilika. Hapo  Zamani  Lilileta maana Nyingine na Huko  Ugiriki Elimu hii iliitwa Jina la “PHILOSOPHY” Na Jina hili  asili yake ni Kigiriki.  Philo ina maana ya  “Kupenda” na  “Sophia” maana yake ni  “”Busara”  Na Ukiunga Philo na Sophia Maana inakuwa  “Love of Wisdom”  yaani  “Kupenda Ubusara” Hii Ndiyo Asili ya Maana ya neno hili. 

The word philosophy comes from the Greek philo (love) and sophia (wisdom) and so is literally defined as “the love of wisdom”

Elimu hii ilizuka hapo zamani ili kujibu masuala  magumu. Na mpaka hivi sasa   Elimu hii  inatumika na inafundishwa mashuleni. Tatizo ni kwamba Watu bado wanahangaika kutafuta Majibu ya Masuali kama vile Dunia Imezuka Vipi. Akili ni kitu gani? Fikra ni Nini? Mungu ni Nani? Mungu alizuka Vipi? Je Ulimwengu Ulizuka Vipi?  Na Masuali Mbalimbali Mengineyo. Haya ndiyo Masuali ya Falsafa. Binaadamu anataka kujua Baada ya Kufariki tunakwenda wapi? Je Mwenyeezi Mungu alizuka Vipi? 

Elimu Hii siyo mbaya kwani ina mazuri yake pia. Elimu hii ndiyo imealisha Sayansi. Kwani  Enzi hizo kulikuwa Hakuna Sayansi kama leo. Kulikuwa Philosophy au Falsafa na baadaye Ikazaliwa  Natural Philosophy yaani Kabla Ya Sayansi. 

Inategemea namna Tunavyoitumia. Ukitumia Elimu yeyote kwa njia nzuri utapata faida na ukitumia Elimu yeyote kwa nia mbaya utapata Hasara.

Ajabu ni kwamba Majawabu ya Masuala haya yalikwisha Kujibiwa Na Mwenyeezi Mungu katika Ujumbe wa Manabii wote kuanzia  Kiumbe wa kwanza Kuumbwa yaani Nabii Adam.  Uislamu  haukuanzia Na Mtume Mohamad bali Tangu  Kuumbwa Dunia. Mwenyeezi Mungu  alituma Manabii  124000 na hawa walitumwa katika Nyakati mbalimbali na Kila mmoja alikuja Na Mfundisho. 

Kwa kawaida Binaadamu ana Masuali mengi sana. Majibu yapo lakini watajitahidi kutafuta kwingineko. Na ndiyo maana Elimu hii ya Philosophy ilizuka. 

Alhamdulilah  Neema Kubwa Ya Uislamu na Pia Dini ya Mbinguni ambazo Mwenyeezi Mungu ametuma Manabii kutoka Kuumba Dunia. Dini  hizi za Mbinguni zilikuja Kujibu Masuala haya Magumu yasiyoweza kujibika kwa kutumia Akili.

Katika Kuruani Kuna Philosophy ya Hali ya Juu ambayo  tutaizungumza baadaye na Ndiyo maana nikasema Elimu hii siyo mbaya iwapo utaitumia vizuri.

Sasa  ni nini Tofauti baina ya Sayansi na Philosophy?

Jawabu rahisi ni kwamba Katika Utafiti  Sayansi Inahitaji Kuona na Majaribio (Experiment)  Lakini  Philosophy inahitaji Utrafiti kwa Kutumia Fikra au Ubongo  peke yake (Reasoning).  Kwa hiyo  Philosopher anafanya utafiti kwa kufikiri  na Mwana Sayansi  anafanya Utafiti kwa Kutumia  Vifaa mbalimbali vya utafiti yaani  Kwa Kuona. Na Hii inajulikana Kama  Empirical Data.

