SCIENTIFIC AND ISLAMIC RESEARCHES

Vita Vikuu/Profesa-3

UTAFITI MBALIMBALI  KATIKA DINI NA SAYANSI

IMEANDALIWA NA  AL-AMIN ALI HAMAD

VITA VIKUU VYA DUNIA, MAAJABU YA NAMBA NA MAAJABU YA KURUANI

Alhamdulilah leo  Tarehe  18/09/2022. Namshukuru Mwenyeezi Mungu  kutupa uzima na Afya. Ni Jumapili Jioni na Hali  ya hewa ni Shwari. Wakati mzuri kuelezea Maajabu ya Namba  zinazohusika na Vita Vya Dunia. Sikupendelea Kuandika Habari hii kwani hakuna anayependa Vita. Na pia sipendelei  Kufuatilia Lugha ya Namba katika Utafiti huu kwani Inababaisha na Jambo la Kuruani Tukufu ni Hatari sana kwani wakati mwingine Namba  huweza kutupa Habari isiyo ya kweli. Kuruni Ni Muujiza Mkubwa sana na Maandishi yake ni Muujiza mkubwa ambao hauna mwisho na pia Unababaisha ukifuatilia kwa njia isiyofaa. Kuruani siyo kitabu cha kupigia Bao  au Kitabu cha Sayansi na kwa hiyo  Tusiifanye kama ni Elimu tu ya maisha kama Elimu nyinginezo lakini Lazima tuelewe kwamba Kuruani ni Maneno makubwa Ya Mwenyeezi Mungu ambayo lengo ni Kutuongoza. Ni Kitabu cha Mafundisho katika Maisha yetu. Ni Muongozo  wa maisha yetu na majini pia. Tuisome Kuruani kwa Kuifahamu na Kuifuata. Tunaposoma Miujiza iwe tu kwa lengo la kutuzidishia Imani lakini sio lingine. Tusiitumie kwa njia nyingine isiyofaa kama vile kazi za Munajim za Bao hiyo ni Haramu na Pia Kuyatumia Maneno ya Kuruani katika Upuuzi Mwingine.

Siku ya Leo Nitawazungumzia utafiti wa Profesa Kutoka Nchi Ya Iraq  .Nilikutana Naye hivi Karibuni na Tulizungumza Habari  za Kushangaza sana. Mazungumzo yalikuwa kwa Lugha ya Kiingereza na Kiarabu. Nimefasiri kwa Kiswahili. Kuna Nyongeza na Pungufu katika Maandishi haya lakini Muhimu uelewe Madhumuni ya Mazungumzo yetu.

PROFESA:Tarehe za Vita Vikuu vya dunia zinashangaza sana tena sana na inatisha sana. Ngojea Nikuelezee Utafiti  wa Tarehe  hizi kisha tufikiri maajabu mengine yanayotokana na Namba hizi. Lakini uelewe tu Muujiza wa Kuruani na usichukulie kama utafiti huu ni sawa na Kupiga Bao au Ramli kwani Ni Haramu

AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Asante sana. Ni habari ya kutisha sana lakini ningependelea kuijua.

PROFESA: Nisikilize  Vizuri.

Vita Vya Kwanza Duniani  Vilifanyika Tarehe

28/7/1914

Unaweza kuhakikisha Tarehe Hii katika Chombo cha  utafiti “Google”  ili uamini. Na Tarehe hii ni ya kweli.

Vita Vya Pili Duniani  Vilifanyika Tarehe

01/09/1939

Unaweza kuhakikisha Tarehe Hii katika Chombo cha utafiti “Google” ili uamini. Na Tarehe hii ni ya kweli.

Na Vita Vya Mwaka Huu Yaani Russia na Ukraine Vilianza Tarehe 

24/02/2022

Unaweza kuhakikisha Tarehe Hii katika Chombo cha utafiti “Google” ili uamini. Na Tarehe hii ni ya kweli.

AL-AMIN ALI HAMAD:Nakusikiliza Vizuri. Endelea Profesa.

