SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Usul Al-Tafsir

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

HISTORIA FUPI YA TAFSIRI YA KURUANI

DIBAJI

Haiwezekani kuelezea historia ya Tafsiri ya kuruani katika sehemu ndogo ya website kama hii. lakini kwa uwezo wake Mwenyeezi Mungu nitajitahidi kuelezea Muhtasari wa Asili  Ya Tafsiri kwa ufupi sana. Na Kwa hiyo siwezi kumaliza kwa siku moja bali masiku mengi na itakuwa kidogo kidogo Mungu akipenda.

UTANGULIZI

Mungu akipenda nitazungumzia katika Mlango huu Historia Fupi ya Kuruani Kuanzia Kushuka kwake, Kuhifadhiwa kwa Kuruani kwanza katika Nyoyo za Mtume Mohamed (Sala Na Amani Yake Mola Imfikie) na Kisha Maswahaba Zake.

Kukusanywa kwa Kuruani katika Kitabu Kimoja Baada Ya Kiongozi  (Amir) Abu Bakar kukubali nasiha liyopewa na Omar Ibn Al-khatab aliyekuwa Kiongozi (Amir) wa Pili baada ya Abu Bakar.

Kuchaguliwa kwa Lahaja (Dialect) Moja ya  kuruani (Dialect) na kuondolewa nyinginevyo (yaani LAHAJA za makabila mengineyo ya wakati huo na LAHAJA ni  Lugha zenye Asili moja lakini kuna tofauti ndogo ndogo za kilugha mfano wa Kiswahili cha Pemba, Zanzibar, Mombasa, Kingazija na nyinginezo)   chini ya Uongozi wa  Othman Ibn Affan.

Nitagusia kuhusu Mazingara  au  ASBAAB AL-NNUZZUL ya  Kushushwa kwa Aya Za Kuruani.

Nitagusia Tafsiri za Makundi Ya Wapotevu  ili tujiepushe nayo.

Nyenzo mbali mbali zilizotumiwa katika Tafsiri.

Maana Ya Misamiati Mbali Mbali ya Elimu Ya Tafsiri.

Masharti au Sifa ambazo  Wafasiri wa Kuruani wanawajibika kuwa  Nayo.

Aina Ya Tafsiri za Kuruani  na Majina Ya Waandishi.

Kwa kifupi haya ndiyo mambo ningependelea kuyazungumzia kwa Ufupi katika Mlango huu na Nia Yangu ni kufupisha na Kwa Njia iliyo Rahisi  Ili tupate Mwanga ambao utatulinda na Njama mbalimbali zenye kunasibisha uongo katika Dini ya Kiislamu.

Kwa mfano Makafiri na Maadui wa Kiislamu wanadai kwamba Versions za Kuruani ni zaidi ya Moja ambazo madhumuni yake yanapingana na hizi zinaonyesha kwamba ni Maandishi Ya Kibinaadamu na siyo Mwenyeezi Mungu na Versions zote hizi zilichomwa Moto katika Enzi ya Othman Ibn Affan na kubakizwa moja tu ambayo tuliyonayo leo hii na ambayo wanafananisha na vitabu vya dini nyinginezo ambavyo vimeguswa kwa kubadilishwa, kuzidishwa na kupunguzwa.

Huu Ni Uongo mkubwa sana kwani  ukweli ni kwamba Kuruani ilishushwa kwa muda wa miaka 23 ya Uhai wa maisha ya Mtume (Sala na Amani Yake Mwenyeezi Mungu Imfikie) lakini katika Dialect au LAHAJA  saba za Makabila yaliyoishi wakati huo.

Kwa hiyo kuruani ni Moja tu kuanzia kushushwa mpaka leo.

Na LAHAJA nyinginezo ziliondolewa kwa sababu mbalimbali na siyo  Versions kwani Version ni Moja tu kuanzia mwanzo wa WAHYI lakini  Maadui wa Kiislamu wanatafuta kila njia ili kutia  Doa katika dini ya  kiislamu. Watu wengi wasiojua wanachanganya kati ya Versions and Dialect.

Inshaallah Nitazungumzia yote haya katika Mlango huu ili Historia hii ieleweke.

Huu ni Utangulizi kwa hiyo nitaongeza na kubadili lakini kwa sasa upate mwanga  yatakayokuja baadaye kwa ufupi. 

IPO KATIKA MAANDALIZI. INSHAALLAH MUNGU AKIPENDA NITAENDELEA HIVI KARIBUNI