Philosopher  waliojulikana duniani kupitia katika Karne Mbalimbali ni wengi  duniani. Ningepedelea kuwataja wachache nao ni:

Greece:Aristotle/Epicurus/Heraclitus/Plato/Pythagoras Socrates. Na Wengineo

Asian/Eastern philosophers:Avicenna/Confucius/ Gautama (the Gautama Buddha)/Omar Khayyám. Na Wengineo ambao Sikuwataja.

Later European/western philosophers: Sikuwataja kwani Wengi

Modern European and American philosophers:

Sikuwataja kwani Wengi

MAANA YA PHILOSOPHY  فلسفة KATIKA KIWANGO CHA  KITAALUMA (ACADEMIC LEVEL)NA MGAWANYIKO WA MASOMO YAKE

Kufuatana Na Masuala mbalimbali Philosophy inafanya Utafiti katika Nyanja Zifuatazo:

1/Metaphysics

Uwanja huu umeganyika katika Nyanja Zingine  Tatu:

1/Ontology. Uwanja huu  unauliza maswali kama vile “Dunia ni Kitu Gani?”  au “Uhakika Ni Kitu Gani?” na Masuala Mengineyo Mbalimbali

2/Falsafa ya Fikra (Mind)

Masuala yanyohusu  Fikra  Na Masuala Mengineyo Mbalimbali

3/Falsafa Ya Dini.

Masuala Ya Kidini  na Masuala Mengineyo Mbalimbali

2/Epistemology

 Uwanja Huu unahusu masuala kama vile. “Elimu ni kitu gani?”  au  “Sayansi Ni  Kitu Gani?” au “Ukweli ni nini? Na Masuala Mengineyo Mbalimbali 

3/Ethics

Uwanja Huu unahusu masuala kama vile  ” Ni nini Zuri Na Baya”  au  “Haki Ni Nini”  au  “Kosa na Sahihi ni Nini?” Na Masuala Mengineyo Mbalimbali.

4/Aesthetics

Uwanja Huu unahusu masuala kama vile.  “Ni nini Uzuri?” “Je vitu Vizuri vinapendeza?” au ” Je vitu vya Ukweli Vizuri?”  Na Masuala Mengineyo Mbalimbali.

5/Logic

Uwanja Huu unahusu masuala kama vile.”Maneno Tunayotumia Yana Maana Gani?”  au “Je mawazo  yanaweza Kuwakilishwa na Lugha?”  au Je kwa vipi tunaweza  Kufikiri  kwa usahihi”? Na Masuala Mengineyo Mbalimbali.

6/Axiology

Uwanja Huu unahusu masuala kama vile. “Je wakati ni Pesa au ni sisi tuliyofanya iwe hivyo?”  au “Kitu gani Kina Thamani? Na Masuala Mengineyo Mbalimbali.

PHILOSOPHY NA KURUANI TUKUFU

Naona Wakati umefika wa Kuanza Kuielezea Kuruani. Nadhani Maelezo  hapa Juu yanatosha  kutoa Mwanga wa Elimu ya Philosophy kwa ufupi. 

Tumeona Milango mbalimbali Ya Utafiti  wa Elimu ya Philosophy na Kwa hiyo  Sasa  tutachagua Mlango mmoja tu ambao ndiyo tutautumia Katika Utafiti  Wa Kuruani.  Kwa kweli Kuruani ndiyo itatufundisha Falsafa na siyo Kinyume. Kuruani siyo  Kitabu cha Sayansi  bali Ni Muujiza ambao umegusia kila kitu  Ulimwenguni kwa hiyo  siyo mbaya Kuisoma kwani Mwenyeezi Mungu amehimiza Tufanye Hivyo. Amesema mara kwa mara Katika Kuruani Tufikiri Aya Zake ili tuone ukubwa na Utukufu wake.

Uwanja Nitakaotumia ni  Elimu Ya LOGIC  na Itabidi pia Tuisome Elimu hii kabla ya Kuruani Tukufu. Tuisome Kwani Ni Elimu kubwa Sana. Kila Uwanja hapa Juu ni Mkubwa kwani kuna Nyenzo  mbalimblai zinazotumiwa na Nyanja Hizi kufuatana na Mazingara yake.