PROFESA: Sasa  Tuone  hapa Chini Maajabu Yafuatayo:

Ngoja Nipange Tarehe hizi kisha Tujumlishe;

28/7/1914=  WWI  (First World War)

01/09/1939=WW2  (Second World War)

24/02/2022=Russia +Kuivamia Ukraine

Hebu Angalia  Maajabu:

Tujumlishe Namba Hizi kisha Tuone Maajabu:

28 + 7 + 19 + 14=68

01 + 09 + 19 + 39=68

24 + 02 + 20 + 22=68

AL-AMIN ALI HAMAD:Profesa  Haya Maajabu Sana. umejumlisha Namba za Vita Ya Kwanza kisha Ya Pili na Vita Hivi vya karibuni na Jawabu ya Tarehe hizi zote Tatu ni sawa yaani 68. Kwa vipi  mbona Inashangaza. Yaani Je Hivi vita vya Russia na Ukraine ni Vita Vya Tatu?  Je tupo mwanzoni mwa Vita Vya Tatu? Mbona Unanitisha?

PROFESA: Nilikuambia Kwamba Usiamini Namba kwani huenda siyo kweli kwani  zinababaisha lakini mimi mwenyewe sijui huenda ni vita vya tatu. Kwa kweli sina uhakika kwani sifanyi kazi ya Bao au Mzimwi. Tusome tu na iishie hapa. Usiogope kwani kuogopa kunatokana  na Mashetani.  Hizi ni Hesabu tu.

AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Profesa kwa kunitia Moyo.Unasema Kweli kwani anayejua Ni Mwenyeezi Mungu tu na Tusiingilie kazi zake. Hatujui ya baadaye.

PROFESA: Jambo  la kushangaza ni kwamba ukitoa Miaka Hii kutoka katika Jumla ya idadi ya Aya za Kuruani tunapata Maajabu Mengineyo.

AL-AMIN ALI HAMAD:Hebu nionyeshe Profesa hesabu hiyo.

PROFESA:Ngoja nipange zile tarehe hapa chini kisha nikuonyeshe maajabu mengine:

28/7/1914= WWI (First World War)

01/09/1939=WW2 (Second World War)

24/02/2022=Russia +Kuivamia Ukraine

Jumla ya Aya za Kuruani  ni  6236 sasa tutoe Miaka tuliyotaja hapo juu tuone maajabu mengineyo:

6236-1914=4322

na  4322-1939=2383

na 2383-2022=361

Na namba hii 361  ni sawa na  19 x19

Je unaona Namba 19 ni namba ambayo imetajika katika kuruani kama ni Mojawapo ya Muujiza Mkubwa na Pia  Ukigeuza Jina La Msikiti  mkubwa wa Kiislamu Huko Palestina  yaani  المسجد الاقصا  au  Masjid  Al-Aqsa

katika Thamani  ya Herufi za Kiarabu zilizitumika Hapo  zamani wakati namba zilikuwa bado  kujulikana. Waarabu na Mataifa Mengineyo  walitumia Herufi Kuwakilisha Namba.  Na Kwa hiyo  Ukitafuta Thamani Ya المسجد الاقصا  utapata  361  pia.

AL-AMIN ALI HAMAD: Kuna uhusiano gani kati ya Msikiti huu na jawabu la Miaka 361 tuliyopata hapa juu ya Vita Kuu za Dunia?

PROFESA: Labda ina maana kwamba huenda Palestina watapata  Uhuru  karibuni  au labda Msikiti usiwe tena chini ya Hukumu ya WaIsraeli. Kwa kweli sipendelei kuingilia mambo ya Baadaye  lakini namba hizi zinaonyesha maajabu  sana. Je huoni Namba zinavyotatanisha?  Je huoni Maajabu siyo madogo?

AL-AMIN ALI HAMAD:Naona bora tumuachie Mwenyeezi Mungu na tusiingilie kazi  zake. Kwa kweli inashangaza sana.

PROFESA:Maajabu hayajakwisha kwani bado sijamaliza:

Hebu tufanye hesabu nyingine tuone maajabu yasiyo na mwisho:

28/7/1914= WWI (First World War)

01/09/1939=WW2 (Second World War)

24/02/2022=Russia +Kuivamia Ukraine

Sasa tujumlishe Namba hizi moja moja tuone jawabu na tulinganishe.