LOGIC المنطق

Kwa kifupi  Elimu  ya Logic ni mojawapo ya Nyanja za Falsafa au Philosophy.

Logic Ni Sayansi ambayo inashughulika na Kutathmini (Evaluate) Hoja (Argument).  au Kwa Lugha ya Kiingereza  tutasema:

Logic is the Science used to evaluate an Argument

Ni Elimu ambayo  itakulinda wewe katika Kujiepusha na Fikra Mbaya, au Uwongo.

Hoja au Argument  ni Maneno ambayo Yanatumika katika Kuthibitisha  Fikra.

Hoja Zimegawanyika katika Sehemu Mbili:

1/Ushahidi  wa Kuthibitisha  Fikra zako (Premises)

2/Na Hitimisho au Jawabu la Ushahidi. (Conclusion)

Kuna  Viashirio (Indicators) vya Kimaneno katika  Ushahidi  na Pia Hitimisho.

Wakati Mwingine Hakuna Viashirio. Na Ikiwa Hakuna Basi Itabidi  Uchunguze Hja Hiyo kwa kufikiri.

Viashirio Vinasaidia Kuelewa Aina Ya hoja Iwapo ni  Deductive au Inductive.  Kwa kiswahili Viashirio husaidia katika kuelewa aina Ya Hoja iwapo ina uhakika (Deductive) au Hakuna Uhakika(Inductive).

Maneno Yanayotumika katika  aina Ya hoja  Deductive au Hoja Inayokubalika kiakili ni kama vile:  

“Kwa hakika” na Maneno mengineyo ya aina hii.

Maneno Yanayotumika katika aina Ya hoja Inductive  au Hoja Isiyo na Uhakika  ni kama vile:

“Labda”  au “Huenda”

Na  Iwapo  Indicators au Viashirio  havipo  basi unaweza kuelewa kwa kuchunguza maana ya Hoja hiyo. Ufikiri vizuri hoja mwelekeo au Mfumo  wa hoja hiyo,

Nadhani Tumepata Picha Ya somo la LOGIC

Sasa Tuanze Kuisoma kuruani Na Tuchunguze Elimu hii ya Philosophy na Uwanja huu wa Logic ili tupate Kuelewa Elimu hii kwa uzuri zaidi. Inshaallah hata kama Hapa Juu haikueleweka Nina Uhakika Kuruani itatupa Mwanga Vizuri Zaidi kwani Unapotatanika Katika Jambo Lolote utapata Jawabu katika Kuruani. Kuruani ni  Mwalimu Mkubwa Kuliko  wote. 

PHILOSOPHY-LOGIC (علم المنطق) (YA KURUANI TUKUFU

Logic Kwa Kiswahili safi ni  “BUSARA”  au “HEKIMA” kwa kiingereza “WISDOM”  au “LOGIC”

Sasa  hebu tuchunguze Aya za Kuruani  Zifuatazo tuangalie Busara aliyotumia Nabii Ibrahim katika Mazungmzo yake Na Mjomba wake  “Azar”  Katika Aya Hizi tutaona Nabii Ibrahim anatumia LOGIC au “Wisdom”  katika Klingania Dini ya Mungu mmoja. Hebu Tuzichunguze kisha Tufanye  Uchambuzi  wa Ki  Logic.

Sura Namba 6  Aya Namba 75 Mpaka 80   Sura Ya Al-Anaam

سُوۡرَةُ الاٴنعَام

وَكَذَٲلِكَ نُرِىٓ إِبۡرَٲهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ (٧٥) فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبً۬ا‌ۖ قَالَ هَـٰذَا رَبِّى‌ۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأَفِلِينَ (٧٦) فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغً۬ا قَالَ هَـٰذَا رَبِّى‌ۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَٮِٕن لَّمۡ يَہۡدِنِى رَبِّى لَأَڪُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ (٧٧) فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةً۬ قَالَ هَـٰذَا رَبِّى هَـٰذَآ أَڪۡبَرُ‌ۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَـٰقَوۡمِ إِنِّى بَرِىٓءٌ۬ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ (٧٨) إِنِّى وَجَّهۡتُ وَجۡهِىَ لِلَّذِى فَطَرَ ٱلسَّمَـٰوَٲتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفً۬ا‌ۖ وَمَآ أَنَا۟ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ (٧٩) وَحَآجَّهُ ۥ قَوۡمُهُ ۥ‌ۚ قَالَ أَتُحَـٰٓجُّوٓنِّى فِى ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَٮٰنِ‌ۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦۤ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّى شَيۡـًٔ۬ا‌ۗ وَسِعَ رَبِّى ڪُلَّ شَىۡءٍ عِلۡمًا‌ۗ أَفَلَا تَتَذَڪَّرُونَ (٨٠)

TAFSIRI

75. Na namna hivi tulimwonyesha lbrahimu ufalme wa mbingu na ardhi (kuwa ni wa Mungu), na ili awe miongoni mwa wenye yakini.

76. Na usiku ulipomwingilia (lbrahimu na hali kakaa na makafiri), akaona nyota, alinena (makusudi kutaka kuwavuta watumie fikira zao): “(Nyota) hii ni Mola wangu.” Ilipotua (ikapotea), alisema (kuwaambia wale makafiri kama kwamba yu pamoja nao katika ibada ile): “Sipendi wale wanaopotea (hawawepo ila wakati makhsusi tu).”

77. Na (usiku wa pili) alipouona mwezi unachomoza alisema (kuwaambia wale maraftki zake wa kikafiri): “Huu (mwezi) ndio Mola wangu.” Ulipotua alisema: “Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu (wapotevu). (Na mola huyu hawezi kuniongoza kwani anakuwa hayupo wakati mwengine).”

78. Na (siku ya tatu) alipoliona jua linachomoza alisema (kuwaambia): “Hili (jua) ndilo Mola wangu. Huyu Mola mkubwa kabisa.” Lilipotua alisema: “Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha (na Mungu).,

79. “Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu) si miongoni mwa washirikina.”

8o. Na watu wake wakajadiliana naye (kwa kumwambia Unaacha ibada ya wazee! Utadhurika)! Akasema: “Je, Mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu, na hali yeye ameniongoa? Wala siogopi wale mnaowashirikisha naye. Isipokuwa Mola wangu akipenda jambo (kuwa, basi litakuwa). Mola wangu anakijua vyema kila kitu. Basi je, hamshiki mauidha (Hamzindukani)?”

SHEREHE

Mwenyeezi Mungu alimpa Nabii Ibrahim  Elimu ya Mantiq au Logic au Philosophy  ya hali ya Juu. Aliruzukiwa Imani Kubwa sana. Katika Tafsiri Hapa Juu angalia  Namna alivyokuwa akihojiana na Makafiri.  Hii ndiyo Philosophy na Logic tuliyoizungumza hapa juu.

Ametoa Hoja  Tatu  katika Siku Tatu.  Kila Siku anawapa Hoja Moja  bila ya Haraka. Kidogo kidogo. Kawapa Ushahidi  kwa Hekima na Busara. Hatua kwa Hatua.

Siku ya kwanza akawapa Hoja au Ushahidi wa kwanza ili kuthibitisha Imani yake aliyoificha mbele ya wale Makafiri kwamba Mwenyeezi Mungu ni Mkubwa na yeye ndiye aliyeumba kila kitu.  Akawaonyesha  Nyota na akawaambia Makafiri  waliokuwa naye kwamba huyu ndiyo Mungu Wake. Na Nyota hiyo ilipotua akawaambia kwamba Yeye hapendi Miungu inayopotea. (Kwani Kupotea kwao kunaonyesha udhaifu na kwamba Imeumbwa na haina faida wakati huo inapopotea)

Siku ya Pili akawapa Hoja au Ushahidi wa Pili  ili kuthibitisha Imani yake aliyoificha mbele ya wale Makafiri kwamba Mwenyeezi Mungu ni Mkubwa na yeye ndiye aliyeumba kila kitu. Akawaonyesha  Mwezi  ulipochomoza akasema tena maneno yale yale kama alivyosema siku ya Kwanza  Kwamba Huyu ndiye Mungu  wake. Na mwezi Ulipotua akasema Ulipotua alisema: “Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu (wapotevu). (Na mola huyu hawezi kuniongoza kwani anakuwa hayupo wakati mwengine).”