Vita Vya Kwanza:

2 + 8 + 7 + 1 + 9 + 1 + 4=32

Vita Vya Pili:

1 + 9 + 1 + 9 + 3 + 9=32

Vita Vya Russia Na Ukraine

2 + 4 + 2 + 2 + 0 + 22=32

Jawabu ni  32  na  linafanana.  Je unaona ya maajabu  namba hizi tatu  zinawiana. Kwa nini  Zinafanana  kiajabu hivi?  kuna siri gani? Hakuna ajuae isipokuwa Mwenyeezi Mungu  peke yake. Tusichokonoe chokonoe  siri za Muumbaji. Tusicheze cheze kwa ujinga kwani  ni hatari  kubwa. Tunapofika Mwisho  wa Elimu au Ujuzi basi Tuseme.  Allahu Akbar. Na Tuombe  Mwenyeezi Mungu Tuepushie Balaa la Vita Lakini Usiendelee  kuchokonoa chokonoa kwani hatukupewa Elimu ya Ghaibu. Tumche Mwenyeezi Mungu na Tumuogope  sana. Vita siyo mchezo na harari  sana. Vita Huleta Njaa na Maafa Makubwa sana tena sana. Allahu Akbar.

AL-AMIN ALI HAMAD:Profesa  Mbona  tarehe ya Vita Vya Russia Na Ukraine hukujumlisha namba  22  moja moja kama vile  

2 + 4 + 2 + 2 + 0 + 2 + 2=14

lakini wewe umeziacha namba hii 22 kama mwanzo  wa hesabu yetu yaani  hivi:

2 + 4 + 2 + 2 + 0 + 22=32

PROFESA: Ili tupate namba 32 imekuwa sina budi  bali kuiacha namba 22 hivyo hivyo kwani ningeliijumlisha moja moja kama vile 2 + 2  basi hesabu ya 32 tusingeipata.  Kwa kweli  inashangaza. Nimeiacha hivyo  hivyo.

lakini  tujaribu hesabu nyingine  kama  unataka namba za mwisho  ziwe mbili mbili na tukifanya hivyo tutapata Muujiza Mwingine wa Kushangaza sana.

Hebu tuone hapa chini:

Vita Vya Kwanza: 28 + 7 + 1 + 9 + 1 + 4=50

Vita Vya Pili:  01 + 9 + 1 + 9 + 3 + 9=32

Vita Vya Russia Na Ukraine

24 + 2 + 2 + 0 + 2 + 2=32

AL-AMIN ALI HAMAD:Sasa  mbona  Namba ya Vita Vya Kwanza tukijumlisha tunapata  jawabu ni  50 na siyo  32 kama tulivyoona mwanzo sasa wapi huo Muujiza?

PROFESA: Naam, Haya ndiyo maajabu kwani ukijumlisha Majawabu Haya Matatu tuliyofanya hapa juu tunapata 32 + 32 + 50=114

Tunapata Namba ya kushangaza sana nayo labda  inaashiria  Jumla ya Sura za Kuruani ambazo ni 114

AL-AMIN ALI HAMAD: Eeeeeeeeee Profesa Yayayayaya  Mbona Haya Maajabu makubwa. Mbona Hizi Namba Zinashangaza..  Kwanza Namba  tulizopata zilikuwa Zinafanana. Kisha Uhuru wa Msikiti  wa Palestina huko Israeli sasa mbona Namba 114 ni Jumla Ya Sura za Kuruani?  Kwa kweli inashangaza sana tena  sana.

PROFESA: Mimi siwezi kukujibu kwani Mara nyingi namba huwa zinadanganya. Uwe macho  usifuatilie sana.

AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa unaaema kweli lakini  ninashangaa sana, sana sana. Kwani Mwenyeezi Mungu ameumba Dunia Kwa Kutumia Namba. Na Kwa kweli Ulimwengu ni Kuruani Tunayoiona kwa macho na Kuruani ni Ulimwengu tunausoma. Kwa nini isiwe kweli? mambo haya yana maajabu sana.

PROFESA: Wakati wa usiku umeingia na ningeona bora tufanye kukutana tena kesho Mwenyeezi Mungu akipenda kwa Mazungumzo  zaidi.

AL-AMIN ALI HAMAD: Profesa Asante sana kwa kunipa  habari mpya  leo hii. Mwenyeezi Mungu akubariki. Leo usiku  nitakapokuwa kitandani nitawaza sana Namba hizi na hasa Vita Vya Dunia Kwani Inatisha sana.

PROFESA:Usiogope  Namba zinababaisha. Usifuatilie mambo  bila ya Uhakika. Mwachie Mwenyeezi Mungu tu. Wewe Omba Dua tu Mwenyeezi Mungu atuepushie na Hatari za Vita Vua Dunia.

AL-AMIN ALI HAMAD: Asante Sana Profesa. Inshaallah Tutatonana Kesho mwenyeezi Mungu akipenda.

PROFESA: Amin

INAENDELEA…………………………………….