Na Siku ya Jua  akawapa Hoja au Ushahidi wa Tatu ili kuthibitisha Imani yake aliyoificha mbele ya wale Makafiri kwamba Mwenyeezi Mungu ni Mkubwa na yeye ndiye aliyeumba kila kitu. Akawaonyesha Jua  Lilipochomoza akasema tena maneno yale yale kama alivyosema siku ya Kwanza Kwamba Huyu ndiye Mungu wake. : “Hili (jua) ndilo Mola wangu. Huyu Mola mkubwa kabisa.” Lilipotua alisema: “Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo Mnayoyashirikisha na Mwenyeezi Mungu.

Na hapo akaendelea kufichua ukweli bila khofu yeyote na kuwaambia  “Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu) si miongoni mwa washirikina.” Na watu wake wakajadiliana naye (kwa kumwambia Unaacha ibada ya wazee! Utadhurika)! Akasema: “Je, Mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu, na hali yeye ameniongoa? Wala siogopi wale mnaowashirikisha naye. Isipokuwa Mola wangu akipenda jambo (kuwa, basi litakuwa). Mola wangu anakijua vyema kila kitu. Basi je, hamshiki mauidha (Hamzindukani)?”

Hii ndiyo  Logic ya Mazungumzo. 

Kwa hiyo  tukitumia Elimu ya  Logic  katika kuchambua  Aya hii utaona  kama ifuatavyo:

1/Siku ya Kwanza (Argument aju Hoja inayojulikana kama  Premises  au Ushahidi wa Kwanza)

2/Siku ya Pili ((Argument au Hoja inayojulikana kama Premises au Ushahidi wa Pili)

3/Siku ya Tatu((Argument au Hoja inayojulikana kama Premises au Ushahidi wa Tatu).

Aya namba  79  ndiyo  inajulikana katika  Elimu ya Logic kama  Conclusion. Kwani ndilo Linalohitaji  Ushahidi. Ushahidi  mara 3 ili kuthibitisha yaliyopo katika Aya namba 79 ambayo inasema:

“Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu) si miongoni mwa washirikina.”

Na ukichunguza Aya hapa juu utaona ni  Deductive kwani Ushahidi  wote ulitolewa Unakubalika bila Shaka Yeyote. Kwani Hakuna Badili. Nyota, Mwezi na Jua  zote ni Viumbe ambavyo havipo Milele bali  huja na kupotea na Siku ya kiyama vitapotea kabisa na hata Sayansi inasema hivyo na siyo Kuruani peke yake. Na  Conclusion pia ni  Sahihi  bila Shaka Yeyote. Kwa hiyo  Ninavyoona mimi huu ni  Mfano Mmojawapo Mzuri sana wa Logic katika Kuruani Tukufu.Kuruani  inatufundisha Elimu ya Logic  katika Madakika Machache na kwa lugha  Rahisi kueleweka. Na Mwenyeezi Mungu anajua zaidi iwapo nimesibu au nimefanya makosa. Ni Utafiti ambao Lengo  ni kupata  Thawabu. Alhamdulilah.

Bado Sijamaliza Kuelezea  Elimu ya Philosophy katika Kuruani kwani kuna Mifano mbalimbali. Kwa leo naishia  hapa. Nia Yangu ni kuendelea baadaye Mwenyeezi Mungu  Akitupa Uhai. Kwa hiyo  tutakutana Tena Hivi karibuni  Inshaallah……………..